Baada Ya Mo Dewj Kunyimwa Simba, Msimu Huu wa Simba Utakuwa mbaya kuliko yote

Baada Ya Mo Dewj Kunyimwa Simba, Msimu Huu wa Simba Utakuwa mbaya kuliko yote

Mimi ni mwanachama hai wa Simba. sina haja ya kuweka namba yangu . Kuna mambo ambayo nayakubali katika mpira bila kupepesa macho siku zote nitasisitiza. Kwa hatua tuliyofika sasa Mpira wetu unataka pesa.

Mo Dewj amenyimwa Simba kwa sababu ambazo siwezi kusema lolote. lakini pia sitaki kusema kama mwarobaini pekee ulikuwa yeye ingawa naamini kama angepewa simba tungepata nafasi ya kuangalia msimu huu anaijengaje na nini matokeo yake.mpira ni pesa. leo tarehe 31/07/1026 nawaambia wanachama wa Simba kama suala la Mo Dewj limepigwa tena danadana na mwishowe kubutuliwa mbali kabisa nje ya uwanja. msimu huu utakuwa ni mmoja ya misimu mibaya kabisa ya Simba. wachezaji wameshaanza kukata tamaa na hili husababisha wauze mechi au wacheze chin ya Kiwango.

Tatizo si kocha, tatizo ni Uongozi na pia ukata ndo utakaoua team ya simba. wachezaji wengi wameonekana kukosa morali baada ya kuona ajenda ya Mo Dewj Kupewa Team imetupiliwa Mbali. wengi wanalalamika kuwa pesa hawapati za kutosha na kwa wakati muafaka. ukiacha mazingira mazuri n.k. watu wasisahau mpira huu wa sasa ni ajira na si mapenzi.

Nafasi hii itasababisha wachezaji wetu wanunuliwe na team zenye pesa wanapocheza nazo na hivyo kupoteza mechi hizo. NAWAHAKIKISHIA SIMBA IKIJITAHIDI SANA MSIMU HUU KAMA HAKUTAFANYIKA MABADILIKO BASI NI NAFASI YA NNE AU TANO NA UKITOKEA MUUJIZA NAFASI YA 3.

Kama Ungozi huu utaendelea ulivyo na Simba ikachukua Ubingwa Nipigwe BAN MILELE HUMU JAMII FORUMS. na ikichukua NAFASI YA PILI NIPIGWE BAN MIEZI MIWILI.

Tunaumia kuona Yanga wananunua mechi ngumu za hapa TZ wanshinda wanaenda kucheza mechi za Kimataifa huku wao wakifurahia tu kupanda ndege na si kwenda Kushindana. Sisi tunataka Simba iende kushindana na si kutaka kupanda ndege.


Mtakumbuka hadithi ile ya JOGOO ALIYESEMA.


Kina Aveva na Kassim Dewji walitumia mamilioni ya pesa kupitia kwa Ndumbaru kuhakikisha wanaingia kwenye uongozi. Kamwe hawataachia uongozi SSC. Wanajua faida wanazopata bila kujali kabisa maendeleo ya timu. Muulize mwanasimba yeyote i wapi timu ya vijana ambayo ilikuwa tishio? Uwanja ambao uliweka matumaini kwa wanasimba kuwa kuna hatua itapigwa uko wapi? Wameshindwa kuuza kile kiwanja kwa kisingizio cha kupata fedha za kununua wachezaji. Kumbuka Aveva aliwahi kuuza gari la club kwa kisingizio kuwa alikuwa anatafuta pesa ya kumnunua mchezaji. Nasikia juzi baada ya wanachama wa SSC kutamka wazi wanamtaka MO kina Dewji na Aveva wamepeleka katapila kwenye uwanja wa Bunju eti wanatengeneza uwanja!!! Hili ni kanyaga boya. Subiri hili vugu vugu la MO lipite. Naamini ule uwanja wa Bunju utauzwa kabla hawa wapiga dili Aveva na Dewji hawajamaliza muda wao wa kikatiba.
 
