Baadhi ya nchi zilizoweka lockdown na kisha baada ya kuondoa, visa vya Corona vimeongezeka kwa kasi, inatufundisha nini juu ya busara za Rais wetu?

Baadhi ya nchi zilizoweka lockdown na kisha baada ya kuondoa, visa vya Corona vimeongezeka kwa kasi, inatufundisha nini juu ya busara za Rais wetu?

Yaani umemaliza Kila kitu mkuu.
Mimi binafsi nimekuelewa Sana [emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106]
1.) Kule ni nyumbani kwake kama wewe unavyoenda nyumbani kwako, ushauri unaotolewa ni kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka, hata wewe unaweza kufuata ushauri ambao Rais anaufanya kwa vitendo, kazi anafanya kwa simu na video conferencing, kwani nesi yule akahudumie wagonjwa? HUNA HOJA

2.) Tunajua nchi nyingi kama ilivyo sisi hawajaweka lockdown ila wamechukua hatua za kueleweka kama sisi pia, tumefunga shule, tumekataza watu kutoka bila barakoa, tumehakikisha kuna ndoo za maji na sabuni kila baada ya mita tatu, tumetoa sharti la watu kuchukua TAKEAWAY na masharti mengine mengi ya social distancing, HUNA HOJA

3.) Lockdown ina maana tu kama itawekwa hadi wagonjwa wabaki 0, pasiwe na mgonjwa hata mmoja aliyebaki maana huyo mmoja atasababisha tena mlipuko, maana hata hapo mwanzo palianza na mgonjwa mmoja tu, ukisema watachukua tahadhari za kujikinga ili mlipuko usirudi nami nitakwambia kwanini wasingechukua tu hizo tahadhari toka mwanzo badala ya kuweka lockdown? Maana cases zilizopo wakati wanatoa lockdown ni nyingi kuliko wakati wanaweka lockdown, so lockdown ina mantiki ipi hapo? HUNA HOJA

4.) Kuna ubaya gani kufunga shule maana wanafunzi hawana uwezo wa kujisimamia kutekeleza tahadhari za kitaalam za social distancing, kunawa, uvaaji barako nk. Halafu kujificha maananyake nini? Mtu kukaa kwake ni kajificha, ulitaka afanye nini wakati wataalam wamesema kama huna ulazima wa kutoka basi usitoke, na yeye anafanya hivyo, hata wewe kama unaweza kufanya kazi kwa simu/ online bila kutoka basi usitoke, maana hayo ndio maagizo ya wataalam. HUNA HOJA.

5.) Mtu ambae kajifungia ndani kwake automatically amelockout kila mtu nje, sasa sijui unamaanisha nini, HUNA HOJA

6.) Unaposema hatuna lolote tulilofanya (ukiacha hiyo lockdown), unamaanisha nini? Haya yote yaliyofanyika including kufunga shule sio chochote? Hizi restrictions zote especially Dar we unaona si chochote? HUNA HOJA

7.) Kweli ujinga ni tatizo, lakini elimu ipo na inatolewa kila kona ili kuondoa ujinga na hatimae umasikini, lakini tofautisha ujinga na kupingana, watu kutofautiana mawazo ni jambo lakawaida, hivyo jitahidi kuonyesha uhalali wa mawazo dhidi ya mawazo ya mtu mwingine kwa kutumia hoja, jenga hoja na utasikikizwa, HUNA HOJA

Sent using LEAGOO M12
 
Teh teh teh.
Nimechemka Sana kwa hii comment yako mkuu.
Ni very obvious kwamba kuchukua tahadhari (staying alert) ndio njia sustainable, hii kufungiana ndani ni sawa na mtu kujibana usiharishe, utanbana weeeee, ila yakifika mahali pake lazima utaachia tu

Sent using LEAGOO M12
 
Ndio maana nasema ujinga bado ni tatizo kubwa nchi hii.

Nimesoma namba moja tu hata sikutaka kuendelea maana tayari nilishajua uwezo wako wa akili.

Kukusaidia kwenye namba moja hapo. Kinachosababisha anaitwa rais ni katiba. Katiba hiyo hiyo imeweka utaratibu wa makazi kwa mtu anaeitwa au aliekalia cheo cha urais, amawekewa utaratibu wa kuanzia makazi na kila kitu. Vinginevyo ikulu isingekuwepo maana kila mtu ana kwao, Nyerere angekua anaishi kwao Butiama, Mkapa angekua anaishi kwao Mtwara, Kikwete angekua anaishi kwao Msoga.

Trump ana kwake ila baada ya kua rais anatakiwa kisheria akaishi white house, Boris Johnson ana kwake au kwao ila anatakiwa aishi Ofice No 10 na viongozi wote Duniani utaratibu ndio huo.

