Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Saa hizi ni usiku mkubwa, usingizi umejigomea, hivyo nimeshuka jf.
Baada ya mwana CCM mwandamizi, ambaye ni born and breed CCM, kusema ukweli kuhusu ushindi wa uchaguzi kwenye baadhi ya maeneo, uchaguzi huendeshwa kwa mtindo wa Mutatis Mutandis!.
Hivyo kwa heshima na taadhima, naomba kuleta ombi maalum na mahsusi kwa watu maalum na mahsusi, hivyo hii thread sio thread ya kila mtu, au watu wote bali ni thread maalum na mahsusi kwa watu maalum na mahsusi na lengo maalum na mahsusi la
kutuma ujumbe maalum mahsusi kabisa kwa watu maalum na mahsusi kabisa!.
Tanzania sio nchi ya watu fulani tuu au chama fulani tuu, Tanzania ni nchi ya Watanzania wote, wa vyama vyote, wa dini zote, wa makabila yote, wa jamii zote, wa jinsia zote, wa rangi zote, wa hali zote za maisha, matajiri na masikini na Watanzania wa circumstances zote.
Mimi nikiwa mwandishi wa habari, nimeshuhudia chaguzi zetu zote za vyama vingi, zimekuwa zikiendeshwa kwa mtindo wa "Mutatis Mutandis" mwana CCM mwandamizi, amelithibitisha hili!.
Hivyo sasa tunapokwenda kwenye uchaguzi, naomba kutoa ombi maalum na mahsusi na angalizo muhimu kwa wahusika wakuu wa uchanguzi huu wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, baada ya kuendesha chaguzi zote zilizopita kwa Mutatis Mutandis, tunaomba uchaguzi wa serikali za mtaa wa mwaka huu wa 2024, usogezwe mbele, ufanyike siku moja na uchaguzi mkuu na kwa sheria moja ya uchaguzi na usimamiwe na uendeshwe na Tume moja huru na Shirikishi ya uchaguzi na utumie kanuni ya Kilatini ya "ceteris paribus" na sio kutumia zile kanuni zetu za kawaida za "Mutatis Mutandis"!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!
Nimesikia sauti, "voices from within" kuwa tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis, kama mwana CCM mwandamizi alivyoeleza, lile janga kama lile lililotokea, litatokea tena!.
Kwasababu hakuna ajuaye sababu ya kutokea lile janga, ni vizuri kusema ili kumkinga huyu akiyepo na majanga ya kujitakia bila kujua!. Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!
Wahusika wakuu wa uchanguzi huu, wakikubali uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu ujao wa 2025 kuunganishwa na kuendeshwa kwa ceteris paribus , taifa Letu litabarikiwa, na viongozi wetu wabarikiwa, na sisi wananchi wa kawaida pia, tutabarikiwa na kupata neema na mafanikio makubwa, na nchi yetu kupata ustawi mkubwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini tukiendelea kutumia ule mtindo wetu wa kawauda wa mutatis mutandis, taifa tutalaaniwa na viongozi wetu watalaaniwa na kuadhibiwa!, and you never know ni adhabu gani viongozi wetu wakuu wataadhibiwa this time around!
Mungu Mbariki Rais Samia, na watendaji wake wapate uwezo, watumie "Ceteris Peribus" kwa vyama vyote na sio kuendeleza "Mutatis Mutandis"
Mungu ibariki Tanzania.
NB. Sijaweka ufafanuzi wa maneno "Ceteris Peribus" na "Mutatis Mutandis" sio kwa bahati mbaya, nimefanya hivi kwa makusudi Mazima, kwa sababu ujumbe huu ni ujumbe maalum na mahsus kwa watu maalum na mahsus ambao mimi nawajua huwa wanatembelea sana jf, kwa vile watu hao, wanayajua maneno hayo. Wengine wasio husika hayawahusu, hivyo sikufafanua ili ujumbe huu uwafikie walengwa maalum na mahsusi tuu.
Hata Mungu alipotaka kumfikishia ujumbe maalum mfalme Belshaza, alimtumia kiganja cha mkono kikaandika kwenye ukuta wake, "Mene Mene Tekeli na Peresi", tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis badala ya kutumia Ceteris Peribus, then kuna siku Mene Mene Takeli na Peresi itakuja kuishukia Tanzania na kumshukia kiongozi wetu!.
Nawatakia Siku Njema,
Paskali.
