Baada ya vita ya Ukraine, Nchi za Afrika zinatakiwa kupata Mateso Makali ya Kiuchumi kutoka kwa EU & USA

Mleta mada kwa taarifa yako, wakati wa vita baridi ya kwanza, nchi za Afrika zilikuwa na unafuu mkubwa. Imeanza vita baridi ya pili nina uhakika, Afrika tutapumua zaidi kama viongozi wetu watatambua umuhimu wa kuhakikisha waafrika wanajitegemea kiuchumi na kijamii.
 
Huko walikuwa wanafurushwa magaidi, wafadhili Ugaidi na vikundi vyao vya Ugaidi.

Sihitaji kusoma historia ya Nyerere, Rais aliyetaifisha mali za watu, Rais aliyefanya mpaka leo Tanzania wananchi wanaishi kijima, akatuachia shetani wa maendeleo CCM.
 
Watu wa green card hawawezi kukuelewa. Umeona majibu yake, Mkuu.
 
Point no moja, huko walifuatwa wafadhili wa Ugaidi na magaidi.

Point no mbili nakubaliana na wewe.

Point no Tatu, hata EU pamoja na kutawala tayari wamerudisha fadhila vya kutosha, USA amekuwa kimbilio la wanamageuzi/wanaharakati na Demokrasia duniani, nchi kama Afrika kusini imejengwa na makaburu pamoja na madhira yote waliyowafanyia waafrika, kwahiyo kama ni fadhila hata EU na USA walipwe fadhila kwa sababu misaada yao ndiyo inainua na kukuza uchumi wa nchi za Afrika.
 
Tutapumua kivipi Wakati uchumi wetu unategemea misaada?

Unalima lakini huwezi kuprocess mwenyewe?

Una rasilimali, lakini huna teknolojia ya kuzitumia, hapo utapumua vipi?
 
Huko walikuwa wanafurushwa magaidi, wafadhili Ugaidi na vikundi vyao vya Ugaidi.

Sihitaji kusoma historia ya Nyerere, Rais aliyetaifisha mali za watu, Rais aliyefanya mpaka leo Tanzania wananchi wanaishi kijima, akatuachia shetani wa maendeleo CCM.
Unajenga hoja kitoto sana, hujakomaa kudiscuss facts na badala yake unaishia kutoa tu kauli za rejareja!

Kuhusu ugaidi, US alisema Iraq Kuna silaha za Nuclear, akavamia na hazikuwepo!
Huko Afghan, Julian Assange aliwaumbua wamarekani Kwa kutoa ushahidi wa war crimes kwenye WikiLeaks, mpaka Leo mmarekani anamtafuta Assange Kwa kutoa nyaraka hizo za Siri!

Yaani mfichua maovu ya matendo ya jeshi la US huko Afghan anatafutwa Kwa kutoa classified information! Na hapo Bado unataka Africa iwe na mtizamo kama anataka US!
Kama US alitumia kigezo Cha ugaidi, Russia yeye kasema anawafagia Nazis huko Ukraine! Kama hujui, Nazis walisababisha warusi milion 27 kuuwawa wakati wa world war 2!
 
Tuambie kuhusu Julian Assange ambaye alitoa Siri za uhalifu wa Kivita za US nchini Afghan!Iweje leo US imtafute Ili imshughulikie Kwa kutoa Siri za jeshi la US?
 
Bwana Bome-e nafurahi kuona unaendelea kujibu hoja zangu za kitoto na reja reja.

Huyo Julian Assange alikuwa kibaraka wa Urusi, kwahiyo ni lazima atafutwe popote alipo ili aje athibitishe mbele ya Mahakama.
 
Majibu yake ya kitoto sana,hajakomaa kifikra kujenga hoja na badala yake Yuko kama kifaranga Cha kuku ambacho kimempoteza mama yake!
Bwana Bome-e hakuna haja ya kupandisha mishipa ya hasira na kumwaga povu namna hii.

Umekereka na hoja za kitoto, unakaa pembeni, yaani hamna haja ya kutumia nguvu sana.
 
1. Usichokijua ni kwamba misaada ya Tunachopewa Africa ni Robo/theluthi ya wanachoendelea Kutuibia. Pesa zote wanazotupa Africa hawatoi mifukoni mwao Bali Gawio la Fedha waliyoingiza kutokana na wizi wa Mali za Africa. Na sasahv hawaji na Bunduki Wala Vifaru, Wanatumia Ubabe wa kiuchumi walionao. Wanafanya intimidation katika Mikataba, rejea Mikataba ya EPA nk.

2. Katika Ku deal na magaidi Kuna mitandao ya Kimataifa ya Kufanya Shughuli hizo ikiwemo Interpol, U.N nk. lakini sio Uvamizi wa Nchi Moja kuivamia Nchi nyingine Kijeshi. Marekani iliivamia Iraq Kijeshi Yaani Total war Kwa kisingizio Inamiliki Mabomu ya Nuclear kitu ambacho Mpaka Leo wameshindwa kuthibisha. Nchi za Ulaya zilivamia Africa na Dunia kutafuta Raslimali Kwa Nguvu na kuua watu lakini mpaka Leo hakuna aliyethubutu kuwawajibisha. Huu ni unafki wa Hali ya Juu.
 
Bwana Bome-e nafurahi kuona unaendelea kujibu hoja zangu za kitoto na reja reja.

Huyo Julian Assange alikuwa kibaraka wa Urusi, kwahiyo ni lazima atafutwe popote alipo ili aje athibitishe mbele ya Mahakama.
Ndio maana nasema hujakomaa na uko misinformed! Julian Assange hatafutwi kuja kuthibitisha mbele ya mahakama, anatafutwa kwasababu ya kuhatarisha usalama wa US Kwa kutoa classified information!

Kwenye mashtaka 17 aliyofunguliwa, yote hayahusiani na kuthibitisha nyaraka zile kama ni aunthetic maana ni kweli they are!

Moja ya nyaraka hizo alizotoa,ni camera onboard kwenye ndege vita ambapo wanajeshi wa US wanaonekana wakishambulia raia wakiwemo watoto halafu wanajeshi hao wanasikika walisema Kwa kebehi "that's what you get for bringing a child into a war zone"!

Fanya utafute interview ya Stephen sackur na Mke wa Assange anayeitwa Stella, utajifunza mengi!
 
Bwana Bome-e hakuna haja ya kupandisha mishipa ya hasira na kumwaga povu namna hii.

Umekereka na hoja za kitoto, unakaa pembeni, yaani hamna haja ya kutumia nguvu sana.
Uko mweupe sana,ni bora ukawa msomaji zaidi kuliko mchangiaji sana Kwa mambo ambayo huna uelewa nayo!
 
Majibu atakayokupa ni mepesi mno mpaka utaishiwa nguvu ya kumjibu!
 
Bwana Bome-e, mashtaka 17 dhidi ya Julian Assange yamefunguliwa peponi?

Kama ni mahakamani, basi umejitoa ufahamu maksudi.
 
Russia ana pesa gani za kutoa misaada ili hali nchi yake ina watu ni masikini kama huku kwetu. Bado hapo ana vikwazo vya kufa mtu.
 
Hujitambui hapa umeandika upuuzi Tu.

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Afrika ilikuwa primitive hizo rasilimali walikuwa hawazijuhi, kuja kwa wakoloni ndiyo wakaambiwa na kuweza kutambua thamani ya rasilimali hizo, kwahiyo hata kama wasingekuja wakoloni bado Afrika ingekuwa masikini wakutupwa maana hizo rasilimali hata matumizi yake walikuwa hawana.

Mpaka sasa Afrika imejaa rasilimali za kutosha karibia kila nchi lakini zimewashinda kutumia kwa hawana teknolojia ya kutosha ya kuwafanya wao wenyewe wazisimamie na wanufaike nazo.


Ni sawa umenunua gari alafu hujuhi kuliendesha, umelipaki tu nyumbani kwako unasubiri aje mtu anayejua kuendesha gari ndo akuendeshe.


Kwahiyo kuwa na rasilimali alafu huna teknolojia ya kutumia ili unufaike nazo, hizo mali ni useless.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…