Bakita iandae utaratibu wa kutoa taarifa kwa Wananchi walau mara moja kwa mwaka.

Bakita iandae utaratibu wa kutoa taarifa kwa Wananchi walau mara moja kwa mwaka.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Moja ya sifa ya lugha yoyote duniani ni pamoja na lugha hiyo kukua.Hujitokeza misamiati,nahau mpya au hata baadhi ya maneno kuchepushwa kutoka kwenye maana take ya asili.Sina utafiti rasmi ila naamini kwa kizazi kilichopo sasa hivi mambo ndio yanaenda kwa kasi Sana.Hivyo basi imekuwa ni ngumu Sana kujua kama maneno au misemo iliyoibuka kama imerasimishwa au la.Na wenye jukumu hilo kwa Tanzania ni Bakita.Ningetamani Taasisi hii iende na wakati uliopo na spidi iliyopo.Nakumbuka kuna hotuba ya Baba wa taifa akishauri Kuwa kama neno limeshika kwenye jamii na hainekani dalili ya kupotea basi lirasimishwe.Sijawahi kusikia mahali neno kama Tapeli,solemba n.k kama yamewahi kurasimishwa. Huenda yapo yanayofanywa na Bakita lakini wengi hatuna taarifa,ila ni vizuri sasa Bakita nanyi muingie mitandaoni tupeane taarifa.
 
Nimekuwa nawaza hili jambo kwa muda mrefu sana. Nimeona kama Oxford wamekuwa wanarasimisha maneno mapya na pia wana keep trend yale yanayoshika kasi kila mwaka.

Kwa kweli kizazi kipya kinaenda kasi sana na pia mabadiliko ya technology yanabadilika kwa haraka zaidi. Tusipokuwa waangalifu, hata ile ndoto ya kusema tunataka kufundisha masomo kwa Kiswahili itachukua muda zaidi.

Binafsi nimechukua hatua kujaribu kusaidia katika hii changamoto ukizingatia sasa hivi Kiswahili kinazungumzwa katika nchi nyingi duniani. Nilichofanya ni kuandika mobile application ya Android inayoitwa KuKi (Kuza Kiswahili), ambayo itajumuisha jamii kuchangia tafsiri ya maneno ya Kingereza ambayo hayana official translation. Application inapatikana tayari Google play na yeyote mwenye simu ya Android anaweza kuipata bure.
 
Back
Top Bottom