Saa hizi ni usiku mkubwa, usingizi umejigomea, hivyo nimeshuka jf.
Baada ya mwana CCM mwandamizi, ambaye ni born and breed CCM, kusema ukweli kuhusu ushindi wa uchaguzi kwenye baadhi ya maeneo, uchaguzi huendeshwa kwa mtindo wa Mutatis Mutandis!.
Hivyo kwa heshima na taadhima, naomba kuleta ombi maalum na mahsusi kwa watu maalum na mahsusi, hivyo hii thread sio thread ya kila mtu, au watu wote bali ni thread maalum na mahsusi kwa watu maalum na mahsusi na lengo maalum na mahsusi la
kutuma ujumbe maalum mahsusi kabisa kwa watu maalum na mahsusi kabisa!.
Tanzania sio nchi ya watu fulani tuu au chama fulani tuu, Tanzania ni nchi ya Watanzania wote, wa vyama vyote, wa dini zote, wa makabila yote, wa jamii zote, wa jinsia zote, wa rangi zote, wa hali zote za maisha, matajiri na masikini na Watanzania wa circumstances zote.
Mimi nikiwa mwandishi wa habari, nimeshuhudia chaguzi zetu zote za vyama vingi, zimekuwa zikiendeshwa kwa mtindo wa "Mutatis Mutandis" mwana CCM mwandamizi, amelithibitisha hili!.
Hivyo sasa tunapokwenda kwenye uchaguzi, naomba kutoa ombi maalum na mahsusi na angalizo muhimu kwa wahusika wakuu wa uchanguzi huu wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, baada ya kuendesha chaguzi zote zilizopita kwa Mutatis Mutandis, tunaomba uchaguzi wa serikali za mtaa wa mwaka huu wa 2024, usogezwe mbele, ufanyike siku moja na uchaguzi mkuu na kwa sheria moja ya uchaguzi na usimamiwe na uendeshwe na Tume moja huru na Shirikishi ya uchaguzi na utumie kanuni ya Kilatini ya "ceteris paribus" na sio kutumia zile kanuni zetu za kawaida za "Mutatis Mutandis"!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!
Nimesikia sauti, "voices from within" kuwa tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis, kama mwana CCM mwandamizi alivyoeleza, lile janga kama lile lililotokea, litatokea tena!.
Kwasababu hakuna ajuaye sababu ya kutokea lile janga, ni vizuri kusema ili kumkinga huyu akiyepo na majanga ya kujitakia bila kujua!. Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!
Wahusika wakuu wa uchanguzi huu, wakikubali uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu ujao wa 2025 kuunganishwa na kuendeshwa kwa ceteris paribus , taifa Letu litabarikiwa, na viongozi wetu wabarikiwa, na sisi wananchi wa kawaida pia, tutabarikiwa na kupata neema na mafanikio makubwa, na nchi yetu kupata ustawi mkubwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini tukiendelea kutumia ule mtindo wetu wa kawauda wa mutatis mutandis, taifa tutalaaniwa na viongozi wetu watalaaniwa na kuadhibiwa!, and you never know ni adhabu gani viongozi wetu wakuu wataadhibiwa this time around!
Mungu Mbariki Rais Samia, na watendaji wake wapate uwezo, watumie "Ceteris Peribus" kwa vyama vyote na sio kuendeleza "Mutatis Mutandis"
Mungu ibariki Tanzania.
NB. Sijaweka ufafanuzi wa maneno "Ceteris Peribus" na "Mutatis Mutandis" sio kwa bahati mbaya, nimefanya hivi kwa makusudi Mazima, kwa sababu ujumbe huu ni ujumbe maalum na mahsus kwa watu maalum na mahsus ambao mimi nawajua huwa wanatembelea sana jf, kwa vile watu hao, wanayajua maneno hayo. Wengine wasio husika hayawahusu, hivyo sikufafanua ili ujumbe huu uwafikie walengwa maalum na mahsusi tuu.
Hata Mungu alipotaka kumfikishia ujumbe maalum mfalme Belshaza, alimtumia kiganja cha mkono kikaandika kwenye ukuta wake, "Mene Mene Tekeli na Peresi", tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis badala ya kutumia Ceteris Peribus, then kuna siku Mene Mene Takeli na Peresi itakuja kuishukia Tanzania na kumshukia kiongozi wetu!.
Nawatakia Siku Njema,
Paskali.