Baba mlezi ananidai fidia kwa kunisomesha

Baba mlezi ananidai fidia kwa kunisomesha

Mafeking

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2018
Posts
225
Reaction score
471
Habirini wana jamvi,
Nimeona nilete kisa hiki jamvini mimi ni kijana nimelelewa na baba MLEZI na kanisomesha Hadi form six, na alitaka niishie hapo nisiendelee mbele.

Mimi nililazimisha kwenda chuo kwasababu malengo yangu hayakuwa niishie form six maana matokeo yangu yaliruhusu kwenda kujiunga na chuo, na hapo ndipo shida, matatizo na migogoro ilipoanzia maana Hadi na apply vyuo sikumwambia sababu hakuwa na point ya yenye uzito ya mimi kutoenda chuo, mfano wa sababu zake zilikuwa "chuo ni kupoteza muda" Sasa ikifika siku ya mimi kwenda kuripoti chuo nilikchokuwa nmechaguliwa niliona ni vyema nimuage Kisha nianze safari, lakini cha ajabu yeye alinijbu " we nenda lakini usiniambie wala usinihusishe Kwa lolote"

Baada ya kufika chuo nikaona nimjulishe kama nmefika salama lakini hakunipokelea simu zangu na hakuwahi kupokea simu zangu kuanzia hapo na hakuwahi ata kunipigia simu nikaona isiwe kesi nikamjulisha mama kuwa sipokelewi simu akajibu " endelea kumpigia usiache" nikaendelea kumpigia simu bila matokeo yoyote
Ikabidi niwe napiga Kwa mama ndipo mama ampatie simu niongee nae nilkuwa naumia ila nilijikaza, na nyumban wakawa hawaelewan ugomvi kila kukicha

Kipindi tunakaribia kufunga chuo nilikuwa sitamani kabisa kurudi nyumbani kwasababu ya hiyo migogoro.

Miaka kadhaa iliyopita mama akaamua kuondoka nyumba sababu yake kubwa anasema ni kunyanyasika na baba akao doka na kuwaacha wadogo zangu watatu

Na hivi karibuni wamefikishana mahakamani mama akidai talaka na mzee nae anadai FIDIA ya kunisomesha na mimi sitaki kuingilia ugomvi wao juzi juzi tu hapo mzee aliniomba mkoa ili tumzuie mama kuhusu hiyo talaka.

Naombeni ushauri juu ya hili kudai fidia maana Toka nilivoondoka nyumba kwenda chuo sijarudi tena tangu 2018 na Sasa nipo mtaani napambana.
 
Sasa we umefika mpaka chuo unashindwa vipi kungamua vitu vidogo kama hivo? Kuna sheria Gani mahakamani ya kudai fidia ya kumsomesha mtu tena kwa hiari yako??

Elimu yetu haisaidii kabisa

Huu ndo wakati sahihi utumie maarifa yako kumsaidia mama Ako acha kulia Lia kijana
 
Sasa we umefika mpaka chuo unashindwa vipi kungamua vitu vidogo kama hivo? Kuna sheria Gani mahakamani ya kudai fidia ya kumsomesha mtu tena kwa hiari yako??

Elimu yetu haisaidii kabisa

Huu ndo wakati sahihi utumie maarifa yako kumsaidia mama Ako acha kulia Lia kijana
Anadai kusomesha mtoto ni kuwekeza sasa ameona wamezinguana na mama kwahiyo anadai alipwe fidia hali yakuwa mama yangu IA amehusikia Kwa kiasi kikubwa kumsomesha mwanae kuanzia sekondari Hadi chuo kikuu.
 
Habirini wana jamvi,
Nimeona nilete kisa hiki jamvini mimi ni kijana nimelelewa na baba MLEZI na kanisomesha Hadi form six, na alitaka niishie hapo nisiendelee mbele.
Mimi nililazimisha kwenda chuo kwasababu malengo yangu hayakuwa niishie form six maana matokeo yangu yaliruhusu kwenda kujiunga na chuo, na hapo ndipo shida, matatizo na migogoro ilipoanzia maana Hadi na apply vyuo sikumwambia sababu hakuwa na point ya yenye uzito ya mimi kutoenda chuo, mfano wa sababu zake zilikuwa "chuo ni kupoteza muda" Sasa ikifika siku ya mimi kwenda kuripoti chuo nilikchokuwa nmechaguliwa niliona ni vyema nimuage Kisha nianze safari, lakini cha ajabu yeye alinijbu " we nenda lakini usiniambie wala usinihusishe Kwa lolote"

Baada ya kufika chuo nikaona nimjulishe kama nmefika salama lakini hakunipokelea simu zangu na hakuwahi kupokea simu zangu kuanzia hapo na hakuwahi ata kunipigia simu nikaona isiwe kesi nikamjulisha mama kuwa sipokelewi simu akajibu " endelea kumpigia usiache" nikaendelea kumpigia simu bila matokeo yoyote
Ikabidi niwe napiga Kwa mama ndipo mama ampatie simu niongee nae nilkuwa naumia ila nilijikaza, na nyumban wakawa hawaelewan ugomvi kila kukicha

Kipindi tunakaribia kufunga chuo nilikuwa sitamani kabisa kurudi nyumbani kwasababu ya hiyo migogoro.

