Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #301
Mkaza...Dah huyu mzee mwanzoni nilimchukulia Kama mtu mwenye elimu kubwa ya historia ya nchi lkn nadhani nilikosea. Ni mtu mwenye maarifa mengi ya UDINI Kila anachokiandika ni kulialia tu mwingine ni FaizaFoxy Hawa watu mh Kama ni dini Basi wameipokea vibaya. Bahati nzuri watanzania waislamu kwa wasio waislamu, wakristo kwa wasio wakristo hawana muda na UDINI lkn wako busy na DINI zao
Ni wazi hawa Wahamiaji wote walisilimu baada ya kuanza kuishi Tanganyika. Ushahidi ni majina yao wakati wanaingia Tanganyika, na haswa huyo Afande Plantan hadi mwanae akaamua kumuita Thomas. Kwa kifupi hayo uliyoeleza hayathibitishi hoja yako kuwa Wazulu walikuwa waumini wa Uislamu huko kwao Uzuluni, bali baada ya kuondoka/kuhama huko Uzuluni na kuanza kuchanganyika na watu wa imani ya Kiislamu.SYL...
Schmidt,
Wamanyema asili yao ni Congo na Wazulu ni Afrika Kusini.
Umesahau kuwataja Wanubi,
Hawa wanatoka Sudan.
Kuhusu dini ya Kiislam kwa Wazulu Kleist Sykes anaeleza katika mswada wake wa kitabu alioandika kabla hajafa mwaka wa 1949 kuwa baba yake Sykes Mbuwane aliingia Germany Ostafrika na ndugu yake Ali Katini.
Hawa Wazulu waliletwa na Hermann von Wismann na kiongozi wa jeshi hili la Wazulu alikuwa Chief Mohosh ambae baadae akiwa Tanganyika alikuja kujulikana kama Affande Plantan.
Affande Plantan ndiyo baba wa Thomas Saudtz Plantan, Schneider Abdillah Plantan na Ramadhani Mashado Plantan.
Katika jeshi hili alikuwapo Machakaomo baba yake Hassan Machakaomo aliyekuja kuwa mmoja wa viongozi wa Yanga miaka ya 1940.
Wote hawa Wazulu na Waislam.
Schneider Plantan yeye alikuwa Katibu wa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir katika Daawat Islamiyya.
Nakuwekea hapo chini kipande kutoka mswada wa kitabu cha Ally Sykes, ''Under the Shadow of British Colonialism in Tanganyika:''
''My aunt came to see me.
When I narrated the family history she broke down in tears.
My aunt took us to Kwa Likunyi a village where my uncle Kattini Mbuwane lived, this village was some few miles from Nyambane where Sykes Mbuwane had originally settled when the clan trekked north from South Africa.
There I was informed that my uncle had died only some few months back.
All that was left me to do was to go and pay respect to his grave, as is the custom for Muslims.
My uncle had left behind three children, my cousins, Abdallah, Ahmed and Asya.
The family was well to do.
Abdallah the eldest child had his own fishing boat and was therefore financially independent.
Somehow my cousins were not too happy to see me, they thought I had gone there to claim property left behind by uncle Kattini.
They did not believe that after fifty years I, the child of a Zulu who had settled in Tanganyika many years ago would spend so much money to travel all the way from Tanganyika to Mozambique just to visit and get to know an uncle I had not even seen.''
(''Under the Shadow of British Colonialism in Tanganyika The Autobiography of Ally Kleist Sykes,'' As told to Mohamed Said)
Mzee Said, next time hoja ikikushinda tupotezee na ile picha yako ukinywa chai Paris. Hii inaboa.Masta...
Hawakuona mbali hata kidogo.
Kwa muda walifanikiwa na historia ikawa ndiyo hiyo uijuayo wewe kwa miaka mingi.
