Balali apewe Kinga!

Balali apewe Kinga!

Status
Not open for further replies.
Mzee ES, sijuia kama unafahamu sheria zetu au la. Tunayo sheria ya kinga. Nilimuuliza Prof. Shivji kabla ya kuandika makala hii na hakukumbuka kama kuna wakati wowote ambapo sheria hiyo imewahi kutumika.

Labda niweke hoja yangu hapa ili watu wasome na kuelewa nilichosema badala ya kuchukua maneno juu juu tu.

Ballali apewe kinga
M. M. Mwanakijiji


KATIKA mapambano dhidi ya ufisadi ambayo ndiyo karibu yanaanza nchini, awali hatukuyatafuta bali yametutafuta sisi, yale ambayo hatukuyafuata, bali yametufuata, na ambayo ushindi wake ni lazima, kuna wakati maamuzi magumu lazima yachukuliwe.

Maamuzi magumu ambayo ni ya lazima, ya msingi na ambayo yatawezesha kushinda vita nzima badala ya pambano moja moja.

Mojawapo ya maamuzi ambayo napendekeza kwa watawala wetu wachukue ni uamuzi ambao kwa kuuangalia haraka haraka au kwa kuangalia kichwa cha habari tu, unaweza kushtua watu, ni wa kumpatia kinga ya kisheria dhidi ya mashitaka, Daudi Ballali, aliyekuwa gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na sasa akiwa uhamishoni kwa kujitakia nchini Marekani, ili arudi na kuwa shahidi wa kwanza dhidi ya waliotuibia huko BoT.

Mpendwa msomaji, leo nitaandika vitu vigumu kidogo lakini ukinivumilia na ukiniamini kwa mara nyingine utaona ni kwa nini wazo la kumpa kinga Ballali si tu kwamba ni zuri, bali pia ni la muhimu.

Linapaswa wazo hilo kuzingatiwa hasa kama kweli tunataka kuvunja mtandao wa uhalifu wa watu wenye tai katika serikali yetu na watendaji wa ngazi mbalimbali, hususan kwenye jungu la BoT.

Kama wengi mnavyojua, mpaka sasa hakuna ‘fisadi mkubwa' ambaye ameibuka katika nchi yetu na ambaye jina lake limetangaa ndani na nje kama la Ballali, anayeaminika kuhusika kwa upotevu wa sh bilioni 133, kutoka akaunti moja (ukiondoa akaunti nyingine ambazo hazijaangaliwa bado).

Kwa wiki kadhaa sasa tangu utenguzi wa Ballali, Rais Kikwete, misumari ya tuhuma za ufisadi imeendelea kugongomewa kwenye ngozi ya Ballali na kuwambwa kwenye miti na kila anayeweza.

Si viongozi wa upinzani tu, bali pia baadhi ya viongozi wa serikalini ambao wanamnyoshea Ballali kidole cha ufisadi. Imefikia mahali kwamba wananchi wenye hasira wamemjua ‘mbaya' wao na wanaanza kujigawia mashamba ya gavana huyo mwenye jina lililochafuka.

Mimi kama ninyi, nimefuatilia kwa karibu pande zote mbili na nimebahatika kuzungumza na watu wachache wanaojua nini kinachoendelea upande wa nyumbani na upande wa huku aliko Ballali. Jambo moja ambalo dhahiri ni jaribio la kitoto la kumrundikia Ballali ufisadi wote na hivyo kufanya iwe vigumu kwake, si tu kujitokeza hadharani bali pia kurudi nyumbani, kwani sasa anaweza kabisa kudai ‘hofu ya mateso ya kisiasa' na hivyo akakimbilia uhamishoni!

Ballali (kama alivyo mwanadamu yeyote yule), atahisi kuwa usalama wake na wa mali zake vipo hatarini (kama tulivyoona) sheria za Marekani zinamruhusu kuomba ukimbizi na kwa vile Tanzania haina mkataba wa kubadilishana washitakiwa na Marekani, basi ndio itakuwa imempa sababu ya kutorudi kabisa nyumbani na mniamini, sheria za Marekani zitamkinga zaidi kuliko kumfutia viza yake.

Ni baada ya kuangalia mambo haya kwa kina na maana yake katika mapambano haya dhidi ya ufisadi nimejitolea kutoa pendekezo ambalo naamini si tu litasaidia Ballali kurudi nyumbani, lakini pia litasaidia katika kuwatambua na kuwanasa mafisadi wengine nyuma ya pazia ambao kutorudi kwa Ballali ni furaha yao na hasa kama atarudi akiwa mshtakiwa pekee wa ngazi za juu.

Hivyo, ninaamini kuna sababu ya serikali yetu kupitia Mwanasheria Mkuu na vyombo vingine kumpatia kinga ya kisheria ili Ballali arudi na kuwa shahidi muhimu katika kuwaumbua mafisadi wote waliochota fedha zetu BoT.

Kuna kinga kubwa za aina mbili ambazo Ballali anaweza kupatiwa, kuna ile kinga ya jumla, kwamba chochote atakachosema mbele ya mahakama (au chombo kitakachochunguza suala hili) hakitatumiwa kama ushahidi dhidi yake katika mashitaka yoyote yale ya kihalifu dhidi yake.

Hii ina maana kama Ballali atasema ‘waziri fulani alinijia na kuniambia tufanye hivi…ushahidi huu hapa' basi mahakama inaweza kumuangalia waziri huyo bila kutumia maneno ya Ballali kama ushahidi wa kujifunga mwenyewe.

Kinga ya pili ni ile ya matumizi, ambapo Ballali kama shahidi atapewa kinga ya mashitaka kwa kadiri ya kile anachosema. Ni kweli na haitatumika dhidi yake mahakamani.

Hata hivyo katika kinga hii, endapo sehemu ya ushahidi wake utathibitika kuwa uongo (perjury), basi yale aliyoyasema yanaweza kutumika dhidi yake.

Wataalamu wanaita aina hizi za kinga kama kinga kamili (full immunity) na ile nyingine kama kinga ya sehemu (partial immunity). Nitawaacha wanasheria wachambue aina nyingine za kinga ambazo zinatokana na ofisi za watu (kama rais, mawaziri, mabalozi), lakini hapa nazungumzia zile zinazohusiana na uendeshaji wa mashitaka dhidi ya watuhumiwa wa uhalifu.

Lengo la kumpatia kinga Ballali ni kumfanya awe huru kurudi nyumbani, kutoa ushahidi wote alionao kuhusu mafisadi wote waliochota fedha zetu bila haya, pasipo yeye mwenyewe kuwa na shaka ya kuishia Keko au Maweni.

Yaani kuhakikisha kuwa kile atakachosema Ballali hakitatumiwa dhidi yake katika mashitaka ya kihalifu.

Kwa kufanya hivyo, si tu tunaweza kuwaangalia kina Basil Mramba, bali pia Zakhia Meghji, Gray Mgonja, mawaziri wengine, kina Jeetu Patel, wafanyabiashara na wahusika wengine na wale wote ambao walihusika na ufujaji mkubwa wa fedha za wakesha macho wa Tanzania kupita BoT.

Hata hivyo kuna sababu nyingine kubwa zaidi za kwanini Ballali apewe kinga. Ya kwanza ni kuwa katika sakata hili la ubadhirifu katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kama kuna mtu anayejua nini kilifanyika na kwanini kilifanyika ni Ballali.

Kwa mujibu wa Sheria ya Benki ya 2006 Ibara ya 13, kifungu cha 3(c) Gavana anaweza yeye peke yake au na maofisa wengine wa benki kutia sahihi nyaraka na mikataba mbalimbali kwa niaba ya Benki Kuu.

Gavana pekee ndiye ambaye ana uwezo huo na hivyo, kuna mengi ambayo ameyaona kwa macho yake na kuyashuhudia katika miaka karibu minane aliyotumikia BoT.

Kama hilo hapo juu ni kweli, basi kumrundikia tuhuma na kutaka kwa haraka awe mtuhumiwa mkubwa na pekee na hivyo kuwezekana kabisa kuharakisha kifungo chake si tu kutamzuia kuelezea ukweli wote na kutoa ushahidi, hasa ukizingatia asili ya tuhuma dhidi yake.

Naamini ni kinga tu, itakayomwezesha Ballali kusimama mbele ya wadai wake na kueleza ‘ukweli mtupu' ili haki iweze kutendeka.

Sababu ya pili inatokana na hiyo ya hapo juu, kwenye akaunti ya EPA ni makampuni 22 yanayotuhumiwa kuchota fedha zetu kama mtu anavyochota mchele kwa pishi.

Hata hivyo katika sakata zima la BoT ndani ya utumishi wa Ballali na akaunti nyingine zote, kuna kampuni zaidi ya themanini ambazo zimefanya vivyo hivyo na wanajulikana ni kina nani hao.

Hivyo, kumpa kinga si tu kwa ajili ya EPA, bali pia kumpa nafasi ya kufunua ni kina nani walihusika na Mwananchi Gold, Deep Green, Meremeta, Tangold na mengine mengi.

Kuna mengine sitashangaa ambayo sisi hatuyajui lakini tukimpa kinga ya kisheria tunaweza kuyajua hata yale yaliyofanywa sirini, chini ya uvungu au darini.

Si tu kujua ni kina nani walihusika, bali pia kujua ni kwa jinsi gani walihusika hadi wakaweza kufanya ufisadi huo. Endapo Ballali atapewa kinga ya mashitaka, lazima iwe kwa masharti yatakayohakikisha kuwa genge la mafisadi nchini linaumbuliwa na kufumuliwa kutoka ngazi zote.

Mtu pekee anayeweza kufanya hivyo kwa mamlaka ni Ballali. Pia kuna sababu nyingine. Anajua fedha zetu zimewekwa wapi na kina nani wameziweka fedha hizo.

Akiwa kama ofisa wa BoT, Gavana Ballali baada ya kupewa kinga anaweza kutueleza fedha zetu karibu dola bilioni moja (sh trilioni moja) zilizopotea BoT zimewekwa wapi.

Hili ni muhimu, kwa sababu hakuna furaha ya kusema fedha zimepotea, kwa sababu pesa huwa hazipotei, zinatoweka na kutumika mahali fulani.

Sh trilioni moja kupotea ndani ya miaka kama minane si mchezo. Katika mojawapo ya nyaraka za Benki ya Dunia (WB) na zile za Shirika la Fedha Duniani (IMF), na zile za taasisi mbalimbali za kiutafiti, inaonyeshwa kuwa ndani ya miaka 30 iliyopita Tanzania imepokea misaada ya karibu dola bilioni mbili.

Kama tukichukulia maneno ya Rais Kikwete kwa mabalozi hivi karibuni kuwa fedha zilizopotea BoT si za wafadhili, basi hatuna budi kukuna vichwa, kwani zilizopotea ni fedha zetu wenyewe.

Na kama alimaanisha kuwa fedha zote zilizopotea BoT si za wafadhili (zile za EPA) kama nilivyoelewa, ina maana zilizochotwa pale ni fedha zetu Watanzania.

Kwa maneno mengine, kama misaada tuliyopokea ni sh bilioni mbili na watawala wetu wakatafuna sh bilioni moja ya fedha zetu wenyewe, ina maana kama wasingetafuna kama mchwa fedha zetu, tusingehitaji msaada wa dola bilioni moja na kuwa omba omba!

Kwa maneno mengine, kama wasingetumbua pesa yetu leo hii kina Bernad Membe, wasingetutambia kuwa rais amekwenda kuomba dola milioni 698, kwani kwa kweli hatukuzihitaji!

Hivyo, kujua fedha zetu zilipo ni jambo muhimu ili si tu tuweze kuzirejesha, bali pia kuhakikisha kama zimebadilishwa na kuwa mali isiyohamishika, itaifishwe kwa manufaa ya umma na fedha zetu zirudi.

Ballali anaweza kufanya hivyo, kichocheo kikubwa itakuwa ni kinga ya kisheria ili si tu atutajie kina nani wamekwapua fedha zetu, bali pia wamezificha wapi, kwani naamini anajua!

Hata hivyo kuna sababu nyingine ya kumpa kinga. Kwa vile baadhi ya watu wanaotajwa kuhusika na kashfa hizi ni watu wakubwa na wengine si tu wana nguvu za fedha, bali wanazo nguvu za madaraka, kuna haja ya kulinda usalama wa Ballali na mali zake.

Tukio la hivi karibuni ambapo wananchi walitaka kujipongeza kwa kugawana mashamba ya Ballali, ni ishara ya kile ambacho kinaweza kumkuta pindi arudipo nyumbani.

Bila kuhakikishiwa usalama wake, wa familia na mali zake itakuwa ni ndoto za Alinacha kudhania Ballali atateremka Kipawa na kukodi ‘teksi' kwenda nyumbani kwake!

Kadiri watu walivyo na shauku naye (kihalali au kimakosa), asije kurudi nyumbani akakutana na wajanja ambao ni wataalamu, wakamnyamazisha milele!

Hivyo kuna haja katika kinga hiyo kumhakikishia usalama wake katika muda wote ambao kesi itakuwa ikiendelea na bila ya shaka si yeye tu, bali pia na mashahidi wengine ambao watakuwa tayari kushuhudia katika kesi hiyo.

Hata hivyo, yeye ana umuhimu wa pekee katika kufunua ufisadi katika nchi yetu, na kutompatia kinga itakuwa ni kumtisha na hivyo kumfanya asiwe shahidi mzuri.

Jambo la kutoa kinga kwa wanaodaiwa kufanya uhalifu si geni duniani, na limetumika katika nchi mbalimbali hasa walipotaka kutokomeza uhalifu mkubwa na magenge ya kihalifu duniani.

Wamarekani walitumia mtindo huo katika kuvunja genge la mafia pale ambapo waliwakatama Mafioso kadhaa na kuwapatia kinga ili wawataje wenzao na jinsi wanavyofanya mambo yao bila ya wao wenyewe kushitakiwa.

Mfano wa hivi karibuni ni pale Bunge la Marekani lilipompa kinga bosi wa Mafia kwenye Jiji la Boston, Francis Salemme, ambaye alikuwa ametoweka na kwenda kusikojulikana, na alikuwa anajua jinsi gani baadhi ya maofisa wa FBI walikuwa wanashirikiana na kundi la Mafia.

Si yeye tu, bali pia kaka yake ambaye alikuwa Rais wa Chuo Kikuu cha Massachusetts, William Bulger, ili alieleze bunge hilo aliko kaka yake bila yeye kushitakiwa.

Kutokana na ushirikiano wake na serikali, mahakama ilimfunga kifungo kifupi hasa baada ya Selemme kuwezesha kushitakiwa na kutiwa hatiani kwa ofisa wa FBI, John J. Connoly.

Hapo baadaye Selemme alijikuta kwenye matatizo mengine ya kisheria yasiyohusiana na kinga yake.

Katika mojawapo ya kesi zinazojulikana sana kutoka Marekani ni lile sakata la Monica Lewinsky na uchunguzi wa Mwendesha Mashitaka, Ken Starr.

Julai 28, mwaka 1998, Ken Starr alikubaliana na timu ya mawikili wa Monica Lewinsky, jambo lililompatia kinga binti huyo ili aseme ukweli kuhusu uhusiano wake na aliyekuwa Rais wa Marekani, Bill Clinton.

Makubalianao yaliyompa kinga Monica yalisaidia pia kumpa kinga mama yake na upande mwingine dada Linda Tripp, na alipewa kinga ya aina fulani ili aseme anayoyajua pasipo hofu ya kushitakiwa.

Kimsingi, hiyo ndiyo hoja yangu, kama tunataka kufahamu nini kilifanyika BoT, nani alifanya nini na kwa kiasi gani basi hatuna budi kulipa gharama hiyo kwa kumpa kinga samaki mmoja ili tutengeneze nyavu ya kuwanasa wengi wakubwa.

Kinga hii ni tishio na sidhani kama serikali itakuwa tayari kufanya hivyo, kwani si tu itafungua uwezekano wa mambo makubwa, bali watakosa mtu wa kumbebesha mzigo wote wa lawama.

Nimezungumza na mmoja wa wanasheria na hakumbuki kama kuna historia ya kutoa kinga katika Tanzania, hasa katika kesi kubwa kama hizi.

Natumaini kama hatujafanya hivyo, naamini hii itakuwa ni nafasi ya kwanza kufanya hivyo kama kweli tunataka ‘watajane'.

Sheria ya kufanya hivyo ipo. Katika mojawapo ya magazeti yaliyotoka juzi yalielezea ni jinsi gani Mwanasheria Mkuu anaangalia ni sheria gani zitamwongoza katika suala hili.

Ametaja sheria tatu kwa kadiri ya gazeti hilo, ile ya Mapato yanayotokana na Uhalifu ya 1991, ile ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya 2007 na ya Usafirishaji Fedha Kinyume cha Sheria ya 2006.

Hata hivyo kwa heshima nipendekeze sheria yetu ya Kuhujumu Uchumi ya 1984 ambayo inazungumzia kuhusu usalama na kinga ya washitakiwa na mashahidi.

Ibara ya 52, 53 na 54 zinaweza na zinapaswa kutumika. Ibara ya 53 kimsingi ndiyo inayoweza kutumika (na mabadiliko yake kama yapo) ili kuweza kumpatia kinga Ballali na hivyo kuwezesha si tu kurudi kwake nyumbani bali pia kuweza kusimama kama shahidi dhidi ya watuhumiwa wa ubadhirifu.

Hata hivyo, swali moja ambalo naogopa jibu lake ni uwezo wa vyombo vyetu vya sheria kuchunguza, kuwatia mbaroni na kuwafikisha mahakamani wahusika, ukizingatia unyeti wa suala hili.

Ukiondoa zile kesi za uhaini za miaka ya 1960 na 1980 yawezekana kabisa kuwa sakata hili litatuletea kesi katika historia ya Jamhuri yetu, kesi ambayo itatufanya tuamue kweli tunataka kwenda wapi kama taifa na jinsi ya kuwasimamia watawala wetu.

Macho yetu yanashuhudia tukio la kihistoria ambalo naomba kwa Mungu vizazi vijavyo visishuhudie tena.

Ni kwa misingi hiyo, kabla sijamaliza nipendekeze kuwa serikali itoe mwaliko rasmi kwa vyombo vyenye uzoefu wa mambo haya kama FBI na New Scotland Yard ili kusaidia katika uchunguzi huru badala ya kuwaachia polisi wetu na waendesha mashitaka kutoka Jumuiya ya Madola waweze kuendesha kesi hii ili iwe huru kabisa.

Kwa kufanya hivyo, si tu haki itatafutwa bali pia itaonekana. Sasa hivi licha ya maneno mazuri ya ahadi, baadhi ya watu nikiwemo hatuamini kuwa serikali ina nia ya kweli ya kuingia ndani na kwenye kina cha kashfa hii kubwa na iliyoumiza mioyo ya watu wengi.

Hii inachangiwa pia na usiri ambao unaendelea kuficha ripoti ya uchunguzi na pia kujaribu kutumia watu waliotakiwa kuwa wasimamizi wa sheria kufanya uchunguzi huo!

Haiingii akilini kuwa Mwanasheria Mkuu ambaye ndiye mshauri mkuu wa serikali katika masuala ya sheria aliridhia kuletwa kwa sheria ya BoT ya 2006, na kwa muda wote wa miaka minane hakuwa jasiri kufanya uchunguzi wake mwenyewe kuhusu uvunjwaji wa sheria hadi pale Waziri Meghji alipotoa ombi na uchunguzi kufanywa na chombo cha nje.

Inasikitisha kuwa Jeshi la Polisi linashirikishwa kwenye uchunguzi huu ambao madai yake yamekuwepo kwa miaka karibu kumi sasa.

Kwa maneno mengine, bila rais kuwatuma kufanya uchunguzi huo wasingeangalia ufisadi BoT na wao kama Takukuru wanasubiri maagizo kutoka juu ndipo waanze kazi zao, na kwa vile hawako huru watafanya uchunguzi na badala ya kuuweka hadharani watarudisha Ikulu ambako rais ataamua kuunda tume nyingine kuchunguza uchunguzi uliochunguzwa na tume ya uchunguzi!

Natoa hoja, tumpatie kinga Ballali kwa misingi niliyoitaja hapo juu na zaidi ili si tu aweze kurudi na kusimama kizimbani bali kutuelekeza wengine walioingia bandani mwetu na kuchukua kuku, kuwachinja na kuwakaanga humo humo bandani, huku wakirusha mifupa na manyoya nje!

Mapambano dhidi ya ufisadi yana uamuzi mgumu, huu ni mmojawapo, je, serikali ipo tayari kumpa kinga Ballali?

Kwa habari, nyaraka na taarifa mbalimbali wakati wote wa siku tembelea: http://www.klhnews.com
Niandikie: mwanakijiji@klhnews.com
 
Hii ya kinga haingii akilini maana ni sawa na kumwachia fisi akuangalizie mishikaki yako halafu utegemee kuikuta ukirudi...
 
inabidi usome kidogo nilichosema na kuona kama mfano wako unaendana nao.
 
Nitasoma na kuchangia hoja ya Mzee Mkjj later. Ila from the outset, Nimeipenda kwa sababu inaangalia ufumbuzi wa muda mrefu na sio hukumu za haraka zenye mafanikio ya kisiasa.
 
mwanakijiji.

Very well written piece,you tried to lay things out so skillfuly...looking forwad to the next dose.Bring it on kamanda ingawaje JF didnt fall in love with your idea!
 
Mzee ES, sijuia kama unafahamu sheria zetu au la. Tunayo sheria ya kinga. Nilimuuliza Prof. Shivji kabla ya kuandika makala hii na hakukumbuka kama kuna wakati wowote ambapo sheria hiyo imewahi kutumika.

Labda niweke hoja yangu hapa ili watu wasome na kuelewa nilichosema badala ya kuchukua maneno juu juu tu.

Ballali apewe kinga
M. M. Mwanakijiji


Ballali (kama alivyo mwanadamu yeyote yule), atahisi kuwa usalama wake na wa mali zake vipo hatarini (kama tulivyoona) sheria za Marekani zinamruhusu kuomba ukimbizi na kwa vile Tanzania haina mkataba wa kubadilishana washitakiwa na Marekani, basi ndio itakuwa imempa sababu ya kutorudi kabisa nyumbani na mniamini, sheria za Marekani zitamkinga zaidi kuliko kumfutia viza yake.
Naomba nirekebishe hapo kidogo, Tanzania na USA wana extradition treaty iliyokuwa signed mwaka 1965. Hii ndio ilitumika kumextradict yule mpemba aliyeshtakiwa kwa kulipua ubalozi
Vile vile Tanzania wanaweza kutumia sheria ya Mutual Assistance in Criminal Matters kumleta Balali kama ana uraia wa nchi ingine. Hii ndio ilitumika kumleta Sailesh Vithlani (Mzee wa Radar)kuja kutoa ushahidi under oath,Mahakama ya Kisutu


Kuna kinga kubwa za aina mbili ambazo Ballali anaweza kupatiwa, kuna ile kinga ya jumla, kwamba chochote atakachosema mbele ya mahakama (au chombo kitakachochunguza suala hili) hakitatumiwa kama ushahidi dhidi yake katika mashitaka yoyote yale ya kihalifu dhidi yake.

Naomba niziilezee vizuri hizi kinga kwa kiingereza nadhani zitaeleweka vizuri zaidi
Prosecutorial immunity (or immunity from prosecution) occurs when a prosecutor grants immunity, usually to a witness in exchange for testimony or production of other evidence. It is immunity because the prosecutor essentially agrees to never prosecute the crime that the witness might have committed in exchange for said evidence.

This form of immunity generally comes in two forms. Blanket immunity (sometimes known as "transactional immunity") completely protects the witness from future prosecution for crimes related to his or her testimony.

Use immunity only prevents the prosecution from using the witness' own testimony against them. However, should the prosecutor acquire evidence substantiating the supposed crime -- independent of the witness's testimony -- the witness may then be prosecuted for same

Source:http://www.answers.com/topic/prosecutorial-immunity

Hii ina maana kama Ballali atasema ‘waziri fulani alinijia na kuniambia tufanye hivi…ushahidi huu hapa' basi mahakama inaweza kumuangalia waziri huyo bila kutumia maneno ya Ballali kama ushahidi wa kujifunga mwenyewe.

Kinga ya pili ni ile ya matumizi, ambapo Ballali kama shahidi atapewa kinga ya mashitaka kwa kadiri ya kile anachosema. Ni kweli na haitatumika dhidi yake mahakamani.

Hata hivyo katika kinga hii, endapo sehemu ya ushahidi wake utathibitika kuwa uongo (perjury), basi yale aliyoyasema yanaweza kutumika dhidi yake.

Wataalamu wanaita aina hizi za kinga kama kinga kamili (full immunity) na ile nyingine kama kinga ya sehemu (partial immunity). Nitawaacha wanasheria wachambue aina nyingine za kinga ambazo zinatokana na ofisi za watu (kama rais, mawaziri, mabalozi), lakini hapa nazungumzia zile zinazohusiana na uendeshaji wa mashitaka dhidi ya watuhumiwa wa uhalifu.

Lengo la kumpatia kinga Ballali ni kumfanya awe huru kurudi nyumbani, kutoa ushahidi wote alionao kuhusu mafisadi wote waliochota fedha zetu bila haya, pasipo yeye mwenyewe kuwa na shaka ya kuishia Keko au Maweni.

Yaani kuhakikisha kuwa kile atakachosema Ballali hakitatumiwa dhidi yake katika mashitaka ya kihalifu.

Hata hivyo kuna sababu nyingine kubwa zaidi za kwanini Ballali apewe kinga. Ya kwanza ni kuwa katika sakata hili la ubadhirifu katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kama kuna mtu anayejua nini kilifanyika na kwanini kilifanyika ni Ballali.

Kwa mujibu wa Sheria ya Benki ya 2006 Ibara ya 13, kifungu cha 3(c) Gavana anaweza yeye peke yake au na maofisa wengine wa benki kutia sahihi nyaraka na mikataba mbalimbali kwa niaba ya Benki Kuu.

Gavana pekee ndiye ambaye ana uwezo huo na hivyo, kuna mengi ambayo ameyaona kwa macho yake na kuyashuhudia katika miaka karibu minane aliyotumikia BoT.

Kama hilo hapo juu ni kweli, basi kumrundikia tuhuma na kutaka kwa haraka awe mtuhumiwa mkubwa na pekee na hivyo kuwezekana kabisa kuharakisha kifungo chake si tu kutamzuia kuelezea ukweli wote na kutoa ushahidi, hasa ukizingatia asili ya tuhuma dhidi yake.

Naamini ni kinga tu, itakayomwezesha Ballali kusimama mbele ya wadai wake na kueleza ‘ukweli mtupu' ili haki iweze kutendeka.

Sababu ya pili inatokana na hiyo ya hapo juu, kwenye akaunti ya EPA ni makampuni 22 yanayotuhumiwa kuchota fedha zetu kama mtu anavyochota mchele kwa pishi.

Hata hivyo katika sakata zima la BoT ndani ya utumishi wa Ballali na akaunti nyingine zote, kuna kampuni zaidi ya themanini ambazo zimefanya vivyo hivyo na wanajulikana ni kina nani hao.

Hivyo, kumpa kinga si tu kwa ajili ya EPA, bali pia kumpa nafasi ya kufunua ni kina nani walihusika na Mwananchi Gold, Deep Green, Meremeta, Tangold na mengine mengi.

Kuna mengine sitashangaa ambayo sisi hatuyajui lakini tukimpa kinga ya kisheria tunaweza kuyajua hata yale yaliyofanywa sirini, chini ya uvungu au darini.

Si tu kujua ni kina nani walihusika, bali pia kujua ni kwa jinsi gani walihusika hadi wakaweza kufanya ufisadi huo. Endapo Ballali atapewa kinga ya mashitaka, lazima iwe kwa masharti yatakayohakikisha kuwa genge la mafisadi nchini linaumbuliwa na kufumuliwa kutoka ngazi zote.

Mtu pekee anayeweza kufanya hivyo kwa mamlaka ni Ballali. Pia kuna sababu nyingine. Anajua fedha zetu zimewekwa wapi na kina nani wameziweka fedha hizo.


MM,

Mimi nakubaliana na mtizamo wako, kuwa Balali ni material witness kwenye BOT saga. Na his testimony is very important not only for EPA account but all other misconducts mentioned and non mentioned(Guarantee Scheme under the Domestic Market ambapo over 75 % of the Govt Guarantee were given to 2 Sugar Plants(One in Morogoro and Kagera belonging to the same shareholders who believed to have strong relationship with former President).

Nadhani mpaka sasa sisi tumefungwa bao na mafisadi maana wameweza kudivert attention to one personal whom we are condeming. Kupewa immunity(specifically use/partial) kwa Balali haina maana kuwa hatoshtakiwa kwa makosa yake kama ushahidi upo wa kumshtaki apart fom his testimony.
 
Mwanakijiji,

Unataka Ballali atusaidie nini ambacho hatukijui? Au JK hakijui?

Tatizo la TZ sio kutokuwajua waliotuibia, tatizo ni kupata kigugumizi inapofika wakati wa kuwachukulia hatua.

Walioiba TZ hawakuiba kwa ujanja mkubwa, ukifuata pesa, unakuta zinakuongoza mpaka mwisho wake lakini JK na kundi lake hawataki na ndio maana hata hawataki kutoa report ya E&Y maana hata hao jamaa inaelekea wameweza kugundua mengi kwa muda mfupi mno.

Kumpa kinga Ballali ni kupoteza muda tu maana kila atakachokisema tayari tuna habari nacho ila tu hatutaki kuwakamata wahusika maana ni ndugu zetu, marafiki zetu na sponsors wetu.

Tatizo la TZ ni uwajibikaji na wala sio kukosa information.
 
Mwanakijiji mimi pia ninashida aliyonayo Koba. Frankly simwoni hapa nchini katika serikali hii ya kisanii ya Jk wa kufanya hayo yote unayopropose kwani in my opinion serikali nzima inahusika ktk hili ndio maana speed ya kulishughulikia inakuwa ya snail. Kwa audit report kama ile hakukuwa na sbb ya JK kuunda tume na kuipa 6 months-ni matusi yalioje kwa watz. Angekuwa hahusiki ilikuwa ni kuchukua hatua right away. Infact hata hiyo audit ilicheleweshwa purposely kupunguza findings otherwise kingekuwa kiama, take it from me.

Kifupi ni kwamba hili nalo limepita,inauma sana sana lakini huo ndio ukweli wenyewe. Na wa kulaumiwa ni sisi wenyewe watanzania kwa ukondoo wetu wa kiwendawazimu. Hv inakuwaje rahisi kwa wanafunzi wa UDSM kuandamana kumlaani Kibaki kwa wizi wa kura huku wakimwacha Mgonja, Meghji na Mramba wakiendelea kupeta? Kwanini wasiandamane pia katika hili au si muhimu kwao na wao ndio wahanga kila siku wa mikopo? What's the problem hapa jamani me sielewi kbs nahisi kuchanganyikiwa kwa kweli.
 
Mimi nafikiri hilo suala la kumpa kinga Balali n la kisheria sana. Wataalum wa pinal code watueleze inawezekana. Maana asije akapewa kinga na huo msaada asiutoe, hapo tutakuwa tumepigwa bao la DOBA. Yaani la aibu
 
Mzee Mwanakijiji ee sasa hiyo kinga unayosema apewe huyu mtuhumiwa wetu apewe na nani? Sirikali yetu? Kama ndio hivyo basi hamna tofauti na kumwachia mbwamwitu kondoo wako akuchungie, matokeo unayajua...
 
Good ideas Mwanakijiji. Lakini binafsi sidhani kwamba Balali anaogopa kurudi kwa sababu ya kushtakiwa. Nafikiri tatizo kubwa kuliko yote ni uhai wake ambao kinga yake haiwezi kupatikana kwa kupewa kinga ya mashataka. Na siamini kwamba tishio la uhai wa Balali linatoka kwa hao wananchi waliovamia mashamba. Tishio halisi la uhai wa Balali linatoka kwa hao mafisadi wenzake ambao sasa wanaonekana kumtoa kafara ili aonekane ni yeye na sio wao. Hawa ndio ambao wangependa kumuona Balali asifungue mdomo wake kama wana uwezo ambao nafikiri wanao!

More importantly, nashtuka kidogo kuona kwamba na wewe inaonekana bado unaamini kwamba suluhisho la muda mrefu la ufisadi litapatika kwa Balali kuwataja wenzake. Kama alivyouliza Mtanzania, ni nani hao ambao hatujawajua hapa tulipo? Hivi ni jina gani sasa likitajwa tutashtuka? Mimi naamini kabisa tena kwa dhati kabisa kuwa madamu CCM inaendelea kubaki madarakani ufisadi hauwezi kwisha, utakuwa unabadili maumbo tu: Richomond, Kiwira, BoT,etc. Na kila umbo jipya litakapojitokeza litafanya tusahau umbo la mwanzo. Kwa mfano, sasa inaonekana akina Richmond ni cha mtoto na Karamag na Lowasa sasa watakuwa wanachekelea tu sasa hivi maana haya matukio ya karibuni yanawafanya wananchi sasa wajue kumbe sio wao tu, wapo na wengine. Kosa kubwa tunalofanya ni kufikiri kwamba haya matatizo yanaweza kutatuliwa katika mfumo tulio nao. Hili haliwezekani kwa sababu ni mfumo huohuo ndio uliyoyatengeneza hayo matatizo tena sio kwa bahati mbaya bali "makusudically" kama njia za kufanya huo mfumo ubaki hapo ulipo. Hii ndio halisi ambayo inauma sana kwa sababu hakuna njia ya mkato ya kuibadilisha!

This is to say, the moment you dismantle the fraudulent network in our country you will have effectively dismantled the existence of the CCM hegemony. Now, are we ready for that, and are they ready?
 
Majina ambayo Balali atataja ni Mkapa, Lowassa, Karamagi, Kapuya, Sumaye etc.....now what's new?
 
Majina ambayo Balali atataja ni Mkapa, Lowassa, Karamagi, Kapuya, Sumaye etc.....now what's new?

Yes, hakuna jipya, lakini kumbuka kuwataja kwake na kutoa vielelzo kutatupa nguvu zaidi ya kuwawajibisha, hata kama si leo lakini ipo siku yaja.. baada ya kuwangusha mafisadi wote na Chama chao cha kifisadi.

So, vyovyote vile, Balali kuwataja washirika wake ni muhimu mno, hata kama si kwa short term.. but with time hata kama balali hatakuwepo au hata sisi hatutakuwepo.. hata hao wajukuu za mafisadi will pay!
 
Majina ambayo Balali atataja ni Mkapa, Lowassa, Karamagi, Kapuya, Sumaye etc.....now what's new?

What's new? It's going to be OFFICIAL (legally) these cowards could be formally brought to justice. Ballali will have evidence which will part from what others are doing (which in court's eyes is just hearsay).

Mzee Mwanakijiji,

Thanks a bunch for such a clear cut explanation of your point. I agree with you 100% about the importance of the URT offering Ballali some sort of immunity, in addition to security. As one of the mdau said, Ballali is fearing harm from the big time fisadist or some members of Fisadi Mkubwa.

I know our evaluations and positions on this issue will reach the decision maker and I am really eager to hear his take on this. Once again, thanks for providing a permanent solution rather than a "bandaid" solution.
 
Yes, hakuna jipya, lakini kumbuka kuwataja kwake na kutoa vielelzo kutatupa nguvu zaidi ya kuwawajibisha, hata kama si leo lakini ipo siku yaja.. baada ya kuwangusha mafisadi wote na Chama chao cha kifisadi.

So, vyovyote vile, Balali kuwataja washirika wake ni muhimu mno, hata kama si kwa short term.. but with time hata kama balali hatakuwepo au hata sisi hatutakuwepo.. hata hao wajukuu za mafisadi will pay!

Ballali kuwataja washirika wake hakuna nguvu yeyote. Nguvu iko kwenye mtililiko wa pesa na watu waliozichukua, kitu ambacho tayari tunajua.

Vita dhidi ya mafia inakuwa tofauti mno, kunakuwa na unknowns ambazo serikali huhitaji kuzitengua hasa kwenye wahusika wakuu na jinsi wanavyo operate, lakini kwenye hili kila kitu kiko wazi, tunahitaji ushahidi gani tena wa Ballali?

Hivi tunahitaji ushahidi upi zaidi kujua Mkapa ni fisadi? Au kujua kwamba RA anahusika.

Tusome kwanza report ya E&Y na kama bado kuna vitu vina utata labda ndio
tufikirie mambo mengine lakini mpaka sasa sioni kabisa hata sababu za kufikiria kinga ya Ballali.
 
Mwanakijiji,

Unataka Ballali atusaidie nini ambacho hatukijui? Au JK hakijui?

Mtanzania, kama uliiona movie ile ya "Training Day" utakumbuka mahali fulani Denzel anamuambia yule rookie kuwa "it not what they know, it is what they can prove".

Baadhi ya watu hapa miongoni mwao mimi, tunahisi tunawajua wahusika wakubwa wa ufisadi. Majina ya Mramba, Mkapa, Mgonja, Patel n.k yako haraka midomoni mwetu tunapozungumzia suala la ufisadi na ubadhirifu wa EPA.

Sasa kwenye mahakama ya sheria ambapo kanuni za ushahidi zinahitajika, haitoshi peke yake kumtuhumu mtu licha ya kila dalili kuonesha anahusika (OJ case would be a classic example).

Ni nini tunachoweza kuleta mahakamani, kikaangaliwa kisheria na kikaonekana ni kweli pasipo chembe ya shaka? Wakati waendesha mashtaka walipoingiza ushahidi wa gloves kwenye kesi ya OJ walidhani wamepata ushahidi usiopingika.

