Baba wa Taifa angekuwepo angeyasema haya kuhusu Bunge

Baba wa Taifa angekuwepo angeyasema haya kuhusu Bunge

Mantombazane

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
579
Reaction score
367
Baba wa taifa Mwalimu Nyerere alikuwa ni jasiri sana kuwanyooshea vidole viongozi wazembe na wasiojielewa huku akitumia maneno makali bila woga muda wowote wanapomkera au wanapofanya ndivyo sivyo. Alitumia maneno kama wahuni, wapumbavu, wajinga nk.

Mfano angekuwepo leo angesema bunge letu linaendeshwa kihuni na kwa maana hiyo wanaoendesha chombo hicho ni wahuni kwakuwa hawafuati sheria, taratibu na katiba ya nchi badala yake wanaoongoza kwa matakwa yao kiasi kwamba hata wabunge wasiokuwa na sifa wanaingizwa bungeni na kulipwa pesa nyingi sana za wananchi wanyonge.

Vile vile angekuwepo leo angesema bunge limejaa upambavu na ujinga mwingi hivyo kushindwa kuisimamia serikali vizuri badala yake limegeuka kama jumuiya ya chama tawala au tawi la wakereketwa na kuwa kijiwe cha mipasho isiyokuwa na tija kwa nchi.

Angekuwepo leo angekemea vikali uvunjwaji wa katiba na uhuni uliofanyika wa kuwaingiza bungeni mamluki hivyo kuitia hasara kubwa nchi hii. Sasa kwakuwa hayupo hakuna tena kiongozi mwingine aliyepo au aliyestaafu anayeweza kukemea wendawazimu huo.
 
Nii jukumu la kila mmoja wetu kukaripia uhuni wa Jobo.

1622640700077.png
 
100% I concur with you, Wazee Waliobaki Wanajua fika kwamba Bunge linaendeshwa kihuni na kwamba halina tija yoyote isipokuwa sehemu ya Kufuja hela la Wavuja jasho. Inakuwaje Unawalipa Pesa watu ambao unajuafika ya kwamba sio wabunge. Je ni kwa faida ya nani?. Kweli Nyerere asingekaa kimya kwa Upuuzi wa COVID - 19
 
Nii jukumu la kila mmoja wetu kukaripia uhuni wa Jobo.

View attachment 1806039
Nimesikiliza mara kadhaa "video clip" ya sakata la vazi la Mbunge sijaona kasoro ya mtoa hoja na Spika.

Suala hilo limekuzwa pasipo sababu kwa lengo la kuwadharilisha wanawake kupitia huyo Mbunge. Mitaani wanawake siku hizi wanavaa hovyo, kuanzia watoto wadogo hadi vikongwe
 
Bahati mbaya hata mama yao ni mwimba tasrabu.
 
Nchi hii kweli tumekosa mtu wa kumwambia Sabufa kwamba anavunja katiba?
Warioba,
Msekwa,
Makinda,
Msuya,
Kikwete,
Shein,
Malecela,
Wapigwe tu,
Sumaye,
Laigwan,
Sasa Nani atatusemea? Najua angekuwepo Sokoine ingekua Jambo dogo sana.
 
Ni ajabu kama Taifa tungemtegemea Mzee wa miaka 99, kumkemea spika.
Taifa lenye Vijana na Wazee wenye nguvu, linaposhindwa kumkemea mtu mmoja anaitwa Spika. Hapo ujue kuna tatizo kubwa zaidi ya Spika.
 
Nchi hii kweli tumekosa mtu wa kumwambia Sabufa kwamba anavunja katiba?
Warioba,
Msekwa,
Makinda,
Msuya,
Kikwete,
Shein,
Malecela,
Wapigwe tu,
Sumaye,
Laigwan,
Sasa Nani atatusemea? Najua angekuwepo Sokoine ingekua Jambo dogo sana.
NAOMBEA VIONGOZI WADINI WAIBUKE NA NYARAKA MAALUM IUU YA KUKANYAGWA KWA KATIBA NA KINGA ZA VIONGOZI.PIA NDUGAI AJIUDHURU NA NAIBU KWA KUISIGINA KATIBA.ILE DUA YA VIKAO VYA BUNGE ITAFSIRIWE NA VIONGOZI WA DINI KWANI HAIAKISI NA JOB
 
Bahati mbaya hata mama yao ni mwimba tasrabu.
Ila mama naye kazubaa sana kwenye hili. Mwendazake alishinikiza uvunjaji wa katiba ilikuwa ni juu yake sasa kurekebisha haraka lakini naona ameanza kuzunguka zunguka kama vile haoni lakini sio sifa nzuri kwake na kwa nchi kwa ujumla. Huyu spika wake ndiye sala zote zinaelekezwa kwake kuwa naye aende zake kwani hasikii na ni mbishi sana anijifanya ndiye kidume aliye baki nchi hii
 
Back
Top Bottom