Baada ya Tito Magoti na mwenzake kutiwa hatiani ni dhahiri kuwa sio kila anayejinasibu mkosoaji wa Serikali anabambikiwa kesi ya Uhujumu Uchumi

Baada ya Tito Magoti na mwenzake kutiwa hatiani ni dhahiri kuwa sio kila anayejinasibu mkosoaji wa Serikali anabambikiwa kesi ya Uhujumu Uchumi

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Kabla ya kwenda moja kwa moja napenda kuweka wazi kuwa mimi ni mtu ambaye sipendi kuona watu wakionewa na hasa kunyimwa haki zao za msingi.

Kumekuwepo na dhana potofu hapa Tanzania kuwa kila mtu anayeikosoa Serikali ya sasa ya awamu ya tano lazima akutane na mkono wa chuma.Dhana ambayo imekuwa ikiwafanya watu wengi wadhanie kuwa kuna ubabe na uvunjifu wa haki za raia hapa BongoTz.

Na mbaya zaidi ni hii ya kuaminisha watu kuwa kila anayeikosoa serikali basi lazima abambikiwe kesi ya uhujumu uchumi ili baadae pesa zimtoke ili akomolewe.

Lakini hivi majuzi baada ya Tito Magoti na mwenzake kukiri kosa ukweli wa mambo umejulikana,na ni wazi kuwa sio wote wanabambikiwa kesi,maana hili la kubambikiana kesi nalo lina siri kubwa.

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi,Tito Magoti na mwenzake waliunda genge la uhalifu ili waweze kueneza proganda za uongo kuwa serikali ya Tanzania inagandamiza haki za binadamu. Na wamekiri kuwa kulikuwa na mtandao unaojiita Tanzania on Twitter ambao ndio uliratibu kuundwa kwa hili genge. Ni genge ambalo linaonekana kujidhatiti ili kuchafua sifa ya nchi yetu.

Tito na mwenzake walipewa namba za simu zilizosajiliwa Holland na walishirikiana na watanzania wanaoishi nje kufanya uhalifu huo,huku wakiahidiwa kujipatia kipato kikubwa tu. Hii ilikuwa ni pamoja na kumiliki programu za komputa ili kufanikisha uhalifu wao.

Wamekiri makosa na kisha kulipa mil 17354535. Na hii inatupa ukweli kuwa sio kila anayeikosoa serikali anakosoa kwa nia njema. Na sio kila anayekosoa anabambikiwa kesi za uhujumu uchumi.

Kwa muktadha huu huenda hata genge la akina Eric na wenzake pia kuna mambo makubwa yaliyojificha nyuma ya pazia,lakini watu kwa kuangalia shilingi upande mmoja waliituhumu serikali kumbambikia kesi.

Maoni; Tujihadhali na wanasiasa kama Zitto ni watu wabaya sana ambao hutumia watu kwa manufaa yao kisiasa, huku wao wakila bata na kunufaika na kuwaacha vijana wenye tamaa wakitiwa nyavuni.
 
Mleta mada jifunze kufikiri kwa kutumia akili zako, sio unafikiri kwa akili za kukopeshwa na Mataga. Hivi wewe uelewe kitu kilichotokea?

Hivi katika zama hizi za Mafuguli unaweza kushtakiwa na jamhuri kwa kesi za kutengenezwa na utawala wake halafu ukashinda kesi?

Huyo jaji au hakimu anajipenda kweli?
Na wewe mshtakiwa unajipenda kweli?
 
Walitiwa hatiani na mahakama ipi? au kwa ujuha wako unadhani ofisi ya DPP imekuwa mahakama siku hizi.

Kila siku mahakamani mnasema upelelezi bado unaendelea halafu leo unasema walitiwa hatiani, hujielewi.
 
Mleta mada jifunze kufikiri kwa kutumia akili zako, sio unafikiri kwa akili za kukopeshwa na Mataga. Hivi wewe uelewe kitu kilichotokea?

Hivi katika zama hizi za Mafuguli unaweza kushtakiwa na jamhuri kwa kesi za kutengenezwa na utawala wake halafu ukashinda kesi?

Huyo jaji au hakimu anajipenda kweli?
Na wewe mshtakiwa unajipenda kweli?
Acha upuuzi,wamekiri kosa na wamekiri kuunda hili genge na kumiliki namba za simu za nje. Kuna mtu aliwalazimisha kukiri?
 
