Pre GE2025 Baada ya Mbowe kutetea uenyekiti wake, masikini Tundu Lissu, kwishney! Je, atabaki ama atatimka? Lissu Cool down, usiitishe Press kumjibu Mbowe!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hayupo anayeongea. Hakuna hata anayethubutu kunong’ona. Ni kama vile walikubaliana kimyakimya kuwa hakuna lolote la kusema. Mtu mmoja, Pascal Mayalla akiwa nje ya Chadema, anaweza kufanya nini?
Mkuu Mdu, mdukuzi , asante kwa hoja hii, humu jf ya kisasa, watu wa hoja deep za kihivi humu, wanahesabika.
Swali linabaki, Tanzania itaamka lini? Tutapambana lini na adui huyu ambaye kila siku anazidi kutufanya watumwa wa wenye nguvu? Labda ni ndoto tu – ndoto inayongoja shujaa wa kuifanikisha. Swali ni; shujaa huyo ni nani? Na atafika lini?
Mungu Saidia!.
P
 
Naujua msimamo wako ni kutokukubaliana na kile unachokiita usultani wa utawala wa Mbowe ndani ya CHADEMA kwa muda mrefu. Ila kwa ukada na samahani kwa msamiati wa sasa unaotamba wa uchawa wako ndani ya CCM umejiunga na upande wa Abdul na mama Abdul ambao Tundu Lissu anautuhumu kwa rushwa.

Kwa Lissu kumtuhumu mama Abdul umerudi upande wa makada wengi wa CCM kumsapoti Mbowe, ingawa wengi wa wachambuzi wa siasa za Tanzania hususan za CHADEMA wameonuesha kuwa Lissu ndio mwenye ushawishi mkubwa kuelekea kwenye uchaguzi wa CHADEMA jan 2025 wewe umembaragaza kuwa anaweza kupata kura moja. Kama itabidi kumsafisha mama Abdul na tuhuma za Lissu bora Mbowe abaki kuwa mwenyekiti. Huu ni unafiki mkubwa ambao umapatikana CCM pekee.

Kwako kwa sababu ukada ni kama imani basi kwa Mbowe kukanusha kuwa hakuna rushwa imekuwa ni uzushi kwa sababu aliowatuhumu ni malaika inashusha credibility ya Pascal licha ya makala ndefu zisizo na uzito kama ile ya kusifia CCM kwa ushindi wa serikali za mitaa wa 2024. Hivi CCM bila unafiki hamuendi?

Ulifanya tafiti yeyote kuthibitisha hoja zako au ukada tu? Hivi kutoka ndani ya kilindi cha moyo wako kwa Mbowe kutangaza kugombea uenyekiti ni mwisho wa Lissu?

Kwa Mbowe kukanisha tuhuma za Lissu tayari Lissu amevuliwa nguo? Siyo wewe uliyesema kuwa Mbowe na sultani? Kuisafisha CCM bora umbagaze Lissu, CCM na umafiki damu damu
 
Wanabodi,

Kitu cha pili ni kumuomba, Please please please, Tundu Lissu, usiitishe press conference yoyote kumjibu Mbowe, huo utakuwa ni utovu wa nidhamu, Kaka yako mkubwa Kaka Paskali.
Baada ya kusikia Lissu ana Press leo saa 6 mchana, nimeona nimkumbushe ushauri huu, autumie vizuri uhuru wake wa kujieleza, ila asimjibu bosi wake Mbowe, asije kuonekana ni mtovu wa nidhamu!.
P
 
😆😆😆😆😆😆😂😂😂😂😂😂

Cc Robert Heriel Mtibeli
 
Unaendeleaje kaka Mayala?
 
Baada ya kusikia Lissu ana Press leo saa 6 mchana, nimeona nimkumbushe ushauri huu, autumie vizuri uhuru wake wa kujieleza, ila asimjibu bosi wake Mbowe, asije kuonekana ni mtovu wa nidhamu!.
P
JPM aliona mbali sana wakafuata...Wajumbe....ujuaji mbaya sana...
 
Nakiri hapa I was wrong!, nili mu under estimates TAL!.
Sasa nimekubali!
One down, two to go!.
October 2025 ule mbuyu unakwenda chini!.
Usikute Lissu ni mpango wa Mungu kwa Tanzania post '25.
Mwacheni Mungu aitwe Mungu!.
Hongera Sana Tundu Lissu!.
P
 
Paskali wewe ulikula ngapi kutoka kwa mbowe ili uandike uchuro wako huo

Koma kulazimisha undugu wakishule na LISU
 
Tupatie matokeo mkuu!! 🤣 🤣 🤣
 
Nakiri hapa I was wrong!, nili mu under estimates TAL!.
Sasa nimekubali!
One down, two to go!.
October 2025 ule mbuyu unakwenda chini!.
Usikute Lissu ni mpango wa Mungu kwa Tanzania post '25.
Mwacheni Mungu aitwe Mungu!.
Hongera Sana Tundu Lissu!.
P
Wee mzee Ni snitch sana,
Marehemu alikua sahii kukuita alivyokuita
 
paschal Mayalla njoo tena kisha toa maoni yako..

Tundu Lissu ndiye Mwenyekiti mpya wa CHADEMA..

Msitegemeage akili na ufahamu wenu corrupt wa kibinadamu ktk kufanya judgement ya situation fulani...

Someni alama za majira na nyakati, kisha toa judgement...

Sisi wengine tulimtetea sana Freeman Mbowe miaka ya nyuma aendelee kuwa kiongozi wa chama hiki..

Lakini safari hii tuliona kabisa, nyakati na majira haziko upande wake...

Tukamshauri, lakini kama tu ambavyo mioyo ya wanadamu ilivyo na asili ya ugumu, akakataa ushauri wetu...

Amerudi square one (palepale) lakini kwa gharama na hasara kubwa..

Tunamshukuru kwa ujasiri wake wa ku - concede..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…