Balozi wa Tanzania nchini Namibia (Kipilimba): Rais Magufuli yuko mzima anachapa kazi

Balozi wa Tanzania nchini Namibia (Kipilimba): Rais Magufuli yuko mzima anachapa kazi

Kwani balozi ndiye amekuwa msemaji mkuu wa serikali? "I smell a very big rat on the whole issue".
Ndio. Balozi ni msemaji wa Serikali yetu huko anakotuwakilisha. Na amesema kwa sababu amehojiwa.
Sijui hapa Bongo waandishi wetu wamejipangaje
Mimi naona kwenye Katiba mpya tuweke kipengele;
Rais lazima aonekane angalau mara 1 ndani ya wiki 2 kama hana cha kufanya nje angalau atoke akamsalimie Mlinzi wa Geti Kuu la kuingilia Ikulu. Pia kiwepo kipengele kuhusu AFYA. Tutaarifiwe kila siku afya ya Rais wetu aajiriwe mtu wa kutoa taarifa hata kama ataenda chooni na tumbo limemchafuka au vimeonekna vidamu tuambiwe.. Isipokuwa tu damu za kawaida kama Rais atakuwa mwanamke na hajaingia kwenye menopause. Yaani ikitokea ameukwaa STD toka kwa side chick wake lazima tuambiwe. Kwa kweli afya ya mkuu ni mali binafsi ya kila Raia.
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Yaani balozi Namibia ndo atoe taarifa, huku waziri wa mambo ya nje yupo, msemaji wa serikali yupo, mkurugenzi wa habari Ikulu yupo, kuna kitu hakipo sawa Tanzania.
Yaani nashangaa kwa kweli................Au labda yuko nchini huko kikazi ndio maana balozi anatuhabarisha.
 
Ndio. Balozi ni msemaji wa Serikali yetu huko anakotuwakilisha. Na amesema kwa sababu amehojiwa.
Sijui hapa Bongo waandishi wetu wamejipangaje
Mimi naona kwenye Katiba mpya tuweke kipengele;
Rais lazima aonekane angalau mara 1 ndani ya wiki 2 kama hana cha kufanya nje angalau atoke akamsalimie Mlinzi wa Geti Kuu la kuingilia Ikulu. Pia kiwepo kipengele kuhusu AFYA. Tutaarifiwe kila siku afya ya Rais wetu aajiriwe mtu wa kutoa taarifa hata kama ataenda chooni na tumbo limemchafuka au vimeonekna vidamu tuambiwe.. Isipokuwa tu damu za kawaida kama Rais atakuwa mwanamke na hajaingia kwenye menopause. Yaani ikitokea ameukwaa STD toka kwa side chick wake lazima tuambiwe. Kwa kweli afya ya mkuu ni mali binafsi ya kila Raia.
Ohooo kumbe alikuwa anawaharisha wananchi wa huko. Ahsante Mkuu
 
Ndio. Balozi ni msemaji wa Serikali yetu huko anakotuwakilisha. Na amesema kwa sababu amehojiwa.
Sijui hapa Bongo waandishi wetu wamejipangaje
Mimi naona kwenye Katiba mpya tuweke kipengele;
Rais lazima aonekane angalau mara 1 ndani ya wiki 2 kama hana cha kufanya nje angalau atoke akamsalimie Mlinzi wa Geti Kuu la kuingilia Ikulu. Pia kiwepo kipengele kuhusu AFYA. Tutaarifiwe kila siku afya ya Rais wetu aajiriwe mtu wa kutoa taarifa hata kama ataenda chooni na tumbo limemchafuka au vimeonekna vidamu tuambiwe.. Isipokuwa tu damu za kawaida kama Rais atakuwa mwanamke na hajaingia kwenye menopause. Yaani ikitokea ameukwaa STD toka kwa side chick wake lazima tuambiwe. Kwa kweli afya ya mkuu ni mali binafsi ya kila Raia.
Ukiachilia mbali na mambo ya AFYA mfumo wa utoaji wa taarifa kuna tatizo ndani ya serikali watu wanatatizo la kusema ukweli hasa tanzania. Badala ya kusema corona ina badalishwa kuwa tatizo la upumuaji beleshi kijiji kubwa tofauti na wakenya kitu kina tamkwa kwa kwa kificho kiasi kwamba majibu hayajitoshelezi kiasi kwamba watu wanahoji hawapati majibu ya kujitosheleza wakihoji wanakamatwa na kuwekwa kizuizini je dawa mtu ajitokeze ili kuvunja mizizi ya uvumi ulipo.
 
