Baadhi ya mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Nne ya Dkt. Jakaya Kikwete (Sehemu ya 1)

Baadhi ya mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Nne ya Dkt. Jakaya Kikwete (Sehemu ya 1)

HUDUMA YA AFYA:
ikiwemo kuendeleza huduma ya afya imekua mojawapo wa mambo muhimu tuliyoyapata, tumekamulisha pia maendeleo ya afya ya msingi (MMAM) ambayo matarajio yetu ni kuutelekeza katika mwaka ujao wa fedha au unaofwata .

Una akili kweli?

Mmeshindwa 'kuendeleza' huduma..sorry, kuanzisha huduma bora za Afya kwa miaka zaidi ya thelathini then unategemea mtafanya mwaka ujao wa fedha? Kutakuwa na tofauti gani na miaka iliyopita? Hivi unajua hata mwaka ujao wa fedha unaanza lini?

Unaweza kuboresha hili katika family level(kwenye huo mwaka ujao wa fedha), lakini si National level kwasababu hamtashika dola mwaka huu wa uchaguzi.
 
Kuombaomba misaada nje ni ubunifu jasiri pia Kama nchi. Kuruhusu uchumi wa nchi umilikiwe na familia wachache si haba. Visasi kwa wwanaotofautiana nawe keeling ubunifu mahiri. Usanii wa uongozi naam! Kama wa kuifagilia rasimu na kuiponda kwa hila....
 
Napingana na wewe - Legacy ya Kikwete ni kama ifuatavyo!


Wakale walisema actions speaks louder than words. Kwa matendo yake, over the last 10 years, it is obvious to everyone kuwa kuwa Falsafa ya Uongozi wa Rais Jakaya Kikwete, na serikali yake ya awamu ya nne ni ile ya OMBAOMBA. Bwana Kikwete anaamini katika omba omba mpaka aliwahi kutetea falsafa hiyo kwa kusema kuwa yeye ni baba na huwa anaondoka nyumbani kila wakati kwenda nje kuhemea ili atuletee watoto (watanzania) fedha za matumizi. Sasa je wachambuzi wabobezi wanasema nini kuhusu falsafa ya Ombaomba?



Kila mtu anaelewa kuwa omba omba huwa haheshimiwi.

Hata wale waungwana ambao kwao ni kawaida kutoa sadaka kila mara, huwa hawawaheshimu ombaomba. Ombaomba hawaheshimiki kwa sababu moja tu, kwamba wanaishi kwa kutegemea fadhila za watu wengine.


Hali inakuwa mbaya zaidi inapokuwa ombaomba anaonekana ni mtu anayeweza kufanya kazi na kujipatia kipato, lakini hafanyi kazi kwa sababu anaona kazi ni ngumu zaidi kuliko kuzurura akikinga bakuli.

Wafadhili wanaotupa misaada wanatushangaa kama sisi wenyewe tunavyowashangaa ombaomba wanaoonekana kuwa na viungo na akili timamu. Rasilimali tulizojaliwa kuwa nazo zinatosha kabisa kutuwezesha kujitegemea iwapo tungezitumia vizuri.

Badala yake tunaona ni rahisi zaidi kuwaachia wageni wachukue rasilimali zetu waende kuzifanyia kazi za kuwanufaisha wao, halafu sisi tuletewe makombo kama misaada. Hapa kuna kitu kimetusibu katika uwezo wetu wa kufikiri, kama vile tumeingiliwa na ‘virus’ katika bongo zetu, na ndiyo maana tunafanya mambo ambayo hayaingii akilini.

Nimewahi kutoa mfano wa tumbili tunaowaona kandokando ya njia katika mbuga ya Mikumi. Wanatoka msituni ambako kuna matunda mengi na yenye ubora wa upya (kwa maana ya ‘fresh’) kuja kushinda barabarani wakisubiri watalii wawarushie maganda mabovu ya ndizi zilizonyauka.

Ndivyo tulivyo, na wahisani hawatuheshimu kwa sababu hatuheshimiki. Kila kitu tunataka tufanyiwe na wengine, hata pale ambapo ni dhahiri kwamba tunaweza kujifanyia sisi wenyewe.

Tuambizane ukweli. Ni kwamba wanatuona sisi ni sawa kabisa na nyani. Dharau waliyonayo kwetu inazidi pale tunapopewa ‘misaada’ kwa masharti fulani, na hayo masharti tunayakubali haraka haraka, lakini tukiisha kukabidhiwa ‘misaada’ hiyo tunayasahau yale masharti na kufanya tunavyotaka.

Suala la kuheshimu makubaliano tuliyoyatilia saini ni muhimu mno. Ndipo tunapata tofauti kati ya muungwana na mhuni. Mhuni atatia saini waraka wowote, (bila hata kuusoma) alimradi kuna kitu anakitaka sasa hivi, lakini katika dhamira yake hana nia ya kuheshimu chochote kilicho ndani ya waraka huo. Akiisha kupata anachohitaji, anaweza wala asiuangalie huo mkataba tena.

Muungwana huheshimu makubaliano aliyoingia na wenzake, na katika kila hatua za utekelezaji ataurejea mkataba huo mara kwa mara kuhakikisha haendi kinyume cha makubaliano. Huo ndio uungwana. Ukiisha kuvunja makubaliano yako na ‘mfadhili’ kwa kulipeleka gari la ‘msaada’ kule ulikokatazwa, unakuwa umejiweka mahali pa kukemewa na mama ambaye alikwisha kutuona kama watu wa hovyo.




Tulipopata uhuru tukaamua kujenga taifa moja kutokana na mipaka ya utumwa wetu, lakini tumefika katikati ya safari tumesahau tulikuwa tunakwenda wapi, na tunachofanya sasa ni kukimbia katika mduara tukifuata mikia yetu: Tulikotoka hatuko tena, na tulikokusudia kwenda hatukumbuki ni wapi. Sasa tunagawana mbao za mashua yetu.

Sasa tumekuwa kama watu waliotekwa kiakili ambao hawawezi kufurukuta katika jambo lolote. Kama hatuna hata lugha tunayoweza kuiita na kuifanya kuwa lugha ya taifa, hatuwezi kujiita taifa. Kuiita lugha ya taifa ni jambo rahisi; tulikwisha kufanya hivyo, na tumefanya hivyo kwa muda wa miongo mitano. Lakini si kweli kwamba Kiswahili ni lugha ya taifa. Ni kama vile ambavyo tumekuwa tukisema kwa miongo minne kwamba Dodoma ndio mji mkuu wa Tanzania wakati tukijua kwamba hilo nalo si kweli. Kila mtu anajua kwamba akitaka makao makuu ya serikali yafanye jambo fulani inabidi aende Dar es Salaam, na kama wahusika wako Dodoma kwa sababu ya kikao cha Bunge, atawasubiri warudi.

Ugumu wa kukubali ukweli katika hili, na hususan kwa watu wanaoiona lugha ya kigeni kama yenye hadhi ya utukufu kuliko lugha yao wenyewe umekuwapo kila mahali duniani. Lakini vile vile, inapotokea kwamba jamii inayojitambua kama taifa, hata kama ni taifa dogo, ikajihisi kwamba lugha yao inahujumiwa, jamii hiyo itachukua hatua za kupambana dhidi ya hujuma hizo, wakati mwingine kwa kumwaga damu.

Ikifikia hatua hiyo, jamii hiyo inakuwa na haki ya kujitambulisha kama taifa, na wakati mwingine utaifa huo unaweza ukawa hauna nchi, hauna ardhi ulipojisimika, lakini utaifa unadumu ndani ya nyoyo za watu wake, kokote kule waliko, hata kama wamesambaa na kutapakaa duniani kote.


Sisi hatuko hivyo.


By Jenerali Ulimwengu
Raiamwema Toleo 396
March 11, 2015

Daaa ipo sawasawa
 
Wakati rais Jakaya Mrisho Kikwete akikaribia kustaafu kwa kuwatumikia Watanzania kutoka pale ikulu ya magogoni, atakumbukwa kwa mambo mengi mazuri hususani kwa watu kutoka mikoani kuanzaia tarafani mpaka wilayani kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa kipindi chake chote cha miaka kumi tangu mwaka 2005 alipoingia madarakani mpaka sasa mwaka huu 2015 anapoondoka madarakani.

Miongoni mwa Sekta amabazo zimfanya rais Kikwete kukumbuka ni sekta ya miundo mbinu ambapo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne, Serikaliimepata mafanikio makubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara namadaraja nchini. Katika kipindi hicho, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa17,762 zimekuwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo barabara zenyeurefu wa jumla ya kilometa 5,568 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami.

Aidha, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 3,873 zinaendelea kujengwakwa kiwango cha lami, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 4,965 zimefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na Serikali inatafuta fedha za kuzijenga kwa kiwango cha lami. Vilevile, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zenye jumla ya kilometa 3,356 unaendelea.

Pia serikali ya rais Jakaya Kikwete itkumbukwa kwa ujenzi ujenzi na ukarabati wa madaraja, hakuna asiyejua kuwa miaka ya nyuma ilikuwa ikifika wakati wa masika kuna wilaya mbali mbali zilikuwa zinakosa mawasiliano na mikoa pmoja na miji mikubwa mpaka hali ya mvua zinapopungu hali hii ilikuwa inawakera sana wananchi kwa kuwa shughuli nyingi za maendelo zilikuwa zinasimama.

Serikali ya awamu ya nne ililiona hilo na ikadiliki kulivali njuga kwa fedha zetu za ndani bila kusubiri wafadhili, katika hili hta kama wapinzani watapinga lakini wanancjhi wanajua ukweli wa hili n hata kama utafunga safari uende katika maeneo ambayo yalikuwa na tata katika madaraja utapa majibu yake. Tumeshudia jumla ya madaraja makubwa 30 yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Kati ya hayo, madaraja makubwa 12 yamekamilika kujengwa, ambayo ni Rusumo (Kagera), Umoja (Mtwara), Mwanhuzi (Simiyu), Kikwete (Kigoma), Nangoo (Mtwara), Ruhekei (Ruvuma), Mbutu (Tabora), Mwatisi (Morogoro), Ruvu (Pwani), Nanganga (Mtwara), Maligisu (Mwanza) na daraja la waenda kwa miguula Mabatini (Mwanza).

