Marekani ameendelea kuwa mwiba mkali dhidi ya miungano ya kikomonisti. Kumbukumbu zinaonyesha alivyofanikiwa kuisambaratisha USSR kupitia mtu wao Gorbachev.
Kwa ukanda huu wa Afrika na mashariki ya mbali alikuwa amebakiza China na Tanzania. Hatimaye, mbinu iliyoboreshwa kutoka ile ilivyotumika kwa USSR imetumika kuubomoa muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Naomba uambatane nami katika mkasa huu wa kihistoria ambapo tutaangazia jinsi ubinasishaji wa bandari zote za Tanganyika kwa mwavuli wa bandari ya Dar ilivyofanikiwa kuibua hisia za utaifa kwa watanganyika ilhali ikikuza utengano na Wazanzibari.