Baba niruhusu nizae

Baba niruhusu nizae

Kumbe tupo wengi.story yake inafanana na yangu kwa asilimia kubwa. mimi nilipofikisha umri huo nikaamua kuzaa bila ndoa. sasa hivi ni 36 na katoto kangu kana miaka miwili. nina mfurahia sana mtoto wangu sasa napambana kwa ajili yake. na nina amani mambo ya ndoa nilishayaweka kwenye dampo la taka sasa ni kupambana tu na maisha. unaweza subiri ndoa mwisho wa siku umri ukakuacha kabisa ndoa ukakosa na mtoto ukakosa vilevile.
Uko sahihi ni afadhali yenu wanawake ukitaka mtoto ni rahisi hasa kama huna matatatizo ya uzazi ila kwetu wanaume ikikutokea unaweza kuzeeka bila mke wala mtoto maana hakuna hata mwanamke anaekubali kukuzalia mtoto hata akipata mimba yako anaitoa
 
sitaki kuolewa na kitunguu maji. kile hivi mtu hajui maisha nini si kwamba ni mtoto mdogo ni mtu mzima na hana familia wala mtoto ila majukumu hataki wa nini sasa.
Huwez kuolewa na kitunguu maji kile ila ulimvulia chupi na kumpanulia mapaja na ukapokea shahawa zake na ukamzalia 😂 akili za wanawake bhana 🙌
 
Miaka 34 bado kijana kabisa huyo,


sarah mke wa Ibrahim Baba yetu wa Imani kwa ulimwengu wote na dini na madhehebu yote alizaa MTOTO akiwa na miaka 90, Yeye huyo ana miaka 34 Hofu ya kutokupata MTOTO imeanza kumuingia kweli?😁


Ndiyo tatizo la kukaa MBALI na UPENDO hivyo anakuwa affected na Time na mambo na space, UPENDO upo nje ya kila kitu na hauathiliwi na chochote na unajitocheleza kwa kila kitu na haja zote, mwenye UPENDO NDANI yake kamwe hawezi kuhisi au kuona amechelewa au amepungukiwa B'se UPENDO umekamilika, UPENDO ni mkamilifu hauna kasoro yoyote hivyo mtu anapoupa ruhusa ya kuchukua nafasi NDANI yake hukamilisha katika kila jambo na kamwe hawezi kuathiliwa na chochote

Acha kuingiza stori za kusadikika kwenye mambo halisia.

Hao kina sara waliozaa na miaka 90 wa kwenye biblia ni fictional character. Huku mwenzake ni real person na tatizo lake ni halisia.

Mfano biblia imeandika nyoka anaongea.. wewe na akili zako unaamini ni kweli kuna nyoka ambaye anaongea ?

Hakuna mtu halisia aliyezaa na miaka 90 zaidi ya hizo hadithi za kwenye biblia
 
Hayo ni maombi ya mdada mmoja ambae,nilimlea toka akiwa na miaka 3 hadi kumfikisha chuo kikuu,kwa ngazi ya shahada ya uzamili,sasa ana miaka 34,hajazaa,hajaolewa.

Kila akipata mwanaume hafiki nae mbali,japo ni mdada ambae hanywi pombe,havuti sigara,sio mtu wa kutoka out na nimemlea kwa dini ya kikatoliki japo mie ni muislamu,kwani ndio dini ya wazazi wake ambao kwa sasa hawako duniani

Ana kazi yake na kipato japo sio kikubwa.Kasubiri sana kupata mchumba hapati,tunaongea nae sana,nilimuomba padri wake anakosali amuombee,lakini hakuna kitu,alipata wanaume kama 3 hivi na kumbe walikuwa wanamtapeli maana wote wana wake.

Sasa jana kanipigia simu,baba niruhusu tu ni zae bila ndoa, umri unapita,aisee bila kuficha nililia sana,mwishowe nimemwambia sawa,fanya roho yako itakavyokuongoza
Yaani unalia as if uchi ni wako?
 
Mimi nafikiri wengi tunaishi bila purpose ( kusudio) .

Kusudio la kuumbwa kwako ni nini!?, Unamatarajio gani na Hilo kusudio lako!?. Hatuwezi kukwepa kuhuzunika lakini ukiwa na lengo ambalo upo tayari kulitimiza, hata usipokuwa na ndoa Wala mtoto haikuumizi sana kichwa.

Mwanamke hakuumbwa kwaajili Moja tu ya kuolewa na kuzaa, kwa Imani yangu lengo lake kuu ni kumuabudu mola wake, akiitengeneza nafsi yake na moyo wake kwamba ndoa na watoto huja kma ziada lakini lengo kuu ni Hilo basi moyo haupati tabu kubwa na unakuwa na amani hata kma utafikisha 30+ bila ndoa Wala mtoto.

Lakini nafsi ikishakaa hapo nataka ndoa , nimekosa ndoa nizae tu, unajikuta unachezewa na wengi, watakuja na gia ya ndoa baada ya hpo haoo wanasepa.
 
Hayo ni maombi ya mdada mmoja ambae,nilimlea toka akiwa na miaka 3 hadi kumfikisha chuo kikuu,kwa ngazi ya shahada ya uzamili,sasa ana miaka 34,hajazaa,hajaolewa.

