Swali ambalo kila wakati nauliza lakini sijawahi kupewa majibu ni haya:
1. Hivi kama si Diamond, leo hii Wema angekuwa anatajwa tajwa kwa lipi?
----Kumbukumbu zangu zinanionesha kwamba, tangu aukwae u-miss 2006, Wema amekuwa kwenye midomo ya watu na mara nyingi haya yamekuwa yakitokana na mahusiano! Alitajwa tajwa sana wakati yupo na Kanumba... walipobwagana, Kanumba bado aliendelea kufahamika coz' alimkuta akiwa tayari star! Akatajwa tajwa sana wakati yupo na Mwinyi... walipobwagana, safari ya Mwinyi ikaishia hapo coz' walipokutana; Mwinyi hakuwa star kwahiyo kufahamika kwake kulichangiwa sana na Wema! Sasa anatajwa tajwa sana na Diamond... Wema alimkuta Diamond tayari akiwa star! Mara ya kwanza Wema alipomwagana na Diamond, Dangote akawa na JOkate kidogo kisha akawa na Penny!
INgawaje Penny na Jokate ni watu ambao wanafahamika sana hapa mjini, lakini walipokuwa na Diamond story zote zikahamia kwao! Kabla ya Diamond, sidhani ni mara ngapi kwa mwaka Penny alikuwa anajadiliwa humu jamvini... lakini alipoanza uhusiano na Diamond, mara kwa mara post za Penny zikawa hazikauki! Baada ya kumwagana, story za Penny hatuzioni tena... hali kadhalika hata story za Jokate nazo ni za ku-beep!
Hivi majuzi zikaja stori za Menninah... majority walikuwa hawamfahamu Menninah... kama alishapata kujadiliwa hapa jamvini basi ni kwa nadra sana! Lakini zilipokuja story za Meninnah na Diamond, ilikuwa haipiti wiki humu jamvini bila kuwapo story kuhusu Meninnah!
Haya sasa tujaribu kushughulisha bongo zetu! Hivi ni kweli katika mazingira kama hayo pasipo na Wema Diamond anafutika? Narudia, kama sio Diamond... assume Wema angekuwa na mtu asiye maarufu kwa muda mrefu; hivi Wema tungemtaja taja kwa jambo lipi? Ametoa movie ngapi mwaka huu? Ametoa movie ngapi mwaka jana? Tungemtaja taja kwa kipi?
Jambo moja sina shaka nalo! Hii couple ni couple inayopendwa na wengi... mashabiki wa Diamond wakagawanya mahaba yao na kwa Wema na mashabiki wa Wema wakafanya hivyo hivyo in favor of Diamond! Kilichotokea, ni Wema kushindwa kutumia opportunity hii! Wakati mwenzake ameweka kazi mbele mapenzi baadae, Wema akaweaka mapenzi mbele kazi mwaka wowote ule! Nashawishika kuamini kwamba, endapo wataachana jumla basi ni labda Wema awe anatoka na mtu maarufu otherwise, baada ya mwaka mmoja hatutakuwa na cha kuongea kuhusu Wema unless akumbuke kwamba ni sanaa ndiyo ilimweka kwenye ramani!