Aidha, madaraja makubwa 6 yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi, ambayo ni Kigamboni (Dsm), Kilombero (Morogoro), Kavuu (Katavi), Sibiti (Singida), Ruvu Chini (Pwani) na Lukuledi II (Mtwara). Madaraja makubwa 12 yako kwenye maandalizi ya kujengwa ambayo ni Momba (mpakani mwa Rukwa na Mbeya), Mwiti (Mtwara), Simiyu (Mwanza), Wami (Pwani), Ruhuhu (Ruvuma), Ubungo Interchange (Dar es Salaam), TAZARA Flover (Dar es Salaam), Selander (Dar es Salaam), Daraja jipya la Wami Chini (Pwani), Pangani (Tanga), Kirumi (Mara) na daraja la waenda kwa miguu la Furahisha (Mwanza).

Sambamba na ujenzi wa madaraja makubwa, madaraja madogo madogo zaidi ya 7,200 yamejengwa na kukamilika. katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 Serikali pia imeimarisha Mfuko wa Barabara ambapo mapato ya Mfuko yameongezeka kutoka Shilingi bilioni 73.08 katika mwaka wa fedha 2005/06 hadi Shilingi bilioni 751.7 katika mwaka wa fedha 2014/15 ikiwa ni ongezeko la asilimia 928.6. ni ajabu sana pale kina Mbowe, Lipumba pamoja na Mbatia wanavyojifanya vipofu katika mafaniko haya ya awamu ya nne ambayo tangu uhuru yalikuwa kero kubwa kwa wananchi.

wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani mwaka 2005, vivuko vya Serikali vilivyokuwa vinatoa huduma vilikuwa kumi na tano (15) tu. Hadi kufikia Aprili, 2015, idadi ya vivuko vya Serikali vinavyotoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini imeongezeka na kufikia ishirini na nane (28).

kwa upande wa nyumba na majengo ya Serikali, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ilijenga nyumba 173 za makazi ya Viongozi wa Umma na kuanza mradi wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi wa Umma ambapo nyumba 643 zilikamilika katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 na nyumba 270 zinaendelea kujengwa.

Aidha,Serikali kupitia TBA imeendelea kuhakikisha kwamba ujenzi wa nyumba na majengo yanayotumiwa na umma unazingatia mahitaji maalum hususan kwa watu wenye ulemavu. Suala hili limeendelea kutekelezwa kupitia miradi ya ujenzi wa majengo yote ya Serikali ambayo Wakala wa Majengo umesanifu na kusimamia kama ifuatavyo: Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara, Majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Bariadi, Rorya, Kilolo, Nyamagana na Mvomero. Mengine ni jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi – Kitengo cha Wakimbizi,

Jengo la hospitali ya Manyara na ukumbi wa mikutano na Vituo vya Afya ya Msingi (Primary Health Centre Institutions – PHCI) – Iringa, majengo ya Ofisi za Wakuu 6 wa Mikoa ya Katavi, Njombe, Geita na Simiyu pamoja na majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya 19 za Buhigwe, Busega, Butiama, Chemba, Gairo, Ikungi, Itilima, Kalambo, Kaliua, Kakonko, Kyerwa, Mbogwe, Mkalama, Mlele, Momba Nyang`hwale, Nyasa, Uvinza na Wanging’ombe.

Katika mwaka wa fedha 2014/15, wakati ambao serikali ya awamu ya imeendelea na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Wizara ya ujenzi inaendelea vizuri. Kwa upande wa barabara kuu, jumla ya kilometa 504.4 kati ya kilometa 539zilizopangwa kujengwa kwa kiwango cha lami zilikuwa zimekamilika hadi kufikia Aprili, 2015. Na kilometa 87.75 zilikua zimekarabatiwa kwa kiwango cha lami. Kwa upande wa barabara za mikoa, kilometa 40.5 zilijengwa kwa kiwango cha lami. Vile vile, kilometa 450 zilifanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe katika kipindi hicho.

Wakati ris Jakaya akiwa anasubiri muda wake ufike akapumzike hataliacha hivi suala la msongamano mkubwa wa magari katika Jiji la Dar es salaam, serikali yake kupitia Wizara ya ujenzi na Mamlaka mbalimbali zikiwemo Halmashauri za Jiji zimechukuliwa hatua mbalimbli za kukabiliana na tatizo hilo la msongamano wa magari. Tayari maandalizi ya ujenzi barabara ya njia sita ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (km 200) sehemu ya Dar es Salaam –Chalinze (km 100) imepangwa kujengwa kwa kiwango cha “Expressway”.

Maandalizi ya mradi huu utakaotekelezwa kwa utaratibu wa ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi (Public Private Partnership - PPP) yamekamilika na yameanza kufanyiwaAprili, 2015, Mshauri Mwelekezi (Transaction Advisor) ambaye ni Kampuni ya Cheil Engineering Company Limited kutoka Korea ya Kusini alikwishateuliwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 7.72 na amekamilisha utafiti wa mwelekeo wabarabara (route survey).

Mwelekeo wa barabara uliochaguliwa unaanzia Charambe katika barabara ya Kilwa kupitia Kisarawe, Kibamba, Kibaha, Mlandizi hadi Chalinze.

Barabara itakuwa na urefu wa kilometa 128 itakuwa ya njia sita (6) na barabara za juu (interchanges) tano (5) katika maeneo ya Charambe, Kisarawe, Kibamba, Mlandizi na Chalinze. Pia itakuwa na vituo vikuu viwili (2) vya kulipia tozo ya barabara (Toll Plaza) maeneo ya Charambe na Chalinze.


Pia barabara hii itakuwa na eneo la kupumzika (rest station) pale Visiga na maeneo mawili (2) ya kuegesha malori ambayo yatakuwa Mbezi na Mbala.

Vilevile Mshauri Mwelekezi atafanya utafiti wa jinsi ya kuunganisha barabara hii kutoka Charambe hadi bandari ya Dar es Salaam. Kwa sasa Mshauri Mwelekezia naendelea na kazi ya kuandaa nyaraka za zabuni na baadaye atasimamia taratibu za kumpata Mbia/Mwekezaji (Concessionaire) wa mradi huu. Gharama za mradi huu wa ujenzi zinakadiriwa kufikia Shilingi Trilioni 2.397 na utatekelezwa kwa njia ya Ubia na Sekta Binafsi (PPP).


Tunajua pia kuwa huwezi kuondoa Msongamano wa magari ya jiji Dar ers Salaam bila kulitaka Daraja la Selander, Rais Jakaya Kikwete anaondoka magogoni akiwa keshalipati ufumbuzi wa kudumu eneo hilo la selander, Serikali ya Korea Kusini imekubali kuipatia Serikali ya Tanzania mkopo wamasharti nafuu kwa ajili ya ujenzi wa Daraja jipya la Selander. Upembuzi yakinifu wa mradi huu umekamilika na maandalizi ya kutiliana saini makubaliano ya mkopo wa kugharamia ujenzi wa daraja kati ya Korea Exim Bank (kwa niaba yaSerikali ya Korea Kusini) na Serikali ya Tanzania yanaendelea.

Daraja hili pamoja na barabara zake za maingilio litakuwa na urefu wa jumla ya kilometa 7.2 na litaanzia eneo la Koko Beach kupitia Kenyatta Drive na kuingia baharini na kisha kuungana na barabara ya Barack Obama eneo la Hospitali ya Aghakan. Mradi huu tagharimu Shilingi Bilioni 197.5. Aidha, Daraja la Kigamboni linaendelea kujengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 236.524.

Ujenzi wa barabara za juu (flyovers na interchanges) na maboresho ya makutano ya barabara katika jiji la Dares Salaam,mpkaAprili, 2015 hali utekelezaji upo kama ifuatavyo kama ifuatavyo: Barabara ya Juu (Flyover) ya TAZARA: Usanifu wa kina umekamilika chini ya ufadhili wa Serikali ya Japan. Taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi atakayekidhi vigezo zinaendelea huko Japan.

Kazi ya ujenzi wa Flyover ya TAZARA ambayo itagharamiwa na Serikali ya Japan ikishirikiana na Serikali ya Tanzania inatarajiwa kuanza katika ya mwaka, 2015. Gharama za mradi huu ni Shilingi Bilioni 93.622. Interchange ya Ubungo Benki ya Dunia imekubali kugharamia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Interchange) katika makutano ya Ubungo. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Interchange ya Ubungo umekamilika. Zabuni ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya usimamizi wa ujenzi zimetangazwa. Serikali inakamilisha taratibu kwa ajili ya kutangaza zabuni za kumtafuta Mkandarasi wa ujenzi.

Vile vile Interchange ya Ubungo itakuwa na levels tatu ambapo magari yanayotoka katikati ya jiji la Dar es Salaam kuelekea Morogoro yatapita chini, magari yanayotoka TAZARA kuelekea Mwenge yatapita juu na magari yanayokata kulia yatapita katikati. Gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa Shilingi Bilioni 126.661. Upanuzi wa barabara ya Gerezani (Bendera Tatu – KAMATA) unakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 29.135. serikali inaendelea na maandalizi ya Maboresho ya Makutano ya Chang'ombe, Magomeni, Mwenge, Tabata, KAMATA, Uhasibu na Morocco yanaendelea.


Serikali ya Kikwete imeendelea kutekeleza miradi ya barabara za kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam zenye urefu wa kilometa 109.35. Barabara hizo ni pamoja na Ubungo Bus Terminal – Mabibo – Kigogo Roundabout (km 6.4); Kigogo Roundabout – Bonde la Msimbazi – Twiga/Msimbazi Jct (km 2.7); Jet Corner – Vituka – Devis Corner (km 10.30); Tabata Dampo – Kigogo (km 1.60); Ubungo Maziwa – External (km 0.65); Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi –Banana (km 14); Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi Mwisho (km 20); Tangi Bovu – Goba (km 9); Kimara Baruti–Msewe (km 2.6); Kimara –Kilungule – External Mandela Road (km 9); na Kibamba – Kisopwa (km 12.0). Pia ukarabati unaoendelea katika barabara za Ukonga – Mombasa –Msongola , Kimbiji – Tundwisongani, Misheni – Kijichi – Zakhem, barabara ya Uhuru, Kutengeneza Mifereji ya Maji, uhamishaji miundombinu maeneo ya miradi, malipo ya fidia, n.k. vyote vinakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 181.795.

