Balile: DPP, IGP, DCI lifutieni taifa aibu kesi ya Mbowe

Balile: DPP, IGP, DCI lifutieni taifa aibu kesi ya Mbowe

Nadhani kwasababu kesi ipo Mahakamani, hizi makala zingekuja baada ya hukumu........Mahakamani ndiyo patamsafisha vizuri.....haki huwa inachelewa tu ila haipotei
 
Na mimi sitanii, nasema hivi, sehemu pekee ya kumsafisha au kumuacha na uchafu ndugu Freeman vivyo hivyo kwa serikali ni Mahakamani tu. Kumshawishi mwendesha mashtaka aifute kesi wakati ameishaueleza umma ana ushahidi ni kuficha uchafu unukao ili uvune uyoga mweupe.

Pia kisingizio cha kibebeo cha filamu ya utalii kwa kutangaza nchi huku tukihatarisha mwenendo wetu wa kujisafisha kuwa ama hatuna uchafu ama tunao uchafu sasa tunausafisha kwa kutumia vyombo muhimu vya kufanya jambo hili la kusafisha halikubaliki.

Tuiamini mahakama kuwa inamudu kulifanyia kazi jambo hili kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ndugu, Balile, mwanasheria msomi na mwandishi wa habari. Mimi hapa
, raia kindakindaki wa Tanzania, sitanii.

Hivi Mandela alisafishwa na mahakama ya afrika ya kusini mbona alifungwa kwa kesi za kutengeneza kama hii. Kwahiyo upo radhi akina kingai watengeneza ushahidi huo wa kubumba na kutumia mahakama kumfungia wakati ukweli unajulikana siyo gaidi. Kwanini kesi is ifutwe tu na DPP. Na hao walio inging nchi kwenye aibu ugaidi wachukuliwe hatua wote walijifanya mashahidi wa uwongo hao. Ili liwe fundisho kwa polisi wengine.
 
“… milele Rais hashinikizwi …”

Hapa ndipo lilipo tatizo kubwa la Tanzania. Huenda ndio moja ya mambo ya “kijinga” aliyosema Nyerere kuwa “viongozi wetu leo wameacha mazuri yetu yote na kuchukua yale ya kijinga”.

Hadi siku tutakapoachana na dhana ya “Rais ni mungu-mtu” ndipo tutaanza kufanya mambo ya maana nchini. Vinginevyo, tutaendelea kuhangaika na mambo ya ovyo sampuli hii siku zote. Bila shaka Mbowe ashukuru sana suala lake limepata international limelight. Na kwamba hii si awamu ya tano. Ama sivyo hatma iliyokusudiwa kwa Lissu 2017 ingemhusu mapemaa.
 
Kesi inajadiliwa wakati wowote na watu wowote, isipokuwa na jaji tu au prosecutor.
Ni ushamba kufikiria kesi ikiwa mahakamani haiwezi kujadiliwa kupitia redio, TV, makala magazetini n.k
Nadhani kwasababu kesi ipo Mahakamani, hizi makala zingekuja baada ya hukumu........Mahakamani ndiyo patamsafisha vizuri.....haki huwa inachelewa tu ila haipotei
 
Niliandika haya muda kidogo. Ramadhani Kingai kuna vyeo alitaka wakati wa JPM. Hii kesi yeye na Sirro wana jambo lao wanalijua. Sirro anamtaka Kingai kwenye nafasi moja juu ya polisi. Hesabu zinagoma kwa sasa.
 
Wazungu wanaachaje kutuita manyani kwa mfano? Fedha za umma zinatumika kuendesha kesi ya kutunga, badala ya kuhudumia wananchi wenye uhitaji. Lengo ni kukidhi utashi wa majizi ya kura yasiyotaka katiba mpya. Halafu wanaoagiza haya wanajiita wasomi, na ni watu wazima walioota nywele kila tundu la mwili!
Hata mdomoni?
 
