Baba Askofu Munga: Je, Askofu Mwamakula ni mfia imani na shujaa?

Baba Askofu Munga: Je, Askofu Mwamakula ni mfia imani na shujaa?

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
Na baba Askofu Stephen Munga

JE, ASKOFU MWAMAKULA NI MFIA IMANI NA SHUJAA?!

Kwa muda sasa tulikuwa tukimsikia Baba Askofu Emmaus Mwamakula akiandaa matembezi ya hiari kwa ajili ya kudai Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Haya ni matakwa ya watu wengi kulingana na maoni yaliyomo katika taarifa ya Tume ya Warioba. Kwa hiyo kwa Watanzania, anachokisema Askofu Mwamakula sio jambo jipya na wala sio matakwa yake bali anakariri maoni ya wengi.

Jana ilisikika kwamba Baba Askofu amechukuliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano. Ni matumaini yangu, kama waonavyo watu wengine, kwamba polisi watatenda kwa haki pasipo kuvunja sheria au kukiuka misingi ya haki za binadamu wanaposhughulikia jambo la Baba Askofu Mwamakula. Tunashukuru kwamba Baba Askofu ameachiliwa kwa dhamana.

Nia yangu hasa ni kutafakari kwa kifupi falsafa muhimu ninayoiona katika juhudi za Askofu Mwamakula. Huu ni ufafanuzi wangu kwa jinsi ninavyomuelewa Baba Askofu kupitia maandiko yake. Askofu Mwamakula ni msomi wa theologia na falsafa kwa hiyo naamini kwamba hapa tunavinjari pamoja katika ukurasa mmoja. Mawazo niwekayo hapa sio hekaya bali ni jambo la msingi katika mijadala katika historia ya Wafia Imani (matyrs) ambao pia huitwa mashujaa wa imani. Nakiri kwamba nilichoandika hapa ni tone tu katika bahari ya maarifa juu ya elime ya Wafia Imani na mashujaa.

Mara kadhaa nilivyokuwa namsoma Baba Askofu Mwamakula nilikuwa najiuliza: Je, ni kwa roho gani anafanya haya? Mbona hana hofu wala wasiwasi? Mbona amejiingiza katika misioni ngumu na ya hatari hivi? Majibu sahihi ya maswali kama hayo anayo Baba Askofu Mwamakula moyoni mwake. Mawazo yangu hapa ni maelezo ya ulinganifu kati ya niliyoyasoma kwa Askofu Mwamakula na maarifa nijuayo kutoka historia juu ya mambo yafananayo na hayo.

Mfia imani ni mtu yule anayechagua kujitoa kafara ya maisha yake. Huyu anakubali maumivu na mateso badala ya kuachilia msimamo/mtazamo wake juu ya kitu anachosadiki kuwa ni kitakatifu au cha thamani kuu. Sifa kubwa ya kundi lao ni kwamba watu wa jinsi hiyo hawamaliziki kwa mateso na vifo. Mateso na vifo ndio kichocheo cha kuwaongezea nguvu, msimamo na ushirikiano. Tena Upo usemi kwamba damu yao inayomwagwa ndio mbegu ya kuzalisha mashahidi wengi zaidi.

Mfia imani ni shujaa. Ushujaa wa mfia imani umo katika kiapo cha kutimiza wajibu au utume/misioni yake. Kwa hiyo kwa shujaa kuutoa uhai wake ni utumishi kwa kutimilika kwa kiapo cha wajibu wake.

Mfia imani na shujaa hufa kila mmoja peke yake. Wafia imani ni wingi wa mfia imani mmojammoja. Mashujaa ni wingi wa shujaa mmojammoja. Kila mmoja hufa kwa kiapo chake. Hata wakifa hamsini kwa mara moja kila mmoja peke yake ni shujaa. Tena katika hao hamsini kifo cha kila mmoja kina nguvu na uzito mkubwa sawa na wote kwa pamoja.

Mwiko na adui mkubwa wa mashahidi wafia imani ni woga. Vilevile mwiko na adui mkubwa wa mashujaa ni woga. Nimesoma historia lakini sijawahi kusikia mfia imani mwoga na shujaa mwoga. Mtu mwoga kwa kawaida hukimbia mateso na kifo. Kukimbia huko kwaweza kuwa kwa njia ya kukana imani au kusaliti kwa kutoa siri za misioni na kundi. Ndio sababu Bwana Yesu aliangaliza kwamba waoga hawataingia mbinguni.

