Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 63,730
- 111,542
With all due respect, mkuu nikuulize ikitokea Lisu apate vikwazo vya kugombea then chadema ndio basi tena? Kingine nini maana ya demokrasia? Huwezi kulazimisha kitu hiyo sio demokrasia. Kingine Nyalandu deserves respect. Huyu alijivua ubunge na kuja chadema pasipo ku demand chochote. Very unfair ukimwita mwa ccm na uki doubt uaminifu wake.
90% ya waliorudi ccm ni wale waliotoka ccm. Sio kwamba walifukuzwa, bali walikosa nafasi huko ccm, wakaona wajitoe kuja cdm. Nyalandu hana record nzuri ya utendaji toka ccm, hivyo akiwa mgombea wa Cdm huku dola ikijua madhambi yake, ni rahisi kumbana mpaka asalimu amri kama Lowassa na Sumaye. Narudia tena, ni nadra sana mwanaccm yoyote, tena aliye na record yenye makandokando kuacha uanaccm wake, ccm ikiwa madarakani, regardless kaondokaje ccm.
Hilo la Lissu kuwekewa vikwazo kutokana na kesi za kubambikiwa tunalifahamu vizuri sana. Lakini sio kigezo cha kuwa na mtu ambaye tuna mashaka naye ya dhahiri, na mifano ya watu wa ccm kama yeye ipo wazi. Hiyo demokrasia unayosema nataka kulazimisha, ndio demokrasia hiyo hiyo hutaki mimi niitumie kumkataa mtu. Sina popote nimewashikia watu bunduki wamkatae Nyalandu, bali nashawishi na sababu naziweka wazi.