Ghafla siku moja gazeti la Africa Events (AE) likachapa makala ya Mohamed Said inaeleza histori ya TANU ambayo watu wengi walikuwa hawaijui.
Huu ulikuwa mwaka wa 1988.
Gazeti likaanza kununuliwa kwa wingi siku ile kwa kile kilichokuwa kimeandikwa.
Taarifa ilipowafikia wahusika haraka magazeti yale yakakusanywa na siku ya pili kila aliyekwenda kuliuliza AE aliambiwa limekwisha.
Hawakuwa wameona mbali kuwa itakuja siku historia hiyo waliyoifuta itaandikwa.
Wataweza kukuwaiysanya kila siku gazeti litakalotoka na stori ya TANU wasiyoipenda watakusanya toleo zima?
Mwaka wa 1990 gazeti la Annuur likaanzishwa na katika gazeti hili likaanza kuchapa historia ya TANU kama ilivyostahili.
Wasomaji wakawa wanalingojea Annur siku ya Ijumaa kwa hamu wanataka kusoma Mohamed Said amekuja na nini leo.
Hawakuwa wameona mbali kama ulivyowasifia.
Kinyume chake wakawa wamejivua nguo hadharani.
Mwaka wa 1998 ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) the Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' kikachapwa London.
Kizazaa kitabu kilipoingia nchini na kuanza kuuzwa.
Hawakuwa wameona mbali.
Kitendo cha kuifuta historia ya kweli kikawafanya watu sasa waanze kuisoma historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika upya.
Kitabu kikaibua wazalendo ambao hawakupata kusikika kabla.
Kitabu kikatafsiriwa na kuchapwa Nairobi 2002 ili watu wakisome kwa Kiswahili.
Sikutegemea hata kwa mbali.
Kitabu kikachapwa mara 4 na sasa tunakwenda toleo la 5.
Hawakuwa wameona mbali.
View attachment 2103289
Day...
Toka uhuru 1961 Waislam ndani ya serikali wamekuwa pungufu katika kila kitu hadi imezoeleka.
Tofauti unakuja pale inapokuwa nafuu kuwa angalau wameongezeka.
Kulikuwa na malalamuliko kwenye board ya parole kwa wajumbe kuelemea upande mmoja, wajumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba, nafasi za elimu kuanzia sekondari hadi chuo kikuu nk. nk.
Hili limekuwa tatizo kubwa na la kudumu.
Sesten...Mzee Said,
Nayakumbuka mambo matatu kama mifano mnasaba wa uzi hu;
1. Bodi Taifa ya Parole hapa nchini iliteuliwa na Frderick Tluway Sumaye aliyekua Waziri Mkuu wakati wa Urais wa Marehemu Benjamin Mkapa. Sumaye aliteuwa wajumbe wote wa bodi wa imani moja bika kuwepo muislam hata mmoja. Miongoni mwao walikuwepo padri mmoja na mchungaji mmoja
Alipoulizwa kwanini kafanya hivyo akajibu kwa ukali sana kwamba watu waache kupanda mbegu za udini maana hatukukelewa hivyo na Mwalimu Nyerere. Uteuzi uliofanyika ulizingatia merits za walioteuliwa!
Siku chache baadae Marehemu Mzee Mkapa akatengua uteuzi wa bodi nzima na akaagiza iundwe upya kwa kuzingatia uwiano wa kijamii kama maeneo wanapotoka wajumbe na pia uwiano wa imani za watu kwa maana ya dini
2. Professor mmoja wa UDOM aliyekua VC alipata malalamiko kuhusu baadhi ya watu kutotendewa haki kwenye admission. Wakati huo TCU ilikua haijaundwa
Alipoamua kuitisha applications zote akakutana na maajabu! Kuna zaidi ya applicants 350 walikua wameachwa huku wakiwa wame qualify huku kukiwa na idadi ya kutosha kabisa wakiwa wamepata admission wengine wakiwa below cutoff point ya Chuo!!!