Wafia imani na mashujaa sio waoga. Hii haina maana kwamba mashujaa wachezee uhai wao na kujiachilia ovyo kwa mateso na vifo. La hasha! Makundi haya yote ni mawakili wa uhai wao kwa kiwango cha juu. Bali inapofikia hatua ya kwamba hakuna vinginevyo ndipo huchagua kifo na mateso baadala ya kukana imani na kusaliti kiapo cha utumishi.

Ikiwa anayofanya Askofu Mwamakula ni roho ya imani yake; na kwamba katika kiapo chake cha kichungaji afanyalo ni wajibu wake; basi hatanyamaza. Hili silo jambo la kuigiza kwani hakuna maigizo katika viapo vya utume. Pia katika mazingira ya jinsi hiyo shujaa yu tayari kufa peke yake kwa sababu ya imani na kiapo. Ndivyo alivyokufa Yohana Mbatizaji; ndivyo alivyokufa Bwana Yesu; na ndivyo walivyokufa Manabii, Mitume na Wafuasi waaminifu wa Kristo. Hawa wote walikufa huku watu wachache wakikubaliana nao bali walio wengi wakiwashutumu na kuwalaumu.

Msukumo wa ndani juu ya malengo ya kampeni hii anayo Baba Askofu Mwamakula. Ameifanya hii kuwa ni misioni yake ya kupigania mambo yale mawili. Namuombea Baba Askofu Mwamakula ili awe na afya njema kimwili na kiroho katika kipindi hiki kigumu kwake. Nawaombea na watu wengine wote waliomo katika mazingira kama hayo ya Askofu Mwamakula. Pia naliombea Jeshi la Polisi ili litimize wajibu wake kwa ufanisi na kutenda haki. Nawapongeza wale wote waliosimama na Askofu Mwamakula na kupaza sauti zao. Bila shaka walifanya hivyo kwa mioyo ya upendo na kiu ya haki. Pia naamini kwamba walipaza sauti wakijua kwamba mamlaka husika, hususan jeshi la polisi, zitasikiliza na kuchukua hatua kama walivyofanya.

Amani iwe kwenu.
 
Nchi hii eti wanaodai katiba mpya ,katiba itakayounda institutions imara za utawala wa nchi yetu,katiba itakayo wezesha nchi kupata viongozi Bora eti wanakamatwa na police na kutangazwa kupuuzwa na police Kisha wachumia tumbo wachache wanaohangaika kutaka mtawala aongezewe muda wanaonekana mashujaa.Unaweza kuita nchi hii jina gani zaidi ya kukubaliana na Trump kuwa viongozi tulionao wamepelekea nchi hii ionekane ni zaidi ya shithole
 
Tuna safari ndefu sana Mkuu lakini hakuna jinsi bali ni kupambana tu na hawa wahuni ambao hawataki kuona usawa kwa Watanzania wote na haki isiyopindishwa popote pale na kwa Mtanzania yoyote yule bila kujali kabila lake, itikadi yake na rangi yake.
Nchi hii eti wanaodai katiba mpya ,katiba itakayounda institutions imara za utawala wa nchi yetu,katiba itakayo wezesha nchi kupata viongozi Bora eti wanakamatwa na police na kutangazwa kupuuzwa na police Kisha wachumia tumbo wachache wanaohangaika kutaka mtawala aongezewe muda wanaonekana mashujaa.Unaweza kuita nchi hii jina gani zaidi ya kukubaliana na Trump kuwa viongozi tulionao wamepelekea nchi hii ionekane ni zaidi ya shithole
 
Dawa pekee ya kuiondoa ccm ni kupitia Tume Huru ya Uchaguzi na pia Katiba ya Wananchi.

Hivyo namuunga mkono huyo Askofu Mwamakula kwa ujasiri wake wa kuwasemea mamilioni ya Watanzania wapenda mabadiliko.
Bila watu kufa nakuhakikishia hawa wabaguzi na wachumia tumbo wa ccm hawawezi achia nchi hii
 
Wako vizuri sana Mkuu. Imagine kama viongozi wote wa dini bila kujali imani zao wangekuwa na misimamo thabiti kama hawa katika kupinga maovu na udhalimu wa huyo anayejiita mwendawazimu, ni lazima angekaa chini na kusalimu amri.


Hawa maaskofu wanaonekana wameenda shule vizuri sana, kila nikayasoma maandiko yao najiona kama nakula chakula fulani cha ubongo ambacho kamwe huwa sichoki kuwasoma mpaka mwisho, hawa kwa hakika ni wateule.
 