E_495e7VEAAGuF-.jpg
 
Na mimi sitanii, nasema hivi, sehemu pekee ya kumsafisha au kumuacha na uchafu ndugu Freeman vivyo hivyo kwa serikali ni Mahakamani tu. Kumshawishi mwendesha mashtaka aifute kesi wakati ameishaueleza umma ana ushahidi ni kuficha uchafu unukao ili uvune uyoga mweupe.

Pia kisingizio cha kibebeo cha filamu ya utalii kwa kutangaza nchi huku tukihatarisha mwenendo wetu wa kujisafisha kuwa ama hatuna uchafu ama tunao uchafu sasa tunausafisha kwa kutumia vyombo muhimu vya kufanya jambo hili la kusafisha halikubaliki.

Tuiamini mahakama kuwa inamudu kulifanyia kazi jambo hili kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ndugu, Balile, mwanasheria msomi na mwandishi wa habari. Mimi hapa
, raia kindakindaki wa Tanzania, sitanii.
Ubishi wenye ujinga ndani yake kama wako huu ndo unatuletea umasikini hapa nchini !!! Kwa nini Mzee Rugemalira ameachiwa huru,huku tukijua kesi yake ya Escrow ilifanya hadi wazungu kurunyima hela za Maendeleo?
Vijana wa kundi la Uamsho,nao wameachiwa huru karibuni kwa makosa ya kudhaniwa kama ya Mbowe!!!
Hii Kesi ya Mbowe kwa hatua za awali tuu za kusikiliza ni vituko na vingi kama vya kubuni.
 
haya sifa za kuajiriwa kama judge zinataka elimu ipi???

elimu haihusiki kabisa kwenye reasoning ya mtu.kama huamini hujastaarabika bado,tena wewe ni hatari kuliko hawa polisi failure.
Waulize polisi kwanini vijana wenye division 1,2 na 3 wapo lakini wao wanataka wenye division 4
 
Kuna member mmoja kwenye ile thread ya kesi ya Mbowe kaandika point ya maana sana; kwamba Jeshi la Polisi ni chombo kinachohusika na haki za wananchi moja kwa moja; is there any oversight body to oversee Police Force? Hakipo!

Yaani wao Polisi wamekabidhiwa mamlaka yote kuhusu haki za wananchi na hakuna chombo huru kinacho-monitor matendo yao? Wanaweza kujifanyia wapendavyo na kuripoti UONGO? Hii haikubaliki; kama taasisi kama TRA, PPRA, LATRA, n.k. ambazo zina oversight bodies kuhakikisha haki inatendeka sembuse polisi wanaohusika na MAISHA ya wananchi? Tena polisi wenyewe ndio hawa wanaoweza kutumika na wanasiasa! Hii ni hatari sana! Katiba Mpya isisahau hili.
Naunga mkono hoja hii
 
Na mimi sitanii, nasema hivi, sehemu pekee ya kumsafisha au kumuacha na uchafu ndugu Freeman vivyo hivyo kwa serikali ni Mahakamani tu. Kumshawishi mwendesha mashtaka aifute kesi wakati ameishaueleza umma ana ushahidi ni kuficha uchafu unukao ili uvune uyoga mweupe.

Pia kisingizio cha kibebeo cha filamu ya utalii kwa kutangaza nchi huku tukihatarisha mwenendo wetu wa kujisafisha kuwa ama hatuna uchafu ama tunao uchafu sasa tunausafisha kwa kutumia vyombo muhimu vya kufanya jambo hili la kusafisha halikubaliki.

Tuiamini mahakama kuwa inamudu kulifanyia kazi jambo hili kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ndugu, Balile, mwanasheria msomi na mwandishi wa habari. Mimi hapa
, raia kindakindaki wa Tanzania, sitanii.
Mahakama ya nchi gani?
 