Kwa “sudfa” au coincidence wote waliokua wameachwa kwa dhulma walikua na majina ya kiislamu na wote walioku admitted walikua na majina ya kikristo!!! VC akatoa order mchakato urudiwe tena japo jambo hilo lilikua down played
3. Miaka ya karibuni kulikua na zoezi la kuwaondoa waalimu wa masomo ya arts sekondari waajiriwa wa serikali kuwarudisha shule za msingi. Zoezi husika halikuwahusu waalimu wa masomo ya sayansi na hesabu
Nilikua mkoa fulani kipindi zoezi hili linaendelea. Kukatokea malalamiko kua zoezi hilo lina sura ya ubaguzi na waathirika ni Waislamu
Ofisa mmoja Muislamu katika idara ya elimu ambaye hapo awali alikua amejaribu kuomba uhamisho kwenda mkoa mwingine kwa zaidi ya miaka miwili bila mafanikio alipokea malalamiko hayo na baada ya kujiridhisha ni genuine akayapeleka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri.
Kikaitwa kikao kati ya Mkurugenzi, Afisa Elimu, Afisa Elimu Taaluma, Ofisa Utumishi na yule ofisa aliyeipeleka issue kwa Mkurugenzi. Wahusika wote kasoro yule aliyepeleka malalamiko walikua wakristo na ilivyoonekana baada ya kikao kuanza ni kutaka kum pin huyo ofisa kwanini analeta udini kwenye utendaji wa kazi za Halmashauri na hususan hilo zoezi la kitaifa
Walianza kumpa maneno makali kabda hata hawajamuuliza kuhusu ushahidi. Walipomuuliza atoe ushahidi wa madai yake akaoonyesha majina wa wahusika waliohamishwa
Shule ina waalimu 68 kati yao Waislamu 18. Waalimu wanaotakiwa kupelekwa primary schools ni 21. Basi wakaondolewa wale wote 18 wenye majina ya kiislamu na hao wengine 3 wasiokua waislamu
Kikao bado kikasema huo sio ushahidi maana Mkuu wa Kituo(Headmaster) ana discretion ya kuchagua mradi anafata secular iliyotolewa na Wizara(TAMISEMI)
Ndipo akaangusha bomu la atomic ambalo alikua hajawaambia before! Kwamba katika wale waalimu waislamu 18 watatu ni wa Mathematics na sita ni wa masomo mengine ya sayansi na akawaonyesha!
Kikao hakikuendelea. Mkurugenzi akamwambia Afisa Elimu akarekebisehe hilo tatizo
Wiki hiyohiyo yule Afisa akapata barua ya uhamisho aliouomba kwa miaka miwili bila mafanikio!!!!!!!!
Schmidt,Mzee Said, next time hoja ikikushinda tupotezee na ile picha yako ukinywa chai Paris. Hii inaboa.
Schmidt,Ni wazi hawa Wahamiaji wote walisilimu baada ya kuanza kuishi Tanganyika. Ushahidi ni majina yao wakati wanaingia Tanganyika, na haswa huyo Afande Plantan hadi mwanae akaamua kumuita Thomas. Kwa kifupi hayo uliyoeleza hayathibitishi hoja yako kuwa Wazulu walikuwa waumini wa Uislamu huko kwao Uzuluni, bali baada ya kuondoka/kuhama huko Uzuluni na kuanza kuchanganyika na watu wa imani ya Kiislamu.
Kama hukubaliani, tuwekee hapa historia ya Uislam ndani ya himaya ya Uzulu aka Zulu Kingdom/Zululand. Jee, Waarabu waliweza kupenyeza hadi huko na kueneza dini yao?
KUKATOKEA MALALAMIKO KUWA ZOEZI HILO LINA SURA YA UBAGUZI NA WAATHIRIKA NI WAISLAMSesten...
Ahsante sana ndugu yangu.