Ni bahati mbaya sana kwa nchi yetu ambapo Jeshi la Tanzania limekuwa ndiye adui mkuu wa Watanzania wanaopigania mazingira ya utawala wa haki. Jeshi la Polisi, wakuu wa Jeshi la Polisi na Rais Magufuli, wajitafakari, wazitafakari nyendo zao, na kujipima katika nafsi zao ili kuona kama wanatembea na Roho wa Mungu au wamekubali kuwa wakala wa shetani katika Taifa letu.

Matendo mengi ya kishetani yaliyofanyika katika awamu hii aslani yanahitaji toba kubwa ili kuepuka laana ya Mungu. Mimi ni sauti tu, lakini yupo aliye mkuu mwenye agizo hili.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ni muda was. Kuchukua Hatua.Hitaji laWatanzania kwa Sasa Ni Katiba mpya na time huru yauchaguzi Wala sio eti Kuongezewa muda. ,Katiba, Katiba Ni Katiba ya wananchi na sio hi ya CCM.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ukigusa maswala ya "KATIBA MPYA" tu ujue umegusa maslahi ya Watawala wa CCM na CCM yenyewe...

Ukigusa sharubu za simba, mrejesho wake ni kurauliwa kisawasawa na simba huyo...

Kwa namna mambosasa alivyokuwa analishughulikia jambo hili la Baba Askofu Mwamakula, na kwa jinsi alivyokuwa anaropoka hovyo kwa lugha isiyo na staha wala maadili yenye nia ya kumdhalilisha Baba Askofu Emmaus Mwamakula, ni wazi kuwa amepewa "go ahead" na watawala kumshughulikia...

Lakini obviously, kwa mwenye akili timamu, na kwa mujibu wa sheria za Tanzania, Baba Askofu hakuna kosa lolote la kisheria alilofanya kwa sababu mtu kusema anahitaji katiba mpya na kuwahamasisha wengine wamuunge mkono si kosa la halijawahi kuwa kosa...

Hivyo kamanda wa polisi Kanda maalumu - DSM, afande Mambosasa anajua hili fika kuwa Askofu hana kosa lolote lakini kaamua kujitoa ufahamu ili kuwafurahisha "mabwana zake", waliomtuma ili wamlipe mshahara ajaze tumbo lake na kwenda chooni kujisaidia tu...!
 
Dawa pekee ya kuiondoa ccm ni kupitia Tume Huru ya Uchaguzi na pia Katiba ya Wananchi.

Hivyo namuunga mkono huyo Askofu Mwamakula kwa ujasiri wake wa kuwasemea mamilioni ya Watanzania wapenda mabadiliko.
Mwamba Mbowe mbona hana ushirikano na Mwamakula?
 
Ni kweli kabisa Mkuu hawa wahuni na majizi ya ccm wanahofia kuhusu uwepo wa Katiba Mpya na Tume Huru ya uchaguzi kwani hivi vikiwepo nchini ndiyo itakuwa kaburi lao hawa wahuni na Watanzania tutawazika rasmi nchini.
 
Naona umetumia maneno mengi sana kumuelezea Mwamakula! Siku hizi maelezo yote hayo unaweza kuyaeleza kwa maneno mawili tu - ANATAFUTA KIKI. Na kila mmoja akakuelewa.

Askofu Mwamakula siyo mfia imani, laiti, angekuwa hivyo - angeanza matembezi hayo bila kujali kuna anaye mfuata au la!
Lakini Mwamakula anataka umati uwepo, apate kiki!
Tunataka atende siyo maneno maneno tu mara ajitangaze kwa waandishi wa habari, mara Twitter etc. Hizo ni kiki! Aanze kutembea tu.
 
Kwa mwenye akili fupi kama ZWAZWA wewe! Kudai katiba mpya na Tume huru ni kutafuta kiki. Watanzania kama wewe ni nzigo mkubwa sana.,
Naona umetumia maneno mengi sana kumuelezea Mwamakula! Siku hizi maelezo yote hayo unaweza kuyaeleza kwa maneno mawili tu - ANATAFUTA KIKI. Na kila mmoja akakuelewa.
Askofu Mwamakula siyo mfia imani, laiti, angekuwa hivyo - angeanza matembezi hayo bila kujali kuna anaye mfuata au la!
Lakini Mwamakula anataka umati uwepo, apate kiki!
Tunataka atende siyo maneno maneno tu mara ajitangaze kwa waandishi wa habari, mara Twitter etc. Hizo ni kiki! Aanze kutembea tu.
 
Back
Top Bottom