Baba amshtaki Mtoto wake akitaka akatwe 20% ya mshahara na apewe yeye ili kutunza familia

Baba amshtaki Mtoto wake akitaka akatwe 20% ya mshahara na apewe yeye ili kutunza familia

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mzee Gideon Kisira Cherowo (73) Mkazi wa Birunda nchini Kenya amemfungulia kesi Mtoto wake aitwaye Washington Chepkombe akitaka akatwe asilimia 20 ya mshahara wake ili apewe Mzee huyo kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya Familia kwakuwa Mtoto wake huyo hampi msaada licha ya kuwa na kazi nzuri na fedha nyingi.

Mzee huyo anasema alilazimika kuuza hadi ardhi yake na mali zake nyingine ili kulipia ada za masomo ya Mtoto wake huyo hadi Chuo Kikuu na akafanikiwa kupata kazi kwenye Mamlaka ya Viwanja vya Ndege lakini baada ya kupata kazi hampi msaada.

Mzee huyo amesema ana Watoto wanne lakini mwenye kazi ni Washington pekee na kusema kwa sasa yeye na Familia yake wanaishi katika nyumba ya udongo kijijini kwao huku Mtoto wao mwenye uwezo akila starehe Mjini.

"Nimepambana sana kumtafutia maisha Mtoto ili atusaidie lakini hatupi msaada kwakuwa mshahara wake ni mzuri nimefungua kesi ili 20% ya mshahara wake nilipwe Mimi"


Millard Ayo
 
Wazazi wasisomeshe Watoto ili waje wawasaidie.. Umemzaa mtoto kwa Starehe zako hajakuomba umzae..Ni wajibu wako kumpatia MAHITAJI ya Msingi ikiwemo Elimu.. mzazi kumsomesha mtoto siyo Fadhila ni wajibu.. Aje akusaidie au Akupotezee ni uchaguzi wake.
 
Vijana wa siku hizi tumekuwa wahuni kupindukia, wazazi hatuwakumbuki jamani. Hata 5% tu kutoa kwa hiari imekuwa ni nongwa hadi mtu afikishwe mahakamani? Aibuuu!

Wakulaumiwa ni nani, wazazi ambao walizembea kwenye jukumu lao la kutumia kiboko ipasavyo? Au ndio yale yale ya raha mjini majuto?
"..... wengine huvuta ndomu wapate matukulele..... bora wachapwe mboko, watoto hawasikii.....".
Shairi la Bakari;
 
Wazazi wasisomeshe Watoto ili waje wawasaidie.. Umemzaa mtoto kwa Starehe zako hajakuomba umzae..Ni wajibu wako kumpatia MAHITAJI ya Msingi ikiwemo Elimu.. mzazi kumsomesha mtoto siyo Fadhila ni wajibu.. Aje akusaidie au Akupotezee ni uchaguzi wake.
etiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii nini
 
Vijana wa siku hizi tumekuwa wahuni kupindukia, wazazi hatuwakumbuki jamani. Hata 5% tu kutoa kwa hiari imekuwa ni nongwa hadi mtu afikishwe mahakamani? Aibuuu!

Wakulaumiwa ni nani, wazazi ambao walizembea kwenye jukumu lao la kutumia kiboko ipasavyo? Au ndio yale yale ya raha mjini majuto?
"..... wengine huvuta ndomu wapate matukulele..... bora wachapwe mboko, watoto hawasikii.....".
Shairi la Bakari;
"People blame this generation but they forget who raised it up "
 
Yapo mpaka madingi masenge yana cash Ila yalitelekeza watoto
 
mzazi kumsomesha mtoto siyo Fadhila ni wajibu.. Aje akusaidie au Akupotezee ni uchaguzi wake

Haiwezekani iwe wajibu kwa mzazi kumsomesha mwanae lakini isiwe wajibu kwa mtoto kumuhudumia mzazi wake. Haiwezekani watoto wawe na haki bila kuwa na wajibu!!! It will lead to lack of equilibrium ; and any society that is not stable is always dysfunctional.
 
Washington chepkombe, mali yake, mshahara wake na kila chake ni mali ya baba yake, labda awe hana dini yeyote ile,
Au awe anaiga wazungu
Hakuna haki bila wajibu na wajibu bila haki pia hakuna
 
Wazazi wasisomeshe Watoto ili waje wawasaidie.. Umemzaa mtoto kwa Starehe zako hajakuomba umzae..Ni wajibu wako kumpatia MAHITAJI ya Msingi ikiwemo Elimu.. mzazi kumsomesha mtoto siyo Fadhila ni wajibu.. Aje akusaidie au Akupotezee ni uchaguzi wake.
Ila mzee akizeeka nae anakuwa kama mtoto tu,ana haki ya kuangaliwa na kutunzwa pia
Vinginevyo kifuatacho ni laana tu,
Labda awe hana dini yeyote ile
 
Pole yake sana... Usimtegemee sana binadamu mwenzako...
 
Tuna wajibu wa kuwatunza wazee wetu jamani. Mafanikio ni hali ya kuwa na uwezo wa kuisaidia familia na wategemezi wako.
 
Back
Top Bottom