Badala ya kuilipisha Simba, tuhoji zoezi la kubadili viti vya Uwanja wa Mkapa limeishia wapi?

Badala ya kuilipisha Simba, tuhoji zoezi la kubadili viti vya Uwanja wa Mkapa limeishia wapi?

ukiacha unazi pembeni sisi mashabiki wa simba sc hatukuwa na sababu za kufanya uharibifu ule na kuwapiga wapinzani wetu sababu:

1. mpira umeisha na point 3 tumechukua.

2. tulipaswa kuwaacha wageni waingie matatizoni kwa kumpiga mwamuzi.

3. kwa vurugu zile tumeiweka timu yetu matatani itakapokwenda tunisia maana washabiki wao wanaweza kuwashambulia wachezaji wetu.
 
ukiacha unazi pembeni sisi mashabiki wa simba sc hatukuwa na sababu za kufanya uharibifu ule na kuwapiga wapinzani wetu sababu:

1. mpira umeisha na point 3 tumechukua.

2. tulipaswa kuwaacha wageni waingie matatizoni kwa kumpiga mwamuzi.

3. kwa vurugu zile tumeiweka timu yetu matatani itakapokwenda tunisia maana washabiki wao wanaweza kuwashambulia wachezaji wetu.
Mashabiki wa simba sc ni washenzi toka tafsiri ya kimombos, "simba sc fans are savages"

A savage means a brutal person
 
Ni zaidi ya mwaka sasa, toka enzi za uzinduzi wa African Football League (AFL) tuliambiwa kuwa viti vyote vya uwanja wa Benjamin Mkapa vingeenda kubadilishwa kama sehemu ya matengenezo makubwa ya uwanja.

Cha ajabu viti vimeendelea kuchakaa na vingine kung'oka huku hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

Baada ya tukio la mechi ya Simba vs CS Sfaxien, nimeshangaa kusikia eti Simba inatakiwa kulipa gharama za vile viti chakavu ambavyo nina uhakika vingine tayari vilikuwa vimeshang'oka. Hili jambo siyo sawa.

Inabidi tuhoji pesa yote ya marekebisho ya uwanja imeenda wapi mbona uwanja unaonekana bado uko vile vile zaidi ya running track ambayo sijawahi kuona ikitumika katika mashindano yoyote ya riadha? Running track imebaki kutumiwa na kina Harmonize, Dj Sinyorita na Dj Ally B wakiwa wanatumbuiza.

ZIADA 1: Sijawaelewa walinzi wa Uwanja wa Mkapa. Tukio la juzi na matukio mengine ya nyuma wanaonekana wako very disorganized, hawako fiti kimwili na ni kama wafanyakazi wasio na mafunzo, weledi wa kazi zao wala mfumo wa uongozi. Juzi walishindwa kabisa kucontrol situation ndogo kama ile ya watu wachache sana, wakabaki kukimbia kimbia kama wehu.

ZIADA 2: Uwanja wa Mkapa una security camera? Matukio kama ya juzi yakitokea, ni muhimu kutoa wazi video za tukio husika ili umma ujiridhishe chanzo na wahusika ni kina nani.

ZIADA 3: Wakati wa uzinduzi wa AFL, tuliambiwa Simba ilijitolea kulipia baadhi ya gharama za matengenezo ya uwanja ikiwemo pitch na vyumbani. Inakuwaje mdau wa karibu aliyefanya juhudi za kuheshimisha na kuutangaza uwanja, halafu linapotokea tukio ambalo lilikuwa nje ya uwezo wake achukuliwe kama mhalifu badala kulizungumza ili serikali ionyeshe inakumbuka mchango wake?
Upumbavu mkubwa.Sipendi kabisa mtu atetetee ujinga kama huo.Lazima wote waliofanya uhuni huo wakamatwe na wachukuliwe kama wahujumu uchumi.

Huo uwanja hautumii pesa za wajomba wao bali sisi watanzania tunaolipa kodi nyingi tu kila mwezi.

Serikali isicheke kabisa na wahuni hao.
Mimi ni Simba ila nilichukizwa sana na huo uhuni.Kama mtu alikuwa na hasira za kipuuzi,kwa nini asirushe simu yake?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Upumbavu mkubwa.Sipendi kabisa mtu atetetee ujinga kama huo.Lazima wote waliofanya uhuni huo wakamatwe na wachukuliwe kama wahujumu uchumi.

Huo uwanja hautumii pesa za wajomba wao bali sisi watanzania tunaolipa kodi nyingi tu kila mwezi.

Serikali isicheke kabisa na wahuni hao.
Mimi ni Simba ila nilichukizwa sana na huo uhuni.Kama mtu alikuwa na hasira za kipuuzi,kwa nini asirushe simu yake?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Ama kwanini hawakujirusha na kujipasua pasua, kama hawakuwa.na hizo simu
 
Ni zaidi ya mwaka sasa, toka enzi za uzinduzi wa African Football League (AFL) tuliambiwa kuwa viti vyote vya uwanja wa Benjamin Mkapa vingeenda kubadilishwa kama sehemu ya matengenezo makubwa ya uwanja.

Cha ajabu viti vimeendelea kuchakaa na vingine kung'oka huku hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

Baada ya tukio la mechi ya Simba vs CS Sfaxien, nimeshangaa kusikia eti Simba inatakiwa kulipa gharama za vile viti chakavu ambavyo nina uhakika vingine tayari vilikuwa vimeshang'oka. Hili jambo siyo sawa.

Inabidi tuhoji pesa yote ya marekebisho ya uwanja imeenda wapi mbona uwanja unaonekana bado uko vile vile zaidi ya running track ambayo sijawahi kuona ikitumika katika mashindano yoyote ya riadha? Running track imebaki kutumiwa na kina Harmonize, Dj Sinyorita na Dj Ally B wakiwa wanatumbuiza.

ZIADA 1: Sijawaelewa walinzi wa Uwanja wa Mkapa. Tukio la juzi na matukio mengine ya nyuma wanaonekana wako very disorganized, hawako fiti kimwili na ni kama wafanyakazi wasio na mafunzo, weledi wa kazi zao wala mfumo wa uongozi. Juzi walishindwa kabisa kucontrol situation ndogo kama ile ya watu wachache sana, wakabaki kukimbia kimbia kama wehu.

ZIADA 2: Uwanja wa Mkapa una security camera? Matukio kama ya juzi yakitokea, ni muhimu kutoa wazi video za tukio husika ili umma ujiridhishe chanzo na wahusika ni kina nani.

ZIADA 3: Wakati wa uzinduzi wa AFL, tuliambiwa Simba ilijitolea kulipia baadhi ya gharama za matengenezo ya uwanja ikiwemo pitch na vyumbani. Inakuwaje mdau wa karibu aliyefanya juhudi za kuheshimisha na kuutangaza uwanja, halafu linapotokea tukio ambalo lilikuwa nje ya uwezo wake achukuliwe kama mhalifu badala kulizungumza ili serikali ionyeshe inakumbuka mchango wake?
Haihalalishi matendo ya simba; siyo mara yao ya kwanza kun'goa viti hivyo; walifanya hivyo miaka kadhaa iliyopita sikumbuki ilikuwa mechi ganii. Simba ina mashabiki wajinga na wapumbavu sana wanaodhani kubomoa viti vya uwanja ndiyo kuonyesha ubora wa timu.

Sasa hivi inatakiwa serikali iweke utaratibu wa kuwafunga pingu mashabiki wa SImba wanapoingia uwanjani ili wasitumie mikono yao kufanya uharibifu wa uwanja. Baada ya mchezo wanaondolewa pingu hizo wakiwa mlangoni kutoka nje ya uwanja.
 
Ni zaidi ya mwaka sasa, toka enzi za uzinduzi wa African Football League (AFL) tuliambiwa kuwa viti vyote vya uwanja wa Benjamin Mkapa vingeenda kubadilishwa kama sehemu ya matengenezo makubwa ya uwanja.

Cha ajabu viti vimeendelea kuchakaa na vingine kung'oka huku hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

Baada ya tukio la mechi ya Simba vs CS Sfaxien, nimeshangaa kusikia eti Simba inatakiwa kulipa gharama za vile viti chakavu ambavyo nina uhakika vingine tayari vilikuwa vimeshang'oka. Hili jambo siyo sawa.

Inabidi tuhoji pesa yote ya marekebisho ya uwanja imeenda wapi mbona uwanja unaonekana bado uko vile vile zaidi ya running track ambayo sijawahi kuona ikitumika katika mashindano yoyote ya riadha? Running track imebaki kutumiwa na kina Harmonize, Dj Sinyorita na Dj Ally B wakiwa wanatumbuiza.

ZIADA 1: Sijawaelewa walinzi wa Uwanja wa Mkapa. Tukio la juzi na matukio mengine ya nyuma wanaonekana wako very disorganized, hawako fiti kimwili na ni kama wafanyakazi wasio na mafunzo, weledi wa kazi zao wala mfumo wa uongozi. Juzi walishindwa kabisa kucontrol situation ndogo kama ile ya watu wachache sana, wakabaki kukimbia kimbia kama wehu.

ZIADA 2: Uwanja wa Mkapa una security camera? Matukio kama ya juzi yakitokea, ni muhimu kutoa wazi video za tukio husika ili umma ujiridhishe chanzo na wahusika ni kina nani.

ZIADA 3: Wakati wa uzinduzi wa AFL, tuliambiwa Simba ilijitolea kulipia baadhi ya gharama za matengenezo ya uwanja ikiwemo pitch na vyumbani. Inakuwaje mdau wa karibu aliyefanya juhudi za kuheshimisha na kuutangaza uwanja, halafu linapotokea tukio ambalo lilikuwa nje ya uwezo wake achukuliwe kama mhalifu badala kulizungumza ili serikali ionyeshe inakumbuka mchango wake?
Mambo ya siasa. Hujaanza kuwa kumshukuru mama
 
Haihalalishi matendo ya simba; siyo mara yao ya kwanza kun'goa viti hivyo; walifanya hivyo miaka kadhaa iliyopita sikumbuki ilikuwa mechi ganii. Simba ina mashabiki wajinga na wapumbavu sana wanaodhani kubomoa viti vya uwanja ndiyo kuonyesha ubora wa timu.

Sasa hivi inatakiwa serikali iweke utaratibu wa kuwafunga pingu mashabiki wa SImba wanapoingia uwanjani ili wasitumie mikono yao kufanya uharibifu wa uwanja. Baada ya mchezo wanaondolewa pingu hizo wakiwa mlangoni kutoka nje ya uwanja.
Hauna hoja wewee. Ungekuwa na hoja ningekujibu.
 
ukiacha unazi pembeni sisi mashabiki wa simba sc hatukuwa na sababu za kufanya uharibifu ule na kuwapiga wapinzani wetu sababu:

1. mpira umeisha na point 3 tumechukua.

2. tulipaswa kuwaacha wageni waingie matatizoni kwa kumpiga mwamuzi.

3. kwa vurugu zile tumeiweka timu yetu matatani itakapokwenda tunisia maana washabiki wao wanaweza kuwashambulia wachezaji wetu.

Upumbavu mkubwa.Sipendi kabisa mtu atetetee ujinga kama huo.Lazima wote waliofanya uhuni huo wakamatwe na wachukuliwe kama wahujumu uchumi.

Huo uwanja hautumii pesa za wajomba wao bali sisi watanzania tunaolipa kodi nyingi tu kila mwezi.

Serikali isicheke kabisa na wahuni hao.
Mimi ni Simba ila nilichukizwa sana na huo uhuni.Kama mtu alikuwa na hasira za kipuuzi,kwa nini asirushe simu yake?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Ukiacha wachezaji na staff wa Sfaxien waliohusika na vurugu, mashabiki waliohusika na vurugu ni wachache sana, hawafiki hata 50. Hauwezi kuhukumu tukio kama hilo kwa klabu nzima. Tukio hili lingeweza kuwa controlled vizuri tu na walinzi wa uwanjani.

Pia ukiangalia vizuri marejeo ya video mbalimbali utagundua wale waarabu waliliamsha makusudi ili kupata reaction ya mashabiki na hata walinzi walipokuwa wanawatuliza na kuwatuliza mashabiki, wao ndiyo zaidi pepo la vurugu likawa linawapanda. Kuna video moja staff wa Sfaxien alimpiga ngumi ya kichogo mlinzi wa uwanjani aliyekuwa anatuliza mashabiki wa jukwaani bila sababu yoyote halafu akajificha ili asijue ni yeye. Katika hili mnalaumu watu wasio sahihi.
 
Ni zaidi ya mwaka sasa, toka enzi za uzinduzi wa African Football League (AFL) tuliambiwa kuwa viti vyote vya uwanja wa Benjamin Mkapa vingeenda kubadilishwa kama sehemu ya matengenezo makubwa ya uwanja.

Cha ajabu viti vimeendelea kuchakaa na vingine kung'oka huku hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

Baada ya tukio la mechi ya Simba vs CS Sfaxien, nimeshangaa kusikia eti Simba inatakiwa kulipa gharama za vile viti chakavu ambavyo nina uhakika vingine tayari vilikuwa vimeshang'oka. Hili jambo siyo sawa.

Inabidi tuhoji pesa yote ya marekebisho ya uwanja imeenda wapi mbona uwanja unaonekana bado uko vile vile zaidi ya running track ambayo sijawahi kuona ikitumika katika mashindano yoyote ya riadha? Running track imebaki kutumiwa na kina Harmonize, Dj Sinyorita na Dj Ally B wakiwa wanatumbuiza.

ZIADA 1: Sijawaelewa walinzi wa Uwanja wa Mkapa. Tukio la juzi na matukio mengine ya nyuma wanaonekana wako very disorganized, hawako fiti kimwili na ni kama wafanyakazi wasio na mafunzo, weledi wa kazi zao wala mfumo wa uongozi. Juzi walishindwa kabisa kucontrol situation ndogo kama ile ya watu wachache sana, wakabaki kukimbia kimbia kama wehu.

ZIADA 2: Uwanja wa Mkapa una security camera? Matukio kama ya juzi yakitokea, ni muhimu kutoa wazi video za tukio husika ili umma ujiridhishe chanzo na wahusika ni kina nani.

ZIADA 3: Wakati wa uzinduzi wa AFL, tuliambiwa Simba ilijitolea kulipia baadhi ya gharama za matengenezo ya uwanja ikiwemo pitch na vyumbani. Inakuwaje mdau wa karibu aliyefanya juhudi za kuheshimisha na kuutangaza uwanja, halafu linapotokea tukio ambalo lilikuwa nje ya uwezo wake achukuliwe kama mhalifu badala kulizungumza ili serikali ionyeshe inakumbuka mchango wake?
Hiyo haiwapi haki wahuni wachache kung'oa viti
 
Timu ya mpira ni taasisi,ikumbukwe kila taasisi ina miundombinu yake, viwanja(vya mazoezi na vya mechi) inapotokea taasisi kubwa kama simba kukosa uwanja wake wa nyumbani haya ndio matokeo yake.
 
Ukiacha wachezaji na staff wa Sfaxien waliohusika na vurugu, mashabiki waliohusika na vurugu ni wachache sana, hawafiki hata 50. Hauwezi kuhukumu tukio kama hilo kwa klabu nzima. Tukio hili lingeweza kuwa controlled vizuri tu na walinzi wa uwanjani.

Pia ukiangalia vizuri marejeo ya video mbalimbali utagundua wale waarabu waliliamsha makusudi ili kupata reaction ya mashabiki na hata walinzi walipokuwa wanawatuliza na kuwatuliza mashabiki, wao ndiyo zaidi pepo la vurugu likawa linawapanda. Kuna video moja staff wa Sfaxien alimpiga ngumi ya kichogo mlinzi wa uwanjani aliyekuwa anatuliza mashabiki wa jukwaani bila sababu yoyote halafu akajificha ili asijue ni yeye. Katika hili mnalaumu watu wasio sahihi.
Hamna sababu ya msingi ya kung'oa Viti
Kama walikarisirika mbona hawakurusha simu zao, kwanini wasitumie mikanda.

Yaani huu uhuni haukubaliki
 
Timu ya mpira ni taasisi,ikumbukwe kila taasisi ina miundombinu yake, viwanja(vya mazoezi na vya mechi) inapotokea taasisi kubwa kama simba kukosa uwanja wake wa nyumbani haya ndio matokeo yake.
Kukosa uwanja siyo sababu ya msingi, tatizo ni nidhamu binafsi, (self discipline or self-control
 
Upumbavu mkubwa.Sipendi kabisa mtu atetetee ujinga kama huo.Lazima wote waliofanya uhuni huo wakamatwe na wachukuliwe kama wahujumu uchumi.

Huo uwanja hautumii pesa za wajomba wao bali sisi watanzania tunaolipa kodi nyingi tu kila mwezi.

Serikali isicheke kabisa na wahuni hao.
Mimi ni Simba ila nilichukizwa sana na huo uhuni.Kama mtu alikuwa na hasira za kipuuzi,kwa nini asirushe simu yake?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Na wewe unawatetea wahuni waliokula bilioni 30 ukarabati wa uwanja walisema watabadilisha viti mimi nawasapoti fans wa Simba unaona uchungu wa viti 256 ila huna uchungu na waliotafuna b 30 uenda na wewe upo kwenye mgao.
 
Point yangu gari tulishaambiwa ilitakiwa kuwa gereji ibadilishwe engine nzima na bodi lake liundwe upya na hadi tukaambiwa matumizi yake yamepunguzwa, inakuwaje tena inaharibika njiani tunaambiwa ni kwa sababu ya ubovu mpya au tatizo ni dereva mpya wakati tunajua engine nzima ilikuwa ibadilishwe na mpaka sasa haijabadilishwa?
Mkuu hapa unajaribu kumaanisha kwamba kama viti vingebadilishwa basi mashabiki wasingeweza kuviharibu?
 
Mkuu hapa unajaribu kumaanisha kwamba kama viti vingebadilishwa basi mashabiki wasingeweza kuviharibu?
Hilo pia linawezekana ingawa haikuwa lengo la uzi huu. Inawezekana uchakavu ulipunguza thamani ya vile viti katika macho ya wahusika.
 
Back
Top Bottom