Bachelorette Shyrose Bhanji

Watu wengi ambao lugha yao ya kwanza ni Kiswahili wenye matatizo ya kusoma, kuandika na kusema Kiingereza hawajaelewa jambo moja, na jambo hili ni kati ya vyanzo vya aibu katika kutojua kusoma, kuandika au kuongea kiingereza.

Kiswahili ni lugha yenye mantiki kuliko Kiingereza. Kiingereza ni lugha ambayo haijakifikia Kiswahili katika mantiki.

Nina maana gani?

Kwenye matamshi, katika Kiswahili, ukishajifunza matamshi ya msingi ya silabi tu, matamshi ni yale yale. Yanajirudia tu. Ni kama ukijifunza matamshi ya msingi, kwingine unaunganisha silabi tofauti kwa matamshi yale yale tu. Lugha ya namna hii inaitwa "phonetic". Huhitaji kujifunza kila neno jipya jinsi ya kulitamka. Kwenye Kiswahili, michepuko kutoka kanuni za matamshi ni michache sana.

Kiingereza kiko na michepuko mingi sana katika matamshi. Ni kama nusu ya lugha inafuata sheria za matamshi, halafu nusu nyingine inachepuka kutoka matamshi hayo. Kwa mtu aliyezoea lugha iliyonyooka kimatamshi kama Kiswahili, kujifunza Kiingereza ni kama kujifunza kutamka kwa makosa mengi sana.

Pia, kanuni za sarufi za Kiingereza nazo zinachepuka hivyo hivyo zikilinganishwa na Kiswahili ambacho kimejikita kwenye kufuata sheria sana. Kwa hiyo, tunapojifunza Kiingereza, tunakuta karibu nusu nzima ya lugha inafuata sheria za matamshi na sarufi, halafu nusu myingine haifuati sheria hizo. Ni lugha inayochanganya sana watu waliozoea lugha yenye mantiki na kufuata sheria kama Kiswahili.

Tatizo watu tunajiona dhalili kwa kutokujua Kiingereza, wakati kwa kiasi kikubwa, tunashindwa kujifunza Kiingereza kwa sababu kina makosa mengi ya kimantiki kwa michepuko karibu nusu nzima ya lugha kutoka kwenye sheria za matamshi na sarufi.

Kwa hiyo tunashindwa kwa sababu lugha yetu tuliyoizoea ni nzuri zaidi, si kwa sababu Kiingereza ni kizuri zaidi.

Ingawa siku hizi watu wengi tu hawajui Kiswahili wala Kiingereza.
 
This is some food for thought and it's deep...like in really DEEP, shikamoo Kiranga!!!

Umemuona Ngabu anaonesha nia ya kushiriki, vipi upande wako, nawe utajitosa?! 🙂
 
This is some food for thought and it's deep...like in really DEEP, shikamoo Kiranga!!!

Umemuona Ngabu anaonesha nia ya kushiriki, vipi upande wako, nawe utajitosa?! 🙂
Mi nishaanza ku pitch idea ya "Sagulaga" kwa Nalendwa

Unaijua Sagulaga? That is more like us.

This Bachelorette thing is more of a foreign concept where I am from.
 
I have gone through every post in this thread, but guess what??

I came up with nothing. What are you people discussing here?

Kiranga nimeipenda sana post yako kuhusu kiswahili. Mi kiingereza sijui na naona kawaida tuu maadam cha kujibia dokezo kipo basi kimaisha.
 
Mi nishaanza ku pitch idea ya "Sagulaga" kwa Nalendwa

Unaijua Sagulaga? That is more like us.

This Bachelorette thing is more of a foreign concept where I am from.


Guess I'll have to work on Sagulaga idea.

Sina ujanja! 😁
 


Wow, umekipamba Kiswahili na kimepambika haswa!
I hope the mass-ive see this.

Was linguistic part of your minor/major?!
You never disappoint! 🙌🙌🙌
 


Bachelorette-In-The-Process Show. 😊
 
Dah!
KIBONGO BONGO,
she has to stoop very low.
HILO TU NDO HOFU YANGU,NA BADO ASIPATE ANACHOKITAMANI AU AKIPATE AKIWA AMESHAPOTEZA MENGI SANA.
NA BADO ILI AENDELEE KUKIPATA ITAMPASA KUPOTEZA MENGINE ZAIDI!!
Nawewe lini twala ubwabwa
 
Lakini, what if wakiji limit, na kuifanya "ki Tanzania" zaidi.

Do you think BASATA bado watatia mguu?
Have you ever seen anywhere around Tz a woman approaching a man and declare it openly that I did approach this man? Talking of male insecurity

If BASATA can keep behind bars songs under the name "kinyume na maadili yetu" do you think it will be possible for them to accept such a show?
Which Tanzanian context will it be applied in such a show?

I don't see it coming but I wish her all the best in making it happen
 


The picture is becoming more clear now. Guess they need to check out JF for 'RESEARCH'
Before they do anything...lol!
But serioulsly!...

Umepiga mulemule girl.
If they can ban a 3-5 minutes song under "Sio Maadili yetu"
What about a, half hour- one hour show, with lots of Romance activities in it!. 😀

Lakini ni hivyo tu sema ndio Utamaduni
Like, what's wrong with looking at someone in the eyes if you like them, and just talking to them??!!!
Again, ni hivyo tu, sema ndio Utamaduni..
 
Haya mambo ya kujitembeza walahi!
CHEMA CHAJIUZA KIBAYA CHAKITEMBEZA!
That’s all
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…