Allah akuzidishie.
Hakika umetusomesha vya kutosha.
Alhamdulilah.
Ukweli ni kwamba hawa wakristo kamwe hawawezi kuusema ukweli,na wala hawatokuwa tayari kukiri uozo huu kwa sababu wao ndiyo wanufaika wa mfumo.Mzee Said,
Nayakumbuka mambo matatu kama mifano mnasaba wa uzi hu;
1. Bodi Taifa ya Parole hapa nchini iliteuliwa na Frderick Tluway Sumaye aliyekua Waziri Mkuu wakati wa Urais wa Marehemu Benjamin Mkapa. Sumaye aliteuwa wajumbe wote wa bodi wa imani moja bika kuwepo muislam hata mmoja. Miongoni mwao walikuwepo padri mmoja na mchungaji mmoja
Alipoulizwa kwanini kafanya hivyo akajibu kwa ukali sana kwamba watu waache kupanda mbegu za udini maana hatukukelewa hivyo na Mwalimu Nyerere. Uteuzi uliofanyika ulizingatia merits za walioteuliwa!
Siku chache baadae Marehemu Mzee Mkapa akatengua uteuzi wa bodi nzima na akaagiza iundwe upya kwa kuzingatia uwiano wa kijamii kama maeneo wanapotoka wajumbe na pia uwiano wa imani za watu kwa maana ya dini
2. Professor mmoja wa UDOM aliyekua VC alipata malalamiko kuhusu baadhi ya watu kutotendewa haki kwenye admission. Wakati huo TCU ilikua haijaundwa
Alipoamua kuitisha applications zote akakutana na maajabu! Kuna zaidi ya applicants 350 walikua wameachwa huku wakiwa wame qualify huku kukiwa na idadi ya kutosha kabisa wakiwa wamepata admission wengine wakiwa below cutoff point ya Chuo!!!
Kwa “sudfa” au coincidence wote waliokua wameachwa kwa dhulma walikua na majina ya kiislamu na wote walioku admitted walikua na majina ya kikristo!!! VC akatoa order mchakato urudiwe tena japo jambo hilo lilikua down played
3. Miaka ya karibuni kulikua na zoezi la kuwaondoa waalimu wa masomo ya arts sekondari waajiriwa wa serikali kuwarudisha shule za msingi. Zoezi husika halikuwahusu waalimu wa masomo ya sayansi na hesabu
Nilikua mkoa fulani kipindi zoezi hili linaendelea. Kukatokea malalamiko kua zoezi hilo lina sura ya ubaguzi na waathirika ni Waislamu
Ofisa mmoja Muislamu katika idara ya elimu ambaye hapo awali alikua amejaribu kuomba uhamisho kwenda mkoa mwingine kwa zaidi ya miaka miwili bila mafanikio alipokea malalamiko hayo na baada ya kujiridhisha ni genuine akayapeleka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri.
Kikaitwa kikao kati ya Mkurugenzi, Afisa Elimu, Afisa Elimu Taaluma, Ofisa Utumishi na yule ofisa aliyeipeleka issue kwa Mkurugenzi. Wahusika wote kasoro yule aliyepeleka malalamiko walikua wakristo na ilivyoonekana baada ya kikao kuanza ni kutaka kum pin huyo ofisa kwanini analeta udini kwenye utendaji wa kazi za Halmashauri na hususan hilo zoezi la kitaifa
Walianza kumpa maneno makali kabda hata hawajamuuliza kuhusu ushahidi. Walipomuuliza atoe ushahidi wa madai yake akaoonyesha majina wa wahusika waliohamishwa
Shule ina waalimu 68 kati yao Waislamu 18. Waalimu wanaotakiwa kupelekwa primary schools ni 21. Basi wakaondolewa wale wote 18 wenye majina ya kiislamu na hao wengine 3 wasiokua waislamu
Kikao bado kikasema huo sio ushahidi maana Mkuu wa Kituo(Headmaster) ana discretion ya kuchagua mradi anafata secular iliyotolewa na Wizara(TAMISEMI)
Ndipo akaangusha bomu la atomic ambalo alikua hajawaambia before! Kwamba katika wale waalimu waislamu 18 watatu ni wa Mathematics na sita ni wa masomo mengine ya sayansi na akawaonyesha!
Kikao hakikuendelea. Mkurugenzi akamwambia Afisa Elimu akarekebisehe hilo tatizo
Wiki hiyohiyo yule Afisa akapata barua ya uhamisho aliouomba kwa miaka miwili bila mafanikio!!!!!!!!
Belo,
Tunaweza tukafanya mjadala wa adabu na heshima bila ya kejeli na kebehi.
Mathalan ukishanisoma na ukaona kuna jambo una fikra tofauti na zangu ukaeleza.
Sasa hii "kulia," na maneno ya kukashifiana yanatoa ladha ya mjadala.
Mzalendo...Shikamoo Mzee Mohamed Said. Huwa nikipata nafasi napitia baadhi ya mada zako. Mzee niseme tu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania idadi ya wanaojiita "Wakristo" ama "Waislam" imekuwa ikiongezeka kila uchwao ijapo "Uadilifu" na "uaminifu vinazidi kupungua kwenye jamii. Mzee Mohamed Said nadhani tungeongeza bidii katika madhabuhu kuongeza idadi ya watu wenye hofu ya Mungu na sio wanaojiita wajina fulani. Mzee Mohamed Said hizi juhudi ya kuwasemea watu wanaojiita majina fulani hazitasaidia taifa letu kabisa, "Nchi yetu inahitaji watu wenye Utu, Ubinadamu, Uadilifu na hofu ya Mungu na sio wa Dini fulani"
Natumaini sijakukwaza
Ahsante
H
Heshima yako Mkuu Mohamed Said. Mwaka wa 1976 au 77 nilipokuwa sekondari tulisoma kitabu " Kiu" kilichoandikwa na mtu mwenye jina la Mohamed Said, je huyu mtu ni wewe? Natanguliza Shukrani zangu
Udini ktk Taifa huru Tz,halikuja kwa bahati mbaya,Bali kulikuwA na mpango mkakati kabla ya Uhuru.Wewe jiulize imekuwaje huyu mtoto wa chifu wa wazanaki,kutaka kupewa na kuitwa MTAKATIFU na kanisa la Warumi,Kuna Mambo gani kawafanyia Warumi wa Tanganyika ,mpaka akapewa daraja la Mwenyeheri?
Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.
Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.
Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?
Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.
Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.
Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:
''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''
Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.
Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.
Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.
Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.
Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.
Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.
Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.
Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.
Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:
''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.
Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.
Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.
Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''
Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?
Waislam hawasemi kweli?
Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.
Tumefikaje katika hali hii?
Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.
Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.
Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.
Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.
View attachment 2096477
View attachment 2096478
Ghassany kaandika kwenye angle ya udini kama wewe.Wewe na huyo ni wafia dini.Ksk,
Nilikuwa msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti historia ya mapinduzi ya Zanzibar.
Kwa njia moja nimesaidia katika kufahamika kwa historia ya Zanzibar.
Nakushauri uisome historia ya Zanzibar vizuri kwanza kabla hujataka kuijadili.
Luku...Ghassany kaandika kwenye angle ya udini kama wewe.Wewe na huyo ni wafia dini.
Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.
Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.
Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?
Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.
Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.
Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:
''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''
Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.
Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.
Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.
Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.
Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.
Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.
Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.
Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.
Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:
''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.
Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.
Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.
Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''
Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?
Waislam hawasemi kweli?
Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.
Tumefikaje katika hali hii?
Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.
Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.
Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.
Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.
View attachment 2096477
View attachment 2096478
King...Ukweli ni kwamba hawa wakristo kamwe hawawezi kuusema ukweli,na wala hawatokuwa tayari kukiri uozo huu kwa sababu wao ndiyo wanufaika wa mfumo.