Kesi inajadiliwa wakati wowote na watu wowote, isipokuwa na jaji tu au prosecutor.
Ni ushamba kufikiria kesi ikiwa mahakamani haiwezi kujadiliwa kupitia redio, TV, makala magazetini n.k
Acha niendelee kubaki mshamba tu,nijuavyo ukweli unapatikana Mahakamani na siyo vijiweni
 
Na Deodatus Balile

Imenichukua muda kuandika makala hii. Ninafahamu kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anashitakiwa kwa tuhuma za kufadhili ugaidi kwa Sh 600,000. Anashitakiwa pia kwa tuhuma za kupanga njama za kulipua vituo vya mafuta katika miji ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam mwaka 2020.

Kubwa zaidi, anatajwa kuwa alitaka kumdhuru Lengai ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mwaka jana. Sabaya yuko mahakamani anashitakiwa kwa wizi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Sitanii, ninafahamu kuna kundi halijakata tamaa. Kila nikiandika ukweli, husambaza taarifa kuwa mimi ni mwanaharakati. Ninadhani katika eneo hili kuna kutojitambua. Kuna tofauti kati ya harakati na uandishi wa habari.

Mwandishi wa habari anasimamia ukweli, ukweli mtupu. Hafanyi kampeni katika jambo analoliandika, bali yeye anaeleza ukweli wa kinachoendelea na kuuonyesha umma ni wapi kuna tundu lizibwe.

Ninafahamu kesi ikiwa mahakamani kifungu cha 114(1)(d) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kinazuia kuijadili, kwa kueleza nani anashinda na nani anashindwa.

Hilo ni jukumu la mahakama, nami sitaingia huko. Ni kwa msingi huo, hata washitakiwa wengine anaoshitakiwa nao Mbowe wala siwataji. Mimi ninalo jambo moja la kitaifa. Sura ya nchi yetu kimataifa.

Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Sylvester A. Mwakitalu, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na Mkurugenzi wa Upelelezi, DCI Kamishna Camillius Wambura mnisikilize kidogo. Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, anaandaa filamu yenye lengo la kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Sitanii, uamuzi wa Rais Samia kuandaa filamu ni wa msingi na wa kuungwa mkono. Yapo mataifa ambayo kamwe hayaifahamu Tanzania. Sisi tuliopata fursa ya kusafiri nje ya nchi, unakuwa kama Washington, ukimwambia Mzungu unatoka Tanzania, anakuuliza: “Tasmania?” Tasmania ni kisiwa cha nchini Australia chenye ukubwa wa kilomita za mraba 90,758. Kina wakaazi 541,000 na kimezungukwa na visiswa vidogo 1,000. Kisiwa hiki ni cha 26 kwa ukubwa duniani. Kinavutia watalii wengi.

Ni nadra sana kukutana na mtu nje ya nchi, tena wakati mwingine wasomi waliobobea wakiifahamu Tanzania.

Uamuzi wa Rais Samia kuitangaza nchi yetu kupitia utalii ni wa kwanza kufanywa na Rais binafsi, bila kutegemea wasaidizi au wageni maarufu kutoka nje ya nchi ndio watangaze utalii wetu. Utalii unakadiriwa kuingiza dola bilioni mbili hapa nchini.

Nchi ya Misri yenye vivutio vichache ukilinganisha na sisi wanaingiza dola bilioni 12 kwa mwaka. Kwa uhalisia, bajeti ya Tanzania ni dola bilioni 14.

Tukiitangaza nchi yetu vizuri, tuna uwezekano wa kupata dola bilioni 15 kama mchezo kutoka kwenye utalii. Ni bahati mbaya, ninasema ni bahati mbaya juhudi hizi anazofanya Rais Samia zinavutwa miguu na uamuzi usio sahihi wa baadhi ya watendaji katika vyombo vya dola.

Sitanii, nimeomba kwa unyenyekevu mkubwa DPP, IGP na DCI mniazime masikio. Kuna makosa tunayafanya, sina uhakika kama ni kwa bahati mbaya au makusudi.

Hili neno ugaidi ni neno baya na la hatari sana katika masikio ya watalii, jumuiya ya wafanyabiashara na wasafiri wa kawaida. Yaliyotokea Septemba 11, 2001 nchini Marekani, bila kusahau ya Agosti 7, 1998 kwa Tanzania na Kenya ni somo kuu la ubaya wa neno gaidi.

Tanzania inapaswa kuwa ya mwisho kumfungulia mtu kesi ya ugaidi au kumtaja mtu kuwa ni gaidi. DCI ameiambia dunia Hamza Mohamed aliyeua askari watatu na mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa gaidi. Inawezekana alikuwa mgonjwa wa akili tu. Neno kama hili halipaswi kutamkwa kamwe kutoka vinywani mwa vyombo vya dola. Mbowe anashitakiwa kwa kufadhili ugaidi, tena kwa Sh 600,000!!! Ugaidi kwa Sh 600,000? Let us be serious.

Sitanii, wanaotafuta nafasi ya kulichafua taifa letu mbele ya jamii ya kimataifa wanakusanya hizi kauli na kueleza kuwa Tanzania kuna ugaidi. Nilisema nitaizungumzia kesi ya Mbowe kwa picha pana. Kila Mbowe anapopelekwa mahakamani, vyombo vya habari vya kimataifa vinaimulika Tanzania na kuhakikisha neno ‘ugaidi’ linatajwa.

Sisi tunaweza kuwa na malalamiko yetu dhidi ya Mbowe. Tena wengine nikizungumza nao wanasema Mbowe alitaka kumshinikiza Rais Samia kwa matamko juu ya Katiba mpya, na milele Rais hashinikizwi. Tunaweza kujikuta katika ‘kujimwambafai’ tunalichafua taifa letu kwa kiwango cha kutisha. Ninashawishika kusema hapa tulipofika tufunge breki.

Tufunge breki tuchague mkondo wa mazungumzo badala ya mabavu. Rwanda na Burundi walipigana kwa mtutu, ila mwisho wa siku walikuja AICC Arusha wakafanya mazungumzo na wakaafikiana.

Ninaomba kusema si kila tatizo la kisiasa tutalitatua kwa kukamata watu na kuwafikisha mahakamani. Kwa kufanya hivyo, tutajikuta tunamchafua Rais aliyeko madarakani na nchi kwa ujumla.

Sitanii, kwa hatua iliyofikiwa DPP nikuombe utumie busara ya Mfalme Suleiman katika kubaini mtoto ni wa nani.

Mama mmoja alisema mtoto auawe, akatwe vipande viwili kila anayedai ni wake apewe kipande akazike. Aliyekuwa mama wa kweli akasema ni bora mama wa kusingizia amchukue huyo mtoto angalau atakuwa anamwona, anampungia mkono akiwa hai. Mfalme Suleiman kwa kauli hizo mbili akabaini mama halisi wa mtoto.

DPP wakati umefika utumie Kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka (CPA) kuondoa kesi ya Mbowe mahakamani. IGP na DCI niwaombe sana neno ugaidi msilitumie tena, linachafua sura ya Tanzania. Mbowe ni Mtanzania. Zungumzeni naye, mwelezeni umuhimu wa uzalendo kwa taifa letu.

Lakini pia msikilize na kesi zake za kuvunjiwa ukumbi wa Bilcanas. Msumeno ukate pande zote. Ninarudia, si kila kesi ya kisiasa tutaimaliza kwa kuifikisha mahakamani. Tuvuke huu msitari unaoleta sura ya ubabe. Mungu ibariki Tanzania.
Jaji Mutungi anataka usuluhishi kuhusu mikutano, Sirro anasema mikutano ya ndani inatia mashaka japo CCM kila kukicha wanafanya! Anasita kusema wazi kuwa hataki wapinzani wafanye! Kwake kukamata ni muhimu kuliko suluhu! Ulichokiandika Sirro hatakubaliana nacho.
 
Back
Top Bottom