Mimi ni mwanachama hai wa Simba. sina haja ya kuweka namba yangu . Kuna mambo ambayo nayakubali katika mpira bila kupepesa macho siku zote nitasisitiza. Kwa hatua tuliyofika sasa Mpira wetu unataka pesa.
Mo Dewj amenyimwa Simba kwa sababu ambazo siwezi kusema lolote. lakini pia sitaki kusema kama mwarobaini pekee ulikuwa yeye ingawa naamini kama angepewa simba tungepata nafasi ya kuangalia msimu huu anaijengaje na nini matokeo yake.mpira ni pesa. leo tarehe 31/07/1026 nawaambia wanachama wa Simba kama suala la Mo Dewj limepigwa tena danadana na mwishowe kubutuliwa mbali kabisa nje ya uwanja. msimu huu utakuwa ni mmoja ya misimu mibaya kabisa ya Simba. wachezaji wameshaanza kukata tamaa na hili husababisha wauze mechi au wacheze chin ya Kiwango.
Tatizo si kocha, tatizo ni Uongozi na pia ukata ndo utakaoua team ya simba. wachezaji wengi wameonekana kukosa morali baada ya kuona ajenda ya Mo Dewj Kupewa Team imetupiliwa Mbali. wengi wanalalamika kuwa pesa hawapati za kutosha na kwa wakati muafaka. ukiacha mazingira mazuri n.k. watu wasisahau mpira huu wa sasa ni ajira na si mapenzi.
Nafasi hii itasababisha wachezaji wetu wanunuliwe na team zenye pesa wanapocheza nazo na hivyo kupoteza mechi hizo. NAWAHAKIKISHIA SIMBA IKIJITAHIDI SANA MSIMU HUU KAMA HAKUTAFANYIKA MABADILIKO BASI NI NAFASI YA NNE AU TANO NA UKITOKEA MUUJIZA NAFASI YA 3.
Kama Ungozi huu utaendelea ulivyo na Simba ikachukua Ubingwa Nipigwe BAN MILELE HUMU JAMII FORUMS. na ikichukua NAFASI YA PILI NIPIGWE BAN MIEZI MIWILI.
Tunaumia kuona Yanga wananunua mechi ngumu za hapa TZ wanshinda wanaenda kucheza mechi za Kimataifa huku wao wakifurahia tu kupanda ndege na si kwenda Kushindana. Sisi tunataka Simba iende kushindana na si kutaka kupanda ndege.
Mtakumbuka hadithi ile ya JOGOO ALIYESEMA.
Kina Aveva na Kassim Dewji walitumia mamilioni ya pesa kupitia kwa Ndumbaru kuhakikisha wanaingia kwenye uongozi. Kamwe hawataachia uongozi SSC. Wanajua faida wanazopata bila kujali kabisa maendeleo ya timu. Muulize mwanasimba yeyote i wapi timu ya vijana ambayo ilikuwa tishio? Uwanja ambao uliweka matumaini kwa wanasimba kuwa kuna hatua itapigwa uko wapi? Wameshindwa kuuza kile kiwanja kwa kisingizio cha kupata fedha za kununua wachezaji. Kumbuka Aveva aliwahi kuuza gari la club kwa kisingizio kuwa alikuwa anatafuta pesa ya kumnunua mchezaji. Nasikia juzi baada ya wanachama wa SSC kutamka wazi wanamtaka MO kina Dewji na Aveva wamepeleka katapila kwenye uwanja wa Bunju eti wanatengeneza uwanja!!! Hili ni kanyaga boya. Subiri hili vugu vugu la MO lipite. Naamini ule uwanja wa Bunju utauzwa kabla hawa wapiga dili Aveva na Dewji hawajamaliza muda wao wa kikatiba.