Nairobi, Kenya

Where is President Magufuli as he goes missing from the public? | INSIDE POLITICS WITH BEN KITILI


Source: KTN News Kenya
 
14 March 2021

NCCR-MAGEUZI YAJITOSA SAKATA LA RAIS MAGUFULI


CHAMA cha upinzani nchini Tanzania – NCCR-Mageuzi – kimekoleza moto katika mjadala unaohusu mahali alipo Rais John Pombe Magufuli. Martha Chiomba, katibu mkuu wa chama hicho, amewaambia waandishi wa habari, leo Jumapili, tarehe 14 Machi2021, makao makuu ya NCCR- Mageuzi, Ilala, jijini Dar es Salaam, kwamba wananchi wanataka kujua, “mahali aliko rais wao kipenzi.”

Kwa niaba ya wanachama wa NCCR- Mageuzi na wananchi wengine, Matha amesema, “wananchi wanataja Rais Magufuli ajitokeze hadharani, ili kumaliza shauku yao, kuhusu mahali aliko rais wao.”

Akisitiza hoja yake, Matha ametumia Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, inayozungumzia uhuru wa maoni na haki kwa wananchi kupewa taarifa, wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli zao.
Source : MwanaHALISI TV
 
15 March 2021
"Mtaa wa Kajificheni", Scandinavia

Samia Suluhu adokeza kuhusu ugonjwa wa Rais Magufuli​

Sofia Wambura15th March 20210 Comments

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu ameongeza neno kuhusu uvumi unaoendelea juu ya hali ya afya ya Rais John Magufuli, akidokeza kuwa kuumwa umwa ni jambo la kawaida.
Samia ametoa kauli hiyo akiwa katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi mkoani Tanga. Akihutubia wananchi katika eneo la Mkata, makamu wa rais alisema: “Ni kawaida binadamu kukaguliwa; mara mafua, mara homa, mara chochote kile… tupo salama… huu ni wakati muhimu kwa Watanzania kushikamana…”
Mara baada ya kauli ya makamu wa rais, msomi mmoja ameiambia SAUTI KUBWA: “Kauli yake imebeba ujumbe mzito. Inathibitisha kuwa rais anaumwa, na anaumwa (mafua ya) Corona. Anaposema tupo salama anamaanisha kuwa nchi ipo salama mikononi mwake (Samia), na anamaanisha tushikamane kujenga umoja wa nchi katika mtikisiko huu kwenye jukumu kubwa alilonalo.”
Kauli hii ya Samia imekuja wakati kuna uvumi kuwa Rais John Magufuli amelazwa tangu tarehe 3 Machi na anatibiwa maradhi ya Corona ambayo yameingilia changamoto za moyo wake. Rais Magufuli hajaonekana hadharani kwa wiki tatu sasa, na matukio kadhaa ambayo alipaswa kushiriki yameahirishwa.
Upo pia uvumi, kwa siku tatu mfululizo sasa, kwamba ameshafariki dunia, na kwamba kinachofanywa na dola ni kusogeza muda ili kuweka mambo sawa.
Vyanzo vingine vinasema hata ziara hii ya Samia ni mbinu ya kiintelijensia ya kutuliza umma kisaikolojia kuhusu hali ya afya ya rais. Kwa kumbukumbu tulizonazo, hii ni ziara ya kwanza ya Samia kutangazwa mubashara tangu 2015. Mara zote, ziara zinazotangazwa mubashara na TBc ni za Rais Magufuli.
Kauli hii ya Samia inapingana na ile ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyotoa wiki iliyopita akisema, “rais yupo salama salimini anachapa kazi.” Majaliwa, ambaye alikuwa ameanza ziara ya mikoa ya Kusini, alilazimika kuahirisha ziara hiyo na kurejea Dar es Salaam kwa dharura.
Taarifa zinasema mawaziri na viongozi wengi wa serikali wamefichwa suala hili ambalo linadhibitiwa na kikosi maalumu cha Idara ya Usalama wa Taifa.
Chanzo kimoja kimesema serikali itakuwa tayari kutoa taarifa kwa umma katikati au mwishoni mwa wiki hii. Zipo taarifa pia kuwa kinachochelewesha serikali kutoa kauli ni kwa kuwa wenye uhakika na kinachoendelea ni watu wachache sana, na kuna mtifuano wa nani atapata nini baada ya Magufuli.
Wakati hayo yakiendelea, wapika propaganda wa serikali wamekuwa wakizusha taarifa feki kuhusu hali ya Magufuli, huku wengine wakisambaza video na picha zinazoonyesha akiwa kwenye matukio ya zamani, na wengine wakidai yupo kwenye mfungo wa Kwaresima.
Chanzo kimoja kimeiambia SAUTI KUBWA: “Sahau. Hajiwezi, na hataamka tena, labda uwe muujiza kama wa Lazaro.”
Kauli ya Samia ndiyo ya kwanza kutoka kwa viongozi wakuu inayodokeza kuwa rais si mzima wa afya tofauti na ilivyodaiwa awali na waziri mkuu.

