Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Bakhresa, Mo Dewji na GSM wajitosa kuwekeza kwenye SGR

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ni vema ukayafahamu haya mapema kwa faida yako

Bali wadau wengi wanajiuliza kwamba ni kitu gani ambacho Serikali ya Tanzania inaweza kufanya, maana unaambiwa ni afadhali hata mtoto mwenye Polio waweza kumpa Magongo akatembea mwenyewe

Screenshot_2024-06-19-20-11-33-1.png

Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.

Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.

Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.

“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.

Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
 
Mmoja tu kutoka CCM asimame athibitishe kwamba yeye ni msomi, ana uchungu na nchi pia anaweza kuitoa nchi hapa ilipo na kuipeleka kwenye maendeleo ni nani nauliza?

Hayupo hata mmoja, walioko huko wote wanawaza ni namna ipi wafanye ili wapate nafasi ya kuiba na kulihujumu Taifa
 
Serikali tunataka tujue hao wawekezaji wanaojitosa kuwekeza kwenye reli ya SGR kwanini Leo ! Au NI mbinu ya serikali kuuza miundo mbinu kijanja kwa hayo makampuni ya GSM LAKE OIL JAMBO NA MOHAMED ENTERPRISES Tanzania imekopeshwa matrion ya fedha kwa ajiri ya mradi huo Leo inageuka kuwapa watu waendeshe huyu mama huyu mama mbona nazidi Sana akumbuke Sheria zinabadilika siku moja atatokea mtu kama magu watu wataanza kunyanga'nywa pesa kwa ajiri ya kusaidia nchi watasema wanaonewa NI za kwao lakini hawatokumbuka kuwa waliibia nchi ngoja siku inakuja pigeni pesa kwa njia rahisi lakini labda mtahama nchi hii maana amini nawaambia watanzania siyo wajinga.
 
Back
Top Bottom