Sihitaji kufurahishwa na mtuSina haja ya kumbeza maana natambua mchango wake kwa CDM, ila kwa sasa hastahili kuendelea kuwa mwenyekiti wa CDM. CDM naikubali niibeze ili ,nikufurahishe ww?
Nchi inaliwa mchana kweupeeeKwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi unaofanywa na wapinzani kwa CCM ila kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.
Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.
Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.
Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.
Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.
Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?
Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM
Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na
1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake kutoka Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU
2. Je ana masilahi binafsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?
3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".
Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Ni hivi,
Mlicho kifanya ni kujusalimisha kwa ccm kwamba sasa hamuwawezi, na sasa wao wanaweza kuwageuka mda wowote msifanye kitu!
Mikutano ipo kikatiba, anapotokea mtu anazuia hupaswi kuiomba mezani unaidai kwa nguvu ikiwezekana damu kumwagika, huo ndio upinzani, jifunzeni hapo kwa wenzenu Kenya tu.
Yani sasa hivi chadema ni mang'ombe tu kwa ccm!
Sihitaji kufurahishwa na mtu
Mbowe bado anaushawishi ndani ya chama chenu na hakuna anayeweza kwenda kinyume naye akasalia ndani ya chama.
Tatizo mkiambiwa huko mitaani hali ni tofauti na humu mitandaoni huwa hamtaki kuelewa, humu mitandaoni watu wako teyari kuingia barabarani ila huko uraiani hali ni tofauti.Ni bora wapige Dili tu kwa sababu Watanzania ukiwaambia tokeni mabarabarani tudai haki zetu hutomuona hata mtu mmoja barabarani !! Mange Kimambi analijua hilo !!
Ulikua unataka chadema ifanye nini?John Cheyo akisoma comment yako anacheeka, anasema mlinisema sana kujiweka karibu na CCM, mbona na nyie mnafanya kama mimi sasa?[emoji16][emoji16]
John cheyo ndio Nani bhana na atupishe.John Cheyo akisoma comment yako anacheeka, anasema mlinisema sana kujiweka karibu na CCM, mbona na nyie mnafanya kama mimi sasa?[emoji16][emoji16]
Endeleeni kutumia uoga wa watanzania kujipa matumizi.Tatizo mkiambiwa huko mitaani hali ni tofauti na humu mitandaoni huwa hamtaki kuelewa, humu mitandaoni watu wako teyari kuingia barabarani ila huko uraiani hali ni tofauti.
Zitto nae anasema chama chake ACT ndio kimepoteza watu wengi kuliko chama chochote.Daah wabongo bana yani mnajifanya mmesahau kabisa miaka mitano ya tabu na mateso kwa Chadema leo hii tunaana kupata mwanga wa kujiimarisha mmeanza majungu hii nchi wanafiki ni wengi sana.
Anachozungumzia Missile of the nation ni siasa za ushindani, si za kuunga mkono juhudi za CCM...Nchi inahitaji siasa mbadala, CCM ishatufilisi vya kutosha! Kina Mbowe wameingia mtego wa panya mroho...!Yes. Ni kweli kabisa..
Sijui kina Missile of the Nation ni kwanini tu wanaendelea kulilia siasa za uhasama za kuviziana na kupigana risasi, kutekana, kupotezana na kuuana ziendelee..
Mimi naona mambo yanaendelea vizuri kabisa. Vyama vya upinzani vinaendelea na siasa za majukwaani vyema Kwa kuikosoa na kuisema CCM kwelikweli. Katika situation kama hii mtu anawezaje kudai upinzani umekufa? Umekufaje Kwa mfano? Kwa kuwa CCM na CHADEMA wameweza kukaa pamoja na kukubaliana kuachana na siasa za uhasama wa kuuana?
Aaah, please give me a break ndugu Missile of the Nation !!
Watanzania sio waoga ila tu nyie mnakosea mnapofikiri haya ya huko mitandaoni ndio hali ipo hivyo mitaani, kama ingekuwa maandamano yanafanyika mitandaoni basi hakuna maandamano ambayo yangefeli nakumbuka hata maandamano aliyoyahitisha Lissu humu mitandaoni watu walionyesha kuwa wataandamana kivyovyote bila kuogopa mikwara ya polisi. Ila mitaani hali ilikuwa tofauti hakukuwa na watu wenye kupanga kuandamana na ndio maana siku ya tukio watu waliamka kuendelea na shughuli zao kama kawaida.Endeleeni kutumia uoga wa watanzania kujipa matumizi.
Hakika Chadema wako sahihi !!Ulikua unataka chadema ifanye nini?
Ifanye siasa za ukweli, siyo siasa za kuunga mkono juhudiUlikua unataka chadema ifanye nini?
Kwani Erythrocyte anasemaje?Kwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi unaofanywa na wapinzani kwa CCM ila kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.
Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.
Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.
Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.
Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.
Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?
Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM
Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na
1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake kutoka Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU
2. Je ana masilahi binafsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?
3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".
Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Mkuu naona umeshikilia msimamo wako[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]hauyumbishwi kabisaWapinzani sisi hatuelewi huo msimamo wa viongozi wa CDM kwa muongozo wa Mbowe. Wao viongozi waendelee na siasa za kujikomba, lakini sisi hatuna muda huo. Kama Mbowe aliweza kumpokea Lowassa na watu wakamvumilia, basi safari hii atajua hana ushawishi huo aliodhani anao. Ni muda mrefu Mbowe alishaonyesha kupoteza mwelekeo.
Huyo Kuna siku ataibuka shujaa pale mbowe atapopolewa chademaMkuu naona umeshikilia msimamo wako[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]hauyumbishwi kabisa
Nadhani hata kipindi Cha nani yule Nyalandu kutaka kupewa nafasi kugombea kwa tiketi ya CDM, ulishikilia msimamo wako kupinga