Babu Tale jipange sana awamu hii; awamu ijayo usiuwaze Ubunge

Babu Tale jipange sana awamu hii; awamu ijayo usiuwaze Ubunge

Ogopa sana una bunge ambalo ukiletwa muswada au bajeti yeye pages hata 20 hawasomi wala kujaribu kuchambua kuelewa kilichomo ndani wao wanajua kupitisha na kumsifia Raisi na serikali yake wenye akili wanabaki wanashangaa tu aina ya uwakilishi yaani badala ya kuwawakilisha wananchi wao wanakua Kama wanaiwakilisha serikali dah tupo kwenye kipindi kigumu sana
 
Kuna muda huwa najiuliza tu kama watanzania tulianza anzaje kuwa na mbunge kama Babu Tale

Mwendazake alifanya kazi ya ubunge iwe ni kama kazi ya kubeti tu. Wanatangaza nafasi mwenye pesa anachukua Form mwenyekiti akimkubali basi ndio anakuwa mbunge, maana hakuna uchaguzi wa haki uliotokea ilikuwa one man say.

Mwendazake alikuwa anasema tu nileteeni huyu na huyu, jaji Lubuva na washirikia wake huko wakurugenzi na kina Polepole wanapitisha tu.

Leo hii tuna mbunge kama babu tale asiye jua ata Bunge lina kazi gani?

Mwendazake alikuwa anatupeleka kuleee shimoni kabisa.

Babu tale, Babu tale, Babu tale nimekwita mara tatu, tumia vuzuri pesa zako za posho 360k za kila siku unazopata hapo bungeni kwa ajiri ya mitano ya baadae.

Tumia vizuri hiyo 10 M ya kila mwezi kama mshahara wako wa ubunge kwa ajiri ya mitano ijayo. Pia utumie vizuri kiinua mgogo chako cha karibia 250M ya ubunge wako punde tu baada ya Rais wa JMT kuvunja Bunge mwaka 2025.

Usidhubutu, usidhubutu, usidhubutu, kurudia tena kuutaka ubunge utamaliza pesa zako za posho, mshahara na kiinua mgogo buree na Ubunge hautaupata tena.

Utapata wafuasi wengi wa kukushawishi ugombee tena. Hao hawana wema watakuwa tu wanataka kuchuma mali kutoka kwako wapuuze waambie tu Mitano uliyohudumu kazi ya ubunge kwako yatosha unaenda kupumzika.

Ukifanya hivyo utanishukuru baadae.

CCM imerudi kwa wenyewe na soon mtaona makucha yao.

Cc Zero IQ
Dr Babu tale
 
Diamond akiutakiwa kulipa kodi anajificha kwenye mwamvuli wa kuwa na huyo mbunge wake
 
Back
Top Bottom