Kila akipata mwanaume hafiki nae mbali,japo ni mdada ambae hanywi pombe,havuti sigara,sio mtu wa kutoka out na nimemlea kwa dini ya kikatoliki japo mie ni muislamu,kwani ndio dini ya wazazi wake ambao kwa sasa hawako duniani

Ana kazi yake na kipato japo sio kikubwa.Kasubiri sana kupata mchumba hapati,tunaongea nae sana,nilimuomba padri wake anakosali amuombee,lakini hakuna kitu,alipata wanaume kama 3 hivi na kumbe walikuwa wanamtapeli maana wote wana wake.

Sasa jana kanipigia simu,baba niruhusu tu ni zae bila ndoa, umri unapita,aisee bila kuficha nililia sana,mwishowe nimemwambia sawa,fanya roho yako itakavyokuongoza
Ni sawa. Azae, tayari umri ushaenda sana. Jioni kwake ishafika. Na after all ni mtu mzima kama wewe. Period!!
 
Mkuu mtoa uzi kwanza pile kwa hayo maswaibu japo ni mambo ya kawaida kwa jamii ya sasa. Kuna mambo nahisi hayapo sawa kwako na kwake pia, kama ni kweli basi akiyarebisha au mkiyarwbisha, basi ataolewa.

1. Inawezekana anatafuta mtu wako hadhi yake kulingana na elimu, kazi na kipato chake. Na hii ndio maana anaangukia kwa watu wenye familia kwa maana kuwa anapowaona for the first time anaona wa hadhi yake, wana maisha, wana kazi nzuri pengine wana push ndinga za maana. Naamini kabisa anatobgozwa na watu wengi ila nadhani atakua ana evaluyna kuona huyu hapana. Kama ndivyo basi aelewe kuwa, asilimia kubwa ya hao anaosema hapana, ndio waowaji ila hawajajipata tu. Aamini kuwa ipo siku nao watajipata watakua kama hao waume za watu wanaomvutia.

2. Kuna uwezekana upo nae karibu sanaa kiasi kwamba watu anaowapata wanapata mashaka juu ya ukaribu wenu. Ni kawaida mtoto wa kike kuwa karibu na mama na kumshiriksha mambo ya siri kama haya ila si kawaida kwa mtoto wa kike ku share mambo ya ndaani kama haya na baba yake, hii ni kwa mujibu wa mila zetu watu weusi. Sasa kama umemfanya sana kuwa mtoto wa baba, basi wanaume anaowapata huamininkabisa kuwa wakimuoa kuna external force itakua inashiriki kuendesha familia ambayo ni wewe baba yake. Wanaume hupenda kutawala kwenye familia zao na sio kuwa na mtu mwingine mwenye kuendesha kwa mfano wa rimont. Yaani kuna uwezekana kuna mambo huwa wanazungumza kama wapenzi halafu binti anasema ngoja nitaongea na baba, sio kitu kibaya ila ikizidi inaleta wasiwasi wa huko mbele itakuaje nikimuoa. Kama hilo lipo basi mzee wangu ni la kurekebisha tu na mambo yatakaa sawa.

Pole tena mkuu. Sema msiwe na hafu kiasi hicho. Wewe ukiwa hivi na hofu kubwa kiasi hiki nani atamwambia kuwa usiogope mambo yatakua sawa?
Moja ya tatizo kubwa la binadamu ni kutafuta dosari kwenye kila kitu,basi tambua yafuatayo:
1.mimi ni suriyama wazazi wangu mmoja alikuwa mtanzania na mwingine anatokea ulaya na makuzi yetu,tumelelewa kwa tamaduni mbili
2.huyo mwanangu hakuwa anachagua watu wenye kipato na ndio maana kaamua kuzaa ni mtu ambae uwezo wake ni mdogo sana
3.ukaribu wangu na mwanangu una mipaka,sio kwamba namtawala au namregulate,la niko nae karibu sana lakini with limitations
4.japo amesoma vizuri lakini ni mwanamke mwenye heshima na nidhamu ya juu sana na namjivunia sana
 
Kumbe tupo wengi.story yake inafanana na yangu kwa asilimia kubwa. mimi nilipofikisha umri huo nikaamua kuzaa bila ndoa. sasa hivi ni 36 na katoto kangu kana miaka miwili. nina mfurahia sana mtoto wangu sasa napambana kwa ajili yake. na nina amani mambo ya ndoa nilishayaweka kwenye dampo la taka sasa ni kupambana tu na maisha. unaweza subiri ndoa mwisho wa siku umri ukakuacha kabisa ndoa ukakosa na mtoto ukakosa vilevile.
NDOA si shida, shida ni kuiishi hiyo NDOA. Ishi namna hiyo ikibidi ili uepuke kuwa Mwanafalsafa wa WANAUME WOTE NI MBWA hapo baadae.
 
Uko sahihi ni afadhali yenu wanawake ukitaka mtoto ni rahisi hasa kama huna matatatizo ya uzazi ila kwetu wanaume ikikutokea unaweza kuzeeka bila mke wala mtoto maana hakuna hata mwanamke anaekubali kukuzalia mtoto hata akipata mimba yako anaitoa
Ndo hivyo ndugu yangu dunia hii haijawahi kuwa na usawa unaepata hili anakosa lile. ila bado watu hataacha kukunyoshea kidole utafikiri wao hawana makosa. kikubwa ni kutokuwajali na kufanya kile unaamini.
 
Back
Top Bottom