Muhimu ni sisi kusimama na kuendelea kuweka bayana ubovu huu bila ya kujali kejeri zao na matusi yao.
Island,Hii ni post ya kijinga sana , Mods poat kama hizi mnazipaje airtime ?
Huyu ni mhalifu tu kama vibaka wengine. A criminal and a felon.King...
Nimeona baada ya Sesten kuweka ushahidi ule wa yanayofanyika na watendaji wa serikali dhidi ya Waislam ukumbi umekuwa kimya sana.
Nimerusha ule ushahidi wake na umesomwa kwa kupasiana na umewafikia watu wengi.
Hili sikutegemea.
Nimehamasika na nimeingia Maktaba kutafuta yale ambayo yanafanana na aliyotueleza Sesten.
Hebu someni kisa kingine hicho hapo chini:
View attachment 2105736
Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi
Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi Lwande Handeni Kosa Lake Kusomesha Wanafunzi Qur'an na Kukataa Kuchakachua Mitihani
Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko alikuwa mwalimu wa shule ya msingi Lwande moja ya vijiji ambavyo mwaka wa 2013 vilivyoshambuliwa kwa tuhuma za ugaidi.
Mwalimu Athmani alikuwa mwalimu mwajiriwa na serikali kusomesha masomo ya kisekula lakini kwa mapenzi yake katika Uislam kwa kuwa walimu wa somo la dini ya Kiislam Shule za Msingi hakuna yeye alijitolea kuwasomesha wanafunzi hawa dini ya Kiislam na kuwatungia mitihani.
Kisa chake ni kisa cha kusikititisha na kuhuzunisha.
Siku za nyuma Mwalimu Athmani alifatwa na walimu wenzake akaelezwa kuwa imetoka amri juu kuwa walimu washirikiane kuwafaulisha watoto darasa la saba kwa kuwakokotolea wanafunzi majibu ya mtihani wa mwisho wa darasa la saba ili kunyanyua ufaulu wa shule na hatimaye wilaya.
Mwalimu Athmani akakataa hili kwa misingi ya Uislam kuwa hicho kitendo ni ghushi yaani udanganyifu.
Akawaeleza kuwa imani ya dini yake inakataza mambo kama hayo.
Udanganyifu huu ukakwama na sababu ikawa ni yeye Mwalimu Athmani.
Hapa ndipo zilipoanza chuki dhidi yake.
Sasa lilipotokea sakata la Lwande askari waliovamia kijiji kwa madai ya kupambana na Al Shabab Mwalimu Athmani akakamatwa, kupigwa na kufunguliwa kesi ya kujeruhi Mahakama ya Handeni.
Mwalimu Athmani sasa hivi ni masikini.
Alipoachiwa gerezani kwa dhamana alikuta nyumba yake imevunjwa na vitu vyake vyote vimeibiwa.
Huyu ndiye ''gaidi'' anaesemekana alikuwa akishirikiana na Al Shabab.
Hapakuwa na ushahidi wa ugaidi hivyo akaachiwa na kazi akaachishwa.
Mwalimu muadilifu anaesomesha watoto kitabu cha Allah na kuwafunza maadili mema kwa mfano, Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko akazuliwa kuwa ni ''Al Shabab,'' bila ya ushahidi.
Haya ni machache.
Yapo mengi katika dhulma hii ya kumfanya mtu akabubujikwa na machozi.
Sasa imepita karibu miaka 9 sijapata taarifa za Mwalimu Mrindoko.
SAKATA LA KILINDI NA MAUAJI YA KILINDI NA MAUAJI YA KIJIJI CHA MADINA - HANDENI, KUPOTEA (KUULIWA) KWA RAJAB OMARI MTANAHuyu ni mhalifu tu kama vibaka wengine. A criminal and a felon.