Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Oky Inaendelea...........


Basi siku yenyewe ilivyofika jamaaa alinishitua kutoka usingizini akaniambia bro ndio siku yenyewe ya maziwa na asali lakini kucheki kwa njee ilikuwa ni kama asubuhi tayari imeshafika nikabaki kujiuliza hivi mganga alituambia twende usiku saa 7 au asubuhi

Ilibidi niamke nianze kujiandaa kila mmoja alikuwa amejipanga jinsi anavyoweza kwa sekeseke nilikuwa nimekutana nalo ilibidi nivae viatu vya michezo wengine wanaita six ,halafu kamba nimezifungia miguuni nimeuganisha na suruali ili tatizo lolote likitokea nikianza kutimua mbio nisipate majeraha au kiatu kisitoke.

Ukiangalia sura zetu sio ma handsome tulikuwa tumetengeneza sura chafu za kukabiliana na kitu chochote mradi tutimize lengo la kupata pesa basi baada ya hapo tukatoka njee lakini siku hiyo upepo ulikuwa unapuliza sana utadhani kuna bahari maeneo ya hapo

Tukajisogeza hadi karibu na barabara halafu kila mmoja akachukua uelekeo wake basi mimi nikaanza kutembea lakini cha ajabu sikukutana na mtu yoyote hata pale tulipokuwa tunakaaa hatukuona mtu yoyote nilimaliza barabara nzima hadi nikamezwa na kichaka sikukutana na mtu wala boda

Nikawa najiuliza mbona leo watu hawaamki basi mimi sikujali nikaendelea kupiga tambo kwenye yale matuta ya majani nikielekea upande wa mwembe ulipo moyoni nilikuwa sina hofu sana nilikuwa najua lazima nitakuta mbegu zimeote yaani nilikuwa na asilimia mia.

Lile eneo ambalo ule muembe ulikuwepo haikuwa mbali sana ila nilijikuta nitembea sana bila kufika hadi nikaanza kuchoka kwa mbali nikaanza kuuona na ukumbuke hapo bado nilikuwa sijakutana hata na kifaranga cha kuku basi nikaongeza mwendo nikazidi kuukaribia ule muombe asee ile na ukaribia vizuri nilisikia kitu kama radi inapiga kwa nguvu halafu likatokea giza totoro hapo sikuwa nimebeba hata tochi

Nikasema sirudi nyuma lolote litakalo nitokea lazima niendee tu nikashuhudie siwezi poteza muda kiasi hiki alafu niishie kurudi tena nyuma basi nikazidi kuusogelea ule muembe kwa haraka zaidi huku nikiwa nimepanic kichwani kama dakika kadhaa nikawa nimefika chini ya ule muembe tatizo nilikuwa sijabeba tochi ikabidi nianze kutafuta lile jiwe nililokuwa nimeegesha maana pembeni yake ndio nilikuwa nimepnda zile mbegu

Basi nikaanza kulitafuta bila mafanikio tafutata sana silioni papasa sana majani yaliyokuwa pale chini hadi nikachoka ikabidi nikae nikaanza kujiuliza au mganga atakuwa amatuchezea changa la macho basi wakati naendelea kujiuliza nikahisi kama kunakitu kimenigusa bega niligeuka fasta kwa spidi ya 5G lakini sikuona mtu yoyote kwanyuma kabisa nikaliona lile jiwe kwa mbali kidogo

Ikabidi niliiendee fasta maana mimi nilikuwa upande mwingine wakati nimelizungukia ghafla tena naona liko upande mwingine basi nikasema wee jamaa usinitanie nalala na wewe mbele hivyo hivyo nikaanza kulizungukia kwa kasi bila mafaniko nilijikuta nimezunguka hadi nimechoka ikabidi nikae chini naishia kulitazama tu.

Akili ya haraka haraka akanijia nikasema hapa nikimbie hadi kule getto nichukuwe zile dawa za mganga ninywe, nioge halafu nichukue stiki ya bangi nivute pamoja na tochi labda inaweza nisaidia halafu nirudi tena kuhakikisha kama nachokiona ni kweli.