Source : www.sautikubwa.org
FAKE NEWS as usual.
 
Hatimaye kwa mara ya kwanza ndani ya wiki mbili kiongozi wa Tanzania amezungumzia kuhusu afya ya Rais na kusema ni mzima tena anachapa kazi wala hana issue. Binafsi namtakia kila la kheri, huwa napenda kutazama hotuba za huyo mzee Magufuli maana akipewa mic na kuanza kusema huwa harembi wala kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Hehehe!

====================

(Reuters) - Tanzania’s President John Magufuli is in good health and working normally, one of his diplomats has told a broadcaster in Namibia, countering reports he had been flown to hospital in Kenya and then India in a critical condition with COVID-19.

Magufuli, 61, who is Africa’s most prominent coronavirus sceptic, has not been seen in public since Feb. 27.

Tanzanian opposition leader Tundu Lissu has cited medical and security sources for information that the president was flown to the private Nairobi Hospital in neighbouring Kenya and then on to India in a coma.

But the Namibian Broadcasting Corporation quoted Tanzania’s ambassador in Windhoek, Modestus Kipilimba, as saying Magufuli was in good health and remained in Tanzania.

“High Commissioner Kipilimba dismissed the reports, saying Magufuli is in Tanzania going about his normal duties,” NBC said, in what would be the first public comments from a Tanzanian official about Magufuli’s situation since questions were raised.

Kenya’s Nation newspaper cited unidentified political and diplomatic sources earlier this week saying that an African leader, which it did not name, was being treated for COVID-19 on a ventilator at the private Nairobi Hospital. [L1N2L80WJ]

The hospital has said nothing.
In power since 2015 and nicknamed “The Bulldozer”, Magufuli has played down the threat from COVID-19, saying God and remedies such as steam inhalation would protect Tanzanians.

He has mocked coronavirus tests, denounced vaccines as part of a Western conspiracy to take Africa’s wealth, and opposed mask-wearing and social distancing.

Tanzania stopped reporting coronavirus data in May last year when it said it had 509 cases and 21 deaths, according to the World Health Organization (WHO), which has urged Magufuli’s government to be more transparent and to implement COVID-19 curbs.

Magufuli, a former chemistry professor from the village of Chato in northwest Tanzania, was first elected president in 2015. He has faced accusations from Western countries and opposition parties of eroding democracy, which he denies.

Asante mkuu
 
Kipilimba ni balozi wa mchongo , Tangu lini balozi akawa msemaji wa serikali ?
 
Back
Top Bottom