Baba mzazi wa Diamond Platnumz Mzee Abdul Juma ametoa wito kwa mwanawe kuelewana na Harmonize

Baba mzazi wa Diamond Platnumz Mzee Abdul Juma ametoa wito kwa mwanawe kuelewana na Harmonize

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2021
Posts
630
Reaction score
1,262
Baba mzazi ya Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma ametoa wito kwa mwanawe kuelewana na mwenzake wa zamani Rajab Abdul Kahali almaarufu kama Harmonize.

Alipokuwa kwenye mahojiano na Mbengo TV hivi majuzi, mzee Abdul alimsihi Diamond ashiriki kikao na Harmonize wazungumzie tofauti zao na waelewane.

Mzee huyo ambaye alitengana na mamake Diamond, Mama Dangote miaka mingi iliyopita ameomba serikali na walio karibu na nyota wale wawili wa Bongo kuwapatanisha kuona kuwa wote wanaipeperusha bendera ya Tanzania.

"Wakae tu waelewane, hii dunia ni mapito basi. Yakitokea maneno kama haya wanaotoa hisia wawaagize waelewane wawe pamoja. Alafu tena waziri wa michezo kama yupo vilevile kuna uwezekano wa kuwaita. Mama Naseeb Sanura na Shamte kama wana uwezo wanaweza wakawaita wakaomgea, wakawaweka chini. Watoto kama watawasikiliza waongee kama ndugu waelewane" Alisema Mzee Abdul.

Mzee Abdul alisema hana kinyongo chochote dhidi ya mwanawe wala mpenzi wake wa zamani, Mama Dangote kwani alishawasamehe na kusahau yaliyopita.

unnamed (1).jpg
 
Mzee anatafuta huruma kwa Tembo? Simba alishamaliza hili swala kifamilia
Na Harmonize akimchukua Baba ake Diamond amlee kama Baba yake itampaisha sana kimuziki, tunasema itampa kiki mana Mondi na mama yake walishamkataa wenyewe so yeye amchukue afanye nae tour kwenye show zake then ampe nafasi ya kuongea machache.

Atammaliza sana Mondi wabongo tunapenda tuvitu vitu vidogo vidogo visivyo na mantiki sana then tunavipa headlines na kuvifatilia sana.
 
Na Harmonize akimchukua Baba ake Diamond amlee kama Baba yake itampaisha sana kimuziki,tunasema itampa kiki mana mondi na mama yake walishamkataa wwnyewe so yeye amchukue afanye nae tour kwwnye show zake then ampe nafasi ya kuongea machache.

Atammaliza sana mondi wabongo tunapenda tuvitu vitu vidogo vidogo visivyo na mantiki sana then tunavipa headlines na kuvifatilia sana.
TUNATAKA MUZIKI SIO KUTUMIA KIKI CHA MUHIMU AJITAHIDI KUTUMIA MUZIKI WAKE KUPATA UMAARAFU NA SIO KUDANDIA KIKI

YEYE ANA NDUGU WANGAPI WANAHITAJI MSAADA NA HAJAWACHUKUA KUWALEA??
 
Baba mzazi ya Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma ametoa wito kwa mwanawe kuelewana na mwenzake wa zamani Rajab Abdul Kahali almaarufu kama Harmonize.

Alipokuwa kwenye mahojiano na Mbengo TV hivi majuzi, mzee Abdul alimsihi Diamond ashiriki kikao na Harmonize wazungumzie tofauti zao na waelewane.
Huyo apumzike tu afanye issues nyingine, kujianika anika kwenye media hizi hakuto msaidia chochote umri umeenda cha msingi akomae kimpango wake na watoto wake alio wapata uzeeni.
 
Back
Top Bottom