Pia Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure – BRT) ambao unajumuisha Ujenzi wa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kivukoni, barabara ya Kawawa kutoka Magomeni hadi Morocco na barabara ya Msimbazi kutoka Fire hadi Kariakoo zenye jumla ya urefu wa kilometa 20.9. Pia kuna vituo vya mabasi 29, vituo vikubwa vitatu namadaraja ya waenda kwa miguu matatu. Pia Ujenzi wa Karakana (Depot) na Kituo cha Mabasi cha Ubungo; Ujenzi wa Karakana (Depot) ya Jangwani; Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi (Terminal) cha Kivukoni; vyote hivyo mchakato wake unaendelea kwa hatua mbali mbali, kwa m,tu ambaye anayeishi mikoani akija nleo Dar es Salaam maeneo ya katikati ya mji atashangaa kasi ya ejenzi inavyoendelea leo.

Pamoja na juhudi kubwa hizo za serikali ya awamu ya nne lakini bado wapinzani wamekuwa wakibeza kuwa miradi mingi haitekwelezi napenda kuwapa changamoto moja wawe wakweli kutoka mioyoni mwao waangali hali ya barabara zetu leo ni sawa na miaka kumi iliyopita

Bado hatujasahu ndugu zetu walivyokuwa wakiliwa na simba njia ya kusini ambapo leo unapamba basi kwenda mtwara kutoka dar es Salaam kwenda mtwara unafika safari yako ndani ya masaa tisa, pia tunakumbuka wakazi wa kanda ya ziwa walivyokuwa wakiteseka kulala njiani mpaka kwa siku tatu wakati leo wanafika ndani ya siku moja.

Hatujasahau ndugu zetu wa Kagera walikuwa wanalazimika kutumia mpaka siku tano kupitia Kenya na Uganda kufika mkoani, kwao hali ni tofauti na sasa ile hali ya kushuka mipakani na kugonga visa hakuna tena na gharama za usafiri na matumizi za kupitia Kenya na Uganda hazipo tena. Haya yaliwezekanaje ndani miaka 10 ya jakaya kikwete na yashindikane hayo mengine, rais Jakaya anamuachia vema rais ajaye kwenye sekta ya miundo mbinu, ambayo ni miongoni mwa kero kubwa tangu uhuru kwa watanzania.

Kwa wale wanaosema rais Jakaya Kikwete hana lolote alilowafanyia watanzania ningependa kuwaasa jambo moja kuwa wanachofanya ni kujidanganya kwani watanzania wanajua mengi na yanaonekana kwa macho.

Vile vile niwaambie wabunge wa upinzani walikuwa wakibeza miradi ya wizara ya ujenzi ya miundo mbinu kuwa miradi hiyo niliyoitaja hapo juu kuwa haitekelezeki napenda kuwaambia hata huu mtandao wa barabara nchini walikuwa wakiubeza lakini leo wapo kimya hawana la kusema. Kwa wale wanaopinga ningewashauri wafunge safari siku moja ya kuzunguuka nchi yetu kwa njia ya barabara watajionea wenyewe, kwanza wangeanza safari Arusha kwenda Singida kupitia Manyara.

Halafu angewauliza wanaotoka Dodoma kwenda Iringa kupitia mtera, halafu nenda njia ya Manyoni hadi kigoma kupitia Tabora, na kwa wakazi wa kusini akawaulize wanaotoka Masasi kwenda Songea kupitia Tunduru. Pia aangalie safari ya kutoka Songea kwenda mpaka Sumbawaga.

Kwa wakazi wa kanda ya ziwa angalie Safari ya kutoka Manyoni kwenda Mwanza kupitia Singida mjini, Nzega, Shinyanga mpaka Mwanza yenyewe. Halafua anzia Shinyanga kwenda Bukoba. Rudi tena anzia Dar es Salaam kwenda Lindi na Mtwara.

Nani asiyejua kuwa miaka kumi iliyopita kwa makazi wa Dar es Salam mwenye asili ya ya mikoa ya Lindi, Mtwara, Kigoma,Rukwa, Simiyu, Geita, Ruvuma na Katazi wakipata misiba kufika kwao ilikuwa shughuli pevu kufika makwao.

Mwisho napenda kumpongeza mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya wizara ya fedha 2014/2015 kwa mara ya kwanza nimemshuhudia akiuunga mkono bajeti kwa kusema wakati anaingia madarakani miaka 4, iliyopita katika jimbo lake kulikuwa na vijiji vitatu tu vyenye umeme katika vijiji 60 kwa sasa jimbo Ludewa ina vijiji 50 vyenye umeme na vingine vitapata umeme kabla ya rais Kikwete kuondoka madarakani, filikunjombe anasema wakati anaingia madarakani kulikuwa hakuna lami lakini kwa sasa kuna kilometer 50 za lami kati ya kilometer `200 za barabara katika jimbo lote la Ludewa na zinaendea kujengwa.

Filikunjombe amesema kuwa kama atapinga mfanikio ya awamu ya nne basi hata wananchi wake watamkataa, alifika mbali zaidi mpaka kutaja idadi ya madaraja tata ambayo yalikuwa yanawasumbua kipindi cha masika lakini kwa sasa yanapitika msimu wote. Napenda kumalizia kwa kumtakia mapumziko mema na afya tele kwa rais waetu Jakaya pale muda wake wa kustaafu utakapofika.

Dah wewe ni muungwana sana mpaka umeyaona hayo yote.
 
Wakati rais Jakaya Mrisho Kikwete akikaribia kustaafu kwa kuwatumikia Watanzania kutoka pale ikulu ya magogoni, atakumbukwa kwa mambo mengi mazuri hususani kwa watu kutoka mikoani kuanzaia tarafani mpaka wilayani kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa kipindi chake chote cha miaka kumi tangu mwaka 2005 alipoingia madarakani mpaka sasa mwaka huu 2015 anapoondoka madarakani.

Miongoni mwa Sekta amabazo zimfanya rais Kikwete kukumbuka ni sekta ya miundo mbinu ambapo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne, Serikaliimepata mafanikio makubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara namadaraja nchini. Katika kipindi hicho, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa17,762 zimekuwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo barabara zenyeurefu wa jumla ya kilometa 5,568 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami.

Aidha, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 3,873 zinaendelea kujengwakwa kiwango cha lami, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 4,965 zimefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na Serikali inatafuta fedha za kuzijenga kwa kiwango cha lami. Vilevile, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zenye jumla ya kilometa 3,356 unaendelea.

Pia serikali ya rais Jakaya Kikwete itkumbukwa kwa ujenzi ujenzi na ukarabati wa madaraja, hakuna asiyejua kuwa miaka ya nyuma ilikuwa ikifika wakati wa masika kuna wilaya mbali mbali zilikuwa zinakosa mawasiliano na mikoa pmoja na miji mikubwa mpaka hali ya mvua zinapopungu hali hii ilikuwa inawakera sana wananchi kwa kuwa shughuli nyingi za maendelo zilikuwa zinasimama.

Serikali ya awamu ya nne ililiona hilo na ikadiliki kulivali njuga kwa fedha zetu za ndani bila kusubiri wafadhili, katika hili hta kama wapinzani watapinga lakini wanancjhi wanajua ukweli wa hili n hata kama utafunga safari uende katika maeneo ambayo yalikuwa na tata katika madaraja utapa majibu yake. Tumeshudia jumla ya madaraja makubwa 30 yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Kati ya hayo, madaraja makubwa 12 yamekamilika kujengwa, ambayo ni Rusumo (Kagera), Umoja (Mtwara), Mwanhuzi (Simiyu), Kikwete (Kigoma), Nangoo (Mtwara), Ruhekei (Ruvuma), Mbutu (Tabora), Mwatisi (Morogoro), Ruvu (Pwani), Nanganga (Mtwara), Maligisu (Mwanza) na daraja la waenda kwa miguula Mabatini (Mwanza).

Aidha, madaraja makubwa 6 yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi, ambayo ni Kigamboni (Dsm), Kilombero (Morogoro), Kavuu (Katavi), Sibiti (Singida), Ruvu Chini (Pwani) na Lukuledi II (Mtwara). Madaraja makubwa 12 yako kwenye maandalizi ya kujengwa ambayo ni Momba (mpakani mwa Rukwa na Mbeya), Mwiti (Mtwara), Simiyu (Mwanza), Wami (Pwani), Ruhuhu (Ruvuma), Ubungo Interchange (Dar es Salaam), TAZARA Flover (Dar es Salaam), Selander (Dar es Salaam), Daraja jipya la Wami Chini (Pwani), Pangani (Tanga), Kirumi (Mara) na daraja la waenda kwa miguu la Furahisha (Mwanza).

Sambamba na ujenzi wa madaraja makubwa, madaraja madogo madogo zaidi ya 7,200 yamejengwa na kukamilika. katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 Serikali pia imeimarisha Mfuko wa Barabara ambapo mapato ya Mfuko yameongezeka kutoka Shilingi bilioni 73.08 katika mwaka wa fedha 2005/06 hadi Shilingi bilioni 751.7 katika mwaka wa fedha 2014/15 ikiwa ni ongezeko la asilimia 928.6. ni ajabu sana pale kina Mbowe, Lipumba pamoja na Mbatia wanavyojifanya vipofu katika mafaniko haya ya awamu ya nne ambayo tangu uhuru yalikuwa kero kubwa kwa wananchi.

wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani mwaka 2005, vivuko vya Serikali vilivyokuwa vinatoa huduma vilikuwa kumi na tano (15) tu. Hadi kufikia Aprili, 2015, idadi ya vivuko vya Serikali vinavyotoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini imeongezeka na kufikia ishirini na nane (28).

kwa upande wa nyumba na majengo ya Serikali, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ilijenga nyumba 173 za makazi ya Viongozi wa Umma na kuanza mradi wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi wa Umma ambapo nyumba 643 zilikamilika katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 na nyumba 270 zinaendelea kujengwa.

