Baada ya Mdau wa JF kuomba msaada Mgonjwa wake afanyiwe upasuaji, MOI yatoa ufafanuzi na maelekezo

Baada ya Mdau wa JF kuomba msaada Mgonjwa wake afanyiwe upasuaji, MOI yatoa ufafanuzi na maelekezo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Oktoba 23, 2024, Mwanachama wa JamiiForums.com aliandika andiko la kuomba msaada wa wapi anapoweza kupata fedha au ufadhili kwa ndugu yake ambaye ni mgonjwa aliyelatwa katika Tasisi ya MOI, akisema kuwa gharama ya upasuaji Tsh Milioni 1.6 ni kubwa kwa familia yake ambayo imejichanga na kupata Tsh. Laki 3 tu.

Kumsoma Mdau bofya hapa: Msaada wa haraka wapendwa, mgonjwa wangu anahitaji Upasuaji MOI na familia haina fedha

Muda mfupi baada ya andiko hilo, Uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) umemjibu Mdau huyo kwa kumpa maelekezo ya nini anatakiwa kukifanya.

Meneja Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi anazungumza
Akizungumza na JamiiForums kuhusu Mdau huyo, amesema "Tumeona kwenye mtandao wenu kuhusu mgojwa kuwa na changamoto ya kifedha, tunamuomba Mgonjwa au anayemuuguza afike Ofisi za Afisa Mahusiano MOI ili asikilizwe. Tutaangalia kama alifuata hatua zinazotakiwa kufuatwa kwa mgonjwa ambaye hana fedha ili aweze kusaidiwa.

“MOI ni Hospitali ya Serikali na ina utaratibu wa kuwa inawasaidia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kifedha, Mkurugenzi huwa anatoa huo uthibitisho wa msamaha wa Wagonjwa hadi wale wa Shulingi Milioni 10.

“Kuna wagonjwa ambao hawana hata ndugu na tunawahudumia, sasa huyo ambaye ana ndugu kwa nini tusimuhudumie?

"Niwaombe tuendelee kuelimishana, fika Ofisi ya Ustawi wa Jamii au ukiona hujapata majibu ya kueleweka fika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji au Afisa Uhusiano utasaidiwa."
 
Oktoba 23, 2024, Mwanachama wa JamiiForums.com aliandika andiko la kuomba msaada wa wapi anapoweza kupata fedha au ufadhili kwa ndugu yake ambaye ni mgonjwa aliyelatwa katika Tasisi ya MOI, akisema kuwa gharama ya upasuaji Tsh Milioni 1.6 ni kubwa kwa familia yake ambayo imejichanga na kupata Tsh. Laki 3 tu.

Kumsoma Mdau bofya hapa ~ Msaada wa haraka wapendwa, mgonjwa wangu anahitaji Upasuaji MOI na familia haina fedha

Muda mfupi baada ya andiko hilo, Uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) umemjibu Mdau huyo kwa kumpa maelekezo ya nini anatakiwa kukifanya.

Meneja Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi anazungumza
Akizungumza na JamiiForums kuhusu Mdau huyo, amesema "Tumeona kwenye mtandao wenu kuhusu mgojwa kuwa na changamoto ya kifedha, tunamuomba Mgonjwa au anayemuuguza afike Ofisi za Afisa Mahusiano MOI ili asikilizwe. Tutaangalia kama alifuata hatua zinazotakiwa kufuatwa kwa mgonjwa ambaye hana fedha ili aweze kusaidiwa.

“MOI ni Hospitali ya Serikali na ina utaratibu wa kuwa inawasaidia wagonjwa ambao hawana uwezo wa kifedha, Mkurugenzi huwa anatoa huo uthibitisho wa msamaha wa Wagonjwa hadi wale wa Shulingi Milioni 10.

“Kuna wagonjwa ambao hawana hata ndugu na tunawahudumia, sasa huyo ambaye ana ndugu kwa nini tusimuhudumie?

