MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Mwaka 2002 nikiwa nyumbani kwa mzee wangu fulani niliemtembelea nilipata bahati ya kutazama albamu ya picha zake. Mnakumbuka enzi hizo hakuna social media hata Tv bado sio sana kwahiyo mgeni kupewa albamu kutazama ilikuwa mojawapo ya kiburudisho. Nilivutiwa na picha za familia alizopiga miaka ya 70 na 80 huko. Zilikuwa picha nzuri sana zilizovutia. Kwa miaka ile kuona picha ya baba kagonga suti huku mke na watoto wamekula viwalo vizuri ilikuwa ni nadra. Yule mzee alipata pesa mapema baada ya kumaliza masomo yake na pia akaoa na kuwa na familia mapema. Zile picha ni ushahidi mzito kwamba ile ilikuwa familia bora.
Lakini kwa wakati huo 2002 yule mzee alikuwa kashaachana na mkewe miaka mingi iliyopita huku akiwa hana mawasiliano wala maelewano mazuri na wanae. Mbele ya jamii alikuwa akionekana mzee mpenda papuchi na asiye mfano wa kuigwa baada ya kuwa anaoa na kuacha. Na kwa wakati huo alikuwa anaishi na mwanamke mmoja ile style "sogea tuishi". Pia kiuchumi alishayumba hata kazi aliyosomea akawa hafanyi.
Kilichokuwa kinamweka mjini ni assets zake kama mashamba na nyumba za kupanga. Ule umaarufu ulishafutika. Mzee huyu alikua akilaumiwa sana kama chanzo cha kuvunjika ndoa yake na kutelekeza watoto. Lakini nikawa najiuliza mbona albamu karibia nzima inaonyesha hii familia ilikuwa njema tu? Kulikuwa na picha za sherehe za kipaimara, ubatizo na matukio mengine ya kifamilia. Pia mbona watu wazima wenzie nao wanakiri mzee alikuwa mtu wa familia sana? Na mbona pamoja na hayo yote ya ndoa kuvunjika kuna wanae ambao hatukupishana nao sana umri alikuwa akiwalipia ada?
Baada ya miaka kadhaa ndo nikaja kugundua kwamba yule mzee hakuwa na tatizo lolote ila kuna mtoto wao mmoja mlemavu hakuzaliwa akiwa hivyo aliupata baadae ambaye ndo chanzo kikubwa cha majanga. Ni kwamba mama mtoto alienda kwa mganga kupata dawa za kumdhibiti mume ambako akapewa dawa zilizotakiwa akalie mumewe ila bahati mbaya wakati kaweka dawa yule mtoto akakalia kiti kabla ya baba. Kilichotokea ni mtoto kupata ulemavu wa miguu na kutumia wheelchair. Kwenye kufuatilia hilo jambo ndo yakaja kugundulika mambo yote hayo na ukawa mwanzo wa mwisho wa ndoa.
Lakini kwa miaka yote hiyo huyu mzee amekuwa akivumilia lawama zote bila kurudisha maneno mabaya. Kisa cha huyu mzee kimenikumbusha kwamba wazee wetu wana siri nzito za mama zetu ila wameamua kulinda heshima zao na za wake zao. Ila wakisema nao waanze kulalamika itakuwa ni balaa. Mpasuko utakuwa mkubwa mno.
Ninawasihi watu wote kua makini sana na lawama za upande wa mama dhidi ya baba zetu. Ni kwenda nazo kwa tahadhari mno.
Lakini kwa wakati huo 2002 yule mzee alikuwa kashaachana na mkewe miaka mingi iliyopita huku akiwa hana mawasiliano wala maelewano mazuri na wanae. Mbele ya jamii alikuwa akionekana mzee mpenda papuchi na asiye mfano wa kuigwa baada ya kuwa anaoa na kuacha. Na kwa wakati huo alikuwa anaishi na mwanamke mmoja ile style "sogea tuishi". Pia kiuchumi alishayumba hata kazi aliyosomea akawa hafanyi.
Kilichokuwa kinamweka mjini ni assets zake kama mashamba na nyumba za kupanga. Ule umaarufu ulishafutika. Mzee huyu alikua akilaumiwa sana kama chanzo cha kuvunjika ndoa yake na kutelekeza watoto. Lakini nikawa najiuliza mbona albamu karibia nzima inaonyesha hii familia ilikuwa njema tu? Kulikuwa na picha za sherehe za kipaimara, ubatizo na matukio mengine ya kifamilia. Pia mbona watu wazima wenzie nao wanakiri mzee alikuwa mtu wa familia sana? Na mbona pamoja na hayo yote ya ndoa kuvunjika kuna wanae ambao hatukupishana nao sana umri alikuwa akiwalipia ada?
Baada ya miaka kadhaa ndo nikaja kugundua kwamba yule mzee hakuwa na tatizo lolote ila kuna mtoto wao mmoja mlemavu hakuzaliwa akiwa hivyo aliupata baadae ambaye ndo chanzo kikubwa cha majanga. Ni kwamba mama mtoto alienda kwa mganga kupata dawa za kumdhibiti mume ambako akapewa dawa zilizotakiwa akalie mumewe ila bahati mbaya wakati kaweka dawa yule mtoto akakalia kiti kabla ya baba. Kilichotokea ni mtoto kupata ulemavu wa miguu na kutumia wheelchair. Kwenye kufuatilia hilo jambo ndo yakaja kugundulika mambo yote hayo na ukawa mwanzo wa mwisho wa ndoa.
Lakini kwa miaka yote hiyo huyu mzee amekuwa akivumilia lawama zote bila kurudisha maneno mabaya. Kisa cha huyu mzee kimenikumbusha kwamba wazee wetu wana siri nzito za mama zetu ila wameamua kulinda heshima zao na za wake zao. Ila wakisema nao waanze kulalamika itakuwa ni balaa. Mpasuko utakuwa mkubwa mno.
Ninawasihi watu wote kua makini sana na lawama za upande wa mama dhidi ya baba zetu. Ni kwenda nazo kwa tahadhari mno.