Aidha,Serikali kupitia TBA imeendelea kuhakikisha kwamba ujenzi wa nyumba na majengo yanayotumiwa na umma unazingatia mahitaji maalum hususan kwa watu wenye ulemavu. Suala hili limeendelea kutekelezwa kupitia miradi ya ujenzi wa majengo yote ya Serikali ambayo Wakala wa Majengo umesanifu na kusimamia kama ifuatavyo: Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara, Majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Bariadi, Rorya, Kilolo, Nyamagana na Mvomero. Mengine ni jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi – Kitengo cha Wakimbizi,

Jengo la hospitali ya Manyara na ukumbi wa mikutano na Vituo vya Afya ya Msingi (Primary Health Centre Institutions – PHCI) – Iringa, majengo ya Ofisi za Wakuu 6 wa Mikoa ya Katavi, Njombe, Geita na Simiyu pamoja na majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya 19 za Buhigwe, Busega, Butiama, Chemba, Gairo, Ikungi, Itilima, Kalambo, Kaliua, Kakonko, Kyerwa, Mbogwe, Mkalama, Mlele, Momba Nyang`hwale, Nyasa, Uvinza na Wanging’ombe.

Katika mwaka wa fedha 2014/15, wakati ambao serikali ya awamu ya imeendelea na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Wizara ya ujenzi inaendelea vizuri. Kwa upande wa barabara kuu, jumla ya kilometa 504.4 kati ya kilometa 539zilizopangwa kujengwa kwa kiwango cha lami zilikuwa zimekamilika hadi kufikia Aprili, 2015. Na kilometa 87.75 zilikua zimekarabatiwa kwa kiwango cha lami. Kwa upande wa barabara za mikoa, kilometa 40.5 zilijengwa kwa kiwango cha lami. Vile vile, kilometa 450 zilifanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe katika kipindi hicho.

Wakati ris Jakaya akiwa anasubiri muda wake ufike akapumzike hataliacha hivi suala la msongamano mkubwa wa magari katika Jiji la Dar es salaam, serikali yake kupitia Wizara ya ujenzi na Mamlaka mbalimbali zikiwemo Halmashauri za Jiji zimechukuliwa hatua mbalimbli za kukabiliana na tatizo hilo la msongamano wa magari. Tayari maandalizi ya ujenzi barabara ya njia sita ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (km 200) sehemu ya Dar es Salaam –Chalinze (km 100) imepangwa kujengwa kwa kiwango cha “Expressway”.

Maandalizi ya mradi huu utakaotekelezwa kwa utaratibu wa ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi (Public Private Partnership - PPP) yamekamilika na yameanza kufanyiwaAprili, 2015, Mshauri Mwelekezi (Transaction Advisor) ambaye ni Kampuni ya Cheil Engineering Company Limited kutoka Korea ya Kusini alikwishateuliwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 7.72 na amekamilisha utafiti wa mwelekeo wabarabara (route survey).

Mwelekeo wa barabara uliochaguliwa unaanzia Charambe katika barabara ya Kilwa kupitia Kisarawe, Kibamba, Kibaha, Mlandizi hadi Chalinze.

Barabara itakuwa na urefu wa kilometa 128 itakuwa ya njia sita (6) na barabara za juu (interchanges) tano (5) katika maeneo ya Charambe, Kisarawe, Kibamba, Mlandizi na Chalinze. Pia itakuwa na vituo vikuu viwili (2) vya kulipia tozo ya barabara (Toll Plaza) maeneo ya Charambe na Chalinze.


Pia barabara hii itakuwa na eneo la kupumzika (rest station) pale Visiga na maeneo mawili (2) ya kuegesha malori ambayo yatakuwa Mbezi na Mbala.

Vilevile Mshauri Mwelekezi atafanya utafiti wa jinsi ya kuunganisha barabara hii kutoka Charambe hadi bandari ya Dar es Salaam. Kwa sasa Mshauri Mwelekezia naendelea na kazi ya kuandaa nyaraka za zabuni na baadaye atasimamia taratibu za kumpata Mbia/Mwekezaji (Concessionaire) wa mradi huu. Gharama za mradi huu wa ujenzi zinakadiriwa kufikia Shilingi Trilioni 2.397 na utatekelezwa kwa njia ya Ubia na Sekta Binafsi (PPP).


Tunajua pia kuwa huwezi kuondoa Msongamano wa magari ya jiji Dar ers Salaam bila kulitaka Daraja la Selander, Rais Jakaya Kikwete anaondoka magogoni akiwa keshalipati ufumbuzi wa kudumu eneo hilo la selander, Serikali ya Korea Kusini imekubali kuipatia Serikali ya Tanzania mkopo wamasharti nafuu kwa ajili ya ujenzi wa Daraja jipya la Selander. Upembuzi yakinifu wa mradi huu umekamilika na maandalizi ya kutiliana saini makubaliano ya mkopo wa kugharamia ujenzi wa daraja kati ya Korea Exim Bank (kwa niaba yaSerikali ya Korea Kusini) na Serikali ya Tanzania yanaendelea.

Daraja hili pamoja na barabara zake za maingilio litakuwa na urefu wa jumla ya kilometa 7.2 na litaanzia eneo la Koko Beach kupitia Kenyatta Drive na kuingia baharini na kisha kuungana na barabara ya Barack Obama eneo la Hospitali ya Aghakan. Mradi huu tagharimu Shilingi Bilioni 197.5. Aidha, Daraja la Kigamboni linaendelea kujengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 236.524.

Ujenzi wa barabara za juu (flyovers na interchanges) na maboresho ya makutano ya barabara katika jiji la Dares Salaam,mpkaAprili, 2015 hali utekelezaji upo kama ifuatavyo kama ifuatavyo: Barabara ya Juu (Flyover) ya TAZARA: Usanifu wa kina umekamilika chini ya ufadhili wa Serikali ya Japan. Taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi atakayekidhi vigezo zinaendelea huko Japan.

Kazi ya ujenzi wa Flyover ya TAZARA ambayo itagharamiwa na Serikali ya Japan ikishirikiana na Serikali ya Tanzania inatarajiwa kuanza katika ya mwaka, 2015. Gharama za mradi huu ni Shilingi Bilioni 93.622. Interchange ya Ubungo Benki ya Dunia imekubali kugharamia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Interchange) katika makutano ya Ubungo. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Interchange ya Ubungo umekamilika. Zabuni ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya usimamizi wa ujenzi zimetangazwa. Serikali inakamilisha taratibu kwa ajili ya kutangaza zabuni za kumtafuta Mkandarasi wa ujenzi.

Vile vile Interchange ya Ubungo itakuwa na levels tatu ambapo magari yanayotoka katikati ya jiji la Dar es Salaam kuelekea Morogoro yatapita chini, magari yanayotoka TAZARA kuelekea Mwenge yatapita juu na magari yanayokata kulia yatapita katikati. Gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa Shilingi Bilioni 126.661. Upanuzi wa barabara ya Gerezani (Bendera Tatu – KAMATA) unakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 29.135. serikali inaendelea na maandalizi ya Maboresho ya Makutano ya Chang'ombe, Magomeni, Mwenge, Tabata, KAMATA, Uhasibu na Morocco yanaendelea.


Serikali ya Kikwete imeendelea kutekeleza miradi ya barabara za kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam zenye urefu wa kilometa 109.35. Barabara hizo ni pamoja na Ubungo Bus Terminal – Mabibo – Kigogo Roundabout (km 6.4); Kigogo Roundabout – Bonde la Msimbazi – Twiga/Msimbazi Jct (km 2.7); Jet Corner – Vituka – Devis Corner (km 10.30); Tabata Dampo – Kigogo (km 1.60); Ubungo Maziwa – External (km 0.65); Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi –Banana (km 14); Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi Mwisho (km 20); Tangi Bovu – Goba (km 9); Kimara Baruti–Msewe (km 2.6); Kimara –Kilungule – External Mandela Road (km 9); na Kibamba – Kisopwa (km 12.0). Pia ukarabati unaoendelea katika barabara za Ukonga – Mombasa –Msongola , Kimbiji – Tundwisongani, Misheni – Kijichi – Zakhem, barabara ya Uhuru, Kutengeneza Mifereji ya Maji, uhamishaji miundombinu maeneo ya miradi, malipo ya fidia, n.k. vyote vinakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 181.795.

Pia Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure – BRT) ambao unajumuisha Ujenzi wa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kivukoni, barabara ya Kawawa kutoka Magomeni hadi Morocco na barabara ya Msimbazi kutoka Fire hadi Kariakoo zenye jumla ya urefu wa kilometa 20.9. Pia kuna vituo vya mabasi 29, vituo vikubwa vitatu namadaraja ya waenda kwa miguu matatu. Pia Ujenzi wa Karakana (Depot) na Kituo cha Mabasi cha Ubungo; Ujenzi wa Karakana (Depot) ya Jangwani; Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi (Terminal) cha Kivukoni; vyote hivyo mchakato wake unaendelea kwa hatua mbali mbali, kwa m,tu ambaye anayeishi mikoani akija nleo Dar es Salaam maeneo ya katikati ya mji atashangaa kasi ya ejenzi inavyoendelea leo.

Pamoja na juhudi kubwa hizo za serikali ya awamu ya nne lakini bado wapinzani wamekuwa wakibeza kuwa miradi mingi haitekwelezi napenda kuwapa changamoto moja wawe wakweli kutoka mioyoni mwao waangali hali ya barabara zetu leo ni sawa na miaka kumi iliyopita

Bado hatujasahu ndugu zetu walivyokuwa wakiliwa na simba njia ya kusini ambapo leo unapamba basi kwenda mtwara kutoka dar es Salaam kwenda mtwara unafika safari yako ndani ya masaa tisa, pia tunakumbuka wakazi wa kanda ya ziwa walivyokuwa wakiteseka kulala njiani mpaka kwa siku tatu wakati leo wanafika ndani ya siku moja.

Hatujasahau ndugu zetu wa Kagera walikuwa wanalazimika kutumia mpaka siku tano kupitia Kenya na Uganda kufika mkoani, kwao hali ni tofauti na sasa ile hali ya kushuka mipakani na kugonga visa hakuna tena na gharama za usafiri na matumizi za kupitia Kenya na Uganda hazipo tena. Haya yaliwezekanaje ndani miaka 10 ya jakaya kikwete na yashindikane hayo mengine, rais Jakaya anamuachia vema rais ajaye kwenye sekta ya miundo mbinu, ambayo ni miongoni mwa kero kubwa tangu uhuru kwa watanzania.

Kwa wale wanaosema rais Jakaya Kikwete hana lolote alilowafanyia watanzania ningependa kuwaasa jambo moja kuwa wanachofanya ni kujidanganya kwani watanzania wanajua mengi na yanaonekana kwa macho.

Vile vile niwaambie wabunge wa upinzani walikuwa wakibeza miradi ya wizara ya ujenzi ya miundo mbinu kuwa miradi hiyo niliyoitaja hapo juu kuwa haitekelezeki napenda kuwaambia hata huu mtandao wa barabara nchini walikuwa wakiubeza lakini leo wapo kimya hawana la kusema. Kwa wale wanaopinga ningewashauri wafunge safari siku moja ya kuzunguuka nchi yetu kwa njia ya barabara watajionea wenyewe, kwanza wangeanza safari Arusha kwenda Singida kupitia Manyara.

Halafu angewauliza wanaotoka Dodoma kwenda Iringa kupitia mtera, halafu nenda njia ya Manyoni hadi kigoma kupitia Tabora, na kwa wakazi wa kusini akawaulize wanaotoka Masasi kwenda Songea kupitia Tunduru. Pia aangalie safari ya kutoka Songea kwenda mpaka Sumbawaga.

Kwa wakazi wa kanda ya ziwa angalie Safari ya kutoka Manyoni kwenda Mwanza kupitia Singida mjini, Nzega, Shinyanga mpaka Mwanza yenyewe. Halafua anzia Shinyanga kwenda Bukoba. Rudi tena anzia Dar es Salaam kwenda Lindi na Mtwara.

Nani asiyejua kuwa miaka kumi iliyopita kwa makazi wa Dar es Salam mwenye asili ya ya mikoa ya Lindi, Mtwara, Kigoma,Rukwa, Simiyu, Geita, Ruvuma na Katazi wakipata misiba kufika kwao ilikuwa shughuli pevu kufika makwao.

Mwisho napenda kumpongeza mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya wizara ya fedha 2014/2015 kwa mara ya kwanza nimemshuhudia akiuunga mkono bajeti kwa kusema wakati anaingia madarakani miaka 4, iliyopita katika jimbo lake kulikuwa na vijiji vitatu tu vyenye umeme katika vijiji 60 kwa sasa jimbo Ludewa ina vijiji 50 vyenye umeme na vingine vitapata umeme kabla ya rais Kikwete kuondoka madarakani, filikunjombe anasema wakati anaingia madarakani kulikuwa hakuna lami lakini kwa sasa kuna kilometer 50 za lami kati ya kilometer `200 za barabara katika jimbo lote la Ludewa na zinaendea kujengwa.

Filikunjombe amesema kuwa kama atapinga mfanikio ya awamu ya nne basi hata wananchi wake watamkataa, alifika mbali zaidi mpaka kutaja idadi ya madaraja tata ambayo yalikuwa yanawasumbua kipindi cha masika lakini kwa sasa yanapitika msimu wote. Napenda kumalizia kwa kumtakia mapumziko mema na afya tele kwa rais waetu Jakaya pale muda wake wa kustaafu utakapofika.

Dah wewe ni muungwana sana mpaka umeyaona hayo yote.
 
Hatutaki kusikia upuunzi wa ccm tena. Kazi waliyofanya haijafika hata 70% ya targets waliotakiwa wafikie, sasa tuipongeze kwa lipi!? Wao wasubiri tuwapunzishe october
 
juzi nilienda hospitali....nikambiwa nikanunue dawa......hivi hayo mafanikio ni kwetu sis wananchi au voongoz wa ccm???
 
mkulima wa kiteto we umevurugwa hahaha kibaya mjini tu mnatumia maji ya chumvi tena yana matope bado unaona mafanikio??
 
Hatutaki kusikia upuunzi wa ccm tena. Kazi waliyofanya haijafika hata 70% ya targets waliotakiwa wafikie, sasa tuipongeze kwa lipi!? Wao wasubiri tuwapunzishe october

sio70% hata 30% hawajafikia
 
Haya mambo yakutulazimisha kukubali kile munachotaka Huwa munanikera sana,Kwanini munalazimisha kuwa JK kafanya mambo makubwa na musiache wananchi wenyewe waseme, Mbona mtu ukifanya jambo jema wala huhitaji kupiga mbiu, wananchi wanaona........ Juzi tu nilikuwa uswahilini kwangu nanunua chips nikakuta mjadala sijui ulianzia Wapi Ila nilisikia wakimsifia Ben kuwa katika utawala wake walikuwa chips mayai kwa shilingi 500 mpk Jamaa anaondoka madarakani,Ila tangu aingie muheshimiwa sana......hah!

Ni kweli mkuu,umetoa hoja ya msingi sana,MAISHA YA WATANZANIA YANAZIDI KUWA MAGUMU HALAFU CCM WANATULAZIMISHA KUAMINI UONGO WAO.
 
Hawa ndio vibaraka wa CCM wanaogaiwa elfu 7 kila mmoja. HATUDANGANYIKI,KURA YETU NI KWA LOWASSA WA CHADEMA,UKAWA.
 
Wakati rais Jakaya Mrisho Kikwete akikaribia kustaafu kwa kuwatumikia Watanzania kutoka pale ikulu ya magogoni, atakumbukwa kwa mambo mengi mazuri hususani kwa watu kutoka mikoani kuanzaia tarafani mpaka wilayani kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa kipindi chake chote cha miaka kumi tangu mwaka 2005 alipoingia madarakani mpaka sasa mwaka huu 2015 anapoondoka madarakani.

Miongoni mwa Sekta amabazo zimfanya rais Kikwete kukumbuka ni sekta ya miundo mbinu ambapo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne, Serikaliimepata mafanikio makubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara namadaraja nchini. Katika kipindi hicho, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa17,762 zimekuwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo barabara zenyeurefu wa jumla ya kilometa 5,568 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami.


Aidha, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 3,873 zinaendelea kujengwakwa kiwango cha lami, barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 4,965 zimefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na Serikali inatafuta fedha za kuzijenga kwa kiwango cha lami. Vilevile, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zenye jumla ya kilometa 3,356 unaendelea.

Pia serikali ya rais Jakaya Kikwete itkumbukwa kwa ujenzi ujenzi na ukarabati wa madaraja, hakuna asiyejua kuwa miaka ya nyuma ilikuwa ikifika wakati wa masika kuna wilaya mbali mbali zilikuwa zinakosa mawasiliano na mikoa pmoja na miji mikubwa mpaka hali ya mvua zinapopungu hali hii ilikuwa inawakera sana wananchi kwa kuwa shughuli nyingi za maendelo zilikuwa zinasimama.

Serikali ya awamu ya nne ililiona hilo na ikadiliki kulivali njuga kwa fedha zetu za ndani bila kusubiri wafadhili, katika hili hta kama wapinzani watapinga lakini wanancjhi wanajua ukweli wa hili n hata kama utafunga safari uende katika maeneo ambayo yalikuwa na tata katika madaraja utapa majibu yake. Tumeshudia jumla ya madaraja makubwa 30 yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Kati ya hayo, madaraja makubwa 12 yamekamilika kujengwa, ambayo ni Rusumo (Kagera), Umoja (Mtwara), Mwanhuzi (Simiyu), Kikwete (Kigoma), Nangoo (Mtwara), Ruhekei (Ruvuma), Mbutu (Tabora), Mwatisi (Morogoro), Ruvu (Pwani), Nanganga (Mtwara), Maligisu (Mwanza) na daraja la waenda kwa miguula Mabatini (Mwanza).

Aidha, madaraja makubwa 6 yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi, ambayo ni Kigamboni (Dsm), Kilombero (Morogoro), Kavuu (Katavi), Sibiti (Singida), Ruvu Chini (Pwani) na Lukuledi II (Mtwara). Madaraja makubwa 12 yako kwenye maandalizi ya kujengwa ambayo ni Momba (mpakani mwa Rukwa na Mbeya), Mwiti (Mtwara), Simiyu (Mwanza), Wami (Pwani), Ruhuhu (Ruvuma), Ubungo Interchange (Dar es Salaam), TAZARA Flover (Dar es Salaam), Selander (Dar es Salaam), Daraja jipya la Wami Chini (Pwani), Pangani (Tanga), Kirumi (Mara) na daraja la waenda kwa miguu la Furahisha (Mwanza).

Sambamba na ujenzi wa madaraja makubwa, madaraja madogo madogo zaidi ya 7,200 yamejengwa na kukamilika. katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 Serikali pia imeimarisha Mfuko wa Barabara ambapo mapato ya Mfuko yameongezeka kutoka Shilingi bilioni 73.08 katika mwaka wa fedha 2005/06 hadi Shilingi bilioni 751.7 katika mwaka wa fedha 2014/15 ikiwa ni ongezeko la asilimia 928.6. ni ajabu sana pale kina Mbowe, Lipumba pamoja na Mbatia wanavyojifanya vipofu katika mafaniko haya ya awamu ya nne ambayo tangu uhuru yalikuwa kero kubwa kwa wananchi.

wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani mwaka 2005, vivuko vya Serikali vilivyokuwa vinatoa huduma vilikuwa kumi na tano (15) tu. Hadi kufikia Aprili, 2015, idadi ya vivuko vya Serikali vinavyotoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini imeongezeka na kufikia ishirini na nane (28).

kwa upande wa nyumba na majengo ya Serikali, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ilijenga nyumba 173 za makazi ya Viongozi wa Umma na kuanza mradi wa ujenzi wa nyumba 10,000 za Watumishi wa Umma ambapo nyumba 643 zilikamilika katika kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015 na nyumba 270 zinaendelea kujengwa.

Aidha,Serikali kupitia TBA imeendelea kuhakikisha kwamba ujenzi wa nyumba na majengo yanayotumiwa na umma unazingatia mahitaji maalum hususan kwa watu wenye ulemavu. Suala hili limeendelea kutekelezwa kupitia miradi ya ujenzi wa majengo yote ya Serikali ambayo Wakala wa Majengo umesanifu na kusimamia kama ifuatavyo: Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara, Majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Bariadi, Rorya, Kilolo, Nyamagana na Mvomero. Mengine ni jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi – Kitengo cha Wakimbizi,

Jengo la hospitali ya Manyara na ukumbi wa mikutano na Vituo vya Afya ya Msingi (Primary Health Centre Institutions – PHCI) – Iringa, majengo ya Ofisi za Wakuu 6 wa Mikoa ya Katavi, Njombe, Geita na Simiyu pamoja na majengo ya Ofisi za Wakuu wa Wilaya 19 za Buhigwe, Busega, Butiama, Chemba, Gairo, Ikungi, Itilima, Kalambo, Kaliua, Kakonko, Kyerwa, Mbogwe, Mkalama, Mlele, Momba Nyang`hwale, Nyasa, Uvinza na Wanging'ombe.

Katika mwaka wa fedha 2014/15, wakati ambao serikali ya awamu ya imeendelea na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Wizara ya ujenzi inaendelea vizuri. Kwa upande wa barabara kuu, jumla ya kilometa 504.4 kati ya kilometa 539zilizopangwa kujengwa kwa kiwango cha lami zilikuwa zimekamilika hadi kufikia Aprili, 2015. Na kilometa 87.75 zilikua zimekarabatiwa kwa kiwango cha lami. Kwa upande wa barabara za mikoa, kilometa 40.5 zilijengwa kwa kiwango cha lami. Vile vile, kilometa 450 zilifanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe katika kipindi hicho.

Wakati ris Jakaya akiwa anasubiri muda wake ufike akapumzike hataliacha hivi suala la msongamano mkubwa wa magari katika Jiji la Dar es salaam, serikali yake kupitia Wizara ya ujenzi na Mamlaka mbalimbali zikiwemo Halmashauri za Jiji zimechukuliwa hatua mbalimbli za kukabiliana na tatizo hilo la msongamano wa magari. Tayari maandalizi ya ujenzi barabara ya njia sita ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (km 200) sehemu ya Dar es Salaam –Chalinze (km 100) imepangwa kujengwa kwa kiwango cha "Expressway".

Maandalizi ya mradi huu utakaotekelezwa kwa utaratibu wa ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi (Public Private Partnership - PPP) yamekamilika na yameanza kufanyiwaAprili, 2015, Mshauri Mwelekezi (Transaction Advisor) ambaye ni Kampuni ya Cheil Engineering Company Limited kutoka Korea ya Kusini alikwishateuliwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 7.72 na amekamilisha utafiti wa mwelekeo wabarabara (route survey).

Mwelekeo wa barabara uliochaguliwa unaanzia Charambe katika barabara ya Kilwa kupitia Kisarawe, Kibamba, Kibaha, Mlandizi hadi Chalinze.

Barabara itakuwa na urefu wa kilometa 128 itakuwa ya njia sita (6) na barabara za juu (interchanges) tano (5) katika maeneo ya Charambe, Kisarawe, Kibamba, Mlandizi na Chalinze. Pia itakuwa na vituo vikuu viwili (2) vya kulipia tozo ya barabara (Toll Plaza) maeneo ya Charambe na Chalinze.


Pia barabara hii itakuwa na eneo la kupumzika (rest station) pale Visiga na maeneo mawili (2) ya kuegesha malori ambayo yatakuwa Mbezi na Mbala.


Vilevile Mshauri Mwelekezi atafanya utafiti wa jinsi ya kuunganisha barabara hii kutoka Charambe hadi bandari ya Dar es Salaam. Kwa sasa Mshauri Mwelekezia naendelea na kazi ya kuandaa nyaraka za zabuni na baadaye atasimamia taratibu za kumpata Mbia/Mwekezaji (Concessionaire) wa mradi huu. Gharama za mradi huu wa ujenzi zinakadiriwa kufikia Shilingi Trilioni 2.397 na utatekelezwa kwa njia ya Ubia na Sekta Binafsi (PPP).

Tunajua pia kuwa huwezi kuondoa Msongamano wa magari ya jiji Dar ers Salaam bila kulitaka Daraja la Selander, Rais Jakaya Kikwete anaondoka magogoni akiwa keshalipati ufumbuzi wa kudumu eneo hilo la selander, Serikali ya Korea Kusini imekubali kuipatia Serikali ya Tanzania mkopo wamasharti nafuu kwa ajili ya ujenzi wa Daraja jipya la Selander. Upembuzi yakinifu wa mradi huu umekamilika na maandalizi ya kutiliana saini makubaliano ya mkopo wa kugharamia ujenzi wa daraja kati ya Korea Exim Bank (kwa niaba yaSerikali ya Korea Kusini) na Serikali ya Tanzania yanaendelea.

Daraja hili pamoja na barabara zake za maingilio litakuwa na urefu wa jumla ya kilometa 7.2 na litaanzia eneo la Koko Beach kupitia Kenyatta Drive na kuingia baharini na kisha kuungana na barabara ya Barack Obama eneo la Hospitali ya Aghakan. Mradi huu tagharimu Shilingi Bilioni 197.5. Aidha, Daraja la Kigamboni linaendelea kujengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 236.524.

Ujenzi wa barabara za juu (flyovers na interchanges) na maboresho ya makutano ya barabara katika jiji la Dares Salaam,mpkaAprili, 2015 hali utekelezaji upo kama ifuatavyo kama ifuatavyo: Barabara ya Juu (Flyover) ya TAZARA: Usanifu wa kina umekamilika chini ya ufadhili wa Serikali ya Japan. Taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi atakayekidhi vigezo zinaendelea huko Japan.

Kazi ya ujenzi wa Flyover ya TAZARA ambayo itagharamiwa na Serikali ya Japan ikishirikiana na Serikali ya Tanzania inatarajiwa kuanza katika ya mwaka, 2015. Gharama za mradi huu ni Shilingi Bilioni 93.622. Interchange ya Ubungo Benki ya Dunia imekubali kugharamia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Interchange) katika makutano ya Ubungo. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Interchange ya Ubungo umekamilika. Zabuni ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya usimamizi wa ujenzi zimetangazwa. Serikali inakamilisha taratibu kwa ajili ya kutangaza zabuni za kumtafuta Mkandarasi wa ujenzi.

Vile vile Interchange ya Ubungo itakuwa na levels tatu ambapo magari yanayotoka katikati ya jiji la Dar es Salaam kuelekea Morogoro yatapita chini, magari yanayotoka TAZARA kuelekea Mwenge yatapita juu na magari yanayokata kulia yatapita katikati. Gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa Shilingi Bilioni 126.661. Upanuzi wa barabara ya Gerezani (Bendera Tatu – KAMATA) unakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 29.135. serikali inaendelea na maandalizi ya Maboresho ya Makutano ya Chang'ombe, Magomeni, Mwenge, Tabata, KAMATA, Uhasibu na Morocco yanaendelea.

Serikali ya Kikwete imeendelea kutekeleza miradi ya barabara za kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam zenye urefu wa kilometa 109.35. Barabara hizo ni pamoja na Ubungo Bus Terminal – Mabibo – Kigogo Roundabout (km 6.4); Kigogo Roundabout – Bonde la Msimbazi – Twiga/Msimbazi Jct (km 2.7); Jet Corner – Vituka – Devis Corner (km 10.30); Tabata Dampo – Kigogo (km 1.60); Ubungo Maziwa – External (km 0.65); Mbezi (Morogoro Road) – Malambamawili – Kinyerezi –Banana (km 14); Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi Mwisho (km 20); Tangi Bovu – Goba (km 9); Kimara Baruti–Msewe (km 2.6); Kimara –Kilungule – External Mandela Road (km 9); na Kibamba – Kisopwa (km 12.0). Pia ukarabati unaoendelea katika barabara za Ukonga – Mombasa –Msongola , Kimbiji – Tundwisongani, Misheni – Kijichi – Zakhem, barabara ya Uhuru, Kutengeneza Mifereji ya Maji, uhamishaji miundombinu maeneo ya miradi, malipo ya fidia, n.k. vyote vinakadiriwa kugharimu Shilingi Bilioni 181.795.

Pia Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit Infrastructure – BRT) ambao unajumuisha Ujenzi wa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kivukoni, barabara ya Kawawa kutoka Magomeni hadi Morocco na barabara ya Msimbazi kutoka Fire hadi Kariakoo zenye jumla ya urefu wa kilometa 20.9. Pia kuna vituo vya mabasi 29, vituo vikubwa vitatu namadaraja ya waenda kwa miguu matatu. Pia Ujenzi wa Karakana (Depot) na Kituo cha Mabasi cha Ubungo; Ujenzi wa Karakana (Depot) ya Jangwani; Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi (Terminal) cha Kivukoni; vyote hivyo mchakato wake unaendelea kwa hatua mbali mbali, kwa m,tu ambaye anayeishi mikoani akija nleo Dar es Salaam maeneo ya katikati ya mji atashangaa kasi ya ejenzi inavyoendelea leo.

Pamoja na juhudi kubwa hizo za serikali ya awamu ya nne lakini bado wapinzani wamekuwa wakibeza kuwa miradi mingi haitekwelezi napenda kuwapa changamoto moja wawe wakweli kutoka mioyoni mwao waangali hali ya barabara zetu leo ni sawa na miaka kumi iliyopita

Bado hatujasahu ndugu zetu walivyokuwa wakiliwa na simba njia ya kusini ambapo leo unapamba basi kwenda mtwara kutoka dar es Salaam kwenda mtwara unafika safari yako ndani ya masaa tisa, pia tunakumbuka wakazi wa kanda ya ziwa walivyokuwa wakiteseka kulala njiani mpaka kwa siku tatu wakati leo wanafika ndani ya siku moja.

Hatujasahau ndugu zetu wa Kagera walikuwa wanalazimika kutumia mpaka siku tano kupitia Kenya na Uganda kufika mkoani, kwao hali ni tofauti na sasa ile hali ya kushuka mipakani na kugonga visa hakuna tena na gharama za usafiri na matumizi za kupitia Kenya na Uganda hazipo tena. Haya yaliwezekanaje ndani miaka 10 ya jakaya kikwete na yashindikane hayo mengine, rais Jakaya anamuachia vema rais ajaye kwenye sekta ya miundo mbinu, ambayo ni miongoni mwa kero kubwa tangu uhuru kwa watanzania.

Kwa wale wanaosema rais Jakaya Kikwete hana lolote alilowafanyia watanzania ningependa kuwaasa jambo moja kuwa wanachofanya ni kujidanganya kwani watanzania wanajua mengi na yanaonekana kwa macho.

Vile vile niwaambie wabunge wa upinzani walikuwa wakibeza miradi ya wizara ya ujenzi ya miundo mbinu kuwa miradi hiyo niliyoitaja hapo juu kuwa haitekelezeki napenda kuwaambia hata huu mtandao wa barabara nchini walikuwa wakiubeza lakini leo wapo kimya hawana la kusema. Kwa wale wanaopinga ningewashauri wafunge safari siku moja ya kuzunguuka nchi yetu kwa njia ya barabara watajionea wenyewe, kwanza wangeanza safari Arusha kwenda Singida kupitia Manyara.

Halafu angewauliza wanaotoka Dodoma kwenda Iringa kupitia mtera, halafu nenda njia ya Manyoni hadi kigoma kupitia Tabora, na kwa wakazi wa kusini akawaulize wanaotoka Masasi kwenda Songea kupitia Tunduru. Pia aangalie safari ya kutoka Songea kwenda mpaka Sumbawaga.

Kwa wakazi wa kanda ya ziwa angalie Safari ya kutoka Manyoni kwenda Mwanza kupitia Singida mjini, Nzega, Shinyanga mpaka Mwanza yenyewe. Halafua anzia Shinyanga kwenda Bukoba. Rudi tena anzia Dar es Salaam kwenda Lindi na Mtwara.

Nani asiyejua kuwa miaka kumi iliyopita kwa makazi wa Dar es Salam mwenye asili ya ya mikoa ya Lindi, Mtwara, Kigoma,Rukwa, Simiyu, Geita, Ruvuma na Katazi wakipata misiba kufika kwao ilikuwa shughuli pevu kufika makwao.


Mwisho napenda kumpongeza mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya wizara ya fedha 2014/2015 kwa mara ya kwanza nimemshuhudia akiuunga mkono bajeti kwa kusema wakati anaingia madarakani miaka 4, iliyopita katika jimbo lake kulikuwa na vijiji vitatu tu vyenye umeme katika vijiji 60 kwa sasa jimbo Ludewa ina vijiji 50 vyenye umeme na vingine vitapata umeme kabla ya rais Kikwete kuondoka madarakani, filikunjombe anasema wakati anaingia madarakani kulikuwa hakuna lami lakini kwa sasa kuna kilometer 50 za lami kati ya kilometer `200 za barabara katika jimbo lote la Ludewa na zinaendea kujengwa.

Filikunjombe amesema kuwa kama atapinga mfanikio ya awamu ya nne basi hata wananchi wake watamkataa, alifika mbali zaidi mpaka kutaja idadi ya madaraja tata ambayo yalikuwa yanawasumbua kipindi cha masika lakini kwa sasa yanapitika msimu wote. Napenda kumalizia kwa kumtakia mapumziko mema na afya tele kwa rais waetu Jakaya pale muda wake wa kustaafu utakapofika.
,
 
Kumekuwepo na utaratibu au utamaduni wa kubeza mafanikio na kutokukubali kwa dhati kabisa na kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali rais Jakaya Kikwetena chama chake cha ccm. kuna wachache walisema hawauoni ubunifu wala utendaji kazi, uchapakazi wa Rais na uadilifu na uawaminifu Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mimi ninaomba nitumie fursa hii kupingana nao hoja na kuwaomba waende wakafanye utafiti kwanza kabla ya kuongea, kubeza na kudharau mafanikio ya Serikali ya CCM ya awamu ya Nne. Lakini pia napenda kuwaasa tuondokane na utamaduni wa kubeza mafanikio na kudharau kila kitu ili mradi tu sisi ni Wapinzani, na kuwa mpinzani si kupinga kila kitu ikiwa pamoja na maendeleo.

Kumekuwepo na mafanikio mengine ya kujivunia tangu tupate uhuru ingawa kuna baadhi ya watu hawalidhishwi na kasi ya maendeleo iliyopo, ni ukweli usiopingika kuwa bado tunachangamoto za hapo na pale lakini yatupasa kuubali ukweli tumetoka mbali na mafanikio yamepatikana na yanaendelea kupatikana katika awamu zote tatu na ya a sasa anayomalizia rais Jakaya Kikwete.

Katika awamu hii ya nne kumekuwa na mafanikio ambayo hayakuwahi kutokea ktk nchi hii hata kama baadhi ya watu hawapendi kusikia hivyo, kwa uchache tumefanikiwa katika sekta mbalimbali kama elimu, afya, miundo mbinu na mambo chungu mzima ambayo tukisema tuyataje hapa hatutapa nafasi ya kutosha.

Tukianzia na elimu sote tunakumbuka kuwa serikali yake ilibua mpango wa ujenzi wa sekondari za kata kwa sababu nafasi za wanafunzi kuingia sekondari zilikuwa zimekuwa finyu kiasi cha kwamba ni asilimia kati ya 6 na 10 ya watoto wote waliokuwa wanamaliza shule za msingi mwaka 2005 walikuwa wanaingia sekondari wakati anaingia madarakani.

Pamoja kejeli nyingi zilizoelekezwa kwa shule za sekondari za kata kiasi cha kuitwa Yeboyebo katika miaka ya mwanzoni ya shule hizo, bado zimekuwa na mafanikio makubwa, ambayo ni sehemu ya mafanikio makubwa ya sekta ya elimu katika miaka tisa ya uongozi wa rais KIkwete.

Rais Kikwete alitangaza hivi karibuni kuwa Serikali yake imefuta katika shule za sekondari zilizo chini ya serikali, ili kuboresha sera ya elimu na kuhakikisha kila mwanafunzi anayeanza darasa kwanza anamaliza kidato cha nne. Hii ya kufuta ada itasaidia kila mtoto anayeanza darasa la kwanza anakuwa na nafasi ya kumaliza sekondari kwa maana ya kidato cha nne mpaka cha sita bila kulazimika kuacha shule kwa sababu ya ada.

Bajeti ya Elimu ndiyo iliyo kubwa kuliko zote kwa miaka mingi na imekuwa ikiongezeka. Kwa mfano, mwaka 2005/2006 zilitengwa shilingi bilioni 669.5 wakati mwaka 2014/2015 zimetengwa shilingi trilioni 3.1. Katika kipindi hicho, bajeti ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 56.1 hadi shilingi bilioni 345. Kwa sababu hiyo idadi ya wanafunzi wanaofaidika imeongezeka kutoka 16,345 mwaka 2005 hadi 98,000 mwaka 2014.

Shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,343 mwaka 2014 na hivyo kufanya idadi ya wanafunzi nayo kukua kutoka milioni 7.54 hadi milioni 8.23. Kwa upande wa sekondari shule zimeongezeka 531 mwaka 2005 hadi 4,576 mwaka 2014. Idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,804.056 mwaka 2014.

Upanuzi huu mkubwa na wa kihistoria umetokea pia kwenye vyuo vya elimu ya ufundi stadi ambapo vyuo vimeongezeka kutoka 184 hadi 744 kati ya mwaka 2005 na 2014. Kwa upande wa elimu ya juu, idadi ya vyuo imeongezeka kutoka 26 hadi 50 kati ya mwaka 2005 na 2014 na kufanya idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu iongezeke kutoka wanafunzi 40,719 mwaka 2005 hadi wanafunzi 200,986 mwaka 2014. Leo hii, hatuna tena tatizo na fursa ya kupata elimu kwa elimu ya msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu.

Mwaka 2005, urari wa wanafunzi kati yetu na wenzetu wa Afrika Mashariki ulikuwa wa chini mno kwa upande wetu. Kenya walikuwa na wanafunzi wa sekondari 925,341 na wa vyuo vikuu 108,407 ikilinganishwa na Tanzania iliyokuwa na wanafunzi 524,325 wa sekondari na 40,719 wa vyuo vikuu. Uganda ilikuwa na wanafunzi 728,393 wa sekondari na 124,313 wa vyuo vikuu.

Sasa hali ni tofauti. Kwa mwaka 2013, kwa mfano, Kenya ilikuwa na wanafunzi wa sekondari 2,104,300 na wanafunzi wa vyuo vikuu 324,600. Katika mwaka huohuo, Uganda walikuwa na wanafunzi wa sekondari 1,362,739 na wa vyuo vikuu 140,403. Ongezeko hili linatuweka katika hali nzuri ya ushindani tunapoelekea katika ushindani wa soko la pamoja ndani ya Afrika Mashariki ikilinganishwa na hali ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.

Tumekuwa nchi ya kupigiwa mfano katika kutekeleza Malengo ya Milenia (MDGs) yanayohusu fursa ya watoto kupata elimu ya msingi, na usawa wa kijinsi baina ya watoto wa kiume na wa kike kupata elimu ya msingi na sekondari.


