Baada ya zama za kubebwa na Yamoto Band kupita, Enock Bella atoa wimbo mbaya kupitiliza

Excellent brother.....ila mtoa posti kanikela roho sana ...anamponda tuu huyu DOGO pasipokumshauri....
 
Nyimbo n nzuri acha roho mbaya
 
We jamaa unaroho mbaya, tukupe tuzo ya uchukiaji. Wimbo ni mzuri sikutegemea
 
Wimbo mzuri,na hata video ni nzuri pia.Watanzania tujifunze kuvipenda vya nyumbani.Na pia kuwapa ushauri chanya wanaovifanya.Mtoa mada,umekosea sana.Kumbuka sio kila wimbo unaweza ukaupenda,au ukawa kwenye mahadhi ya kile unachotarajia kukisikia.Acha wanaopenda muziki mzuri,wapate ladha wanayoitaka.Wewe subiri ,ladha za muziki unazozitaka.Chuki hazina maana.
 
Kama sijui mziki na iwe hivyo, ila wimbo mzuri nimemsikiliza mara 3
nimependa wimbo na sauti pia
 
Wimbo mtamuuuuu balaaaaa, big up kijana
 
Mtoa post utakuwa umegombana na jamaaa so,umeamua kuja kumchafua huku kwenye mitandao,acha kjana atafute riziki,kwani hao wengine wanaimba vitu vya maaana?
 
Huyu mleta mada inaonekana ni masikini wa fikra na kipato. Huwezi kuwa mwanaume mnafiki na mmbeya kama huyu. Mwenzio yuko kwenye utafutaji wewe unamkatisha tamaa na kushawishi wateja wasione hata bidhaa yake. Mimi siyo mpenzi wa bongo fleva ila sipendi wachawi
 
Acha ushamba na wivu wa kijinga.usituaminishe kuwa wewe ndio quality assuarance wa nyimbo za wenzio imba wewe tukusikie....
 
Mleta mada umewahi kushika mic na kuimba angalau kwenye birthday party ya jirani yako au ndugu yako?!

Upondaji wako upo too personal! Kwamba eti Fella alifanya kila ushawishi ili mradi tu aimbe ukijaribu kuonesha hakutakiwa kuwa mwimbaji hata huko Yamoto unaonekana wazi huufahamu muziki na mipangilio yake na umuhimu wa mtu kama Enock pale Yamoto!!

Hata hii single yake, kabla ya kukashifu kwa kiwango kikubwa kiasi hicho ulitakiwa kwanza kufahamu taste yako kwenye muziki hasa ni nini!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…