Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Belo,
Tunaweza tukafanya mjadala wa adabu na heshima bila ya kejeli na kebehi.

Mathalan ukishanisoma na ukaona kuna jambo una fikra tofauti na zangu ukaeleza.

Sasa hii "kulia," na maneno ya kukashifiana yanatoa ladha ya mjadala.
Mwalimu was a genious
 
Pep,
Nakuhakikishia hutajuta.

Niulize swali lolote kuhusu harakati za uhuru kuanzia 1929 wazee wangu walipounda African Association hadi uhuru 1961 na changamoto zlizotokea kupelekea wazee wangu wote kufutwa katika historia hii.
Una hati miliki ya historia ya Uhuru wa Tanganyika?Kwa nini unataka kutuaminisha wewe kuwa unayoyasema kuhusu mada za uhuru wa Tanganyika ni kweli peke yake.Wewe peke yako ndo unafanya tafiti?Wewe peke yako ndo unaandika paper?Wasomi.wote wa historia nchi hii hawajui kitu isipokuwa wewe?Una hati miliki ya ukweli?
 
Kong...

Uadilifu II

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.


Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.

Una kazi
 
Una hati miliki ya historia ya Uhuru wa Tanganyika?Kwa nini unataka kutuaminisha wewe kuwa unayoyasema kuhusu mada za uhuru wa Tanganyika ni kweli peke yake.Wewe peke yako ndo unafanya tafiti?Wewe peke yako ndo unaandika paper?Wasomi.wote wa historia nchi hii hawajui kitu isipokuwa wewe?Una hati miliki ya ukweli?
Nan...
Hapana sina hati miliki ya historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nilichonacho mie ni ujamaa na wengine nasaba na baadhi ya wapigania uhuru wa Tanganyika.

Mathalan Mzee Kleist, Mzee bin Sudi, Ali Jumbe Kiro, Mzee Iddi Tosiri, Mzee Iddi Faiz Mafongo kwa kuwataja wachache ni babu zangu katika ujamaa na katika Umanyema ukimtoa Mzee Kleist.

Salum Abdallah mmoja katika waasisi wa TANU Tabora ni babu yangu khalis.

Mimi ni Mohamed Said Salum Abdallah mjukuu wa Salum Abdallah aliyeongoza migomo mitatu mikubwa ya Tanganyika Railways 1947, 1949 na 1960 miezi michache kabla ya Tanganyika kukabidhiwa madaraka ya ndani.

Mwaka wa 1954 akawa mmoja wa waasisi wa TANU na 1955 pamoja na Kassanga Tumbo wakaasisi Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Mgomo huu wa mwaka 1960 ulidumu siku 82 na kuvunja rekodi ya mgomo wa siku 62 ulioitishwa na Makhan Singh, Kenya.

Kuhusu ukweli wa historia ya uhuru wa Tanganyika ambao upo katika kitabu cha Abdul Sykes sikuwa na sababu ya kuandika uongo.

Hawa ndiyo wazee wangu nilioeleza mchango wao katika kupigania uhuru.

Baadhi ya babu zangu hawa nimewadiriki wakiwa hai na wengine sikubahatika kuwaona.

Juu ya hayo simlazimishi mtu kuamini historia yao kama waasisi wa African Association (1929), Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika (1933), walimpokea Julius Nyerere 1952, waasisi wa TANU 1954 na wapigania uhuru.

Kuhusu kuwa mimi ndiye peke yangu niliyefanya tafiti hili swali umelileta sipo.

Hali kadhalika kuwa mimi peke yangu ndiye mwandikaji paper na wasomi wengine hawajui kitu haya maswali yangu mie kukupa majibu.

Ulitakiwa uwaulize Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam Idara ya Historia.

Kuhusu hati miliki ya ukweli ni kuwa mimi ndiye mwenye hati miliki ya kitabu cha Abdul Sykes na vingine nilivyoandika kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Bado nasisitiza kuwa simlazimishi yeyote kuamini historia niliyoandika.

Uko huru kuamini historia ya TANU iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni.

1713639516561.png

Kushoto: Iddi Faiz Mafungo, Sheikh Mohamed Ramiyya, Julius Nyerere, Saadan Abdul Kandoro na Haruna Iddi Taratibu, Dodoma 1955/56
Picha hii nimeipa jina: ''Wamanyema Wanne na Mzanaki Mmoja.''
(Picha kwa hisani ya Maktaba ya Sykes)
1713639415505.png

Mzee bin Sudi
(!896 - 1972)
1713639837710.jpeg

Salum Abdallah (mshale) na kuliani kwake ni Kassanga Tumbo na viongozi wa TRAU
1713639982867.jpeg

 


Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.

Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.

Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?

Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.

Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:

''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''

Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.

Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.

Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.

Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.

Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.

Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.

Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.

Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.

Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.

Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.

Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.

Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''

Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?

Waislam hawasemi kweli?

Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.

Tumefikaje katika hali hii?

Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.

Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.

Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.

Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.

View attachment 2096477
View attachment 2096478

Kipenzi cha Mtume Muhammad (s.a.w)
 
Zanzibar pale kanisa lilichomwa moto na padri akauwawa kwa sababu za kidini. Kuna watu dini yao wanaiona ya muhimu sana kuliko dini za atu wengine; kila wakiamka wanafikiria dini tu. Ukipitia hapa JF, ndugu yangu Mohamed Said mada zake zote zinahusu dini ya uislamu na Nyerere tu.

Nyerere huingia katika mada zake kwa vile ndiye aliyekuwa wa mtu kwanza kuongoza chini hii baada ya uhuru wakati yeye siyo mwislamu. Iwapo Nyerere angefanya yale yale aliyofanya wakati wa utawala wake lakini akiwa mwislamu, usingesikia kelele na lawama za Mohammed.

Najaribu kuangalia maisha ya wakaristo yangekuwaje iwapo nchi yote hii ingekuwa kama Zanzibar; au iwapo Nyerere angeongoza nchi hii kwa maono anayotaka Mohamed.
 
Zanzibar pale kanisa lilichomwa moto na padri akauwawa kwa sababu za kidini. Kuna watu dini yao wanaiona ya muhimu sana kuliko dini za atu wengine; kila wakiamka wanafikiria dini tu. Ukipitia hapa JF, ndugu yangu Mohamed Said mada zake zote zinahusu dini ya uislamu na Nyerere tu.

Nyerere huingia katika mada zake kwa vile ndiye aliyekuwa wa mtu kwanza kuongoza chini hii baada ya uhuru wakati yeye siyo mwislamu. Iwapo Nyerere angefanya yale yale aliyofanya wakati wa utawala wake lakini akiwa mwislamu, usingesikia kelele na lawama za Mohammed.

Najaribu kuangalia maisha ya wakaristo yangekuwaje iwapo nchi yote hii ingekuwa kama Zanzibar; au iwapo Nyerere angeongoza nchi hii kwa maono anayotaka Mohamed.
Kichuguu,
Huko unakonipeleka mie siko huko.

Mimi nimeiandika kitabu kueleza historia ya kweli ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Leo wote tunasoma historia iliyotakiwa kuwepo miaka mingi.
 
Zanzibar pale kanisa lilichomwa moto na padri akauwawa kwa sababu za kidini. Kuna watu dini yao wanaiona ya muhimu sana kuliko dini za atu wengine; kila wakiamka wanafikiria dini tu. Ukipitia hapa JF, ndugu yangu Mohamed Said mada zake zote zinahusu dini ya uislamu na Nyerere tu.

Nyerere huingia katika mada zake kwa vile ndiye aliyekuwa wa mtu kwanza kuongoza chini hii baada ya uhuru wakati yeye siyo mwislamu. Iwapo Nyerere angefanya yale yale aliyofanya wakati wa utawala wake lakini akiwa mwislamu, usingesikia kelele na lawama za Mohammed.

Najaribu kuangalia maisha ya wakaristo yangekuwaje iwapo nchi yote hii ingekuwa kama Zanzibar; au iwapo Nyerere angeongoza nchi hii kwa maono anayotaka Mohamed.
Nyerere aliwapuuza wazee wake Mohammed kwa sababu walikuwa wabaguzi wa kidini kama Mohammed.Nyerere aliwaneutralize hawa wajinga kwa sababu walitaka kuisilimisha nchi.Nyerere alikuwa genious
 
Nyerere aliwapuuza wazee wake Mohammed kwa sababu walikuwa wabaguzi wa kidini kama Mohammed.Nyerere aliwaneutralize hawa wajinga kwa sababu walitaka kuisilimisha nchi.Nyerere alikuwa genious
Nan...
Hapana haikuwa hivyo.

Waislamu wangekuwa hivyo Nyerere asingekuwa kiongozi wa TANU.

Jitulize uisome historia ya uhuru wa Tanganyika utapata maarifa mengi sana.

Nakusihi uzuie mdomo wako kutamka matusi.

Hilo neno "wajinga," halikustahili.

Hakuna aliyebaguliwa katika TANU.
 
Nan...
Hapana haikuwa hivyo.

Waislamu wangekuwa hivyo Nyerere asingekuwa kiongozi wa TANU.

Jitulize uisome historia ya uhuru wa Tanganyika utapata maarifa mengi sana.

Nakusihi uzuie mdomo wako kutamka matusi.

Hilo neno "wajinga," halikustahili.

Hakuna aliyebaguliwa katika TANU.
Sijatukana mtu ila nakumbushia tu kwamba katika hotuba zake,Nyerere aliwarefer watu wenye hoja za udini na ukabila ili kupata political regitimacy kama WAJINGA.Na indeed ni wajinga
 
Sijatukana mtu ila nakumbushia tu kwamba katika hotuba zake,Nyerere aliwarefer watu wenye hoja za udini na ukabila ili kupata political regitimacy kama WAJINGA.Na indeed ni wajinga
Nan...
Watu hao uwasemao wewe kuwa Nyerere kawaita wajinga kwa kutafuta uhalali kupitia Uislam sidhani kama ni hawa ambao mimi nimeandika historia zao wakiwa na Nyerere kuanzia alipofika Dar es Salaam 1952 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.

Angalia picha hizo hapo chini:

1713757951397.jpeg

Baraza la Wazee wa TANU
1713758040902.png

Kulia: Chiku bint Said Kisusa, Bibi Titi Mohamed
Kushoto Tatu bint Mzee na katikati ni Julius Nyerere wakimsindikiza safari ya kwanza UNO 1956
Dhifa ya kumuaga ilifanyika katika jengo la Al Jamaiatul Islamiyya fi Tanganyika
1713758470490.jpeg

Kulia: Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi​

Kitabu cha Abdul Sykes kinaeleza historia ya wazalendo hawa ambao walikuwa na Mwalimu Nyerere bega kwa bega kupigania uhuru wa Tanganyika.

Unadhani Nyerere alikuwa katika hiyo hotuba yake aliwakusudia hawa na kuwaita wajinga?
 
Lengo la Uzi huu ni Nini mbona kama sielewi naona malalamiko tu ambayo hayana tija kwa taifa hili
 
Nan...
Watu hao uwasemao wewe kuwa Nyerere kawaita wajinga kwa kutafuta uhalali kupitia Uislam sidhani kama ni hawa ambao mimi nimeandika historia zao wakiwa na Nyerere kuanzia alipofika Dar es Salaam 1952 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.

Angalia picha hizo hapo chini:

View attachment 2970618
Baraza la Wazee wa TANU
View attachment 2970619
Kulia: Chiku bint Said Kisusa, Bibi Titi Mohamed
Kushoto Tatu bint Mzee na katikati ni Julius Nyerere wakimsindikiza safari ya kwanza UNO 1956
Dhifa ya kumuaga ilifanyika katika jengo la Al Jamaiatul Islamiyya fi Tanganyika
View attachment 2970622
Kulia: Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi​

Kitabu cha Abdul Sykes kinaeleza historia ya wazalendo hawa ambao walikuwa na Mwalimu Nyerere bega kwa bega kupigania uhuru wa Tanganyika.

Unadhani Nyerere alikuwa katika hiyo hotuba yake aliwakusudia hawa na kuwaita wajinga?
Nimekuuliza swali hili mara nyingi lakini umekuwa ukinikwepa.Hawa wazee wako walipambania uhuru wa Tanganyika kama watanganyika ama waislam?
 
Nimekuuliza swali hili mara nyingi lakini umekuwa ukinikwepa.Hawa wazee wako walipambania uhuru wa Tanganyika kama watanganyika ama waislam?
Nan...
Sijakukwepa.
Nikwepe nini na kitabu kinajieleza?

Mimi si wa kujibu maswali ya ndiyo hapana.
 
ufahamishwe tu kuwa Sisi watu kubwa tumeshaanza kuhama kutoka kuwa wafuasi wa Dini yoyote, tumeamua kuwa wafuasi wa Mungu tu.

Dini tunaiweka kwenye vitu chonganishi Kwa sababu dini in it, it is people's way of living, it has nothing to do with God 's creation of human being ndio maana kila mtu huhudimiwa na Mungu kuanzia hewa na mvua bila kujali Dinii zenu

Fikiria huyu Mzee angekuwa ndio Mungu!
(God forgive) Angetupanga Kwa cha 666 kichwani huyu kibabu!
 
Back
Top Bottom