Baada ya Shinikizo la Kimataifa, Viongozi wa CHADEMA Waanza kuachiwa, Mbowe, Lissu na Lema Waachiwa

Mungu atuondolee na huyu wa sasa kama alivyofanya kwa yule mwingine.

Aliona nchi ni kama mali yake ila kaicha kama alivyoikuta.

Mungu fundi sana. Bado huyu nae kaota mapembe.
Lkn huyu hajafikia hata robo ya yule, yule alikuwa Beduwi.
 
Mtu ambaye hujaenda popote huwezi kuyajua haya, endelea kuvishwa fulana za ccm
 
Lazima kesho au kesho kutwa Tundu Lissu atakwea pipa kwenda Ubelgiji. Atarejea baada ya wiki 3 au 4 kuja kukinukisha tena. Ni mkurukutabu wa kuzaliwa aka original.
 
Nilijua tu, Samia anajitekenya na kucheka mwenyewe,acheze na wengine lakini sio Anko Sam(USA), ataumia, vibaya Sana, Anko Sam akiamua ku "destabilize" Samia ataiona hata kizmkaz pa moto,
 
Maskini Mnyika wa watu, kakimbia hadi kaingia kanisani na kachukua biblia anasali humo ndani kwenye altare, anaomba Mungu hiki kikombe kisimfike, mseminari wa watu analazimishwa tu kuandamana..!!
 
Mtu ambaye hujaenda popote huwezi kuyajua haya, endelea kuvishwa fulana za ccm
Kwenda popote maana yake nini? Fikra zako zinakuelekeza kuabudu wazungu.
Wazungu ni wezetu, tunaishi nao, tunafanya harakati za maisha nao, ofisi moja na wapo wajinga wengi kuliko hata wewe.
Jambo muhimu ni kujua ukweli wenye manufaa kwa taifa (weusi) bila kujali chama.
Hayo mawazo ya kizamani kuhusu kwenda nje ya nchi yalishapitwa na wakati, siyo hoja tena. Hata wajinga huenda popote duniani. Zama zimebadilika. Usiwe kijibwa (puppet).
Elewa kwamba, mtu mweye akili, anajadili hoja kwa weledi, kwa faida ya taifa kwanza, vyama na makundi yake baadaye.
Hata mataifa makubwa duniani yalianza hivyo.
 
Faida ya Taifa ni kumuua Mzee Ally Kibao?
 
Nilijua tu, Samia anajitekenya na kucheka mwenyewe,acheze na wengine lakini sio Anko Sam(USA), ataumia, vibaya Sana, Anko Sam akiamua ku "destabilize" Samia ataiona hata kizmkaz pa moto,
Una fikra za kitumwa,Samia ana Presidential powers kwa taarifa yako! Somo la Presidential power ni siku nyingine tena!!!
 
Maskini Mnyika wa watu, kakimbia hadi kaingia kanisani na kachukua biblia anasali humo ndani kwenye altare, anaomba Mungu hiki kikombe kisimfike, mseminari wa watu analazimishwa tu kuandamana..!!
Hivi hata huko kanisani Mnyika anasali huku anasema Samia must Gooooooooo!!!?? Au ana slogan mpya Mbowe must goooooo!!??
 
Hamna cha shinikizo la Kimataifa wala nini.

Kazi iliotakiwa kufanyika imeshafanyika. Waendelee kushikiliwa wa nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…