Bahari mpya kuligawa bara la Afrika, Tanzania kuwa sehemu ya Kisiwa

Bahari mpya kuligawa bara la Afrika, Tanzania kuwa sehemu ya Kisiwa

Nashukuru hayo yakitokea nikiwa sipo dunian[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

Vizaz vijavyo vitakuja kushuhudia maajabu ambayo itawalazimu kuyaweka ktk makala za kihistoria na maumivu makali sana(tusiombe yatokee).

Tuelekeako ni kubaya kulko tulikotoka, majanga mengi ambayo hata hayajawai kushuhudiwa yanaweza kuja kuikumba dunia.

Tuweni macho na umakini mkubwa sana, tuelimike jaman tuache ujuaji wa kubishana na sayansi[emoji23]
 
Hakuna kitu kama hvyo hapo watafiti wanatafuta mkate tu
 
Usiogope ni kawaida tu, kama wewe unavyofanya ukarabati wa Nyumba yako kwa kupaka rangi mpya ama kufunga kitasa kipya ndivyo MUNGU wetu Mkuu anavyofanya
Sema Mungu wenu katiri sana na gaidi kwan hawez kufanya huo uharamia wake wa kuijenga dunia apendavyo bila kuharibu maisha ya watu na kuacha maumivu?

Emu acheni kumsingizia huyo Mungu, mambo mengine tumieni akili, majanga yanatokea sababu ya kijiografia na sio sababu za Mungu, yeye alishaumba hahusiki tena kuedit uumbaji wake, maana alishasema kila alichoumba ni sahihi so how arekebishe tena??

Elimikeni.
 
Hio ndoto ya huyo mzungu haina tofauti na ile ya yule alietengeneza filamu 2015 ambayo itaonyeshwa rasmi 2115

100 Years: The Movie You Will Never See

Sasa hii naona itatimia miaka million 500 ijayo, kipindi hicho hata fuvu langu sijui lilipo sijui litakua Makumbusho km lilivyowekwa fuvu cha Chief Mkwawa..
 
..bandari za Dsm, Bagamoyo, Tanga, na Mombasa, zitakufa.

..meli zikitoka mediterranean sea zitakuwa zinafika Tz kwa urahisi zaidi kupitia upande wa magharibi.

..pia vita vya Congo vitakuwa vimepata suluhisho la kuduma. Congo na Rwanda zitatenganishwa na bahari.
 
Mungu anaendelea kuboresha uumbaji wake kwa kutengeneza umbo alitakalo Duniani.... Kama ilivyo kwenye Nyumba zetu ujenzi hauishi kuna kuwa na maboresho ya mara kwa mara ili kupata kitu bora machoni pa Mmiliki wake
[emoji3590][emoji3590][emoji3590][emoji3590] hili ni jibu sahihi kabisa
 
Sasa tetemeko la Congo na habari za Milima zina uhusiano gani na swala la Crack za mwamba wa bahari?
Mtikisiko wa magma huko chini na hayo maeneo ya Congo ndio pua za kupumulia.

Ukicheki kwenye hiyo ramani pendekezwa ,Lake Tanganyika na eastern Congo vitakuwa sehemu ya Bahari Mpya
 
Itakuwa Mungu amechoshwa na ujinga wa waafrica acha atusongeze na Australia huko labda kipande chetu tutabadilika na kushine kidogo.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Nashukuru hayo yakitokea nikiwa sipo dunian[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

Vizaz vijavyo vitakuja kushuhudia maajabu ambayo itawalazimu kuyaweka ktk makala za kihistoria na maumivu makali sana(tusiombe yatokee).

Tuelekeako ni kubaya kulko tulikotoka, majanga mengi ambayo hata hayajawai kushuhudiwa yanaweza kuja kuikumba dunia.

Tuweni macho na umakini mkubwa sana, tuelimike jaman tuache ujuaji wa kubishana na sayansi[emoji23]
Tunavyosoma mambo ya nadharia za drifting na plate tectonics Hadi kugawanyika Kwa Dunia kwenye mabala 8 ndivyo nao watasoma maana inaweza kuja kutokea mamilioni ya miaka ijayo
 
Back
Top Bottom