Moja kati ya timu ambazo Yanga alipiga mbele-nyuma (yaani, kampa ... kampa tena) ni Simba. Ina maana Yanga alinunua mechi za Simba au kwa maneno mengine Simba ni ____ poa?

Mimi nawashangaa sana wamatopeni. Kwani wakati ule Simba inafadhiliwa na Azim Dewji, tulikuwa hatuwabandui nyie?

Halafu mihemko ya kuzungumzia mechi za Yanga, mnaishia kwenye matokeo au mnaangalia na kiwango cha mpira kinachopigwa? Kama Yanga amenunua mechi, siku mliotandikwa bao moja (cha nguruwe) na Toto Africa, na wao walinunua mechi? Hebu acheni mambo ya kipuuzi, jadilini mambo yenu ya hina huko, mwanaume muacheni.

Kwa kuwasaidia tu...NI YANGA TU NDIO ILIWAHI KUTOKA NJE YA MIPAKA NCHI, IKATIMUA TIMBWILI NA KUJA NA NDOO HOME. Nyie ni mama wa nyumbani, kama kwenye kabati lenu kuna chochote, basi kimepatikana hapa hapa nyumbani. Ubavu wa kwenda kwenye ardhi ya watu kukinukisha nyie hamna. Mbwa koko habweki ugenini...kaeni kimya

View attachment 373936
Huwa tuna msimamo mmoja kwenye mambo Fulani, lakini huku umenitwanga hadi kizunguzungu. Pamoja na mapenzi kwa mnyama lakini kuna mengi kama yana gusa penyewe hivyo uungwana ngoja nichutame.
 
Mkuuu Sodoku usitake kutuharibia timu...haya mawazo yako mgando nenda kashauri kwenye timu yako ya JANGWANI...aka kafungwa kafungwa tena!
 
Kwani kikao tayari wamekaa, mi nashauri apewa Mo atasaidia
 
Ninavyojua Mimi uongozi umesema ni wazi wanachama wanataka mabadiliko hii ilitokana na wanachama kuanza kupiga kelele kuwa wanamtaka Mo baada ya Aveva na Azim kuanza kukwepesha kwepesha kama kwamba haiwezekani ndipo alipokatishwa kwa makelele ya wanachama hao hivyo basi kinachofata ni kamati tendaji kwa kushirikiana na wanacheria walifanyia kazi...
 
Mimi ni mwanachama hai wa Simba. sina haja ya kuweka namba yangu . Kuna mambo ambayo nayakubali katika mpira bila kupepesa macho siku zote nitasisitiza. Kwa hatua tuliyofika sasa Mpira wetu unataka pesa.

Mo Dewj amenyimwa Simba kwa sababu ambazo siwezi kusema lolote. lakini pia sitaki kusema kama mwarobaini pekee ulikuwa yeye ingawa naamini kama angepewa simba tungepata nafasi ya kuangalia msimu huu anaijengaje na nini matokeo yake.mpira ni pesa. leo tarehe 31/07/1026 nawaambia wanachama wa Simba kama suala la Mo Dewj limepigwa tena danadana na mwishowe kubutuliwa mbali kabisa nje ya uwanja. msimu huu utakuwa ni mmoja ya misimu mibaya kabisa ya Simba. wachezaji wameshaanza kukata tamaa na hili husababisha wauze mechi au wacheze chin ya Kiwango.

Tatizo si kocha, tatizo ni Uongozi na pia ukata ndo utakaoua team ya simba. wachezaji wengi wameonekana kukosa morali baada ya kuona ajenda ya Mo Dewj Kupewa Team imetupiliwa Mbali. wengi wanalalamika kuwa pesa hawapati za kutosha na kwa wakati muafaka. ukiacha mazingira mazuri n.k. watu wasisahau mpira huu wa sasa ni ajira na si mapenzi.