Hoja ya kitaahila eti ni kwao kwani hao marais wengine hawakua na kwao? Museveni hana kwao? Kenyata hana kwao mbona hawajakimbia kwenda kwao?

Sishangai kwa sababu mmejaa ujinga, haya anayoyaongea Ndugai ndio kama unayoyasema wewe. Zero brain kabisa.

Namba 2 hadi mwisho yote ni uharo.
Nimekujibu hoja zote, sasa kuniambia umesoma moja tu inamaana umeshindwa kunipa hadhi ya kujadili na wewe kwenye meza moja, ahsante, naondoka.
 
Tumepata taarifa kupitia vyombo mbali mbali vya kimataifa juu ya nchi kadhaa zilizoweka total lockdown na baada ya uchumi kuyumba na njaa kuwa kali wakaamua kuondoa lockdown, kisha visa vya Corona vikashoot juu kwa kasi kwa mara nyingine tena, na sasa wanafikiria kurudisha tena lockdown. Nchi hizo ni kama Germany na South Korea.
Uingereza nao wanatoa lockdown na wamesema wakihisi tu visa vinapaa tena basi hawatasita kuwafungia tena ndani wananchi, (Total lockdown).
Je, hii inatufundisha nini juu ya busara za mheshimiwa Rais?

Fahamu kwa undani nadharia ya ‘Lockdown YOYO effect’ , mchezo wa kujaza maji ndoo ilitoboka - JamiiForums

Boris Johnson: Tujifunzeni kuishi na Corona tutakuwa nayo kwa muda mrefu - JamiiForums
Herd immunity itatuokoa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1.) Kule ni nyumbani kwake kama wewe unavyoenda nyumbani kwako, ushauri unaotolewa ni kaa nyumbani kama huna ulazima wa kutoka, hata wewe unaweza kufuata ushauri ambao Rais anaufanya kwa vitendo, kazi anafanya kwa simu na video conferencing, kwani nesi yule akahudumie wagonjwa? HUNA HOJA

2.) Tunajua nchi nyingi kama ilivyo sisi hawajaweka lockdown ila wamechukua hatua za kueleweka kama sisi pia, tumefunga shule, tumekataza watu kutoka bila barakoa, tumehakikisha kuna ndoo za maji na sabuni kila baada ya mita tatu, tumetoa sharti la watu kuchukua TAKEAWAY na masharti mengine mengi ya social distancing, HUNA HOJA

3.) Lockdown ina maana tu kama itawekwa hadi wagonjwa wabaki 0, pasiwe na mgonjwa hata mmoja aliyebaki maana huyo mmoja atasababisha tena mlipuko, maana hata hapo mwanzo palianza na mgonjwa mmoja tu, ukisema watachukua tahadhari za kujikinga ili mlipuko usirudi nami nitakwambia kwanini wasingechukua tu hizo tahadhari toka mwanzo badala ya kuweka lockdown? Maana cases zilizopo wakati wanatoa lockdown ni nyingi kuliko wakati wanaweka lockdown, so lockdown ina mantiki ipi hapo? HUNA HOJA

4.) Kuna ubaya gani kufunga shule maana wanafunzi hawana uwezo wa kujisimamia kutekeleza tahadhari za kitaalam za social distancing, kunawa, uvaaji barako nk. Halafu kujificha maananyake nini? Mtu kukaa kwake ni kajificha, ulitaka afanye nini wakati wataalam wamesema kama huna ulazima wa kutoka basi usitoke, na yeye anafanya hivyo, hata wewe kama unaweza kufanya kazi kwa simu/ online bila kutoka basi usitoke, maana hayo ndio maagizo ya wataalam. HUNA HOJA.

5.) Mtu ambae kajifungia ndani kwake automatically amelockout kila mtu nje, sasa sijui unamaanisha nini, HUNA HOJA

6.) Unaposema hatuna lolote tulilofanya (ukiacha hiyo lockdown), unamaanisha nini? Haya yote yaliyofanyika including kufunga shule sio chochote? Hizi restrictions zote especially Dar we unaona si chochote? HUNA HOJA

7.) Kweli ujinga ni tatizo, lakini elimu ipo na inatolewa kila kona ili kuondoa ujinga na hatimae umasikini, lakini tofautisha ujinga na kupingana, watu kutofautiana mawazo ni jambo lakawaida, hivyo jitahidi kuonyesha uhalali wa mawazo dhidi ya mawazo ya mtu mwingine kwa kutumia hoja, jenga hoja na utasikikizwa, HUNA HOJA
Safi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom