Balozi Dkt Lumbanga asifu ujasiri wa Rais Samia

Balozi Dkt Lumbanga asifu ujasiri wa Rais Samia

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
1685959500707.png

Picha: Balozi Dkt Marten Lumbanga

Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Dkt Marten Lumbanga amesifu ujasiri na uwazi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye uongozi kiasi cha kukaribisha mawazo huru kutoka vyama vya siasa kwa manufaa ya nchi pamoja na kuruhusu vyama vya siasa vifanye mikutano ya hadhara kwa kuwa wanaokutana ni Watanzania.

Balozi Lumbanga alisema hayo nyumbani kwake Masaki Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari wa kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).

Kiongozi huyo mzaliwa wa Mlimba mkoani Morogoro alihoji nchi ilinufaika na nini kwa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na je hilo ndilo taifa lilihitaji katika mazingira ya sasa.
 
Kiongozi huyo mzaliwa wa Mlimba mkoani Morogoro alihoji nchi ilinufaika na nini kwa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na je hilo ndilo taifa lilihitaji katika mazingira ya sasa.
Yaani hawa jamaa siwaelewi kabisa, sasa anamuulizaje swali marehemu?
 
Huyu Mzee asili yake ni Mngeta Morogoro kama sijakosea. Kwa miaka yote aliyo hudumu kama Katibu Mkuu enzi za Rais Benjamin Mkapa.

Alishindwa kabisa kuwa mzalendo wa nyumbani kwake, hata kwa kuwapelekea tu barabara ya lami. Yeye mara zote aliigeuza Dar kuwa nyumbani kwake.

Sidhani kama kuna kitu cha kujifunza kutoka kwake. Mwenzake Philemon Luhanjo, alijitahidi kweli kuipandisha hadhi Wilaya yake ya Wanging'ombe.
 
Back
Top Bottom