Basi nikatesti mara ya mwisho kwanza kulifikia kabla sijaondoka lakini hali ikawa bado iko vilevile, nasema ukweli toka moyoni kama sikuile siku changanyikiwa sewezi tena kuugua ukichaa maishani mwangu maana nilipanic kweli kweli .Kunajamaa hapo juu alicomment eti naeleza haya yote itakiwa bado na moshi wa bangi unanisumbua kichwani niseme tu leo hata mungu akaondoa vilevi vyote kuanzia cocaine hadi pombe za kienyeji bado tu watu waliochanganyikiwa wataendelea kuwepo

Oky tuendelee nilitoka pale nikiwa na nguvu za kutosha na kuanza mchaka mchaka hadi nikatika getto lakini kabla sijaingia nikamkuta yule mama mwenye nyumba amesimama mlangoni ameshikilia na mkono mmoja kwa jinsi nilivyokuwa nimechanganywa kichwani nikamsalimia nikaingia ndani ile nafungua mlango nikakimbia moja kwa moja kuwasha sola tulikuwa tunatumia zile zenye kichuma flani hivi zakuanika kwa njee wale wa vijijini watakuwa wanazifaamu vizuri.

Nikawasha ili nichukue zile dawa nikaoge nyingine ninywe basi ile nimewasha tu nikaona damu zimejaa chini ya sakafu wala sikujali nikachukua maji kwenye dumu la njano nikaweka kwenye kindoo changanya dawa fasta nikaenda kuoga kurudi nikaanza kuvaa nyingene dawa nikanywa halafu nikachukua bangi nikaanza kuvuta mule mule getto

Wakati naendelea kuvuta tena nikipiga pagu haraka haraka nikachukua kisimu changu tecno jeneza nikaangalai wakati nikakuta ni saa 9 usiku kama na madakika nikazidi kuchanganyikiwa nikavaa viatu haraka haraka nikachukua ile tochi ya sola nikaondoka tena kurudi kwenye ule muembe

Sasa ile natoka tu kuanza safari nikakutana na agustino ananiuliza vipi unaenda wapi nikamwabia bado sijaona zile mbegu na rudi kwa mara nyingine nilikuwa nimesahau tochi ndio akaniambia ulisahauje usiku wote ule nikamwabia usiku gani na tulitoka asubuhi daaa aliangua kicheko cha kufa mtu nikamuuliza wewe umeona mbegu zako zimeota daa akaniambia ndio asee hapo ndio nilizidi kuchanganyikiwa nilitoka na spidi ya kimbuga kuelekea kwenye ule muembe huku nikisika sauti ya kicheko cha agustino ikitokeza nyuma yangu

Sio kwamba alikuwa ananicheka kwa nia mbaya laahasha kulingana na situation iliyokuwepo kwa kweli kama ingekuwa ni kwenye nyumba za watu wengine wadadisi tungekuwa tumeshatimuliwa pale kwa sababu ya ushirikina

Wakati natimua riadha kuelekea kwenye ule muembe kidogo nilikuwa natumaini kuwa namimi nitakuta zimechomoza kulingana na maneno ya agustino niliendelea kukimbia huku hofu ikiendelea kunijaa moyoni....



Sent using Jamii Forums mobile app
Endelea mkuu!!

ukitaka utume simulizi hata kama iwe ndefu kiaje, nenda kwenye whasapp, fungua group la muda mfupi unaweza mtu mmoja au wawili unaiandika huko yote ukimaliza unaikopi , then unaipaste hapa. very simple.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Oooky Inaendelea.............


Niliendelea kukimbia haraka haraka kuelekea ule muembe ulipokuwa baada ya muda kidogo nikaanza kuuona kwa mbali haikuchukua muda nikawa nimefika mahala pale chini ya ule muembe bangi nilizokuwa nimevuta na ule mchaka mchaka ilikuwa imeshapanda kichwani sikuwa na uoga wowote nikawasha ile taa ya sola ,mdogo mdogo nikaanza kusogelea kile kipande cha jiwe.

Nilisogea karibu hadi nikakifikia kisha nikakikanyaga kile kipande cha jiwe halafu nikaanza kumulika na tochi kutafuta kama zile mbegu zimechipua nilitafuta mulika pande zote pale chini sikuona kitu chochote tafuta sana fukua majani bila mafanikio piga tochi pande zote kuzunguka lile jiwe wapi hakuna kitu.