Sote tu mashahidi ya kuwa Rais Kikwete alivyoingia alikutana na changamoto mbalimbali ikiwamo ukame ambapo tathimini inaonyesha kuwa mwaka 2006 jumla ya ngombe 250,000, mbuzi 130,000 kondoo 122,000 pamoja na punda zaidi 700 walikufa kutokana na ukame wa ukosefu wa maji, jumla ya mifugo yote hiyo ilikuwa na thamani ya zaidi ya billion 45.3

Baada ya ukame kupungua serikali ya rais kikwete ikakutana na mtihani mwingine wa kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kusababisha ongezeko la bei katika sekta ya usafiri. Mtihani mwingine kwa serikali ya rais Kikwete ilikuwa ilikuwa ni mtikisiko wa wa uchumi duniani ambayo uliathiri kwa kiasi kikubwa kwa mataifa yanayoendelea na yaliyokuwa yameandelea na kuathiri bajeti za chi kadhaa duniani, lakinin kwa uimara wa serikali yake hatukuyumbishwa na mtikisiko huu wa uchumi wa dunia mwaka 2009.

Rais kikwete pia amefanikiwa kuondoa uhasama wa visiwani unguja na pemba uliodumu kwa miaka 10 ambapo aliyemstaafu Benjamini Mkapa aliwahi kukiri baada ya kutoka madarakani kuwa mgogoro wa visiwa hivyo vya Karafuu ulikuwa unamnyima usingizi wakati wa utawala.

Mgogoro huo wa kisiasa ulifikia hatua mbaya kiasi ambacho hata ndugu wa baba mdogo na mkubwa walishindwa kuzikana pamoja na kuombana maji kutokana na misimamo na itikadi ya vyama vyao, lakini leo twaona wazanzibar wote wamekuwa wamoja na wakimbizi waliokwenda Mombasa walirejea nchini.
Kikwete kasoma lini PhD mpaka aitwe Doctor?
 
Kumekuwepo na utaratibu au utamaduni wa kubeza mafanikio na kutokukubali kwa dhati kabisa na kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali rais Jakaya Kikwetena chama chake cha ccm. kuna wachache walisema hawauoni ubunifu wala utendaji kazi, uchapakazi wa Rais na uadilifu na uawaminifu Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mimi ninaomba nitumie fursa hii kupingana nao hoja na kuwaomba waende wakafanye utafiti kwanza kabla ya kuongea, kubeza na kudharau mafanikio ya Serikali ya CCM ya awamu ya Nne. Lakini pia napenda kuwaasa tuondokane na utamaduni wa kubeza mafanikio na kudharau kila kitu ili mradi tu sisi ni Wapinzani, na kuwa mpinzani si kupinga kila kitu ikiwa pamoja na maendeleo.

Kumekuwepo na mafanikio mengine ya kujivunia tangu tupate uhuru ingawa kuna baadhi ya watu hawalidhishwi na kasi ya maendeleo iliyopo, ni ukweli usiopingika kuwa bado tunachangamoto za hapo na pale lakini yatupasa kuubali ukweli tumetoka mbali na mafanikio yamepatikana na yanaendelea kupatikana katika awamu zote tatu na ya a sasa anayomalizia rais Jakaya Kikwete.

Katika awamu hii ya nne kumekuwa na mafanikio ambayo hayakuwahi kutokea ktk nchi hii hata kama baadhi ya watu hawapendi kusikia hivyo, kwa uchache tumefanikiwa katika sekta mbalimbali kama elimu, afya, miundo mbinu na mambo chungu mzima ambayo tukisema tuyataje hapa hatutapa nafasi ya kutosha.

Tukianzia na elimu sote tunakumbuka kuwa serikali yake ilibua mpango wa ujenzi wa sekondari za kata kwa sababu nafasi za wanafunzi kuingia sekondari zilikuwa zimekuwa finyu kiasi cha kwamba ni asilimia kati ya 6 na 10 ya watoto wote waliokuwa wanamaliza shule za msingi mwaka 2005 walikuwa wanaingia sekondari wakati anaingia madarakani.

Pamoja kejeli nyingi zilizoelekezwa kwa shule za sekondari za kata kiasi cha kuitwa Yeboyebo katika miaka ya mwanzoni ya shule hizo, bado zimekuwa na mafanikio makubwa, ambayo ni sehemu ya mafanikio makubwa ya sekta ya elimu katika miaka tisa ya uongozi wa rais KIkwete.

Rais Kikwete alitangaza hivi karibuni kuwa Serikali yake imefuta katika shule za sekondari zilizo chini ya serikali, ili kuboresha sera ya elimu na kuhakikisha kila mwanafunzi anayeanza darasa kwanza anamaliza kidato cha nne. Hii ya kufuta ada itasaidia kila mtoto anayeanza darasa la kwanza anakuwa na nafasi ya kumaliza sekondari kwa maana ya kidato cha nne mpaka cha sita bila kulazimika kuacha shule kwa sababu ya ada.

Bajeti ya Elimu ndiyo iliyo kubwa kuliko zote kwa miaka mingi na imekuwa ikiongezeka. Kwa mfano, mwaka 2005/2006 zilitengwa shilingi bilioni 669.5 wakati mwaka 2014/2015 zimetengwa shilingi trilioni 3.1. Katika kipindi hicho, bajeti ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 56.1 hadi shilingi bilioni 345. Kwa sababu hiyo idadi ya wanafunzi wanaofaidika imeongezeka kutoka 16,345 mwaka 2005 hadi 98,000 mwaka 2014.

Shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,343 mwaka 2014 na hivyo kufanya idadi ya wanafunzi nayo kukua kutoka milioni 7.54 hadi milioni 8.23. Kwa upande wa sekondari shule zimeongezeka 531 mwaka 2005 hadi 4,576 mwaka 2014. Idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,804.056 mwaka 2014.

Upanuzi huu mkubwa na wa kihistoria umetokea pia kwenye vyuo vya elimu ya ufundi stadi ambapo vyuo vimeongezeka kutoka 184 hadi 744 kati ya mwaka 2005 na 2014. Kwa upande wa elimu ya juu, idadi ya vyuo imeongezeka kutoka 26 hadi 50 kati ya mwaka 2005 na 2014 na kufanya idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu iongezeke kutoka wanafunzi 40,719 mwaka 2005 hadi wanafunzi 200,986 mwaka 2014. Leo hii, hatuna tena tatizo na fursa ya kupata elimu kwa elimu ya msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu.

Mwaka 2005, urari wa wanafunzi kati yetu na wenzetu wa Afrika Mashariki ulikuwa wa chini mno kwa upande wetu. Kenya walikuwa na wanafunzi wa sekondari 925,341 na wa vyuo vikuu 108,407 ikilinganishwa na Tanzania iliyokuwa na wanafunzi 524,325 wa sekondari na 40,719 wa vyuo vikuu. Uganda ilikuwa na wanafunzi 728,393 wa sekondari na 124,313 wa vyuo vikuu.

Sasa hali ni tofauti. Kwa mwaka 2013, kwa mfano, Kenya ilikuwa na wanafunzi wa sekondari 2,104,300 na wanafunzi wa vyuo vikuu 324,600. Katika mwaka huohuo, Uganda walikuwa na wanafunzi wa sekondari 1,362,739 na wa vyuo vikuu 140,403. Ongezeko hili linatuweka katika hali nzuri ya ushindani tunapoelekea katika ushindani wa soko la pamoja ndani ya Afrika Mashariki ikilinganishwa na hali ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.

Tumekuwa nchi ya kupigiwa mfano katika kutekeleza Malengo ya Milenia (MDGs) yanayohusu fursa ya watoto kupata elimu ya msingi, na usawa wa kijinsi baina ya watoto wa kiume na wa kike kupata elimu ya msingi na sekondari.


Sote tu mashahidi ya kuwa Rais Kikwete alivyoingia alikutana na changamoto mbalimbali ikiwamo ukame ambapo tathimini inaonyesha kuwa mwaka 2006 jumla ya ngombe 250,000, mbuzi 130,000 kondoo 122,000 pamoja na punda zaidi 700 walikufa kutokana na ukame wa ukosefu wa maji, jumla ya mifugo yote hiyo ilikuwa na thamani ya zaidi ya billion 45.3

Baada ya ukame kupungua serikali ya rais kikwete ikakutana na mtihani mwingine wa kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kusababisha ongezeko la bei katika sekta ya usafiri. Mtihani mwingine kwa serikali ya rais Kikwete ilikuwa ilikuwa ni mtikisiko wa wa uchumi duniani ambayo uliathiri kwa kiasi kikubwa kwa mataifa yanayoendelea na yaliyokuwa yameandelea na kuathiri bajeti za chi kadhaa duniani, lakinin kwa uimara wa serikali yake hatukuyumbishwa na mtikisiko huu wa uchumi wa dunia mwaka 2009.

Rais kikwete pia amefanikiwa kuondoa uhasama wa visiwani unguja na pemba uliodumu kwa miaka 10 ambapo aliyemstaafu Benjamini Mkapa aliwahi kukiri baada ya kutoka madarakani kuwa mgogoro wa visiwa hivyo vya Karafuu ulikuwa unamnyima usingizi wakati wa utawala.

Mgogoro huo wa kisiasa ulifikia hatua mbaya kiasi ambacho hata ndugu wa baba mdogo na mkubwa walishindwa kuzikana pamoja na kuombana maji kutokana na misimamo na itikadi ya vyama vyao, lakini leo twaona wazanzibar wote wamekuwa wamoja na wakimbizi waliokwenda Mombasa walirejea nchini.
Kwenye Elimu, uchumi na Miundombinu JK atasalia kwenye historia miaka Mingi na ni Moja ya legacy zake..

Ni wapuuzi tuu ndio wlaikuwa wanasema hakuna kitu kafanya mara Ufisadi nk but tulitegemea Mwendazake alioingia angekomesha hao Mafisadi na Ufisadi matokeo yake akakwapua 1.5T zikafichwa China nk na wakala plea bargaining na wapuuzi wenzie huku walifanya propaganda ya Sgr and such nonsense.
 
Back
Top Bottom