Baada ya Mwl. Mussa Iddy kulalamika, HESLB yatoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa urejeshaji mikopo

Baada ya Mwl. Mussa Iddy kulalamika, HESLB yatoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa urejeshaji mikopo

Nadaiwa mkuu Mimi wa asilimia 8% nili sign mikopo sasa nadaiwa 15% ya mkopo nje ya mkataba huo si wizi wa mchana kweupe kabisa
Hahahah hii ni sawa na ile ya kuagiza gari kwa kodi ya million 5 ilifika unaambiwa utalipa 12 sababu mwaka umebadilika. Haina mjadala😂
 
Hahahah hii ni sawa na ile ya kuagiza gari kwa kodi ya million 5 ilifika unaambiwa utalipa 12 sababu mwaka umebadilika. Haina mjadala[emoji23]
Yani ni shida hafu Ada yangu kwa mwaka ilikuwa milion Moja imagine hzo retention fee zibaji double tu. Huu ujinga wa mkopo ni janga
 
Na wenyewe utawasikia wakitoa gawio kwa serikali kwa pesa hii hii ya wizi wanayoita retention fee.
 
Sijaona majibu yeyote ya maana kutoka loan board zaidi ya kumtisha iddy tu na kutuaminisha eti iddy ameelewa na atakuwa balozi....ameelewa nini kwenye yale malalamiko yake? Retention fees ndio kitu gani? kwani ule mkpo ni biashara? Nimrodi Mkono alituanzishia janga la kitaifa.

Hivi kumbe lilikuwa wazo la Nimrodi, au ndo sababu anateseka saivi!!
 
Yani ni shida hafu Ada yangu kwa mwaka ilikuwa milion Moja imagine hzo retention fee zibaji double tu. Huu ujinga wa mkopo ni janga
Hahahahah we utafikisha billion 47 kama mwenzio yule. Ushaanza kupunguza deni lakini?
 
Hahahahah we utafikisha billion 47 kama mwenzio yule. Ushaanza kupunguza deni lakini?
Sijaanza kwa hii Sheria za kiuonevu watajiju wenyewe ningetaka ningeanza kulipa Ila kwa utaratibu wa kulipa Deni na kutokupungua sijihangaishi
 
Retention fee ni pale serikali inapodai ila serikali inapodaiwa Kama malimbikizo ya haya maalimu areas hakuna retention fee.

MIALIMU bana.
Unapoint nzuri sana. Serekali inajali thaman ya pesa yao lakini wapo watu wanaidai serekali miaka na miaka lakini wakijalipa wanalipa kiasi kile kile pasipo kujali thaman ya pesa ilishashuka.
 
Silipi labda wanipe ajira bila hivyo silipi. Kama kulipa tuanzie mwaka 60mababu zetu walipo anza kusoma , je walilipa tuanzie hapo. Akina kikwete, lowasa, RIP S. Sita , Lipumba na wengineo . Kama hawakulipa sasa mm nitalipaje Sasa. Acheni uonevu nimekula hela zangu.
 
Jina nililokuwa natumia chuo sio hili nalotumia sasa, yaani yote yamebadilika..pia sipo kwenye ajira rasmi.
Halafu cha kushangaza nilishawahi kuangalia kama jina langu lipo kwenye list ya wadaiwa sikuliona, sisi tulikuwa wa mwanzo kupata mkopo enzi hizo 2004..ilikuwa simple sikumbuki kama nilijaza form..tuliandika majina, course unayosoma na account namba..baada ya wiki mbili mkopo ukaingia..

Hadi namaliza sikumbuki kujaza form yoyote. Nimehisi labda hawakuweka details vzr kwenye system. Sijawahi wauliza wenzangu kama wao wanadaiwa au la...
Jipe moyo kuna watu wa 2003 wanakatwa
 
Mwaka 2013 nilipoenda kuangalia deni langu bodi lilikuwa Tsh 12,908,741 (hii inajumuisha hela halali niliyotumia mwenyewe pamoja na ada ilikuwa Tsh 11,394,700, Administration fee Tsh 113,947, retention fee Tsh 1,192,422).

Baada ya miaka 6 kupita huku nikiendelea kulipa deni lilifikia Tsh 14,101,163.82 hii inaonesha kulikuwa na ongezeko la Tsh 1,192,422.82 ambayo kwao walisema ni retention fee.

Mwajiri alipeleka deni la awali la Tsh 12,908,741 na hii ndio walikuwa wanapunguza huko kila nikilipwa salary na naishukuru serikali ilipoongeza 15% ilinisaidia kuwahi kumaliza kulipa deni hili la awali maana nilitakiwa kumaliza 2024 au 2025 kama wangeendelea kukata 8% lakini kwa maamuzi magumu ya serikali ikanifanya nimalize deni hilo 2019.

Hii Tsh 1,192,422.82 ambayo iliongezeka na haikuwekwa kwenye deni la awali bado natafakari namna ya kuilipa maana sijaridhika na hili ongezeko la retention fee kipindi nilichokuwa nalipa.

Na kama ni halali mbona serikali huwa tunaidai hela kwa mda mrefu hata zaidi ya miaka hiyo 6 lakini wao wakija kutulipa hawatulipi na retention fee?

Nawaza nilipe hili deni lililobaki au nisubiri hadi serikali itakaponilipa hela ninayoidai kwanza ndio nimalizie kuwalipa bodi ya mikopo.
Ni mwaka na sehemu umepita bado sijapata jibu kama niwalipe au nisubiri AREAS kwanza.

Note:
Niliwauliza watu wa bodi ya mikopo kama hii retention fee nisipolipa nayo ina retention fee?
Walisema kama ukimaliza kulipa principal loan basi retention fee huwa haiongezeki tena, inabaki hiyo hiyo hata ukidelay kulipa.
Sasa kwa majibu hayo waliyonipa yalinipa kiburi cha kusubiri serikali inilipe kwanza AREAS za kuanzia 2019 ndipo nimalizie kuwalipa. Hadi wa leo sijarudi kuangalia kama retention bado iko hiyo hiyo au nayo wameifanyia retention.

Ila niwatie moyo tu kuwa deni la bodi linalipika na linaisha as long as unalipa hata kama ni kidogo kidogo.
HABA NA HABA HUJAZA KIBABA
6% ya retention fee kila mwaka huwa ni ya deni la awali au deni linalobaki?
 
Back
Top Bottom