Wakati naendelea kutafuta kupiga tochi kwa mbele nikaona tena kipande kingine cha jiwe chini ya ule muembe kinafanana na kile kile nilicho kuwa nimekikanyaga ndipo nikarudi kuangalia vizuri kwenye mguu wangu nilipokuwa nimekanyaga asee alikurupuka bonge la paka akatimkia kwenye vichaka vilivyokuwa pande zile .

Kumbe muda wote nilidhani nimekanyaga jiwe kumbe ilikuwa ni paka ikabidi nisogee kwenye lile jiwe lingine nikawa naangalia kwa umakini kulizunguka kama mbegu zitakuwa zimeota maana ndio kitu pekee nilichokuwa nimeweka kama alama ya kumbu kumbu.

Baada ya kuangalia kwa umakini ndio nikabahatika kuona zile mbegu zimeota pembeni ya lile jiwe nikaona ndio ile sehemu niliokuwa nimechimba mchanga nakufukia asee kweli niliamini uchawi huendi kwa mentali baharia nimelamba Jokel ,kama ingekuwa kwa wale jamaa wa kubet wangesema nimeshinda jackpot.

Nikatoka pale kwa spidi ya 100km/h mpaka nikafika getto nikamkuta jamaa yangu agustino amepiga usingizi kucheki pale chinj zile damu nilizokuwa nimeziacha hazipo nukamuamsha jamaa tukaanza kupiga story swali la kwanza aliloniuliza akanimbai umeona zimechomoza kwa tabasamu la bashasha nikamwabia ndio aseee akaanza kucheka nikamuuliza niliona humu getto kuna damu zimetapaka hapa chini zimeenda wapi akaniambia hajaziona sikutaka kuendelea kumuuliza ikabidi nivute shuka nijilaze

Wakati nimelala niliwaza pesa zikianza kuingia ninunue vitu vingi magari, nyumba, starehe, mademu ,nifanye anasa zote niliendelea kuwaza hadi usingizi ukanipitia nilikuja kuamka muda umekwenda sana tukaanza kuweka mipango tutatumiaje pesa ambazo tukaanza kuzipata pia ilikuwa imebaki kama wiki moja tu tufungue shule

Siku hiyo ilibidi agustino ampigie simu yule jamaa wa kule shinyanga akamwabia tumefanikisha wote maana mbegu zimetoa majani sasa tunasikilizia tuanze kuvuna tulichokipanda jamaa kwa haraka kabisa akasema tumpigie mganga tumwabie tumefanikisha lile jambo kwa ustadi wa kiwango cha lami.

Tulijaribu kumpigia mganga siku nzima simu inaita tu haipokelewi hadi jioni mida ya saa moja mgamga akampigia agustino basi waliongea mambo mengi kidogo ila mganga akasema yaani kama tumefanikisha kila kitu kimeenda sawa mizimu imesaidia sana kwani imetukubali lazima nayenyewe ipate zawadi kama shukurani ya kutupokea katika ulimwengu wa watu wenye fedha

Mganga akasema zawadi ya mizimu ni hayo mazao mliyoyasumbukia yeye malipo yake anataka fedha na mifugo tumpelekee maana kuanzia leo pesa zitaanza kuhangaika kututafuta tulipo mizimu imevunja nature ya ulimwengu kwamba pesa tutaitafuta kwa jasho badala yake sisi pesa ndio itatumia jasho kututafuta asee agustino alikuwa ameweka loud speaker nilikuwa nimetegesha sikio hakuna siku nimefurahi kama ile kusikia maneno yenyewe kutia moyo kama yale

Basi akaendelea kusema zawadi ya mizimu ni zile mbegu zilizochipua usiku wa saa saba twende tukazichume tukazitupe njia panda na hayo ndio yatakuwa malisho ya mizimu na jinsi watu watakavyokuwa wanaendelea kupita huku na huku kwenye ile njia mchana hadi usiku ndivyo pia pesa zitaendelea kutua kwenye mifuko yetu

Pia akatupa angalizo kuwa hayo ndio maneno ya mwisho kuongea nae kwenye simu kazi yake amesha maliza maelekezo yote ametupatia anachosubiria ni sisi atuone kule kwenye boma lake siku tunaenda kumpatia zawadi zake kama yule jamaa wa kule shinyanga alivyofanya baada ya hapo akakata simu.

