Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Baba wa Taifa na tatizo la Udini

ufahamishwe tu kuwa Sisi watu kubwa tumeshaanza kuhama kutoka kuwa wafuasi wa Dini yoyote, tumeamua kuwa wafuasi wa Mungu tu.

Dini tunaiweka kwenye vitu chonganishi Kwa sababu dini in it, it is people's way of living, it has nothing to do with God 's creation of human being ndio maana kila mtu huhudimiwa na Mungu kuanzia hewa na mvua bila kujali Dinii zenu

Fikiria huyu Mzee angekuwa ndio Mungu!
(God forgive) Angetupanga Kwa cha 666 kichwani huyu kibabu!
Master...
Mimi ninapoona mtu analeta kejeli, matusi na "name calling" huwa namkwepa simjibu.

Ila nakujibu wewe kutaka kukuongezea maarifa ili uelimike na ukipendezewa ujifunze adabu.

Mimi ukiniita "Kibabu," katika msamiati wetu watu wa Pwani unakuwa umekosea ikiwa nia yako ilikuwa kunitukana.

Ungeniita, "Kizee."

Ungefanya hivyo ungekuwa umenitukana kama ulivyokusudia.

Kikwetu, "Kibabu," ni jina anapewa mtoto mchanga wa kiume ambae bado hajapewa jina na akiwa mwanamke anaitwa, "Kibibi."
 
Mzee mi nadhani kubali tu,umeathiriwa sana na kutazama mambo kwa jicho la dini yako.Huo ni ugobjea ulionao na hauwezi kupona.Turuhusu tu tutambue kwamba huo ndo ulemavu ukionao.
Uko very parokial.
Mbona hauzunugumzii jamii nyingine nje ya uislam.Tufundishe korani kabisa basi tujue moja.
 
Maada karibu 50 zote unalialia

Machozi yamekauka, ila bado yumo tu. Na hakuna lolote la maana aliloweza kukamilisha. Muda ukuta. Kila kitu kina mwanzo na mwisho wake.

Tusije kuishia kutengeneza vicheko na kejeli baada ya haya maisha. Sisi binadamu, ni wepesi sana wa kusahau. Na nina uhakika, mfupa uliomshinda fisi, mbwa atapata nao tabu sana, waswahili wanasema
 
Kong...

Uadilifu II

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.


Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.


Mzee wangu unaweza kutuwekea takwimu kama hizi Kwa awamu hii? Kama hautojali pia utuwekee na Baraza la awali kabisa wakati wa Mwalimu, lililomjumuisha Mzee wetu Kawawa.
 
Mzee mi nadhani kubali tu,umeathiriwa sana na kutazama mambo kwa jicho la dini yako.Huo ni ugobjea ulionao na hauwezi kupona.Turuhusu tu tutambue kwamba huo ndo ulemavu ukionao.
Uko very parokial.
Mbona hauzunugumzii jamii nyingine nje ya uislam.Tufundishe korani kabisa basi tujue moja.
Insp....
Tuanze hapa.

Nini kilifanya historia ya uhuru wa Tanganyika kugeuzwa?
Unadhani nani mgonjwa.

Yule aliyeigeuza au yule aliyeiweka sawa?
Nani kilema.

Akataae ukweli au yule mwenye kuukubali ukweli?
 
Smart...
Ni hatari kuliko hatari yenyewe.

Ukiwa na watu wa dini moja wamehodhi fursa zote wakati wenzao wako nje ya hizo fursa unajenga chuki katika jamii.

Lazima hali hii iondoshwe.
Usikute Magufuli alichagua tu watu katika hizo nafasi katika tu hali ya kawaida ila nyie mnaoendekeza udini ndio mnajifanya mahodari wa kupekenyua majina kubaini waislamu wangapi wameteuliwa ni upumbavu uliotukukuka
 
Machozi yamekauka, ila bado yumo tu. Na hakuna lolote la maana aliloweza kukamilisha. Muda ukuta. Kila kitu kina mwanzo na mwisho wake.

Tusije kuishia kutengeneza vicheko na kejeli baada ya haya maisha. Sisi binadamu, ni wepesi sana wa kusahau. Na nina uhakika, mfupa uliomshinda fisi, mbwa atapata nao tabu sana, waswahili wanasema
Belo anasema nalialia.
Tangawezi unasema hakuna lolote la maana nililokamilisha.

Tuanze na kulialia.
Mimi silii.

Mimi nimeandika historia ya harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika kwa kiasi ambacho vitabu vilivyotangulia havikufikia kiwango changu.

Nini ushahidi wa haya nisemayo?

Kitabu changu kimefanyiwa review tatu na mabingwa wa African History: John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Review hizi zote zimechapwa katika Cambridge Journal of African History.

Baada ya haya nikatiwa katika miradi miwili ya kuandika historia ya Afrika.

Mradi wa kwanza Oxford University Press, Nairobi (2007).

Wamechapa kazi zangu.

Mradi wa Pili Harvard na Oxford University Press, New York (2008) kuandika Dictionary of African Biography (DAB)(2011).

Nimeshiriki katika mradi wa kuandika Nyerere Biography (2020).

Huu mradi wa tatu.

NImeshiriki katika mradi wa kuandika historia mpya kama alivyoagiza Rais Magufuli.

Mradi wa nne.

Haya ni baadhi ya mambo ambayo Mola kanijaalia kukamilisha.

Yapo mengi lakini kwa leo nimekuwekeeni hayo kukujibuni kuhusu ''kulialia'' na mimi kugeuka kuwa ''kichekesho.''

1716236933027.png

1716236993127.jpeg

Kitabu cha Abdul Sykes pembeni ya kitabu cha Julius Nyerere
Kitabu cha Abdul Sykes kimechapwa mara nne.
(Angalia majadala tofauti kwa kila toleo)
 
Back
Top Bottom