Bagamoyo: Mwanamke ashindwa kuzika mwili wa mumewe. Mgogoro wasababisha afunge geti marehemu alikopaswa kuzikwa na kutokomea kusikojulikana

Bagamoyo: Mwanamke ashindwa kuzika mwili wa mumewe. Mgogoro wasababisha afunge geti marehemu alikopaswa kuzikwa na kutokomea kusikojulikana

Wanyantuzu wako tofauti na wasukuma wengine wana roho za kinyama yani isingekuwa kusema huyo mke ningejua unamsema mdingi wangu mkubwa,, ye ilikuwa binti wa mkewe(ni wa huko simiyu, na wakati anaolewa na huyo mshua tayari alikuwa na mtoto wa kike), basi maisha yameenda ila mshua ni mkoloni sasa binti akaona ya nini kutesa mama yake akamtilia sumu kwenye msosi, ila mshua hiyo siku hakujisikia kula hivyo kikamwagwa jalalani,, baada ya muda walikuta mbwa kafia hapo hapo ndo kufatilia ikajuljkana ni binti wa huyo maza,, alimtimua mpk leo hajakanyaga pale,
Hiyo kumtimua pekee haikutosha.
 
USIOGOPE ndoa.

Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971, Sura ya 29, Kipengele cha 5, Ibara ya 58 iinasema, ndoa isiwe sababu ya kumzuia mtu kutafuta chake, wala kumiliki chake, wala kuuza chake kivyake vyake.

Nje ya hiyo nyumba ya wanandoa unaruhusiwa kuwa na chako, iwe umechuma kabla au ndani ya ndoa. Ukiwa na vijumba vingine ukaweka wapangaji sawa, hizo haziguswi na mke au mme. Mradi ina jina lako na hamuishi humo.

Lakini mule mnamoishi na mkeo kaa ukijua huna mamlaka pale. Haiuziki bila idhini yake mpaka kifo kiwatenganishe. Na ukifa huna mamlaka ya kuzuia mjane kupauza. Au kuingiza ki ben 10 chake aishi nacho. Wala wewe kuandika wosia eti uzikwe mlango wa mbele. Sio eneo lako!

Kazikwe kijijini kwenu maporini huko au kwenye hizo nyumba zako za kupangisha zenye jina lako peke yako kama unataka kuzikwa mlango wa mbele.
"Na ukifa huna mamlaka ya kuzuia mjane kupauza. Au kuingiza ki ben 10 chake aishi nacho"
[emoji115][emoji115]
Na je akifa yeye nitakuwa na mamlaka ya kuingiza slay queen wangu ndani ya nyumba hiyo?
 
Mwanamke gani wa kibongo atakubali kusaini akose Mali?, Wengi wanafuata Mali kwako si dudu maana kama ni dudu mbona wanakua wanazo nyingi tu b4 ww
Hakika. Na unafuu wa maisha pia! "Wengi wanafuata mali kwako na si dudu, kama dudu wanazo za kutosha hata kabla yako"
[emoji115]
Tuishi humo
 
Janet alimfix masawe mwez August..Hali ikaanza kuzorota mwili ukaanza kupata shida...kwikwi na kiungulia ndo ugonjwa uliomtoa dunian...dalili zote za mwamke kuwa nyuma ya kifo chake ziko dhahili..dada kamuua Mume wake....lkn nae antavuna alichopanda mda si mrefu
Huyo wakudili naee fwakenii kabisaa...
 
Kila mtu kwa wakat flan kwenye dunia hii huwa ana roho mbaya. Sasa unajua kilichotokea? Yule mwanaume baada ya kuoa anataka kufukuza wanae aliozaa na marehemu mke wa kwanza ambaye yule marehem mali zote yeye ndo alichuma.
Hii dunia haina formula ndo maana watu wanawindana
Umeona mbali sana,kwenye mazingira kama hayo mtu akipata nguvu na nafasi anaweza kufanya lolote maana kwa muda huo roho inageuka anakuwa mnyama kutokana na mateso aliyopitia.
 
Yaani kwa Tz hizi tafsiri za sheria hazina mantiki kabisa, na ina shangaza jinsi jamii inavyoshadadia kudhalilishwa kwa mke wa mhusika!
Mimi naona mahakimu waliohukumu hiyo kesi wako sahihi.
Kwenye kuhukumu kesi kuna busara pia huwa zinatumika kutokana na mazingira halisi,sio kila hukumu watumie guidance ya makaratasi kama marking scheme italeta hatari ya watu kukosa haki zao au kunufaika mtu asiyestahili na ukizingatia pia kuna wosia wa marehemu umeongeza uzito zaidi.
Kwa mfano kwenye hili sakata wewe kama ndio hakimu unaona dalili zote kabisa kwamba mwanamke hakuwa na mapenzi na mme wake ila amekuja kwa lengo la kuvizia mali tu bado wewe kama hakimu utampa upendeleo wa ushindi mwanamke huyo?
Mtu ambaye unaambiwa hadi amefumaniwa akifanya ufuska na watu wengine kabla mme wake hajafariki.
 
Sheria za au maamuzi ya mahakama za Tz huwa zinaniacha hoi!
Wenzetu walioendelea, wanamheshimu Sana mume au mke wa mtu, kuliko hata wazazi na ndugu zake.
Hapa kwetu ni kinyume kabisa! Huyu mke anadharauliwa, na hapo mume kazikwa bila ya mkewe kuwepo, mke wa Mengi naye anadharauliwa, wosia wa marehemu unadharauliwa, ni nini maana ya sheria kwa Tz?!!
Mazingira ya Ulaya na huku ni tofauti mkuu,wakisema wakopi sheria zote jinsi zinavyotumika Ulaya huku hazitafanya kazi.
Kwa sababu watu wa Ulaya ni waaminifu ukilinganisha na watu wa huku kwetu ambapo watu wanafeki maisha kuingia kwenye ndoa kwa sababu ya njaa ya mali sasa ukiwapa sheria inayowabeba kwa asilimia 100 huoni kwamba vifo vitaongezeka zaidi kila siku maana sheria itakuwa imewapa guarantee kwamba mme akifa ndugu hawakuingilii maamuzi yako itakuwa hatari sana.
 
Marehemu alishaacha wosia azikwe Bagamoyo. Mke ndo amegoma kwa sababu za kibiashara. Mahakama imetoa amri mke ametoroka hajazika mumewe. Na hapo awali mke alishafumaniwa na picha zake zilichafua hali ya hewa kwa mange
Kamuua huyo
 
Ndoa sio mbaya kitu wanachofeli watu wengi kwenye ndoa ni uchaguzi wa huyo mwenza. Mtu unamkuta kitabia na kifamilia alikotoka ni class D anataka kujichomeka kuoa mwanamke aliezaliwa na kukulia class A.. Hio ndoa haitakaa idumu. ndio maana mataifa ya wenzetu kuna classes huwezi kuivuka kwenda kuoa huko juu ingawaje nao sometimes ndoa hazidumu. Kama wewe ni class D unatakiwa uoe class G Au H huko toka kijijini. sasa siku hizi mtu kapata vipesa kidogo tu kaona Tako anataka ndoa... lazima uliwe hapo .
 
Back
Top Bottom