singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,536
Kumekuwepo na utaratibu au utamaduni wa kubeza mafanikio na kutokukubali kwa dhati kabisa na kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali rais Jakaya Kikwetena chama chake cha CCM. kuna wachache walisema hawauoni ubunifu wala utendaji kazi, uchapakazi wa Rais na uadilifu na uawaminifu Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mimi ninaomba nitumie fursa hii kupingana nao hoja na kuwaomba waende wakafanye utafiti kwanza kabla ya kuongea, kubeza na kudharau mafanikio ya Serikali ya CCM ya awamu ya Nne. Lakini pia napenda kuwaasa tuondokane na utamaduni wa kubeza mafanikio na kudharau kila kitu ili mradi tu sisi ni Wapinzani, na kuwa mpinzani si kupinga kila kitu ikiwa pamoja na maendeleo.
Kumekuwepo na mafanikio mengine ya kujivunia tangu tupate uhuru ingawa kuna baadhi ya watu hawalidhishwi na kasi ya maendeleo iliyopo, ni ukweli usiopingika kuwa bado tunachangamoto za hapo na pale lakini yatupasa kuubali ukweli tumetoka mbali na mafanikio yamepatikana na yanaendelea kupatikana katika awamu zote tatu na ya a sasa anayomalizia rais Jakaya Kikwete.
Katika awamu hii ya nne kumekuwa na mafanikio ambayo hayakuwahi kutokea ktk nchi hii hata kama baadhi ya watu hawapendi kusikia hivyo, kwa uchache tumefanikiwa katika sekta mbalimbali kama elimu, afya, miundo mbinu na mambo chungu mzima ambayo tukisema tuyataje hapa hatutapa nafasi ya kutosha.
Tukianzia na elimu sote tunakumbuka kuwa serikali yake ilibua mpango wa ujenzi wa sekondari za kata kwa sababu nafasi za wanafunzi kuingia sekondari zilikuwa zimekuwa finyu kiasi cha kwamba ni asilimia kati ya 6 na 10 ya watoto wote waliokuwa wanamaliza shule za msingi mwaka 2005 walikuwa wanaingia sekondari wakati anaingia madarakani.
Pamoja kejeli nyingi zilizoelekezwa kwa shule za sekondari za kata kiasi cha kuitwa Yeboyebo katika miaka ya mwanzoni ya shule hizo, bado zimekuwa na mafanikio makubwa, ambayo ni sehemu ya mafanikio makubwa ya sekta ya elimu katika miaka tisa ya uongozi wa rais KIkwete.
Rais Kikwete alitangaza hivi karibuni kuwa Serikali yake imefuta katika shule za sekondari zilizo chini ya serikali, ili kuboresha sera ya elimu na kuhakikisha kila mwanafunzi anayeanza darasa kwanza anamaliza kidato cha nne. Hii ya kufuta ada itasaidia kila mtoto anayeanza darasa la kwanza anakuwa na nafasi ya kumaliza sekondari kwa maana ya kidato cha nne mpaka cha sita bila kulazimika kuacha shule kwa sababu ya ada.
Bajeti ya Elimu ndiyo iliyo kubwa kuliko zote kwa miaka mingi na imekuwa ikiongezeka. Kwa mfano, mwaka 2005/2006 zilitengwa shilingi bilioni 669.5 wakati mwaka 2014/2015 zimetengwa shilingi trilioni 3.1. Katika kipindi hicho, bajeti ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 56.1 hadi shilingi bilioni 345. Kwa sababu hiyo idadi ya wanafunzi wanaofaidika imeongezeka kutoka 16,345 mwaka 2005 hadi 98,000 mwaka 2014.
Shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,343 mwaka 2014 na hivyo kufanya idadi ya wanafunzi nayo kukua kutoka milioni 7.54 hadi milioni 8.23. Kwa upande wa sekondari shule zimeongezeka 531 mwaka 2005 hadi 4,576 mwaka 2014. Idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,804.056 mwaka 2014.
Upanuzi huu mkubwa na wa kihistoria umetokea pia kwenye vyuo vya elimu ya ufundi stadi ambapo vyuo vimeongezeka kutoka 184 hadi 744 kati ya mwaka 2005 na 2014. Kwa upande wa elimu ya juu, idadi ya vyuo imeongezeka kutoka 26 hadi 50 kati ya mwaka 2005 na 2014 na kufanya idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu iongezeke kutoka wanafunzi 40,719 mwaka 2005 hadi wanafunzi 200,986 mwaka 2014. Leo hii, hatuna tena tatizo na fursa ya kupata elimu kwa elimu ya msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu.
Mwaka 2005, urari wa wanafunzi kati yetu na wenzetu wa Afrika Mashariki ulikuwa wa chini mno kwa upande wetu. Kenya walikuwa na wanafunzi wa sekondari 925,341 na wa vyuo vikuu 108,407 ikilinganishwa na Tanzania iliyokuwa na wanafunzi 524,325 wa sekondari na 40,719 wa vyuo vikuu. Uganda ilikuwa na wanafunzi 728,393 wa sekondari na 124,313 wa vyuo vikuu.
Sasa hali ni tofauti. Kwa mwaka 2013, kwa mfano, Kenya ilikuwa na wanafunzi wa sekondari 2,104,300 na wanafunzi wa vyuo vikuu 324,600. Katika mwaka huohuo, Uganda walikuwa na wanafunzi wa sekondari 1,362,739 na wa vyuo vikuu 140,403. Ongezeko hili linatuweka katika hali nzuri ya ushindani tunapoelekea katika ushindani wa soko la pamoja ndani ya Afrika Mashariki ikilinganishwa na hali ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.
Tumekuwa nchi ya kupigiwa mfano katika kutekeleza Malengo ya Milenia (MDGs) yanayohusu fursa ya watoto kupata elimu ya msingi, na usawa wa kijinsi baina ya watoto wa kiume na wa kike kupata elimu ya msingi na sekondari.
Sote tu mashahidi ya kuwa Rais Kikwete alivyoingia alikutana na changamoto mbalimbali ikiwamo ukame ambapo tathimini inaonyesha kuwa mwaka 2006 jumla ya ngombe 250,000, mbuzi 130,000 kondoo 122,000 pamoja na punda zaidi 700 walikufa kutokana na ukame wa ukosefu wa maji, jumla ya mifugo yote hiyo ilikuwa na thamani ya zaidi ya billion 45.3
Baada ya ukame kupungua serikali ya rais kikwete ikakutana na mtihani mwingine wa kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kusababisha ongezeko la bei katika sekta ya usafiri. Mtihani mwingine kwa serikali ya rais Kikwete ilikuwa ilikuwa ni mtikisiko wa wa uchumi duniani ambayo uliathiri kwa kiasi kikubwa kwa mataifa yanayoendelea na yaliyokuwa yameandelea na kuathiri bajeti za chi kadhaa duniani, lakinin kwa uimara wa serikali yake hatukuyumbishwa na mtikisiko huu wa uchumi wa dunia mwaka 2009.
Rais kikwete pia amefanikiwa kuondoa uhasama wa visiwani unguja na pemba uliodumu kwa miaka 10 ambapo aliyemstaafu Benjamini Mkapa aliwahi kukiri baada ya kutoka madarakani kuwa mgogoro wa visiwa hivyo vya Karafuu ulikuwa unamnyima usingizi wakati wa utawala.
Mgogoro huo wa kisiasa ulifikia hatua mbaya kiasi ambacho hata ndugu wa baba mdogo na mkubwa walishindwa kuzikana pamoja na kuombana maji kutokana na misimamo na itikadi ya vyama vyao, lakini leo twaona wazanzibar wote wamekuwa wamoja na wakimbizi waliokwenda Mombasa walirejea nchini.
Mimi ninaomba nitumie fursa hii kupingana nao hoja na kuwaomba waende wakafanye utafiti kwanza kabla ya kuongea, kubeza na kudharau mafanikio ya Serikali ya CCM ya awamu ya Nne. Lakini pia napenda kuwaasa tuondokane na utamaduni wa kubeza mafanikio na kudharau kila kitu ili mradi tu sisi ni Wapinzani, na kuwa mpinzani si kupinga kila kitu ikiwa pamoja na maendeleo.
Kumekuwepo na mafanikio mengine ya kujivunia tangu tupate uhuru ingawa kuna baadhi ya watu hawalidhishwi na kasi ya maendeleo iliyopo, ni ukweli usiopingika kuwa bado tunachangamoto za hapo na pale lakini yatupasa kuubali ukweli tumetoka mbali na mafanikio yamepatikana na yanaendelea kupatikana katika awamu zote tatu na ya a sasa anayomalizia rais Jakaya Kikwete.
Katika awamu hii ya nne kumekuwa na mafanikio ambayo hayakuwahi kutokea ktk nchi hii hata kama baadhi ya watu hawapendi kusikia hivyo, kwa uchache tumefanikiwa katika sekta mbalimbali kama elimu, afya, miundo mbinu na mambo chungu mzima ambayo tukisema tuyataje hapa hatutapa nafasi ya kutosha.
Tukianzia na elimu sote tunakumbuka kuwa serikali yake ilibua mpango wa ujenzi wa sekondari za kata kwa sababu nafasi za wanafunzi kuingia sekondari zilikuwa zimekuwa finyu kiasi cha kwamba ni asilimia kati ya 6 na 10 ya watoto wote waliokuwa wanamaliza shule za msingi mwaka 2005 walikuwa wanaingia sekondari wakati anaingia madarakani.
Pamoja kejeli nyingi zilizoelekezwa kwa shule za sekondari za kata kiasi cha kuitwa Yeboyebo katika miaka ya mwanzoni ya shule hizo, bado zimekuwa na mafanikio makubwa, ambayo ni sehemu ya mafanikio makubwa ya sekta ya elimu katika miaka tisa ya uongozi wa rais KIkwete.
Rais Kikwete alitangaza hivi karibuni kuwa Serikali yake imefuta katika shule za sekondari zilizo chini ya serikali, ili kuboresha sera ya elimu na kuhakikisha kila mwanafunzi anayeanza darasa kwanza anamaliza kidato cha nne. Hii ya kufuta ada itasaidia kila mtoto anayeanza darasa la kwanza anakuwa na nafasi ya kumaliza sekondari kwa maana ya kidato cha nne mpaka cha sita bila kulazimika kuacha shule kwa sababu ya ada.
Bajeti ya Elimu ndiyo iliyo kubwa kuliko zote kwa miaka mingi na imekuwa ikiongezeka. Kwa mfano, mwaka 2005/2006 zilitengwa shilingi bilioni 669.5 wakati mwaka 2014/2015 zimetengwa shilingi trilioni 3.1. Katika kipindi hicho, bajeti ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 56.1 hadi shilingi bilioni 345. Kwa sababu hiyo idadi ya wanafunzi wanaofaidika imeongezeka kutoka 16,345 mwaka 2005 hadi 98,000 mwaka 2014.
Shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,343 mwaka 2014 na hivyo kufanya idadi ya wanafunzi nayo kukua kutoka milioni 7.54 hadi milioni 8.23. Kwa upande wa sekondari shule zimeongezeka 531 mwaka 2005 hadi 4,576 mwaka 2014. Idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,804.056 mwaka 2014.
Upanuzi huu mkubwa na wa kihistoria umetokea pia kwenye vyuo vya elimu ya ufundi stadi ambapo vyuo vimeongezeka kutoka 184 hadi 744 kati ya mwaka 2005 na 2014. Kwa upande wa elimu ya juu, idadi ya vyuo imeongezeka kutoka 26 hadi 50 kati ya mwaka 2005 na 2014 na kufanya idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu iongezeke kutoka wanafunzi 40,719 mwaka 2005 hadi wanafunzi 200,986 mwaka 2014. Leo hii, hatuna tena tatizo na fursa ya kupata elimu kwa elimu ya msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu.
Mwaka 2005, urari wa wanafunzi kati yetu na wenzetu wa Afrika Mashariki ulikuwa wa chini mno kwa upande wetu. Kenya walikuwa na wanafunzi wa sekondari 925,341 na wa vyuo vikuu 108,407 ikilinganishwa na Tanzania iliyokuwa na wanafunzi 524,325 wa sekondari na 40,719 wa vyuo vikuu. Uganda ilikuwa na wanafunzi 728,393 wa sekondari na 124,313 wa vyuo vikuu.
Sasa hali ni tofauti. Kwa mwaka 2013, kwa mfano, Kenya ilikuwa na wanafunzi wa sekondari 2,104,300 na wanafunzi wa vyuo vikuu 324,600. Katika mwaka huohuo, Uganda walikuwa na wanafunzi wa sekondari 1,362,739 na wa vyuo vikuu 140,403. Ongezeko hili linatuweka katika hali nzuri ya ushindani tunapoelekea katika ushindani wa soko la pamoja ndani ya Afrika Mashariki ikilinganishwa na hali ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.
Tumekuwa nchi ya kupigiwa mfano katika kutekeleza Malengo ya Milenia (MDGs) yanayohusu fursa ya watoto kupata elimu ya msingi, na usawa wa kijinsi baina ya watoto wa kiume na wa kike kupata elimu ya msingi na sekondari.
Sote tu mashahidi ya kuwa Rais Kikwete alivyoingia alikutana na changamoto mbalimbali ikiwamo ukame ambapo tathimini inaonyesha kuwa mwaka 2006 jumla ya ngombe 250,000, mbuzi 130,000 kondoo 122,000 pamoja na punda zaidi 700 walikufa kutokana na ukame wa ukosefu wa maji, jumla ya mifugo yote hiyo ilikuwa na thamani ya zaidi ya billion 45.3
Baada ya ukame kupungua serikali ya rais kikwete ikakutana na mtihani mwingine wa kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kusababisha ongezeko la bei katika sekta ya usafiri. Mtihani mwingine kwa serikali ya rais Kikwete ilikuwa ilikuwa ni mtikisiko wa wa uchumi duniani ambayo uliathiri kwa kiasi kikubwa kwa mataifa yanayoendelea na yaliyokuwa yameandelea na kuathiri bajeti za chi kadhaa duniani, lakinin kwa uimara wa serikali yake hatukuyumbishwa na mtikisiko huu wa uchumi wa dunia mwaka 2009.
Rais kikwete pia amefanikiwa kuondoa uhasama wa visiwani unguja na pemba uliodumu kwa miaka 10 ambapo aliyemstaafu Benjamini Mkapa aliwahi kukiri baada ya kutoka madarakani kuwa mgogoro wa visiwa hivyo vya Karafuu ulikuwa unamnyima usingizi wakati wa utawala.
Mgogoro huo wa kisiasa ulifikia hatua mbaya kiasi ambacho hata ndugu wa baba mdogo na mkubwa walishindwa kuzikana pamoja na kuombana maji kutokana na misimamo na itikadi ya vyama vyao, lakini leo twaona wazanzibar wote wamekuwa wamoja na wakimbizi waliokwenda Mombasa walirejea nchini.