Baada ya 'Royal Tour', Serikali sasa yaja na filamu nyingine iitwayo 'Amazing Tanzania'

Baada ya 'Royal Tour', Serikali sasa yaja na filamu nyingine iitwayo 'Amazing Tanzania'

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa Bungeni leo wakati akiwasilisha Hotuba ya kuhusu Makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi yake kwa mwaka 2024/25 amebainisha kuwa Serikali kutokana na mafanikio ya programu ya The Royal Tour, Serikali imetengeneza filamu nyingine yenye hadhi ya kimataifa ya kutanganza Utalii ijulikanayo kama 'Amazing Tanzania'.

Filamu hii kama ilivyokuwa kwa Roya Tour imerekodiwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar, Hussein Ali Mwinyi na mwigizaji nguli kutoka China aitwaye Jin Dong.

Filamu hii imeandaliwa kwa lengo la kuvutia watalii hususani soko la China na inatarajiwa kuzinduliwa Mei 2024.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Na Amiri Jeshi mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Dkt Mama Samia Suluhu Hasssan jasiri muongoza na shujaa wa Afrika, kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt Husseni Mwinyi wamerekodi kwa pamoja Filamu ya kipekee kabisa kuwahi kutokea katika ardhi ya Tanzania na nje ya mipaka, filamu inayoelezea na kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana hapa Nchini, ambavyo huwezi kuvipata mahala pengine popote pale Duniani.

Katika filamu hiyo imemshirikisha pia muigizaji Nguli na wa kimataifa kutoka nchini china Jin Dong. Hii Maana yake nini ndugu zanguni?

Hii maana yake filamu hii ambayo imekuwa gumzo ulimwengu kwote itatizamwa na Na watu wasio pungua Billion 2 siku tu itakapozinduliwa, kwa sababu China Pekee Ina watu zaidi ya Billion moja na million kadhaa yaani watu wengi zaidi ya idadi yote ya bara la Afrika lenye nchi takribani 55. Lakini pia filamu hii itavuka mipaka hadi nchi ya india ambayo nayo ina watu zaidi ya Billion moja.

Hapo bado sijaweka kwa nchi zingine ambazo nazo zitakuwa zikifuatilia kwa karibu uzinduzi huo ,ambao unakwenda kuweka rekodi ya kidunia pengine na kuingia katika vitabu vya Historia.

Kwa hakika Rais Samia ni kiongozi mbunifu, anafahamu nini anafanya na nini afanye kuteka macho na masikio ya Dunia,anafahamu namna ya kufanya shughuli na shughuli ikawa ni kama shughuli ya Dunia nzima utafikiri sherehe za uzinduzi wa kombe la DUNIA.

Maana yake anakwenda kuliteka soko la watalii kutoka Bara la Asia Ambalo ni bara lenye idadi kubwa ya watu hapa Duniani ukilinganisha na Bara lolote lile kati ya mabara yote saba yaliyopo hapa Duniani.

Maana yake watanzania tunakwenda kushuhudia mafuriko na kumiminika kwa Watalii kuja hapa Nchini utafikiri maji yatiririkayo kutoka katika bomba lililopasuka. Tanzania tunakwenda kuwa kitovu cha utalii na chaguo nambali moja la watalii hapa barani Afrika.

Rai yangu ni kwa Wafanyabiashara wa ndani kujiandaa na fursa hiyo inayoletwa na serikali ya Rais Samia, kwa kuhakikisha kuwa mnawekeza katika hoteli kubwa za kitalii zenye hazi ya kimataifa.

Makampuni ya watalii hapa nchini kujiandaa kuteka na kuchukua fursa za ujio wa watalii. Anzeni kujiandaa mapema maana kunakuja kutokea gharika la watalii watakaokuwa wanafurika na kumiminika kuja hapa Nchini.

IMG-20240315-WA0027.jpg
IMG-20240309-WA0011.jpg
 
Wameshindwa kutumia mbinu jinsi kukuza uchumi wamejikita bongo movie!
Huelewi kuwa filamu hiyo ina manufaa makubwa sana kiuchumi.kwasababu itavutia Watalii ambao watakuja na pesa za kigeni ambazo tunazitumia katika kuwekeza katika maeneo mengine .lakini pia pesa hizo za kigeni zitaisaidia kununua bidhaa nje ya nchi kama vile dawa za binadamu n.k.lakini pia itavutia wawekezaji mbalimbali
 
Hiyo filam ioneshe kuwa mwezi wa ramadhani Zanzibar watalii hawali Wala kunywa mchana hata kma wanaumwa
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Na Amiri Jeshi mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Dkt Mama Samia Suluhu Hasssan jasiri muongoza na shujaa wa Afrika ,kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt Husseni Mwinyi wamerekodi kwa pamoja Filamu ya kipekee kabisa kuwahi kutokea katika ardhi ya Tanzania na nje ya mipaka, filamu inayoelezea na kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana hapa Nchini ,ambavyo huwezi kuvipata mahala pengine popote pale Duniani.

Katika filamu hiyo imemshirikisha pia muigizaji Nguli na wa kimataifa kutoka nchini china Jin Dong . Hii Maana yake nini ndugu zanguni? Hii maana yake filamu hii ambayo imekuwa gumzo ulimwengu kwote itatizamwa na Na watu wasio pungua Billion 2 siku tu itakapozinduliwa.kwa sababu China Pekee Ina watu zaidi ya Billion moja na million kadhaa yaani watu wengi zaidi ya idadi yote ya bara la Afrika lenye nchi takribani 55. Lakini pia filamu hii itavuka mipaka hadi nchi ya india ambayo nayo ina watu zaidi ya Billion moja.

Hapo bado sijaweka kwa nchi zingine ambazo nazo zitakuwa zikifuatilia kwa karibu uzinduzi huo ,ambao unakwenda kuweka rekodi ya kidunia pengine na kuingia katika vitabu vya Historia. Kwa hakika Rais Samia ni kiongozi mbunifu, anafahamu nini anafanya na nini afanye kuteka macho na masikio ya Dunia,anafahamu namna ya kufanya shughuli na shughuli ikawa ni kama shughuli ya Dunia nzima utafikiri sherehe za uzinduzi wa kombe la DUNIA.

Maana yake anakwenda kuliteka soko la watalii kutoka Bara la Asia Ambalo ni bara lenye idadi kubwa ya watu hapa Duniani ukilinganisha na Bara lolote lile kati ya mabara yote saba yaliyopo hapa Duniani.maana yake watanzania tunakwenda kushuhudia mafuriko na kumiminika kwa Watalii kuja hapa Nchini utafikiri maji yatiririkayo kutoka katika bomba lililopasuka .Tanzania tunakwenda kuwa kitovu cha utalii na chaguo nambali moja la watalii hapa barani Afrika.

Rai yangu ni kwa Wafanyabiashara wa ndani kujiandaa na fursa hiyo inayoletwa na serikali ya Rais Samia ,kwa kuhakikisha kuwa mnawekeza katika hoteli kubwa za kitalii zenye hazi ya kimataifa. Makampuni ya watalii hapa nchini kujiandaa kuteka na kuchukua fursa za ujio wa watalii. Anzeni kujiandaa mapema maana kunakuja kutokea gharika la watalii watakaokuwa wanafurika na kumiminika kuja hapa Nchini.View attachment 2952819View attachment 2952820
Utahangaika sana lakini kamwe huwezi kuteuliwa kwa sababu huna akili
 
Huelewi kuwa filamu hiyo ina manufaa makubwa sana kiuchumi.kwasababu itavutia Watalii ambao watakuja na pesa za kigeni ambazo tunazitumia katika kuwekeza katika maeneo mengine .lakini pia pesa hizo za kigeni zitaisaidia kununua bidhaa nje ya nchi kama vile dawa za binadamu n.k.lakini pia itavutia wawekezaji mbalimbali
Well ni Jambo jema sana,
Ila mkuu,tubaki tegemea fedha za kigeni kutoka kwa watalii tu...
Why not kutanua wigo wa Kuuga Mazao ,huko arabuni.
Why not tusiwauzie matunda Ulaya
Why not kuuza mifugo nje
Why not tusidhibiti wizi na ulanguzi wa madini....


Hii watalii watalii, usijkuta wanakuja kutuangalaia sasa badala ya Mbuga..mans tuna vichekesho vingi...
Why not kuunda products za viwanda nje
Why not tusipunguze mikopo isiyo na ulazima
 
Kwa hakika Rais Samia ni kiongozi mbunifu, anafahamu nini anafanya na nini afanye kuteka macho na masikio ya Dunia,anafahamu namna ya kufanya shughuli na shughuli ikawa ni kama shughuli ya Dunia nzima utafikiri sherehe za uzinduzi wa kombe la DUNIA.
Kama hivyo ndivyo sawaaaa!!! Tatizo kapu lake la kujazia ndururu anaruhusu manyang'anyi yanajizoleatu. CAG amebainisha lakini mpaka sasa hakuna alietenguliwa
Asije na kigezo cha kusema eti kazi yake nikupeleka bungeni. Wale wakwake awaondoe kwenye nafasi.
Kwakufanya hivyo wananchi wataona umuhimu wa harakati zote hizo
 
Well ni Jambo jema sana,
Ila mkuu,tubaki tegemea fedha za kigeni kutoka kwa watalii tu...
Why not kutanua wigo wa Kuuga Mazao ,huko arabuni.
Why not tusiwauzie matunda Ulaya
Why not kuuza mifugo nje
Why not tusidhibiti wizi na ulanguzi wa madini....


Hii watalii watalii, usijkuta wanakuja kutuangalaia sasa badala ya Mbuga..mans tuna vichekesho vingi...
Why not kuunda products za viwanda nje
Why not tusipunguze mikopo isiyo na ulazima
Vyote vinafanyika na hakuna kinachobakia nyuma wala kutelekezwa.kikubwa kinachofanyika ni kukusanya sent kutoka vyanzo mbalimbali kuanzia kupitia utalii kilimo,biashara, uwekezaji n.k.
 
Back
Top Bottom