Miaka kadhaa iliyopita mama akaamua kuondoka nyumba sababu yake kubwa anasema ni kunyanyasika na baba akao doka na kuwaacha wadogo zangu watatu
Na hivi karibuni wamefikishana mahakamani mama akidai talaka na mzee nae anadai FIDIA ya kunisomesha na mimi sitaki kuingilia ugomvi wao juzi juzi tu hapo mzee aliniomba mkoa ili tumzuie mama kuhusu hiyo talaka.

Naombeni ushauri juu ya hili kudai fidia maana Toka nilivoondoka nyumba kwenda chuo sijarudi tena tangu 2018 na Sasa nipo mtaani napambana.


1. Usimjibu vibaya ila moyoni mpuuze.
2. Hana halali yeyote ya kudai.
3. Ni vyema Mama yako akaondoka.
4. Usiwaingilie maaumuzi au utashi
5. Mama akitaka kurudiana mwache.

Mwombe na Mungu
 
Ww hapo ni kimbelembele endelea na maisha yako hawakuhusu .mambo ya wazazi usijiingize huyo mzee ukipata chochote mtumie na usimwambie mama yako.na ww wa kiume acha kuongea sana na mama yako kuhusu Babako ww mpende bila kuhusisha mamako
 
Mwanae yupi? mbona stori yako haina muunganiko
Iko hivi mzee alimuoa mama akiwa tayari na watoto wengine Kwa mke wake wa kwanza, kwahiyo jukumu la kumsomesha lilikuwa la mama kwasababu alikuwa akifanya biashara kinacho patikana wanamlipia kaka yetu asome hadi kamaliza chuo na mtaji kapewa lakini kwangu niliambiwa niishie kidato cha sita.
 
1. Usimjibu vibaya ila moyoni mpuuze.
2. Hana halali yeyote ya kudai.
3. Ni vyema Mama yako akaondoka.
4. Usiwaingilie maaumuzi au utashi
5. Mama akitaka kurudiana mwache.

Mwombe na Mungu
Asante sana mkuu mimi sina kinyongo nae nishamsamehe ila kurudi kwake ndio siwezi nafanya maisha yangu kwasasa
 
Anadai kusomesha mtoto ni kuwekeza sasa ameona wamezinguana na mama kwahiyo anadai alipwe fidia hali yakuwa mama yangu IA amehusikia Kwa kiasi kikubwa kumsomesha mwanae kuanzia sekondari Hadi chuo kikuu.
Mwambie akupatie risiti za matumizi ili uanze kumlipa.

Nadhani alifanya roho mbaya baada ya kukuona utasoma na kupata elimu ambayo itakukomboa. Hata hivyo usifanye roho mbaya kwa wadogo zako wa mama mmoja endelea kuwasaidia na kuwapenda kama vile haakuna issue yo yote ile.

Na wala usimjibu vibaya wala kumsema wewe mwambie asante baba kwa kunisaidia kupata elimu nzuri iliyonifungulia ufunguo kwenye maisha. Mwisho atajiona kama amekosea.
 
Mwambie akupatie risiti za matumizi ili uanze kumlipa.

Nadhani alifanya roho mbaya baada ya kukuona utasoma na kupata elimu ambayo itakukomboa. Hata hivyo usifanye roho mbaya kwa wadogo zako wa mama mmoja endelea kuwasaidia na kuwapenda kama vile haakuna issue yo yote ile.

Na wala usimjibu vibaya wala kumsema wewe mwambie asante baba kwa kunisaidia kupata elimu nzuri iliyonifungulia ufunguo kwenye maisha. Mwisho atajiona kama amekosea.
Sawa Asante Kwa ushauri wako
 
Mnaooa single mother, mkumbuke akiwa na mtoto wa kiume kataa, kimbia au ujiandae na vita mbeleni.
Maana katakuja kuwa kikwazo kwenye maisha yako baadaeb, ukimsoma na kuchambua kwa makini utagundua huyu kijana yupo upande mmoja na mama yake.
 
Back
Top Bottom