Basi tukasema kazi iliyobaki ni ndogo sana kiukweli kutokana na kutembea usiku mara kwa mara nikawa nimesha zoea naona kitu cha kawaida siku hiyo agustino akaniambia twende kule kwa babu tulianza safari tukavuka kijimto tulivyofika hatukumkuta tukasema ngoja tuendelew kumsubiri ili akifika atupatie zile stiki za bangi alizokuwa tayari amezitengeneza sasa baada ya kukaa kwa madakika tukamuona kwa mbali anatokea shambani kumwagilia matikiti alivyofika tukamueleza shida ikabidi atupatie mabaki akamwabia agustino inabidi mzigo mwingine uletwe maana stock yote amemaliza

Tukapiga kweli ganja za maana kujiweka sawa kwenda kumaliza mchezo, ule usiku tulipita mahali tikapiga msosi tukaelekea hadi getto tukanywa zile dawa, nyingine tukaogea tena wakati tunataka kuondoka tukapiga tena bangi kisha kila mmoja akashika njia yake.

Mimi nikaanza kutembea mpaka nikaacha barabara kuu nikaanza kuingia vichakani basi nikaendela kuongeza mwendo huku nimeshikilia tochi yangu lakini sikuwa nimeiwasha basi sijui nini kiliniambia geuka nyuma kwa mbali nikaona mwanamke kama mama mwenye nyumba amesimama ananitazama nikaendelea kutembea kugeuka sikuona kitu chochote tena.

Basi nikaanza kutembea mpaka nikakaribia ule muembe kufika pale chini nikawasha tochi bahati mbaya kutafuta sikuona kitu chochote tafuta sana guys asikwambie mtu pesa ya shetani ni mgumi balaa nilitafuta hadi nikasanda ikabidi niondoke wakati nageuka nyuma naangalia pale niliona jopo la watu wengi wakiwa wamewasha moto mkubwa unaunguza hadi matawi ya ule muembe ikabidi nianze mbio nimekimbia sana kufika getto namkuta agustino amelala pembeni ya kitanda kuna damu kibao halafu nikaanza kumshitua.

Wakati nimemkuta amelala nikajua jamaa atakuwa amesha kamilisha mpango nilijuta kwanini nilichagua kupanda mbegu chini ya ule muembe nilihisi na mkosi nilio usababisha mimi mwenyewe nikaanza kumuita agustino kwa nguvu jamaa bado ameuchapa ikabidi nianze kumvuta anipe habari mambo yake yaliendaje vipi

Nikamtikisa sana wala jamaa anisemeshi wala haongei ndio nikazidi kuchanganyikiwa kuangalia uvunguni nakuta matone ya damu tena freshi nikabaki kujiuliza huyu agustino nini kitakuwa kimempata au niite mama mwenye nyumba aje anisaidie lakini roho inakataa ikabidi nitoke njee nichote maji nideki zile damu na nitoe ile shuka halafu nione kama nitaweza pata msaada kwa watu

Basi baada ya hapo nikachukua kindoo nikatoka njee nikafungua kisima kilikuwa kimezibwa na bati kwa juu nikachota maji wazo la kwanza nikasema ngoja nimwagie labda atazinduka nikachota kikomba kizima kikamwagia wapi daa nikaona hii ishu ninaelekea babaya nikachukua simu nikampigia yule jamaa wa shinyanga simu haipatikani nikasema jamani mimi nitafanya nini nitakimbila wapi...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Endelea mkuu!!

ukitaka utume simulizi hata kama iwe ndefu kiaje, nenda kwenye whasapp, fungua group la muda mfupi unaweza mtu mmoja au wawili unaiandika huko yote ukimaliza unaikopi , then unaipaste hapa. very simple.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo naona kazi mzigo wote uko kichwani mimi naangalia post ya mwisho imefikia wapi naanza kutiririka tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Oooky Inaendelea.............


Niliendelea kukimbia haraka haraka kuelekea ule muembe ulipokuwa baada ya muda kidogo nikaanza kuuona kwa mbali haikuchukua muda nikawa nimefika mahala pale chini ya ule muembe bangi nilizokuwa nimevuta na ule mchaka mchaka ilikuwa imeshapanda kichwani sikuwa na uoga wowote nikawasha ile taa ya sola ,mdogo mdogo nikaanza kusogelea kile kipande cha jiwe.

Nilisogea karibu hadi nikakifikia kisha nikakikanyaga kile kipande cha jiwe halafu nikaanza kumulika na tochi kutafuta kama zile mbegu zimechipua nilitafuta mulika pande zote pale chini sikuona kitu chochote tafuta sana fukua majani bila mafanikio piga tochi pande zote kuzunguka lile jiwe wapi hakuna kitu.

Wakati naendelea kutafuta kupiga tochi kwa mbele nikaona tena kipande kingine cha jiwe chini ya ule muembe kinafanana na kile kile nilicho kuwa nimekikanyaga ndipo nikarudi kuangalia vizuri kwenye mguu wangu nilipokuwa nimekanyaga asee alikurupuka bonge la paka akatimkia kwenye vichaka vilivyokuwa pande zile .

Kumbe muda wote nilidhani nimekanyaga jiwe kumbe ilikuwa ni paka ikabidi nisogee kwenye lile jiwe lingine nikawa naangalia kwa umakini kulizunguka kama mbegu zitakuwa zimeota maana ndio kitu pekee nilichokuwa nimeweka kama alama ya kumbu kumbu.

Baada ya kuangalia kwa umakini ndio nikabahatika kuona zile mbegu zimeota pembeni ya lile jiwe nikaona ndio ile sehemu niliokuwa nimechimba mchanga nakufukia asee kweli niliamini uchawi huendi kwa mentali baharia nimelamba Jokel ,kama ingekuwa kwa wale jamaa wa kubet wangesema nimeshinda jackpot.

Nikatoka pale kwa spidi ya 100km/h mpaka nikafika getto nikamkuta jamaa yangu agustino amepiga usingizi kucheki pale chinj zile damu nilizokuwa nimeziacha hazipo nukamuamsha jamaa tukaanza kupiga story swali la kwanza aliloniuliza akanimbai umeona zimechomoza kwa tabasamu la bashasha nikamwabia ndio aseee akaanza kucheka nikamuuliza niliona humu getto kuna damu zimetapaka hapa chini zimeenda wapi akaniambia hajaziona sikutaka kuendelea kumuuliza ikabidi nivute shuka nijilaze

Wakati nimelala niliwaza pesa zikianza kuingia ninunue vitu vingi magari, nyumba, starehe, mademu ,nifanye anasa zote niliendelea kuwaza hadi usingizi ukanipitia nilikuja kuamka muda umekwenda sana tukaanza kuweka mipango tutatumiaje pesa ambazo tukaanza kuzipata pia ilikuwa imebaki kama wiki moja tu tufungue shule

Siku hiyo ilibidi agustino ampigie simu yule jamaa wa kule shinyanga akamwabia tumefanikisha wote maana mbegu zimetoa majani sasa tunasikilizia tuanze kuvuna tulichokipanda jamaa kwa haraka kabisa akasema tumpigie mganga tumwabie tumefanikisha lile jambo kwa ustadi wa kiwango cha lami.

Tulijaribu kumpigia mganga siku nzima simu inaita tu haipokelewi hadi jioni mida ya saa moja mgamga akampigia agustino basi waliongea mambo mengi kidogo ila mganga akasema yaani kama tumefanikisha kila kitu kimeenda sawa mizimu imesaidia sana kwani imetukubali lazima nayenyewe ipate zawadi kama shukurani ya kutupokea katika ulimwengu wa watu wenye fedha

Mganga akasema zawadi ya mizimu ni hayo mazao mliyoyasumbukia yeye malipo yake anataka fedha na mifugo tumpelekee maana kuanzia leo pesa zitaanza kuhangaika kututafuta tulipo mizimu imevunja nature ya ulimwengu kwamba pesa tutaitafuta kwa jasho badala yake sisi pesa ndio itatumia jasho kututafuta asee agustino alikuwa ameweka loud speaker nilikuwa nimetegesha sikio hakuna siku nimefurahi kama ile kusikia maneno yenyewe kutia moyo kama yale

Basi akaendelea kusema zawadi ya mizimu ni zile mbegu zilizochipua usiku wa saa saba twende tukazichume tukazitupe njia panda na hayo ndio yatakuwa malisho ya mizimu na jinsi watu watakavyokuwa wanaendelea kupita huku na huku kwenye ile njia mchana hadi usiku ndivyo pia pesa zitaendelea kutua kwenye mifuko yetu

Pia akatupa angalizo kuwa hayo ndio maneno ya mwisho kuongea nae kwenye simu kazi yake amesha maliza maelekezo yote ametupatia anachosubiria ni sisi atuone kule kwenye boma lake siku tunaenda kumpatia zawadi zake kama yule jamaa wa kule shinyanga alivyofanya baada ya hapo akakata simu.

Basi tukasema kazi iliyobaki ni ndogo sana kiukweli kutokana na kutembea usiku mara kwa mara nikawa nimesha zoea naona kitu cha kawaida siku hiyo agustino akaniambia twende kule kwa babu tulianza safari tukavuka kijimto tulivyofika hatukumkuta tukasema ngoja tuendelew kumsubiri ili akifika atupatie zile stiki za bangi alizokuwa tayari amezitengeneza sasa baada ya kukaa kwa madakika tukamuona kwa mbali anatokea shambani kumwagilia matikiti alivyofika tukamueleza shida ikabidi atupatie mabaki akamwabia agustino inabidi mzigo mwingine uletwe maana stock yote amemaliza

Tukapiga kweli ganja za maana kujiweka sawa kwenda kumaliza mchezo, ule usiku tulipita mahali tikapiga msosi tukaelekea hadi getto tukanywa zile dawa, nyingine tukaogea tena wakati tunataka kuondoka tukapiga tena bangi kisha kila mmoja akashika njia yake.

Mimi nikaanza kutembea mpaka nikaacha barabara kuu nikaanza kuingia vichakani basi nikaendela kuongeza mwendo huku nimeshikilia tochi yangu lakini sikuwa nimeiwasha basi sijui nini kiliniambia geuka nyuma kwa mbali nikaona mwanamke kama mama mwenye nyumba amesimama ananitazama nikaendelea kutembea kugeuka sikuona kitu chochote tena.

Basi nikaanza kutembea mpaka nikakaribia ule muembe kufika pale chini nikawasha tochi bahati mbaya kutafuta sikuona kitu chochote tafuta sana guys asikwambie mtu pesa ya shetani ni mgumi balaa nilitafuta hadi nikasanda ikabidi niondoke wakati nageuka nyuma naangalia pale niliona jopo la watu wengi wakiwa wamewasha moto mkubwa unaunguza hadi matawi ya ule muembe ikabidi nianze mbio nimekimbia sana kufika getto namkuta agustino amelala pembeni ya kitanda kuna damu kibao halafu nikaanza kumshitua.

Wakati nimemkuta amelala nikajua jamaa atakuwa amesha kamilisha mpango nilijuta kwanini nilichagua kupanda mbegu chini ya ule muembe nilihisi na mkosi nilio usababisha mimi mwenyewe nikaanza kumuita agustino kwa nguvu jamaa bado ameuchapa ikabidi nianze kumvuta anipe habari mambo yake yaliendaje vipi

Nikamtikisa sana wala jamaa anisemeshi wala haongei ndio nikazidi kuchanganyikiwa kuangalia uvunguni nakuta matone ya damu tena freshi nikabaki kujiuliza huyu agustino nini kitakuwa kimempata au niite mama mwenye nyumba aje anisaidie lakini roho inakataa ikabidi nitoke njee nichote maji nideki zile damu na nitoe ile shuka halafu nione kama nitaweza pata msaada kwa watu

Basi baada ya hapo nikachukua kindoo nikatoka njee nikafungua kisima kilikuwa kimezibwa na bati kwa juu nikachota maji wazo la kwanza nikasema ngoja nimwagie labda atazinduka nikachota kikomba kizima kikamwagia wapi daa nikaona hii ishu ninaelekea babaya nikachukua simu nikampigia yule jamaa wa shinyanga simu haipatikani nikasema jamani mimi nitafanya nini nitakimbila wapi...

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji16][emoji16][emoji16] huu mkeka unaenda kuchanika, siti ya mbele kama kawaida hapa naisubiri kwa hamu mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom