Uhakika Bro
JF-Expert Member
- Mar 29, 2022
- 3,644
- 4,315
Jana nimekaa nikatafakari sana;
Hivi ni nani anayesemaga kwamba waafrika hawajagundua chochote cha maana?
Isije ikawa cha maana anachokiona yeye ni mawasiliano tu, sijui na kupaa au kurusha vitu angani😢
Kimsingi ugunduzi huwa unatakiwa kutatua changamoto ya watu husika kwanza kabla haujafika kimataifa. Na hilo ndio la maana kwao hao watu.
Tusimshadadie saana anayesisitiza kuwa teknolojia ni kumwagilia kwa drones, tukampondea yule aliyekuwa anachota maji kwa ndoo na sasa amegundua chemchemu akachimba mfereji. Kiukweli hata kama angeendelea kutumia ndoo kama ndiyo amegundua yeye apewe pongezi zake ametatua changamoto (ukame) zake bwana alaa!
Tukizungumzia mfano hii changamoto ya njaa. Baa la njaa lilikuwa likiumiza kaya na jamii nyingi tu za kiafrika kwa muda mrefu.
Kwa hiyo yeyote aliyegundua teknolojia ya kuhifadhi chakula huyo alikuwa mbabu jiniazi tena shujaa wa kijiji chake.
Sijui kuhusu mila za makabila mengine sana lakini hebu chukulia Wasukuma kama mfano;
Waligundua maparage
Wakagundua matoborwa
Na kuna hii kitu tunaita Mbutee hiiiiii😋
Na vingine vingi tu kama kukausha na kusaga msusa na mlenda halafu unakuja kupikwa na karanga (nimelisahau jina)
Mbogamboga ni nyingi tu mfano kuna nsansa pia
Jamii ikishakuwa na uhakika wa chakula bora, mlo kamili kwa mwaka wote hivi bado tena utajiuliza ni kwa nini Wasukuma wanazaliana sana?
Ni wakati sasa wa kuamka na kila jamii ikajifunze kwa jamii nyingine namna ya kukabili changamoto mbalimbali za kijamii ili tuimarishe uchumi wetu na afya zetu pia.
Ongezea na wewe teknolojia zilizopo katika jamii yako na zilivyotatuliwa ki locally tujivunie vya kwetu na vya kwenu(vyetu tu).
Hivi ni nani anayesemaga kwamba waafrika hawajagundua chochote cha maana?
Isije ikawa cha maana anachokiona yeye ni mawasiliano tu, sijui na kupaa au kurusha vitu angani😢
Kimsingi ugunduzi huwa unatakiwa kutatua changamoto ya watu husika kwanza kabla haujafika kimataifa. Na hilo ndio la maana kwao hao watu.
Tusimshadadie saana anayesisitiza kuwa teknolojia ni kumwagilia kwa drones, tukampondea yule aliyekuwa anachota maji kwa ndoo na sasa amegundua chemchemu akachimba mfereji. Kiukweli hata kama angeendelea kutumia ndoo kama ndiyo amegundua yeye apewe pongezi zake ametatua changamoto (ukame) zake bwana alaa!
Tukizungumzia mfano hii changamoto ya njaa. Baa la njaa lilikuwa likiumiza kaya na jamii nyingi tu za kiafrika kwa muda mrefu.
Kwa hiyo yeyote aliyegundua teknolojia ya kuhifadhi chakula huyo alikuwa mbabu jiniazi tena shujaa wa kijiji chake.
Sijui kuhusu mila za makabila mengine sana lakini hebu chukulia Wasukuma kama mfano;
Waligundua maparage
Wakagundua matoborwa
Na kuna hii kitu tunaita Mbutee hiiiiii😋
Na vingine vingi tu kama kukausha na kusaga msusa na mlenda halafu unakuja kupikwa na karanga (nimelisahau jina)
Mbogamboga ni nyingi tu mfano kuna nsansa pia
Jamii ikishakuwa na uhakika wa chakula bora, mlo kamili kwa mwaka wote hivi bado tena utajiuliza ni kwa nini Wasukuma wanazaliana sana?
Ni wakati sasa wa kuamka na kila jamii ikajifunze kwa jamii nyingine namna ya kukabili changamoto mbalimbali za kijamii ili tuimarishe uchumi wetu na afya zetu pia.
Ongezea na wewe teknolojia zilizopo katika jamii yako na zilivyotatuliwa ki locally tujivunie vya kwetu na vya kwenu(vyetu tu).