BAKWATA waiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini Bungeni

BAKWATA waiomba serikali kutenga viti vya uwakilishi wa Taasisi za kidini Bungeni

Expert sikubaliani na mawazo yako,kwahiyo waache kupinga mambo haramu kwakuwa hawajatoa solution ya nini kifanyike,naona hapo umeingia chaka

Kwa maana nyingine hawa viongozi wa dini au taasisi za dini zisikemee uovu kisa hawajatoa njia mbadala? Hivi kabla ya betting watu walikuwa wanaendeshaje maisha yao?

Unazungumzia sijui wananyima tende,hivi una ushahidi au na wewe yale unayoyasikia vijiweni nawe unayaamini tu,natambua kama wewe ni muislamu tunaambiwa katika qur'aan tukufu kwamba anapo wajia mtu na kuwapa habari yoyote basi kwanza muichunguze ili msije mkawa dhuru watu bure pasina kujua

sasa expert mwenzangu,je umejiridhisha na habar hii au unataka kuwavunjia watu heshima bure,tuchunge sana vinywa vyetu
Akhy, nashukuru kwa mchango wako!

Binafsi si mbetiji na siungi mkono suala la betting. Imam Ghazali anasema unapotaka kutibu tatizo kwanza dili na chanzo chake.

Hata kwenye dini mtu akiiba hakatwi mkono papo hapo! Ni lazima kwanza ichunguzwe kwa nini kaiba. Ikiwa kama wizi wake ni kutokana na hali ngumu ya kimaisha inatakiwa awezeshwe! Ila ikowa ni sababu nyenginezo ambazo hazina mashiko hukumu itampitia.

Vijana wengi wao kwa sasa wanabeti kutokana na hali ngumu ya maisha. Ajira hakuna na hata kujiajiri kwenyewe kunaitaji kuwezeshwa na hizo fursa hakuna. Kijana kama huyu unafikiri kipato chake kitatokana na nini kama siyo betting ambayo sasa imefanywa shughuli rasmi?

Bakwata ingejikita kwanza kuishauri serikali itanue wigo wa raia wawe na shughuli rasmi na za kihalali ambazo zinakwenda sambamba na maadili ya jamii zetu pamoja na maadili ya dini zetu.

Kwa namna hiyo ingeishauri serikali kwa namna kama wataalamu wa masuala.ya uchumi wanavyo washauri. Baada ya hapo ndipo wangetoa ushauri wao huu. Yaani kwa kufanya hivyo, itasaidia vijana kujiepusha na betting kwani ni suala baya linaongeza umasikini. Kwa misingi hiyo tunaishauri serikali ipige marufuku kwa kulinda maadili na kukiokoa kizazi.
 
Dola siku zote ni chombo kandamizi, viongozi hawa wanatakiwa wasiwe sehemu ya wafanya maamuzi katika vyombo vya dola.

Viongozi wa kidini waendelee kukemea maovu ya kila aina wakiwa huru nje ya vyombo hivi wanavyolilia wapewe viti maalum vya ubunge.
 
Na walivyokuwa wapuuzi waliyozidi kiwango mfano hai kipindi cha Magu alipokuja mfalme wa Morocco.

Magu kawapigia pande waombe msaada, wao wananyanyuka wanaomba msikiti mpaka Magu aliwashangaa!

Akawaambia nyinyi badala ya kuomba mjengewe taasisi za elimu kama vyuo nyinyi mnaomba mjengewe msikiti?

Mimi mwenyewe muislamu mwenzao nikabaki nimeshangaa! Hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Kwenye dini kuna kitu kinaitwa amalin swaaliha! Yaani fanya jambo jema lililostahiki kwa mazingira husika.

Unaweza ukafika mahali ukajenga msikiti, sawa utapata thawabu, lakini lile eneo shida yao si msikiti. Shida yao ni maji! Hivyo unatakiwa ujenge visima vya maji.

Bakwata badala ya kuomba wajengewe mashule n.k wao wanaomba wajengewe msikiti. Hatukatai msikiti, lakini swali hapa Dar kuna misikiti mingapi?

Leo wamekuja wanataka uwakilishi bungeni!!!!!

Kwa heshima ya Mufti kwa vile ni kiongozi wetu wa kiislamu sitaki niizungumze vibaya zaidi. Ila hii taasisi ni 🙌
Kazi kweli kweli
 
Sasa kuroga si kama kunywa maji tu 😀 unazunguka tu nyuma ya nyumba ha ha h
Aah wapi ndugu yangu!

Mambo ya kutupiana majini nawaachia wao wenyewe.

Viongozi wapo kwa maslahi yao binafsi na hawapo kama dini inavyofundisha.
 
Aloo nimecheka as I reacted to your post
Amini Mkuu Scars.

Na ndiyo maana kibongo bongo viongozi wa dini wanaojielewa na wenye hofu ya Mungu kwa namna ya mafundisho yanavyosema wamechagua kutojihusihsa kwenye mambo ya kiuongozi wa Taasisi mfano wa Bakwata.

Wao wanafundisha watu dini na kuwalea malezi ya kiroho. Na huwa hawapendi kuonekana kwenye TV.
 
Back
Top Bottom