Baadhi ya Walokole kwanini wako hivi?

Mlokole akitenda dhambi utasikia anajisemea "nimeanguka kiroho" "napitishwa kwenye majaribu"

Akitenda mwingine basi wanamuona ibilisi
Nimecheka sana.

Kuna mwanamke nilimzalisha nikarudi kwa mchungaji na kumuomba kurudi kundini nikiwa na mke na mtoto wangu.

Mchungaji akakubali ni sali.

Aisee wale waumini wanaonitambua wakaanza kunitenga mdogo mdogo ukiwasalamia hawaaitikii.

Kiukweli nilikwazika.

Nikiangalia wanaoitwa wa dunia wananipa kampani na kufurahia maisha.

Mara mchungaji anaiita ananiambia siwezi kuendelea kusali kwakwe mpaka anifungishe ndoa serikalini .

Lakini hapo hapo kuna mtoto wa mchungaji mmoja na yeye alikuwa ana Kesi same na mimi yule wanamfungisha ndoa ya kifahari mimi wanasema nikafunge ya kiserikali au ofisini kwake.

Kiukweli nikaacha kusali kwake
 
Mkuu we nenda kasali Mungu atakubariki, haya mambo uliyoyataja ni sifa za mtu mweusi...
Majungu, Ngono, Kutosaidiana hii inatokana na umaskini wetu
Nitarudi tu maana nina mtoto tayari hawezi kulelewa kipagani hata mimi siwezi kuendelea kuishi hivi.
 
Watu watakubishia ila maisha ya ulokole jamani.

Hapo sijazungumza wanaosali kwa kapola maana nishawahi kwenda.

Bado wale wa mwamposa

Mambo ni mengi
 
Ila walokole wanajua kubanduana wenyewe kwa wenyewe.

Mkeo akiwa mlokole andika kilio, ujue ni chakula ya wana wa kilokole. Kuanzia baba mchungaji mpaka waumini.

Ukisikia mkesha wa maombi ujue ni mwendo wa kusimamia ukucha.
Umenifurahisha sana kuna demu alikuwa anaaga anaenda kwa mkesha kumbe anakuja kwangu aisee
 
Natamani kujua mtu anaposema hayo maneno kwenye bold huwa anamaanisha nini?
 
Mimi binafsi ndugu zangu wengi ni walokole, na kuna kipindi walishajaribu kunivuta na nikaenda, japo sikuwahi kuingia ile deep sana nikaachana nao.

Nilichojifunza ni kwamba;

1. Walokole wengi hawamtafuti Mungu, wao wanamfata mchungaji. Ndio maana leo utasikia wako kwa mchungaji huyu, kesho wanahamia kwa yule.. hakuna mlokole anaedumu sehemu moja wao kila siku ni kuhama hama kufuata "upepo". Tatizo wakihama sehemu, immediately wanaanza kulaumu na kusema mapungufu ya mchungaji huyo, kanisa lake nk.

2. Walokole wao kwa wao hawapendani hata kidogo! Mlokole anaesali kwa pasta A na anaesali kwa pasta B ni kama maadui. Huwezi kukuta wanashirikiana kwa chochote. Kutwa kusemana mapungufu ya mapasta/makanisa yao tena kwa maneno makali (mf yule anatumia nguvu za giza)

3. Walokole wengi ninaowajua ni wanafki na wana roho mbaya balaa. Yaani wengi wao hata ule upendo wa kawaida wa kibinadamu bado ni changamoto. Unajiuliza kama huyu asingekua mlokole ingekuaje?

4. Wengi wa walokole wanafanya dhambi ZOTE tunazozifanya sisi, kuanzia zinaa, kunywa pombe, wizi/ubadhirifu kazini, ulanguzi, uongo, utapeli nk. Japo sijui kwanini wao wanajiona kuwa ni watakatifu.

5. Suala la kunena kwa lugha ndio lilinifanya nikachoka kabisa. Walokole WOTE wananena kwa lugha moja, maneno ni yale yale na ukisali kule mda mfupi tu nawewe unayakariri. Cha ajabu wenyewe hua wanaona kama kunena kwa lugha ni hatua ya juu kabisa ya maombi!

Kikubwa ninachowalaumu hawa ndugu zangu ni kukaa kwenye ulokole zaidi ya miaka 20 na hawajaweza kufungua hata ka kanisa wapige hela.

 
Nilimgonga demu mmoja wa kidini dini mazingira hayo hayo ya kidini tena yeye aliniforce nimgonge kimazingira shetwani kabisa yule tena dry ulichosema ni kweli
Niliwahi kumtongoza dada mmoja kiongozi wa kwaya ya kanisa moja la kilokole. Siku ya kwanza nimemtoa out jioni tumekaa sehemu, mimi kwa kujistukia nikaagiza soda, yule dada bila aibu akaagiza KONYAGI NDOGO!! Na akaifuta chap wala hajapepesuka. Sitakaa nisahau ile siku karibu nizimie kwa mshangao.
 
Pole sana ndugu kwa uliyokutana nayo, umeiacha imani kwasababu ulikuwa husomi neno la Mungu ukajiongeza maarifa na kujiimarisha mwenyewe katika imani, ukisoma Biblia Yesu alikuwa anapambana sana na mafarisayo na makuhani, na ndio waliomhukumu hata Pilato mwenyewe ambaye alikuwa mpagani aliona Yesu hana kosa lakini hao makuhani na mafarisayo walimshambulia Yesu.

Hoja yangu ni nini mlokole ni nani, ni mzinzi aliyeacha uzinzi, kahaba aliyeacha ukahaba, mchawi aliyeacha uchawi, jambazi aliyeacha ujambazi, kiufupi hakuna mlokole ambaye hakuwa na dhambi, sasa dhambi ina tabia ya kurudi kwa sababu ibilisi anashinda kanisani hashindi bar, kwahiyo hayo uliyoyataja yanaweza kufanyika kanisani, Ukisoma neno la Mungu ukalielewa huwezi kuacha imani et kwa sababu mwanakwaya amezaa nje ya ndoa, sijui shemas anatembea na mke wa mtu, safari ya mbinguni ni ya mtu mmoja sio kundi la watu ninaamini kama uliamua kuokoka kuna vitu unavitamani kwenye maisha yako kupitia huo wokovu pambana mpaka uvipate acha kuangalia watu
 
Kama nilikotoka nimetoka kwasababu watu (hasa viongozi) ni wazinzi, walevi, wanazaa nje nk halafu nakuja kwenye ulokole nakuta tena yale yale, kwanini nisibaki tu kwenye imani yangu maana hakuna tofauti yoyote?
 
Ukiwa na mke au gelefrendi mlokole we ndo unaongoza kwa hasara hapa duniani, ni waongo, wanafiki, akili za kushikiwa hawanaga maamuzi yao binafsi, ndo maana ni rahisi kumpa mzigo mchungaji wake na viongozi wengine kanisani, kingine vinajua kujiliza vina machozi mengi na ya karibu, wanaishigi na mapepo nadhani maana kila wakiombeana lazima waanguke kwa mapepo,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…