Bajeti ya Kenya ni Tsh. Trilioni 78, Tanzania ni Tsh. Trilioni 34 na Uganda Tsh. Trilioni 30

Bajeti ya Kenya ni Tsh. Trilioni 78, Tanzania ni Tsh. Trilioni 34 na Uganda Tsh. Trilioni 30

Halafu pia tunapaswa kujua kuwa ufisadi kwa Kenya ni kama wamechanjiwa
Bajeti kubwa sio necessarily utendaji mkubwa / mzuri inaweza ikawa ni ufujaji... kipimo kizuri ni kuangalia bajeti zimefanya nini ?
 
Wakenya wanatuzidi utapeli na huku Sisi tumezubaa..

Mfano asilimia 80 ya watalii wetu wanapitia Kenya...

Tungekuwa wajanja tungeifanya KIA kuwa the biggest Transit Airport in Africa...
Ingesaidia mno watalii wanakuja wanatua kwanza KIA halafu ndo wanaamua kwenda Kenya au Dar au Zanzibar...

Hili kufanyika linahitaji brains sio blah blah

Hii ni takwimu za zamani,siku hizi hiyo gap imepunguzwa mno.

Kabla ya janga la Covid ndege za kimataifa zilizokuwa zinatua KIA zilikuwa zaidi ya 16.Miaka kumi nyuma zilikuwa ndege mbili tu yaani Ethiopia na KLM.

Mtalii ambaye anapanga kuja Tanzania kupitia Kenya ni nadra sana labda kama anataka kutembelea Kenya na Tanzania.
 
Nauli ya kufika Mombasa kutoka mwanza ni sh ngapi? Maisha ya TZ yanachosha akili na mwili pia
 
Kama asingekuwa Mwl. Julius Nyerere na sera mbovu baada ya vita dhidi ya Uganda sisi tulipaswa kuwa nchi yenye uchumi mkubwa ukanda huu wa Afrika mashariki.

Miaka 36 baada ya mwalimu kung'atuka, wakipitita marais 5, bado unalia lia na Nyerere? Hii sasa ndio mindset ya zama za ujima. Kutafuta wa kumlaumu isipokuwa wewe mwenyewe.

Nyerere ana share yake ya makosa na alilisema na kulikubali. Ila kumlaumu baada ya kuwa na nafasi ya miaka 36 na marais 5 ni upumbavu mkubwa!
 
Kwa Bajeti hizi za Africa Mashariki Kenya itazidi kupaa sana. Bajeti ya Kenya ni takriban mara mbili ya Bajeti ya Tanzania. Ukijumlisha Bajeti ya Tanzania na Uganda bado haifikii Bajeti ya Kenya.

Hii inaonyesha Kenya inaweza Kuendelea mara Mbili zaidi ya Tanzania na Uganda. Nadhani kuna kitu Tanzania tunahitaji kufanya. Kenya hawezi kua na Bajeti mara mbili kutuzidi wakati sisi Tanzania tuna Mambo mengi wezeshi kuwazidi.

Imeniumiza Roho sana hii.
Ujinga mtupu unakusumbua.

Haya tueleze madeni wanayopashwa kulipa hao Kenya kwa mwaka huo wa pesa ni kiasi gani?

Tueleze pia ni kiasi gani wanatakiwa kukopa kujazia kiasi ambacho hawawezi kukikusanya.

Umetazama bajeti za kila mwaka ukaona kiasi cha utekelezaji wa hiyo bajeti, na ukajuwa kwamba kiasi hicho cha pesa ni kweli ndicho kitakachotumika?

Ni watu kama wewe ndio mnaopapatikia vitu bila kujuwa maana yake ni nini.

Na bado hujaweka fungu litakaloenda kwa "tenderpreneurs na Cartels", au yote haya wewe huyajui? Unayojuwa ni kusoma manamba makubwa tu na kushangaa basi?

Bure kabisa.
 
Wakenya kuwa mbele yetu isiwe sababu na wala tusiwachukie kwasababu hiyo, tujiulize shida yetu inaanzia wapi, binafsi naamini shida yetu imeanzia kwa hii kitu inaitwa CCM na vyote vilivyomo ndani yake.
Hapa ndipo uwezo wetu unapoishia, shida sio CCM, trust me. Shida ni uwezo mdogo wa kufikiri, ubinafsi na kukosa uzalendo kwa mtanzania.
 
Trilioni 34 ndiyo bajeti ya watu milioni 60 wakati tajiri mmoja wa Marekani anayeitwa Jeff Bezos ana utajiri wa zaidi ya trilioni 354. Yaani mtu mmoja ana utajiri wa zaidi ya mara 10 ya bajeti yetu ya watu milioni 60. Fikiria hilo kwanza ndiyo utajua ni jinsi gani Ujamaa ulivyotuchelewesha kimaendeleo na kuturudisha nyuma.
 
Tanzania, bado tunasumbuliwa na fikira za kijamaa (ujamaa wa Nyerere) ambazo haziko mbali sana na ujima! Inahitajika mkakati kabambe wa kufutilia mbali fikira za kijima ambapo ni pamoja na kusikia watu wanajivunia kuitwa 'wanyonge', kujisifu kuwa ni 'matajiri' huku unafungia wenye mitaji na teknolojia milango, nk
Tukikuuliza utueleze hayo uliyoandika hapa huna lolote ujualo, bali unaimba kama kasuku tu basi!

Hopeless!
 
Unalinganisha volume na value ya bajeti bila ya kufanya mazingatio ya maana katika uendeshaji wa uchumi wa nchi hizi mbili. Angalia madeni, mishahara ya watumishi na viongozi wa kisiasa, aina ya vyanzo vya kodi na kodi halisi inatokusanywa pamoja na athari zake katika ujuaji wa uchumi na maendeleo ya ustawi wa jamii.

Ndugu mtaalam, ulinganifu unaoufanya utakunyanyasa bure maskini. Sio kwamba natetea serikali ya URT kwa kuwa na bajeti ndogo kulinganisha na Kenya, ila hujatenda sawa kulinganisha variable mbili zennye tabia tofauti tena bila ya kuweka ama kuchagua vigezo mahsusi vya kufanya ulinganifu unaoutaka.

Angalia mgawanyo wa bajeti yenyewe katika maeneo mahsusi, kwa mfano, fedha zilizotengwa kwa miradi ya maendeleo, fedha zilizotengwa kwa matumizi ya kawaida. Pengine angalia aina ya vyanzo vipya vya makusanyo, ongezeko la kodi katika maeneo yenye kugusa maisha na ustawi wa jamii wa mtumishi wa ngazi ya chini na mwananchi wa kawaida.

Aaaaaa kiongozi wangu haya mambo ya bajeti za serikali wakati mwengine tuzitazame tuu. Mwisho wa siku unaeza kuta jumla ya fedha zilizotumika mwisho wa mwaka wa bajeti ni 55% tuu ya zile zilizokadiriwa kukusanywa na kutumika.

Na haswa kwa hawa mabepari wa kikikuyu na kikamba walivyo na mafuta ya uso ndio usiseme. Kwao wao lolote linawezekana.

KARIBU KIBERA MKUU.
 
Ujinga mtupu unakusumbua.

Haya tueleze madeni wanayopashwa kulipa hao Kenya kwa mwaka huo wa pesa ni kiasi gani?

Tueleze pia ni kiasi gani wanatakiwa kukopa kujazia kiasi ambacho hawawezi kukikusanya.

Umetazama bajeti za kila mwaka ukaona kiasi cha utekelezaji wa hiyo bajeti, na ukajuwa kwamba kiasi hicho cha pesa ni kweli ndicho kitakachotumika?

Ni watu kama wewe ndio mnaopapatikia vitu bila kujuwa maana yake ni nini.

Na bado hujaweka fungu litakaloenda kwa "tenderpreneurs na Cartels", au yote haya wewe huyajui? Unayojuwa ni kusoma manamba makubwa tu na kushangaa basi?

Bure kabisa.
Unajifanya Mjuaji. Porojo nyingi.
Je sisi Tanzania ni lini tuliweza kutekeleza Bajeti kwa asilimia 100 au hata 50.
Hata hii tu Bajeti kwa kiasi kikubwa tunategemea wahisani.
Tanzania tukiwa Serious tunaweza kufanya Makubwa kuliko yeyote Afrika Mashariki.
Kuna jambo sote kama raia na serikali tunapaswa kufanya.
 
Jadiri hoja iliyowekwa mezani, (kwanini budget ya Kenya ni karibu mara mbili ya budget ya Tanzania?)...
Kwa sababu uchumi wa Kenya ni mkubwa, karibia mara mbili ya uchumi wa Tanzania.
 
Ukweli mchungu Jiwe alichezea uchumi miaka 5 bila budget kuongezeka wala kuwa na graph inayopanda

Sasahivi tungekuwa kwenye trion 50 ila utoto wa kuchezea walipa kodi na kuwafirisi ndio zao lake hili.
Wewe ni kilaza mkubwa mno. Bajeti ya Magufuli ilitekelezwa kwa kiasi kikubwa
 
Bajeti kubwa haiimaanishi kwamba ndio inaleta maendeleo. Kenya wanabandika manamba makubwa kwa sababu kwa sehemu kubwa wanatumia Expenditure-Driven budget yaani sehemu kubwa wanapanga bajeti kwa ajili ya matumizi zaidi kuliko maendeleo na kulipa madeni pia. Mpaka ninapoandika hapa Kenya inakopa zaidi ya nchi zote ukimjulisha kwa pamoja hapa Afrika mashariki ili kujazilishia bajeti yao.

Binafsi naamini tupaswa kuwa na bajeti isiyozidi trilioni 30 maana uwezo wa ukusanyaji wetu wa mapato ni trilioni 25 tu. Tuwe na bajeti inayotokana na mapato zaidi (Revenue-Driven budget) halafu tufanye miradi michache ila ipate uwekezaji mkubwa na serikali ipunguze gharama za uendeshaji ikiwemo kuyaondoa mashirika ya umma yanayojishughulisha na biashara kama ATCL, wao wajikite ktk kutoa huduma tu.

Wakenya kiujumla wana akili ndogo sana kichwani. Kama asingekuwa Mwl. Julius Nyerere na sera mbovu baada ya vita dhidi ya Uganda sisi tulipaswa kuwa nchi yenye uchumi mkubwa ukanda huu wa Afrika mashariki. Edwin Mtei alijitoa nafasi yake kama waziri wa fedha baada ya Mwl kukataa sera ambazo Rais Ali Mwinyi na Rais Benjamini Mkapa walikuja kuzitekeleza baadae na nchi ikasimama kidogo kuliko tulivyozidi kupotea.
Kwa usimamizi na mkakati mzuri tz inaweza kukusanya hata zaidi ya 40T
 
Kwa Bajeti hizi za Africa Mashariki Kenya itazidi kupaa sana. Bajeti ya Kenya ni takriban mara mbili ya Bajeti ya Tanzania. Ukijumlisha Bajeti ya Tanzania na Uganda bado haifikii Bajeti ya Kenya.

Hii inaonyesha Kenya inaweza Kuendelea mara Mbili zaidi ya Tanzania na Uganda. Nadhani kuna kitu Tanzania tunahitaji kufanya. Kenya hawezi kua na Bajeti mara mbili kutuzidi wakati sisi Tanzania tuna Mambo mengi wezeshi kuwazidi.

Imeniumiza Roho sana hii.
Mikopo zaidi wakati ya Tanzania na Uganda ni mapato ya ndani kwa asilimia 70
 
Kazi kusifia Wakenya badala ya kusifia mazuri ya Tanzania.

Chadema wakiambiwa tujenge Tanzania ya viwanda ili tuwe na uzalishaji mkubwa wanapinga.

..mnasema Tz ya viwanda halafu mnakwenda kununua midege ya matrilioni toka kwa makampuni ya mabeberu.
 
True..!
Ukiona watu wanakomalia udaku na mambo mepesi...wanang'angana na kupigania Diamond atolewe BET badala ya kujadili mambo ya msingi, hapo ujue tuna safari ndefu sana kama taifa
We jamaa, umeongea ukweli tupu!!

Tunamijitu inaroho mbaya, Acha roho mbaya, yaani inatumua muda mwingi kufanya mambo ya kijinga kuliko mambo ya mhimu
 
Wakenya wanatuzidi utapeli na huku Sisi tumezubaa..

Mfano asilimia 80 ya watalii wetu wanapitia Kenya...

..Ni vigumu KIA kushindana na uwanja wa ndege wa Nairobi.

..Nairobi ni mji mkuu wa Kenya, lango la watalii wanaotembelea Kenya, na vilevile wana-host mashirika na makampuni mengi ya kimataifa.

..Mpaka hapo utaona kwamba Nairobi inahudumia wasafiri wa aina nyingi, ukilinganisha na KIA ambayo inahudumia watalii peke yake.

..Hali hiyo ndiyo inayopelekea ndege nyingi kutua Nairobi na watalii wanaotarajia kutembelea Tanzania [ north circuit of tourism] kutumia uwanja huo.

NB:
..kitu ambacho tunatakiwa kufanya sasa hivi ni kuhakikisha jiji la Dsm linakuwa kitovu cha utalii wa fukwe za bahari. Dsm isiishie kuwa jiji la biashara peke yake, tuongeze na utalii.
 
Kamfukue mwendazake ndio karudisha nyuma nchi hii,miaka 5 imeenda bure Kenya wakapanua wigo na Uganda wanatupumulia
 
Back
Top Bottom