J. Cochran alivunja kile kilichooneshwa kwa kumpa OJ gloves azijaribu, hazikumfit na ndipo ule msemo maarufu wa "if it doesn't fit, you must acquit". Na hilo lilikuwa goli la kihistoria!

Sasa tuwapeleke Mkapa, Mramba, Mgonja mahakamani kwa ushahidi gani? Ushahidi ambao siyo wa mazingira bali wa kihalifu ambao mtu akioneshwa anasema "those gloves fit, so we can't acquit"!

Tatizo la TZ sio kutokuwajua waliotuibia, tatizo ni kupata kigugumizi inapofika wakati wa kuwachukulia hatua.

Wakati mwingine tunadhani fulani ndiye katuibia kwa sababu alikuwa karibio na tukio. Hivi jana/juzi kijana mmoja ameachiliwa na mahakama ya Marekani baada ya kutumikia miaka tisa ya kifungo cha maisha kwa mauaji ya mwanadada mmoja.

Ushahidi uliomtia hatiani ni kuwa alikutwa karibu na mwili wa marehemu karibu na nyumba yake (huyo kijana) na wakaongeza mambo mengi hatimaye kumfunga jela.

Hata hivyo ushahidi wa kisayansi (forensics) umeonesha pasipo shaka kuwa haiwezekani kuwa huyo kijana ni muuaji wa huyo binti.

Hatutaki hilo litokee. Hatutaki tu kwa sababu fulani alifanya kazi Benki Kuu basi na yeye ni mwizi kama hatuna ushahidi wa kuonesha hivyo.

Ndugu zangu, hiyo ndiyo gharama ya utawala wa sheria. Hatuwezi kupinda sheria ili kuwapata wabaya wetu! Hatuwezi kuona kuwa sheria inatumiwa hivi kwa yule na vile kwa huyu. Kama tunaamini kuwa hakuna kiongozi yeyote aliyejuu ya sheria, hatuna budi kuamini na kukubali pia kuwa hakuna kiongozi aliye chini ya sheria. Sisi sote ni sawa mbele ya sheria!

Kama aliyeiba kuku anafikishwa mahakamani na ushahidi kutolewa wa jinsi gani aliingia bandani, kuchagua kuku wa "kizungu", na hatimaye kwenda kumkaanga huku manyoya yake yakikutwa kwenye karo la maji nje ya nyumba yake na yeye mwenyewe akikutwa ameshikilia kichwa, basi hatuna budi kuhakikisha hata wanaoiba zaidi ya kuku na wenyewe wanafuatiliwa kwa mujibu wa sheria.

Walioiba TZ hawakuiba kwa ujanja mkubwa, ukifuata pesa, unakuta zinakuongoza mpaka mwisho wake lakini JK na kundi lake hawataki na ndio maana hata hawataki kutoa report ya E&Y maana hata hao jamaa inaelekea wameweza kugundua mengi kwa muda mfupi mno.

Waliiba kwa ufundi mkubwa ndio maana leo hii tunashangazwa na jinsi walivyoiba. Ni watu wachache sana ambao wameweza kufanya uhalifu uliobobea (perfect crime). Wahalifu by the very definition of the word ni watu ambao hufanya makosa. Na mara nyingi hufanya makosa, na ni jukumu la upelelezi kutafuta makosa hayo kuyaonesha.


Kumpa kinga Ballali ni kupoteza muda tu maana kila atakachokisema tayari tuna habari nacho ila tu hatutaki kuwakamata wahusika maana ni ndugu zetu, marafiki zetu na sponsors wetu.

That is such a bold statement kuwa "kila atakachosema", "Tunacho habari zake". Mwenzetu una uhakika kuwa "Kila" atakachozungumzia tunacho habari zake maana nadhani wewe mwenyewe unaweza kuwa shahidi mzuri sana kwa sababu binafsi sijui Balali anataka kusema na kwa hakika sina habari za yote atakayosema!

Tatizo la TZ ni uwajibikaji na wala sio kukosa information.

Believe, tatizo siyo uwajibikaji bali ni kukosa information za kuwafanya watu wawajibike!

Ninasoma michango yenu yote na mnanipa mawazo ya kupanua kidogo hoja kwani naweza kuona changamoto zilizowazi. Na wale ambao mmechangia kwenye podomatic pia nimesoma michango yenu yote na ninashukuru.
 
Good ideas Mwanakijiji. Lakini binafsi sidhani kwamba Balali anaogopa kurudi kwa sababu ya kushtakiwa. Nafikiri tatizo kubwa kuliko yote ni uhai wake ambao kinga yake haiwezi kupatikana kwa kupewa kinga ya mashataka. Na siamini kwamba tishio la uhai wa Balali linatoka kwa hao wananchi waliovamia mashamba. Tishio halisi la uhai wa Balali linatoka kwa hao mafisadi wenzake ambao sasa wanaonekana kumtoa kafara ili aonekane ni yeye na sio wao. Hawa ndio ambao wangependa kumuona Balali asifungue mdomo wake kama wana uwezo ambao nafikiri wanao!


Kinga ambayo nazungumzia siyo ya kisheria tu bali pia usalama wake. Sheria niliyoinukuu hapo juu iko wazi kuhusu mambo hayo yote mawili. Hata huku watu kama kina McVeigh walipewa ulinzi hadi siku wanadungwa sindano! Ni jukumu la serikali kuwalinda wahalifu au mashahidi muhimu. Mnaweza kuona jinsi Dito alivyolindwa...

More importantly, nashtuka kidogo kuona kwamba na wewe inaonekana bado unaamini kwamba suluhisho la muda mrefu la ufisadi litapatika kwa Balali kuwataja wenzake
.

Nadhani, umerahisisha mno hapo. Sijaangalia tatizo kubwa la ufisadi in general nazungumzia ule wa BoT na katika hilo nazungumzia kujua na kutambua nini kimetokea na nani wanahusika. Mtu pekee anaweza kuzungumza kwa mamlaka na ushahidi ni Balali.

Kama alivyouliza Mtanzania, ni nani hao ambao hatujawajua hapa tulipo? Hivi ni jina gani sasa likitajwa tutashtuka?

Tadhafali angalia jibu langu kwa Mtanzania kuhusu mada hiyo, it is not who we know, but who we can indict and bring evidence that can stand the scrutiny of a judicial mind!

Mimi naamini kabisa tena kwa dhati kabisa kuwa madamu CCM inaendelea kubaki madarakani ufisadi hauwezi kwisha, utakuwa unabadili maumbo tu: Richomond, Kiwira, BoT,etc. Na kila umbo jipya litakapojitokeza litafanya tusahau umbo la mwanzo. Kwa mfano, sasa inaonekana akina Richmond ni cha mtoto na Karamag na Lowasa sasa watakuwa wanachekelea tu sasa hivi maana haya matukio ya karibuni yanawafanya wananchi sasa wajue kumbe sio wao tu, wapo na wengine. Kosa kubwa tunalofanya ni kufikiri kwamba haya matatizo yanaweza kutatuliwa katika mfumo tulio nao. Hili haliwezekani kwa sababu ni mfumo huohuo ndio uliyoyatengeneza hayo matatizo tena sio kwa bahati mbaya bali "makusudically" kama njia za kufanya huo mfumo ubaki hapo ulipo. Hii ndio halisi ambayo inauma sana kwa sababu hakuna njia ya mkato ya kuibadilisha!

This is to say, the moment you dismantle the fraudulent network in our country you will have effectively dismantled the existence of the CCM hegemony. Now, are we ready for that, and are they ready?


Nitaacha siasa kwa wanasiasa kwa sasa, for me naangalia suala hili kama tishio kubwa kabisa la uhuru wetu na mafanikio ya Watanzania. Kabla hatujaanza kwenda kwingine, we need to deal with BoT once and for all, na siyo juu juu bali ndani kabisa na kuchambua hadi punje za mwisho.
 
Mwanakijiji Makala yako ni nzuri na imebeba maana kubwa.Nafikiri imefika wakati sasa,Kizazi hichi cha wasomi kujaribu kutatua matatizo kwa kung'oa mizizi.Ukweli wa mambo ni kwamba Serikali yetu inaendeshwa kwa Bla Bla,na maamuzi yenye Mitazamo ya kisiasa.Hatuwezi kupiga hatua yoyote ya maendeleo kama hatutokuwa makini kuziba mianya ya Uizi na kung'oa kabisa mizizi ya Ugonjwa huo.

Kwa kumpa Kinga ya Kisheria Dr.Balali tutajua mengi kuliko hayo ya Uizi wa EPA,Ni wazi kwamba hatokubali kwenda mwenyewe!!,Atawataja wote waliohusika na Uchotaji pesa hapo BOT.Hivi Waungwana Mmeshasahau Press Conference alofanya Balali kabla ya kuondoka!,Aligusia hawa wezi!!,Kwa vyovyote itakavyokuwa nae atakuwemo kundini hata kwa Uzembe kama sio Uizi,lakini ni Bora awaweke wazi na Wengine!!!
 
Hii inatoka katika sheria ya "Kuhujumu Uchumi" kwa kiingereza "Economic and Organized Crime Control Act - 1984"


Security of Witness 52: Where he is satisfied on reasonable grounds that there is any danger or real possibility of danger of interference with any case under this Act
through interference with or threats of harm to any witness or potential
witness, the Inspector-General of Police
Protection
of witnesses
may, on his own motion or after
consultation with the Director of Public Prosecutions, arrange for the
provision of security for the witness or potential witnesses concerned
and, if necessary, the family or families of that witness or potential
witness or witnesses,

Immunity
53.-(1) Without prejudice to the provisions of any written law
conferring a right to refuse to disclose official secrets, where in any
proceeding arising under this Act, any witness refuses to answer any
of witnesses question on the ground that the answer to it may incriminate him, or to
testify or provide other information on the ground that the information
is privileged or he is not authorised to disclose it, and the Court is of the
opinion that such is not the case, the Court may make an order requiring
the witness to answer the question, testify or provide that other information.
(2) Where a witness is required to do so pursuant to subsection (1),
he may not refuse to comply with the order requiring him to answer a
question, to testify or to provide that other information, save that no
testimony or other information compelled under the order, or any information
directly or indirectly derived from such testimony or other information,
may be used against the witness in any criminal case, other than a prosecution
for perjury, giving a false statement or otherwise failing to comply
with the order.
(3) Where it appears to any party to any proceedings arising under this
Act that any person who has been or may be summoned as a witness by
him or the adverse party-
(a) has refused or is likely to refuse to answer any question to testify or
provide other information on the basis of his privilege against
self-incrimination; or
(b) where the information is privileged, that the information to be
produced from that person may be necessary to the public interest,
that party may request that an order be made under subsection (1)
compelling the person to answer a question, to testify or to provide such
other information.
(4) Where a person is required to answer any question, to testify or
give such other information pursuant to subsection (3), the provisions
of subsection (2) as to immunity shall apply to him in relation to his
testimony.

Note:

Nitawawekea sheria hizi zote kwenye "Pics and Docs" kwenye KLH ili wanaotaka wanaweza kuzipitia.
 
Mwanakijiji,

Kama hao waliiba kwa ufundi mkubwa, bali hilo neno unalitumia vibaya. Watu wengi tu walijua huo wizi ila walikuwa wanaogopa kusema.

Wale watu wa SA waligundua, wakaguzi wa serikali waligundua, naamini hata kuna wafanyakazi wengi tu walijua. Ila shauri ya woga hawakuwa tayari kusema.

Uchunguzi wa masuala ya pesa ni rahisi sana kuliko uchunguzi kwenye mambo mengine. Kwenye pesa documents halali huwa zinatumika.

Hata Ballali aseme kwa mdomo kwamba alitumwa na Mkapa, hiyo haitoshi mahakamani. Itakuwa ni maneno ya kwake dhidi ya yale ya Mkapa.

Ninachoamini mimi ni kwamba kuna documents mbalimbali ambazo zilitumika kuiba hizo pesa na ukifuata pesa zinakoenda mambo mengi yatakuwa clear.

Kinachokosekana Tanzania ni will ya JK na serikali yake kuwachukulia hatua wahalifu na matokeo yake hata tukimpa kinga Ballali bado hiyo taarifa yake haitafanyiwa kazi.

Tuna mifano ya hao Wahindi na pesa walizoiba mpaka yule jamaa wa radar na eti mpaka leo hajapatikana. Sijui kama kweli wanamtafuta, au ndio danganya toto nyingine.

Case ya wizi wa BOT iko wazi mno, huenda hata hakukuwa na haja ya kuwalipa E&Y kufanya uchunguzi, tayari JK na Meghji walikuwa na taarifa tosha za kuwafanya kuchukua hatua. Labda wananchi mwaka 2010 ndio wataamua, lakini kwa speed hii siamini kabisa JK anataka kukomesha ufisadi huu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom