Baada ya wamachinga, malori Kariakoo ni shida mpya

Baada ya wamachinga, malori Kariakoo ni shida mpya

Kariakoo bado kuna kero ya msongamano...
Kweli ipo na wala haitaisha,
Lakini hii ya malori ni too much,
Yaani haileti maana kuondoa wamachinga walio wengi na kuacha malori yanayomilikiwa na wachache,
Huu ni uonevu wa hali ya juu
 
we jamaa vp hujui msimu wa sikukuu huu watu wanashusha mali hapo tusio enda china tunaenda kulangua china ya kkoo
Tatizo ni vikampuni vya usafiri vyenye ofisi katikati ya mitaa ya kariakoo,
Sasa ina maana gani kuondoa wamachinga na kuruhusu mizigo barabarani?
Au ndio kukomoana?
Kweli magu atakumbukwa kwa mengi
 
Hii issue siyo ya kudharau, naamini iko siku madhara makubwa yatatokea baina ya malori na either waendesha gari ndogo au watumiaji wengine wa barabara, haiwezekani mtu afunge njia akipakia mizigo kisa analipia posho au rushwa ya 20,000 au 50,000 sijui kima sahihi hjku wengine wakuteseka barabarani
Leo hii saa kumi na mbili jioni watu wamepigana visu mtaa wa narun'gombe na muheza kisa malori yameziba njia na ofisi ya mizigo wamemwaga mizigo mpaka barabarani,
Nimejipitia zangu taratiiiibu huku nikisema nilitabiri haya,
Bado risasi tu kurindima sasa
Nyie mamalka endeleeni kudharau hili
Kwa ajili ya kujifrahisha kidogo
 
Back
Top Bottom