Uchaguzi 2020 Baada ya mbinu hii, Uchaguzi wa 2020 tulidhani Magufuli atapita bila kupingwa

Uchaguzi 2020 Baada ya mbinu hii, Uchaguzi wa 2020 tulidhani Magufuli atapita bila kupingwa

Nkobe

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2013
Posts
2,204
Reaction score
3,277
Tangu Rais Magufuli aingie madarakani, tumeshuhudia kila mbinu imetumika kuhakikisha mwenye mawazo mbadala hatoi maoni yake kwa namna yoyote ile. Kwa miaka 5 vyazo vyote vya habari vilitekwa, kila chombo cha habari kilihakikisha kinatangaza sifa za mfalme, kuna TV zimediliki hata kuacha mipangilio yao ya vipindi na kupiga kambi kwenye jumba la mfalme ili kurusha uapisho wa mkuu wa wilaya Live ili sifa na taarifa za mfalme zifike kila kona ya nchi, walishindwa tu kuingia chumbani kwa mfalme.

Baadhi ya TV zilienda mbali, zilihakikisha 80% matangazo yake ni vipindi maalum kwa ajili ya kusifu madege ya bombadier, fly over nk. Baadhi ya vyombo vya habari kama Tanzania Daima hadi sasa limefungiwa kwa sababu halikuweza kumsifu mfalme inavyotakiwa, lakini waliofanikiwa kumsifu mfalme tena kwa kutukana wapinzani wameachwa (Uhuru, Jamvi la habari, nk).

Upande wa wapinzani; Wapinzani wamefumbwa mdomo kwa miaka mitano, hawakuruhusiwa hata kufanya mikutano yao ya ndani, wakifanikiwa kufanya basi taarifa zao zitokee youtube yenye usajili wa nje ya nchi. Wafanyakazi wa serikali walitakiwa kabla ya kutoa hotuba/speech ni lazima asifu jina la mfalme ndipo iwe kheri yake.

Pamoja na hayo yote juu, tulitarajia kuwa upinzani umekufa kabisa na mfalme arudi bila kupingwa, cha kustaajabisha kuna wagombea zaidi ya 15 wamejitokeza kupambana na mfalme. Lakini jambo la kushangaza, tangu mwana wa risasi 16 aliporejea nchini, Watanzania wameonesha kuwa pamoja na vyanzo vyote vya habari kuhakikisha wanamsifu mfalme, bado upinzani unaonekana kuwepo kuliko ilivyodhaniwa.
 
Watu wamechoshwa na uchumi wa maigizo huku wamejaa shida tupu hivyo wanahitaji mtu sahihi anayejua shida zao na kuzitatua.
Watanzania wamegundua miradi yote mikubwa kuna wizi ufisadi 10% za wajanja wachache huko CCM wamegundua CCM ni ile ile wizi wa mali za umma upo palepale hakuna jipya ingawa wanajinadi kuleta maendeleo.
 
Hawa machingaz na bodaboda wanatakiwa wajiongeze, vitambulisho vikifutwa inamaana nao hawako rasmi na kisheria wajiandae kuburuzwa kama wakimbizi katika nchi yao.

Katika watu wanaotakiwa wamuogope Lissu kama ukoma ni machingaz na bodaboda Wakimshadadia Lissu anaweza akawake katika wakati mgumu sana baada ya uchaguzi huu kwisha na pengine atakuwa kajirudia zake Ubeligiji huku akiwacha machingaz katika kilio na kusaga meno.

#Tutashitakiwa MIGA
Lisu atawapa vitambulisho bure siyo kuwauzia kama wewe na CCM yako mnavyowaibia kwa njia haramu za kishetani
 
Nchi ina miaka 59 haina maendeleo licha ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani, kama siyo CCM mda huu Tanzania ingekuwa na kura ya Veto ingekuwa ipo kwenye G5 Duniani, level ile ya America, Urusi, German, England, China, Japan na mataifa yale tajiri Duniani, pesa za kujengea viwanda kila kata vyuo vikuu kila wilaya Hosptal za rufaa kubwa zenye madaktari Bingwa kila mkoa barabara vijijini madaraja toka Dsm mpaka Zanzibar na pemba yote inatumika kuidhoofisha chadema kurejesha mfumo wa chama kimoja, pesa nyingi inapotelea kwenye mambo yasiyo na Tija kwa Taifa na endapo CCM wangekuwa wamezitumia hizo pesa kwenye maendeleo wasingekuwa wanahaha kuwabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani, wangevuna kura kiwepesi pasipo kutumia nguvu.
 
Unyanyasaji wa CCM kwa wapinzani ndiyo umewapa nguvu sasa
 
Hawa machingaz na bodaboda wanatakiwa wajiongeze, vitambulisho vikifutwa inamaana nao hawako rasmi na kisheria wajiandae kuburuzwa kama wakimbizi katika nchi yao.

Katika watu wanaotakiwa wamuogope Lissu kama ukoma ni machingaz na bodaboda Wakimshadadia Lissu anaweza akawake katika wakati mgumu sana baada ya uchaguzi huu kwisha na pengine atakuwa kajirudia zake Ubeligiji huku akiwacha machingaz katika kilio na kusaga meno.

#Tutashitakiwa MIGA
Mtapata tabu sana vitambulisho vitafutwa ili wasinyonywe na wafanye kaz bila usumbufu wowote bure na sio huo mradi wa bashite na mgombea wenu magufuli
 
UCHAGUZI HUU UKIISHA ....KUNA WATU MAGUFULI ATAWAFUKUZA KAZI AU ATAWAMALIZA ..KWA MIAKA MITANO WAMEKUWA WAKIMUAMINISHA HAKUNA UPINZANI NCHINI NA WENGINE WAKAWANUNUA ,,,LAKINI IMEISHIA KUWA FEDHEHA ...
INAONYESHA WAZI KUWA MBINU KAMA ZA KIKWETE ZA KUACHA SIASA IENDELEE ZIILIKUWA NZURI ZINAFANYA NCHI INAPUMUA NA HOJA INAJIBIWA KWA HOJA ...LEO HII NANI ANGEKIMBILIA KUWASIKILIZA WAPINZANI >> WANGEKUA HAWANA HOJA
 
Chema chajiuza kibaya chajitembeza , unatenda mazuri utahangaika na televisheni zikuonyeshe wewe tu kutwa kucha lakini wapi watu wamemgundua muuza nyumba za serikali kwa ufisadi , kuendeleza kwenye ndege , Standard Gauge, Stiegersgorge hata aibu hana kutuletea mandege used.
 
Back
Top Bottom