Baada ya Ndoa kuvunjika, sheria inasemaje kuhusu matunzo ya mtoto? Ni hiari au ni lazima Wazazi kutunza watoto?

Mkuu good,

Pole sana kwa jamaa.kama mwanamke hataki kuendelea asimlazimishe huenda mwanamke amechoka vitu anavyopitia katika ndoa hiyo, sababu mpaka kuvunja simu kuna jambo linaendelea.

suala zima mwanamke kasema anataka kwenda kukaa mwenyewe, na kiasi cha pesa kama matumizi ya mtoto.
Nafikiri ustawi wanaangalia na hali ya mwanaume na si mwnamke anasema nini. Wapo wanaume wanafanya kazi gereji na wanatunza kuendana na uwezo wao si standard anayosema mwanamke.

suala la mwanamke kuishi kivyake ni sawa tu ila yeye ahudumie mtoto wake kwa kiwango cha uwezo wake hilo ndio la muhimu.
 
steveachi njoo ujifunze waungwana wanavyojibu maswali.
Hakuna kumchekea nyani bloangu,si umemsikia kanijibu kuwa hapati hata mia.

Sasa mtu kama huyo pamoja na ushauri huo ulioniletea wa kiungwana anatakiwa kujibiwaje manake inaonekana kaupuuza kwani ni wazi inanyesha tayari alishakuwa na maamuzi yake kichwani hapa alikuja kutuchora tu.

Ndio maana watu wa dizaini hii hakuna kumung'unya maneno,ni kuwachana ukweli tu ili baadae asije sema hakuambiwa
 
So unamshauri nini kulingana na swali lake au mke hajaenda ustawi kuvunja ndoa ila anadai matunzo ya kijana wao?.
 
Haya bhana, ila unapomchana ukweli matusi unaweza ukayaacha tu, ukatumia lugha za kiungwana.
 
Jiwahi ustawi wa jamii usije filisiwa na mtalaka wako ukaja kumchukia mtoto
 
Ni haki kutoa matunzo ya mtoto kwa kiasi akitakacho mwanamke alieamua kuvunja ndoa na kuondoka na mtoto?
Tukiachana na mambo ya haki. Je we unaona ni sawa Mtoto wako ashinde njaa usimhudumie chochote kile kisa tu Mama yake ndio aliamua muachane??

Wewe moyoni haikuumi hata? Haujihisi guilty kwa hilo? Mtoto huyo anahusika katika maugomvi yenu yaliyowaachanisha? Au kuja kwake duniani kulitegemea ridhaa yake? Au ni starehe zenu tu siku hiyo ukamwaga ndani??

Sasa why umtese Kwa njaa na mahitaji mengine kisa tu maamuzi ya mama yake?

Ushauri wangu iwe ni haki au Sheria au isiwe hivyo we hudumia tu huyo mtoto. Maamuzi ya mama yake mtawajibishana na kiadhibiana kivingine kwenye mambo mengine.
 
We mpumbavu nini,mtoto anahusikaje na ugomvi wenu?

Timiza wajibu wako acha kutaka kukwepa jukumu lako la kumlea uliyemleta duniani.

Ningekuwa karibu na wewe ningekulamba bonge la klebu,kmmq

Una bahati sana
Kwa hiyo na wwe ukiamrishwa na Mkeo kiasi cha matunzo hata kama hukubaliani nacho utatoa kisa ana mtoto wako!? Utakuja shangazwa mtoto si wako siku moja! Hoja ya mtoa maada kwa nini Mwanamke ndiyo apange kiwango badala ya Mamlaka husika!??
 
Jamaa yako fala sana,anampisha Mwanaume mwenzie ndanii ya nyumba yake,alafu yeye anaenda kupanga!! Hahaaaa!!!
Kuna wakati maisha yanakuta uwe fala ili uishi kwa amani ya nafsi. Vinginevyo ndio ile ya kugawana majengo ya serikali
 
Salaam,

Nianze kwa kutoa background fupi kati ya mimi na mzazi mwenzangu.

Ni mwanamke ambaye nimezaa nae mtoto mmoja, kipindi amejifungua alikuwa akiishi kwa wazazi wangu mkoa tofauti na ninaoshi (nilifanya hivyo kuwa kuwa nilikuwa kwenye utafutaji, hivyo sikuwa mtu wa kutulia).

Baada ya muda aliamua kuondoka na kwenda kwa wazazi wake, sikuwa na shida na hilo kwa kuwa nilitaka akae mahali anapoona ana uhuru, niliendelea na bado naendelea kutoa fedha ya matumizi kwa mtoto. (yeye anajishughulisha kupata chochote kwa matumizi yake binafsi)

Ila sasa imefika hatua ambapo naona ananifanya mgodi wa fedha kwa kuongeza gharama ya vitu visivyo vya lazima kwa mtoto jambo ambalo lipo nje ya uwezo wangu.

Lengo la uzi huu naomba kujua je, Nitakuwa sawa kisheria kusitisha kumpa fedha ya matumizi, badala yake anitajie mahitaji ya mtoto kwa mwezi ninunue hivyo vitu mwenyewe na kumpatia?
 
suluhu muoe
 
Wewe na yeye bado mna uhusiano wa kimapenzi? Ukiendaga kumuona mtoto 'unamchungulia' na mama yake?
 
Habari wakuu,
Swala la "single mothers" nadhani sio geni kulisikia maskioni mwetu, hapa nazungumzia mwanamke aliyezalishwa na kuterekezwa na mwanaume wake. Hali inayompelekea kulea mtoto peke yake bila mchango wa mwanaume aliyemzalisha.

Hoja yangu inakuja kwenye huyo mtoto aliyezaliwa haki zake kwa baba yake hapo imekaaje?

1. Je ikatokea huyo mwanaume akafunga ndoa na mwanamke mwingine. Sheria inamlinda vipi huyu mtoto?

2. Je kama ikitokea swala la kifo kwa baba sheria itamtambua huyu mtoto kweli? Au ndio imekukla kwake.

Maana naona kama wimbi la hawa watoto linaongezeka kwa kasi. Ebu wajuzi wa sheria mtusaidie kwa ufafanuzi kidogo ili kuwaokoa hawa watoto ili hawa single mothers wapate hints.

Kulea mtoto mzazi mmoja bila usaidizi wa upande wa pili ni changamoto mno, hakika tuwape maua yao.

Nawasilisha kwenu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…