"Niwaombe tuendelee kuelimishana, fika Ofisi ya Ustawi wa Jamii au ukiona hujapata majibu ya kueleweka fika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji au Afisa Uhusiano utasaidiwa."
Asanteni sana ndugu zangu naanza ufatiliaji.
 
Majibu yamekaa kama kisiasa fulani hivi maana ukifika huko ofisini danadana kibao na mwisho wa siku unaambiwa mkono mtupu haulambwina

Majibu yamekaa kama kisiasa fulani hivi maana ukifika huko ofisini danadana kibao na mwisho wa siku unaambiwa mkono mtupu haulambwi
Hii mambo ya ustawi wa jamii, sijui msamaha wa matibabu kwa wagonjwa umekaa siasa nyingi
Back in those days nikiwa hospital moja hapa nchini (jina kapuni ), aliletwa dada mmoja na wasamaria wema, yule dada alikuwa mhudumu wa bar (barmaid) ambae baada ya kumsikiliza maelezo yake ni kwamba alijisikia kuumwa, akamuomba boss wake amsaidie pesa aende hospital, lakini hakupewa. Hyo siku akiwa anarudi home akaanguka na kupoteza fahamu Hadi alioojikuta hospital
Hospital ilifanya mawasiliano na ndugy zake, wa karibu alikuwa bibi ake aliyekuwa mkoani huko nae akasema Huwa anamtegemea Binti ili kuilisha familia hvyo Hana Cha kufanya.
Utaratibu wa kupata kibali Sasa kutoka ustawi wa jamii, ulichukua zaidi ya wiki nzima. Hapo Binti Hana sawa, chakula, madaktari wakifika wanakipita kitanda chake
Hadi anakuja kupata kibali, ni ameteseka vya kutosha

Kwahyo...nakubaliana na ww kwamba Kuna siasa nyingi sana and they are so selective kwa watu wa kuwasaidiaa

Kikubwa, tutafute pesa na tutunze afya zetu tu.
Hospital nyingi zipo kwenye biashara
 
Hamna kitu hapo.hata ufate utaratibu wote kupata huduma ni ngumu sana bila pesa huwezi kupata huduma.Nimeshuhudia wagonjwa wa namna hiyo wengi tu.Zaidi anaweza kuandikiwa dawa aende akanunue mwenyewe.Tanzania hakuna Cha bure.wanaopata Cha Bure ni viongozi tu wanaohudumiwa na Kodi zetu
 
Hii mambo ya ustawi wa jamii, sijui msamaha wa matibabu kwa wagonjwa umekaa siasa nyingi
Back in those days nikiwa hospital moja hapa nchini (jina kapuni ), aliletwa dada mmoja na wasamaria wema, yule dada alikuwa mhudumu wa bar (barmaid) ambae baada ya kumsikiliza maelezo yake ni kwamba alijisikia kuumwa, akamuomba boss wake amsaidie pesa aende hospital, lakini hakupewa. Hyo siku akiwa anarudi home akaanguka na kupoteza fahamu Hadi alioojikuta hospital
Hospital ilifanya mawasiliano na ndugy zake, wa karibu alikuwa bibi ake aliyekuwa mkoani huko nae akasema Huwa anamtegemea Binti ili kuilisha familia hvyo Hana Cha kufanya.
Utaratibu wa kupata kibali Sasa kutoka ustawi wa jamii, ulichukua zaidi ya wiki nzima. Hapo Binti Hana sawa, chakula, madaktari wakifika wanakipita kitanda chake
Hadi anakuja kupata kibali, ni ameteseka vya kutosha

Kwahyo...nakubaliana na ww kwamba Kuna siasa nyingi sana and they are so selective kwa watu wa kuwasaidiaa

Kikubwa, tutafute pesa na tutunze afya zetu tu.
Hospital nyingi zipo kwenye biashara
Kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom