BAKWATA waiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini Bungeni

BAKWATA waiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini Bungeni

Wanajukwaa! Mmesikia huko

Naona Bungeni ni patamu sana kila mtu anataka akale utamu wa Bunge
=================

Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania (BAKWATA) kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake, Sheikh Mohamed Khamis, wameitaka serikali kupunguza gharama za matibabu pamoja na kuboresha maslahi ya walimu ili kuendelea kukuza nguvu za kiuchumi na kujenga jamii iliyoelimika kuelekea mwaka 2050.

Sheikh Khamis ametoa kauli hiyo Jumatatu, Januari 13, 2025, katika Mkutano wa Kamati ya Dini Mbalimbali Kuhakiki Rasimu ya Dira hiyo, uliofanyika Ukumbi wa TEC, Kurasini, Dar es Salaam, ikiwa ni Kundi la Mwisho kufikiwa na Tume ya Mipango kwaajili ya Mapitio ya rasimu hiyo.

Soma Pia: Kesi ya Kikatiba dhidi ya Serikali na BAKWATA imetajwa leo 26.11.2024, Mahakama Kuu

Sheikh Khamis, amehimiza pia umuhimu wa serikali kusimamia ratiba na mapumziko kwa wanafunzi wa shule za Serikali na za binafsi kama sehemu ya kuhakikisha kuwa kunakuwa na ulinganifu wa masomo na mapumziko kwa wanafunzi.

Bakwata wameiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ulivyo uwakilishi mwingine kwenye chombo hicho muhimu cha kutunga sheria.

View attachment 3201110
Waunde tu chama cha siasa. Wananiudhi tu kelele ya masipika hasa maeneo ya kunduchi mtakuja pale
 
Dawa ya huu ujinga wote ilikuwa ni ile Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba. Sema ndiyo hivyo tena; wanasiasa kutokana na ubinafsi wao, wameona waturudishe miaka zaidi ya 40 nyuma.
 
Kujisimamia wenyewe tu hawawezi ,chuo kikuu mpaka Mzee Mkapa akawapa majengo, kwanza kila mwaka wawe wanaenda Lupasu kuhiji, huko bungeni watawakilisha nini, watafute vyama wakagombee, waliopo mule tunaona wengi sana alaa! Wakatafute mapori walime huko!
 
Wanajukwaa! Mmesikia huko

Naona Bungeni ni patamu sana kila mtu anataka akale utamu wa Bunge
=================

Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania (BAKWATA) kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake, Sheikh Mohamed Khamis, wameitaka serikali kupunguza gharama za matibabu pamoja na kuboresha maslahi ya walimu ili kuendelea kukuza nguvu za kiuchumi na kujenga jamii iliyoelimika kuelekea mwaka 2050.

Sheikh Khamis ametoa kauli hiyo Jumatatu, Januari 13, 2025, katika Mkutano wa Kamati ya Dini Mbalimbali Kuhakiki Rasimu ya Dira hiyo, uliofanyika Ukumbi wa TEC, Kurasini, Dar es Salaam, ikiwa ni Kundi la Mwisho kufikiwa na Tume ya Mipango kwaajili ya Mapitio ya rasimu hiyo.

Soma Pia: Kesi ya Kikatiba dhidi ya Serikali na BAKWATA imetajwa leo 26.11.2024, Mahakama Kuu

Sheikh Khamis, amehimiza pia umuhimu wa serikali kusimamia ratiba na mapumziko kwa wanafunzi wa shule za Serikali na za binafsi kama sehemu ya kuhakikisha kuwa kunakuwa na ulinganifu wa masomo na mapumziko kwa wanafunzi.

Bakwata wameiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ulivyo uwakilishi mwingine kwenye chombo hicho muhimu cha kutunga sheria.

View attachment 3201110
HUU NI UPUUZI,DINI ZA NINI BUNGENI WAKATI NCHI HAINA DINI?

HIVI MTU HADI KUWAZA KIWANGO HIKI KUWA AMETOKA KULA NINI?
 
Na walivyokuwa wapuuzi waliyozidi kiwango mfano hai kipindi cha Magu alipokuja mfalme wa Morocco.

Magu kawapigia pande waombe msaada, wao wananyanyuka wanaomba msikiti mpaka Magu aliwashangaa!

Akawaambia nyinyi badala ya kuomba mjengewe taasisi za elimu kama vyuo nyinyi mnaomba mjengewe msikiti?

Mimi mwenyewe muislamu mwenzao nikabaki nimeshangaa! Hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Kwenye dini kuna kitu kinaitwa amalin swaaliha! Yaani fanya jambo jema lililostahiki kwa mazingira husika.

Unaweza ukafika mahali ukajenga msikiti, sawa utapata thawabu, lakini lile eneo shida yao si msikiti. Shida yao ni maji! Hivyo unatakiwa ujenge visima vya maji.

Bakwata badala ya kuomba wajengewe mashule n.k wao wanaomba wajengewe msikiti. Hatukatai msikiti, lakini swali hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Leo wamekuja wanataka uwakilishi bungeni!!!!!

Kwa heshima ya Mufti kwa vile ni kiongozi wetu wa kiislamu sitaki niizungumze vibaya zaidi. Ila hii taasisi ni 🙌
Halafu wenzao wanaendelea wanaanza kulalamika wanapendelewa, hivi tasisi wamejenga hosp na vifaa wameweka serikali itashindwa kuwalipa wafanyakazi ili hali wanasaidia wananchi! Sijui wapoje wale watu.
 
Na walivyokuwa wapuuzi waliyozidi kiwango mfano hai kipindi cha Magu alipokuja mfalme wa Morocco.

Magu kawapigia pande waombe msaada, wao wananyanyuka wanaomba msikiti mpaka Magu aliwashangaa!

Akawaambia nyinyi badala ya kuomba mjengewe taasisi za elimu kama vyuo nyinyi mnaomba mjengewe msikiti?

Mimi mwenyewe muislamu mwenzao nikabaki nimeshangaa! Hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Kwenye dini kuna kitu kinaitwa amalin swaaliha! Yaani fanya jambo jema lililostahiki kwa mazingira husika.

Unaweza ukafika mahali ukajenga msikiti, sawa utapata thawabu, lakini lile eneo shida yao si msikiti. Shida yao ni maji! Hivyo unatakiwa ujenge visima vya maji.

Bakwata badala ya kuomba wajengewe mashule n.k wao wanaomba wajengewe msikiti. Hatukatai msikiti, lakini swali hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Leo wamekuja wanataka uwakilishi bungeni!!!!!

Kwa heshima ya Mufti kwa vile ni kiongozi wetu wa kiislamu sitaki niizungumze vibaya zaidi. Ila hii taasisi ni 🙌
Ni waislamu wachache wanaweza kuwa na vision kama yako.
 
Bakwata ni Taasisi ya kijinga sana!

Nimeona wanaishauri serikali iwazuie vijana na betting.

Hekima ya dini yenyewe inakutaka kama umezuia mlango huu basi onyesha mlango mwengine wa kupitia.

Badala ya wao waishauri serikali iwezeshe kukuza taasisi binafsi ili nazo ziweze kuajiri kwa wingi ili kusaidia kupunguza ukosefu wa ajira.

Ishauri serikali iwezeshe kwenye nyanja nyengine ili vijana waweze kujiajiri na kulitumikia taifa. Wawezeshwe kwa njia rafiki kwenyw kilimo, ufugaji wa wanyama na samaki n.k

Baada ya haya angalau ndiyo utoe na ushauri wa masuala ya betting.

Wao wanakuja tu na tamko, serikali zuieni betting. Hii taasisi ina watu wana akili kweli?

Kama watu wanaficha msaada kama tende zifike kwa waislamu wenzao, yaani tende kitu kidogo tu! Huwa wananishangaza sana!

Ashakum si matusi! Ila hii taasisi ni mavumbi matupu!
Expert sikubaliani na mawazo yako,kwahiyo waache kupinga mambo haramu kwakuwa hawajatoa solution ya nini kifanyike,naona hapo umeingia chaka

Kwa maana nyingine hawa viongozi wa dini au taasisi za dini zisikemee uovu kisa hawajatoa njia mbadala? Hivi kabla ya betting watu walikuwa wanaendeshaje maisha yao?

Unazungumzia sijui wananyima tende,hivi una ushahidi au na wewe yale unayoyasikia vijiweni nawe unayaamini tu,natambua kama wewe ni muislamu tunaambiwa katika qur'aan tukufu kwamba anapo wajia mtu na kuwapa habari yoyote basi kwanza muichunguze ili msije mkawa dhuru watu bure pasina kujua

sasa expert mwenzangu,je umejiridhisha na habar hii au unataka kuwavunjia watu heshima bure,tuchunge sana vinywa vyetu
 
Nchi itaongozwa zaidi kwa maombi badala ya kazi na ubunifu tukiruhusu ajenda hii ya maaskofu na masheikh

Wamealika sana katika mikutano ya kiserikali na kisiasa, sasa wamenogewa wanataka madaraka ya ki sekuka secular wafaidi mambo ya kidunia

Baadaye watakuwa wanapokea amri kutoka Rome, Jerusalem, Mecca, Najaf, Karbala, Alexandria, Tehran n.k kuzileta bungeni zijadiliwe, hii ni hatari ipo siku kila kitu kitaangliwa kidhehebu dhehebu na kiimani badala ya kiuchumi, kidemokrasia, kijamii na kisayansi kutokana na akili za mtu mweusi kupeleka akili zao kwa imani za kigeni.
 
Kuna Mzee mmoja sheih nani sijui mweupe hivi alikuwa na meno ya mbalimbali sijamuona siku nyingi mada za dini walikuwa sana chanel 10 hivi yupo wapi? Ha ha ha hii hajachangia kweli Mzee mdini yule mmm!
 
Ni waislamu wachache wanaweza kuwa na vision kama yako.
Nikiliweka hili suala kiujumla, si kwamba najizungumzia mimi kwa sababu binafsi bado najijua ni mdogo sana kimaarifa ila nafahamu hili kuhusu Bakwata: Bakwata huwa hawahitaji waislamu wenye elimu na wenye kujielewa. Ukiwa na hizo sifa watakupiga vita humo ndani.

Hili suala aliniambia baba yangu tangu mwaka 2003 kipindi hicho nipo naye sebuleni tunatizama tv Bakwata viongozi wa dini wakihojiwa stesheni ya TVT. Kulikuwa na muislamu mmoja ni PhD holder na amesoma dini alikuwa anahitaji nafasi ya u-Mufti.

Ila baada ya kukua nikajua viongozi wa Bakwata wengi sana wanaendekeza ushirikina, si ajabu wakakuroga.
 
Nikiliweka hili suala kiujumla, si kwamba najizungumzia mimi kwa sababu binafsi bado najijua ni mdogo sana kimaarifa ila nafahamu hili kuhusu Bakwata: Bakwata huwa hawahitaji waislamu wenye elimu na wenye kujielewa. Ukiwa na hizo sifa watakupiga vita humo ndani.

Hili suala aliniambia baba yangu tangu mwaka 2003 kipindi hicho nipo naye sebuleni tunatizama tv Bakwata viongozi wa dini wakihojiwa stesheni ya TVT. Kulikuwa na muislamu mmoja ni PhD holder na amesoma dini alikuwa anahitaji nafasi ya u-Mufti.

Ila baada ya kukua nikajua viongozi wa Bakwata wengi sana wanaendekeza ushirikina, si ajabu wakakuroga.
Sasa kuroga si kama kunywa maji tu 😀 unazunguka tu nyuma ya nyumba ha ha h
 
Nchi itaongozwa zaidi kwa maombi badala ya kazi na ubunifu tukiruhusu ajenda hii ya maaskofu na masheikh

Wamealika sana katika mikutano ya kiserikali na kisiasa, sasa wamenogewa wanataka madaraka ya ki sekuka secular wafaidi mambo ya kidunia

Baadaye watakuwa wanapokea amri kutoka Rome, Jerusalem, Mecca, Najaf, Karbala, Alexandria, Tehran n.k kuzileta bungeni zijadiliwe, hii ni hatari ipo siku kila kitu kitaangliwa kidhehebu dhehebu na kiimani badala ya kiuchumi, kidemokrasia, kijamii na kisayansi kutokana na akili za mtu mweusi kupleka akili zao kwa imani za kigeni.
Bora hata amri ya Roma maana ni watu wenye elimu zao zakutosha, hawaokotani kama kuchambua chuya.
 
Wanajukwaa! Mmesikia huko

Naona Bungeni ni patamu sana kila mtu anataka akale utamu wa Bunge
=================

Baraza Kuu la Waislamu nchini Tanzania (BAKWATA) kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake, Sheikh Mohamed Khamis, wameitaka serikali kupunguza gharama za matibabu pamoja na kuboresha maslahi ya walimu ili kuendelea kukuza nguvu za kiuchumi na kujenga jamii iliyoelimika kuelekea mwaka 2050.

Sheikh Khamis ametoa kauli hiyo Jumatatu, Januari 13, 2025, katika Mkutano wa Kamati ya Dini Mbalimbali Kuhakiki Rasimu ya Dira hiyo, uliofanyika Ukumbi wa TEC, Kurasini, Dar es Salaam, ikiwa ni Kundi la Mwisho kufikiwa na Tume ya Mipango kwaajili ya Mapitio ya rasimu hiyo.

Soma Pia: Kesi ya Kikatiba dhidi ya Serikali na BAKWATA imetajwa leo 26.11.2024, Mahakama Kuu


Sheikh Khamis, amehimiza pia umuhimu wa serikali kusimamia ratiba na mapumziko kwa wanafunzi wa shule za Serikali na za binafsi kama sehemu ya kuhakikisha kuwa kunakuwa na ulinganifu wa masomo na mapumziko kwa wanafunzi.

Bakwata wameiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ulivyo uwakilishi mwingine kwenye chombo hicho muhimu cha kutunga sheria.

View attachment 3201110
Walivyosikia "Separation of Church and State" wakasema "Sisi wa msikitini haituhusu hiyo" 😂😂😂
 
Labda viongozi wa Dini wapewe nafasi ya ''observers" lakini wasiwe wabunge, wakuu mnaonaje?
 
VIONGOZI WA KIDINI KUAMUA KUWA CHAWA, WALILIA KUWA WABUNGE WA VITI MAALUM KUSHIRIKIANA NA MIHIMILI KANDAMIZI

Fast forward 2025 viongozi wa kidini karne hii nchini Tanzania kuwa chawa, mawakala, madalali, vibaraka na mamluki wa mstari wa mbele kabisa kutetea ubeberu na ukoloni mamboleo, kunyamazia unyanyasaji, mauaji, nini kimewapata wazee wa mjini wa kileo ambao mababu zao wa miaka ya 1950 walipinga kuwa watwana ndani ya nchi yao...

Je kuna tatizo kwa baadhi ya viongozi wa madhehebu mbalimbali wa dini ya Uislamu, Ukristo nchini Tanganyika kukemea ukoloni kwa sasa ?


Nyerere azungumzia dini ziwe mstari wa mbele katika ukombozi wa kweli

21 Mar 2020
Managua, Nicaragua

Julius Nyerere - Nini Kimewapata viongozi wa dini mmeamua kukaa kimya huku mnaona uonevu ukitamalaki !

View: https://m.youtube.com/watch?v=TAP6O3MeqiA
Description
 
Nikiliweka hili suala kiujumla, si kwamba najizungumzia mimi kwa sababu binafsi bado najijua ni mdogo sana kimaarifa ila nafahamu hili kuhusu Bakwata: Bakwata huwa hawahitaji waislamu wenye elimu na wenye kujielewa. Ukiwa na hizo sifa watakupiga vita humo ndani.

Hili suala aliniambia baba yangu tangu mwaka 2003 kipindi hicho nipo naye sebuleni tunatizama tv Bakwata viongozi wa dini wakihojiwa stesheni ya TVT. Kulikuwa na muislamu mmoja ni PhD holder na amesoma dini alikuwa anahitaji nafasi ya u-Mufti.

Ila baada ya kukua nikajua viongozi wa Bakwata wengi sana wanaendekeza ushirikina, si ajabu wakakuroga.
Aloo nimecheka as I reacted to your post
 
haya maV8 mjapan anayotoa inasababisha waafrika kutoana roho, Kila mtu anapambana akae kwenye kilo ale keki ya nchi.
 
Na walivyokuwa wapuuzi waliyozidi kiwango mfano hai kipindi cha Magu alipokuja mfalme wa Morocco.

Magu kawapigia pande waombe msaada, wao wananyanyuka wanaomba msikiti mpaka Magu aliwashangaa!

Akawaambia nyinyi badala ya kuomba mjengewe taasisi za elimu kama vyuo nyinyi mnaomba mjengewe msikiti?

Mimi mwenyewe muislamu mwenzao nikabaki nimeshangaa! Hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Kwenye dini kuna kitu kinaitwa amalin swaaliha! Yaani fanya jambo jema lililostahiki kwa mazingira husika.

Unaweza ukafika mahali ukajenga msikiti, sawa utapata thawabu, lakini lile eneo shida yao si msikiti. Shida yao ni maji! Hivyo unatakiwa ujenge visima vya maji.

Bakwata badala ya kuomba wajengewe mashule n.k wao wanaomba wajengewe msikiti. Hatukatai msikiti, lakini swali hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Leo wamekuja wanataka uwakilishi bungeni!!!!!

Kwa heshima ya Mufti kwa vile ni kiongozi wetu wa kiislamu sitaki niizungumze vibaya zaidi. Ila hii taasisi ni 🙌
gTurn Ritz FaizaFoxy Malaria 2
 
Back
Top Bottom