Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Kwani Bashite hakupigwa ban ya kuingia USA na Pompeo?
Ni sakata la Ndugu Erick Kabendera,

Kila mtu ana lake...Wengine watatunga ili kufurahisha nafsi zao na watu wao. Tafadhali ukipata habari yoyote kuhusu hii ishu ni vema ukaihakiki kabla ya kuiweka humu... Na wewe uliyeikuta humu ihakiki pia kabla ya kuisambaza kwa wengine.

Nimeandika sababu nimeshazishuhudia habar kadhaa za hivyo mpaka sasa na pia ni kutokana na kasumba ya baadhi ya wanajf hasa kwa matukio yanayotrend nchini mfano ni ile ishu ya Pompeo na Makonda.

Ni hayo tu.

In God we Trust
 
Ni sakata la Ndugu Erick Kabendera,

Kila mtu ana lake...Wengine watatunga ili kufurahisha nafsi zao na watu wao. Tafadhali ukipata habari yoyote kuhusu hii ishu ni vema ukaihakiki kabla ya kuiweka humu... Na wewe uliyeikuta humu ihakiki pia kabla ya kuisambaza kwa wengine.

Nimeandika sababu nimeshazishuhudia habar kadhaa za hivyo mpaka sasa na pia ni kutokana na kasumba ya baadhi ya wanajf hasa kwa matukio yanayotrend nchini mfano ni ile ishu ya Pompeo na Makonda.

Ni hayo tu.

Wewe ni nani hasa hapa JamiiForums hadi utake Kuwapangia Watu nini cha Kuandika au Kujadili? Hili ni Jukwaa huru sawa?
 
Ulipokuwa unaandika lengo lilikuwa ni nn? Bw pskal

Tuanzie hapo,
Lengo lako lilikuwa kuleta uelewa wa taarifa au ubatili wa taarifa?

Kwa sasa paskal umekataa kutuacha tufanye uchambuz wenyewe wa taarifa zako juu ya right and wrong

Sasa umeegemea kwenye ubatili wa kila taarifa inayomhusu rais, ikulu hata serikali na ni hapo ndipo tunakuita wewe ni snitch

Umetusaliti sote humu jf kabla hujajifunua na baada ya kujifunua ulikuwa vizur ila 2019 duh


Lkn huwa naitafari sana kauli " remember you have a family to feef not a community to empress"

Lkn mkeo na watoto wako marekani wanagreen gurd kwa nn usiwe sehemu sympathazition ya nchi !

Sent using Jamii Forums mobile app
Pompeo anapaswa kurevoke hizo rights kwa familia snitch kama huyu.
 
Kaka umefika Mbali sna huyo ni binadam tusichoke kumueleza ukweli ni kweli ameshindwa kuvumilia Njaa yke lkn bado ni Kaka yetu. Kaka Pascal kwenye ili ilikuwa kheri kwako kukaa kmy jambo likapita tu hata Mtt mdogo anajua Erick amekubari kulipa pesa ili kununua Uhuru wake na ww umechangia kwenye mtihani wake kikubwa naomba nikkumbushe kaka mkubwa Kuna maisha baada hiyo teuzi unayoipigania wakt ukifika utupata tu teuzi hkn sababu kujitoa Utu wako...
Pascal, wewe ndie ulienifanya mimi nikajiunga JF na nlikuwa nakuheshimu sana. Ila natangaza tena kama nlivyowahi kutangaza hapo kabla, sikuheshimu kamwe na nlidhani kweli wewe ni mtu Bora ila hufai kutokana na mengi uliyoyaandika humu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee..!! Tusipende kuongozwa na mihemko/fikra zetu kwenye kudhania mambo ambayo hatuna uhakika nayo. Kwani dhana ni dhambi hata Mungu hapendi tudhaniane kwenye vitu ambavyo havina ukweli lkn pia hatuja vithibitisha kwa macho yetu,kumwambia mtu kuwa amefanya jambo fulani ili hali hajafanya inauma sana jamani, Je ingelikuwa wewe umezushiwa jambo ambalo hakuwahi/hukutarajia kufanya nafsi yako ingekuwa na amani???....Mkuu Pasco huu ni mtihani kama mitihani mingine ambayo aliyo-wahi kukufika kwenye maisha yako,kama ile ilipita na hili nalo litapita kikubwa ni subra zako na kumuomba Mungu akuongoze katika hili.TUSIPENDE KUHUKUMU NDUGU ZANGU..Siasa sizitufanye kuchukiana na kuombeana mabaya na kuzushiana mabalaa.
 
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Baada ya mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kukamatwa na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.
Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusamehe hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.
UMEELEWEKA
 
Tatizo ni moja brother mayala punguza shobo na utawala wa sasa, samahani kama nimetumia neno lenye ukakasi maana ningesema punguza kihele hele lingekuwa baya zaidi

Kaa ujitathimi wewe mwenyewe kipindi gani wadau wengi hapa JF wamekuwa wakikuona ufai na umepoteza muelekeo ni kipindi ambacho unasupport vitu bavyo kwa akili ya kawaida vipo tofauti ila unasupport tu bila soni yani umeshayumbishwa misimamo yako pascal mayala tuliyemjua JF hapa miaka mitatu nyuma siyo huyu wa leo JF hueleweki unataka nini usamehewe kodi, upewe dili za serikali, au upate teuzi

Mwanzoni hata miye nilipinga wewe kuhusuka na issue ya kukamatwa kabendela ila baadae nilivyoona uandishi wako nikasems hapana bro mayala hapa ile tuhuma inamuhusu, kwaiyo kusema kuwa ukweli umebainika unatusamehe hapana kama wewe cause ulichotegemea ndio hicho kishatokea kakamatwa ukweli uliotakwa kwa kabendela umejulikana nani source ni wewe

Ombi punguza shobo na awamu ya tano kuwa kati si kwamba hatuoni makubwa yanayofanywa na awamu hii tunaona ila JF ni sehemu ya kuambiana ukweli siyo kusifia tu hata ambayo hayapaswi kusifiwa


WE LOVE YOU BRO RUDI KWENYE MSTARI UJACHELEWA
 
Kilichonisikitisha ni unafiki wa kiwango cha PhD cha Waafrika.
Wanajifanya kinafiki kuzitukana nchi za magaharibi na kuwaita Mabeberu wasio na nia njema na nchi zetu. Na kujifanya kuwa wenye nia njema na nchi zetu ni wachina; lakini cha ajabu familia zao zinaishi America na Ulaya na sio China.
Wanasafiri kwenda kupumzika na kula raha America na sio Urusi.
Wanawasomesha watoto wao Amerika na sio China wala Korea ya Kaskazini.

Ukweli utatuweka huru.

Kuna wajati Teacher aliona Mbali akalalamika kuwa Tumeanza kutajana kwa makabila sijui tunataka kutambika karne hii.
Ingekua leo hii angeitwa kwenye kamati Fulani ahojiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka umefika Mbali sna huyo ni binadam tusichoke kumueleza ukweli ni kweli ameshindwa kuvumilia Njaa yke lkn bado ni Kaka yetu. Kaka Pascal kwenye ili ilikuwa kheri kwako kukaa kmy jambo likapita tu hata Mtt mdogo anajua Erick amekubari kulipa pesa ili kununua Uhuru wake na ww umechangia kwenye mtihani wake kikubwa naomba nikkumbushe kaka mkubwa Kuna maisha baada hiyo teuzi unayoipigania wakt ukifika tupata teuzi hkn sababu kujitoa Utu wako...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa kaka
 
Hakuna kitu kibaya sana kama kumsingizia mtu kwa jambo usilokuwa na uthibitisho nalo. Ni sawa na mtu kahisi fulani anatoa rushwa ya ngono, halafu mara vuuu jamaa anakuja kuanzisha uzi JF na majina mkononi. Tunaharibu majina ya watu, saikolojia yao na maisha yao ya kila siku kwa kitu tulichohisi ni kidogo tu kumbe kina madhara makubwa.

Pascal Mayalla pole sana kwa changamoto ulizozipitia. May God give you more and more grace and peace.
 
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Naomba nitoe pole sana kwa mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kwa anayopitia, na hayuko peke yake katika hayo, kuna wengi wengine pia wanapita katika mapito kama hayo japo ni kwa njia tofauti tofauti, yote haya ni mapito tuu na kuna siku yatafika mwisho na yatapita.

Toka kukamatwa kwake na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa huko nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.

Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusamehe hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.
Wewe jamaa ushamtia mwenzio matatizoni alafu unatuletea porojo zako hapa.. Subiria zamu yako inakuja
 
P acha utoto yaani serikali imeshindwa kuleta ushahidi mahakamani kwa miezi 7 mpaka mtuhumiwa akiri mwenyewe? Huu ni ujambazi na uporaji wa kidola
 
Back
Top Bottom