goodhearted
JF-Expert Member
- Feb 15, 2015
- 978
- 1,237
Jamaa amezinguana na mkewe.
Mkewe kakimbilia kufungasha mizigo na vyombo vya ndani. Ameacha amefanya uharibifu kwa kuvunja simu ya msela kwa makusudi. Simu hiyo alinunuliwa na mme wake sasa wakati anaondoka mme alimtaka aiche (lengo mme akague kuona kama kuna ajenda iliyojificha yq yeye kuondoka)
Sasa mke kakimbilia ustawi wa jamii anataka matunzo ya mtoto. Mtoto ana miaka miwili.
Hii imekaaje, jamaa adai mwanae akae nae(uwezo wa kumlea anao) au ni lazima tu apeleke matuzo getoni
kwa mama wa mtoto alieamua kuondoka mwenyewe bila kufukuzwa wala kupigwa?
=======
Baada ya ndoa au mahusiano yaliyokuwa yamepata mtoto kuvunjika, imezoeleka mtoto au watoto mara nyingi walio chini ya miaka 7 hubaki au kuondoka na Mamama yao na kuanza maisha mapya. Kwa ndoa zinazovunjwa mahakamani hutolewa amri ya mahakama kuhusu uangalizi na matunzo ya watoto.
Haki ya kuishi na watoto hutegemea umri wa mtoto au watoto, uwezo wa kifedha wa kuwatunza na ustawi wa mtoto mwenyewe.
Mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 7 hupaswa kuishi na mama kwaajili ya ustawi wake kama mtoto, lakini ni lazima ionekane wazi kuwa mama ana tabia njema na ustawi wa mtoto hautaathiriwa.
Mtoto mwenye miaka zaidi ya saba anaruhusiwa kuchagua kuishi na baba au mama. Baba atawajibika kutoa matunzo ya kifedha kadri ya uwezo/kipato chake kama mahakama itakavyoona inafaa.
Endapo mama ana tabia za ulevi uliopindukia, uchangudoa n.k mtoto au watoto wataishi kwa baba kwaajili ya ustawi bora wa watoto.
Hata hivyo, kwa mujibu wa RITA hali ya mtoto wa umri wa miaka 7 kuishi na mama inaweza kuwa tofauti kwa mujibu wa mabadiliko ya sheria ya mtoto ya mwaka 2009 kwa kipengele kichachosema "Best Interest of the Child" yaani maslahi Makuu au Muhimu ya mtoto ambapo best intrest ya mtoto inaweza kuwa tofauti na mama husika na hivyo kulelewa na mtu tofauti au mtu kutoka upande wa baba.
Pia soma:
Mkewe kakimbilia kufungasha mizigo na vyombo vya ndani. Ameacha amefanya uharibifu kwa kuvunja simu ya msela kwa makusudi. Simu hiyo alinunuliwa na mme wake sasa wakati anaondoka mme alimtaka aiche (lengo mme akague kuona kama kuna ajenda iliyojificha yq yeye kuondoka)
Sasa mke kakimbilia ustawi wa jamii anataka matunzo ya mtoto. Mtoto ana miaka miwili.
Hii imekaaje, jamaa adai mwanae akae nae(uwezo wa kumlea anao) au ni lazima tu apeleke matuzo getoni
kwa mama wa mtoto alieamua kuondoka mwenyewe bila kufukuzwa wala kupigwa?
=======
Haki ya kuishi na watoto hutegemea umri wa mtoto au watoto, uwezo wa kifedha wa kuwatunza na ustawi wa mtoto mwenyewe.
Mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 7 hupaswa kuishi na mama kwaajili ya ustawi wake kama mtoto, lakini ni lazima ionekane wazi kuwa mama ana tabia njema na ustawi wa mtoto hautaathiriwa.
Mtoto mwenye miaka zaidi ya saba anaruhusiwa kuchagua kuishi na baba au mama. Baba atawajibika kutoa matunzo ya kifedha kadri ya uwezo/kipato chake kama mahakama itakavyoona inafaa.
Endapo mama ana tabia za ulevi uliopindukia, uchangudoa n.k mtoto au watoto wataishi kwa baba kwaajili ya ustawi bora wa watoto.
Hata hivyo, kwa mujibu wa RITA hali ya mtoto wa umri wa miaka 7 kuishi na mama inaweza kuwa tofauti kwa mujibu wa mabadiliko ya sheria ya mtoto ya mwaka 2009 kwa kipengele kichachosema "Best Interest of the Child" yaani maslahi Makuu au Muhimu ya mtoto ambapo best intrest ya mtoto inaweza kuwa tofauti na mama husika na hivyo kulelewa na mtu tofauti au mtu kutoka upande wa baba.