Sio kwa mazingira haya ya utawala wa awamu hii, huo ni upenyo wa kisheria unaotumiwa na watawala kuwakandamiza raia wake hasa wale wanaoikosoa serikali.
Ndugu usidhani wao ni wajinga mpaka wanakubali kosa,kama upelezi umeanika hadi namba walizopewa ulitegemea iwe vipi?
 
Ndugu usidhani wao ni wajinga mpaka wanakubali kosa,kama upelezi umeanika hadi namba walizopewa ulitegemea iwe vipi?
Kama huo upelelezi umeanika kila kitu kwanini msiupeleke mahakamani kesi iendelee kusikilizwa ili watuhumiwa wapate nafasi ya kujitetea?

Una hakika gani hizo namba walipewa? kwanini umeamua kuwaamini hao prosecutors wa serikali badala ya kuamini uamuzi wa mahakama?
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya mtu mzalendo, mpole na ni Rais mwenye huruma na Moyo wa upendo kwa RAIA wake
Lakini wahuni na wapiga dili lazima muumie maana mianya imeziba
 
Kwani kesi haikuwa mahakamani?
Kwanini iendelee kukaa huko mahakamani mwaka mzima kila siku mnasema upelelezi haujakamilika, hivi ulikuwa unafuatilia hiyo kesi kweli?

Jiulize, kwanini watuhumiwa wa uhujumu uchumi kesi zao zinachukua muda mrefu mahakamani wanakaa jela zaidi ya mwaka mpaka wanaamua kukiri kosa?
 
Kwanini iendelee kukaa huko mahakamani mwaka mzima kila siku mnasema upelelezi haujakamilika, hivi ulikuwa unafuatilia hiyo kesi kweli?
Kwani ulikuwa umekamilika? Hujui kuwa ni Murder case na uhujumi uchumi ndio hujuchukia muda mrefu?
 
hilo genge liko wap? yaan serikali hii uwe na genge la
uhalifu wakuachie ukaliendeleze?? wadogo wameamua kuununua uhuru wao bas! maana wakijifanya vichwa ngumu mpaka miaka mitano unafaidika nini?? dunia inajua watanzania tunajua hata ww unajua ila unajaribu kutafuta uhalalj kwa halamu
 
hilo genge liko wap? yaan serikali hii uwe na genge la
uhalifu wakuachie ukaliendeleze?? wadogo wameamua kuununua uhuru wao bas! maana wakijifanya vichwa ngumu mpaka miaka mitano unafaidika nini?? dunia inajua watanzania tunajua hata ww unajua ila unajaribu kutafuta uhalalj kwa halamu
Swali gani la kipuuzi unauliza wanaume tumelala na wake zetu?
 
Acha upuuzi,wamekiri kosa na wamekiri kuunga hili genge na kumiliki namba za simu za nje. Kuna mtu aliwalazimisha kukiri?
Kaka siku hizi kila mtu anaemiliki simu janja ni msomi,mwanasheria,ni vurugu tupu ila umesema ukweli bila chenga.
Wamekiri kwa sababu ni kweli na hata hiyo hela imetoka kwenye genge hilo hilo.
 
Mleta mada jifunze kufikiri kwa kutumia akili zako, sio unafikiri kwa akili za kukopeshwa na Mataga. Hivi wewe uelewe kitu kilichotokea?

Hivi katika zama hizi za Mafuguli unaweza kushtakiwa na jamhuri kwa kesi za kutengenezwa na utawala wake halafu ukashinda kesi?

Huyo jaji au hakimu anajipenda kweli?
Na wewe mshtakiwa unajipenda kweli?
Wewe ndio unamlazimisha mtoa mada atumie akili yako,tujiulize ni kweli walikiri kufanya makosa au hawakukiri?
 
Wewe ndio unamlazimisha mtoa mada atumie akili yako,tujiulize ni kweli walikiri kufanya makosa au hawakukiri?
Wamekiri kuunda genge la uhalifu ili kueneza uongo dhidi ya nchi yao kuwa inakiuka haki za binadamu ili wapate pesa. Kuna kundi linaitwa Tanzania onTwitter lilipanga njama zote. Pia wamekiri kupatiwa namba za simu za nje. Aibu kubwa sana.
 
Back
Top Bottom