Nafasi hii itasababisha wachezaji wetu wanunuliwe na team zenye pesa wanapocheza nazo na hivyo kupoteza mechi hizo. NAWAHAKIKISHIA SIMBA IKIJITAHIDI SANA MSIMU HUU KAMA HAKUTAFANYIKA MABADILIKO BASI NI NAFASI YA NNE AU TANO NA UKITOKEA MUUJIZA NAFASI YA 3.

Kama Ungozi huu utaendelea ulivyo na Simba ikachukua Ubingwa Nipigwe BAN MILELE HUMU JAMII FORUMS. na ikichukua NAFASI YA PILI NIPIGWE BAN MIEZI MIWILI.

Tunaumia kuona Yanga wananunua mechi ngumu za hapa TZ wanshinda wanaenda kucheza mechi za Kimataifa huku wao wakifurahia tu kupanda ndege na si kwenda Kushindana. Sisi tunataka Simba iende kushindana na si kutaka kupanda ndege.


Mtakumbuka hadithi ile ya JOGOO ALIYESEMA.
MO alishindwa Singida United,African Lyon ataiweza simba????
 
MO kama anamapenzi ya dhati na Simba amwage fedha pale kuisaidia timu msimu huu wa 2016/2017 na si anachotaka kufanya. Afadhiri timu isajiri,ijenge uwanja wake
Yaani awape pesa wakahonge michepuko Tu?
 
Mo anachukua team hutaki acha, na pesa ya kuendesha tram anatoa....wanachama tumelipitisha hilo kwenye mkutano, tunataka mabadiriko.
 
Jamani mwenye maazimio ya mkutano mkuu Juu ya hatma ya mo kuchukua timu atujuze ili tujue nasiii
 
Mo anachukua team hutaki acha, na pesa ya kuendesha tram anatoa....wanachama tumelipitisha hilo kwenye mkutano, tunataka mabadiriko.
Ndiyo ninanyo jua nashangaa huyu mleta mada sujui katoka wapi...
 
Nilitaman sana kuona kile kizazi kinachojibu hoja kwa hoja. nasikitika kumekuwa na kizazi ambacho wazaz wake wamepoteza muda mwingi kuwafunza watoto wao matusi kuliko hoja. Hili ni taifa la ajabu sana. Kila anayeweza kutumia JamiiForums kwa sasa anahikikisha kwanza amejifunza matusi kadiri awezavyo ili mwingine atakpokuwa na msimamo tofaut naye amtukane mpaka mtukanaji mdomo wake uwe kama choo. ni mioyo hiyo hiyo inayosukuma damu ndo inayozalisha matusi hayo?

Tunahitaj mabadiliko makubwa kwenye Elimu .
 
Nilitaman sana kuona kile kizazi kinachojibu hoja kwa hoja. nasikitika kumekuwa na kizazi ambacho wazaz wake wamepoteza muda mwingi kuwafunza watoto wao matusi kuliko hoja. Hili ni taifa la ajabu sana. Kila anayeweza kutumia JamiiForums kwa sasa anahikikisha kwanza amejifunza matusi kadiri awezavyo ili mwingine atakpokuwa na msimamo tofaut naye amtukane mpaka mtukanaji mdomo wake uwe kama choo. ni mioyo hiyo hiyo inayosukuma damu ndo inayozalisha matusi hayo?

Tunahitaj mabadiliko makubwa kwenye Elimu .



Umeona ukiongelea upumbavu wenu na huyo Mo Dewj wenu haitoshi hadi uitaje Yanga si ndio ???
 
Kwa hiyo timu apewe MO ili naye anunue mechi ?
Afadhali umemuuliza swali zuri. Watu wamekaa mchangani hadi akili zimepotea kabisa.
Umebaki ujinga mtupu. Wanamtaka anunue mechi kwa ufinyu wa akili
 
Back
Top Bottom